Posts

Showing posts from March, 2017

Viumbe watano wanaopewa heshima jeshini mbali na binadamu

Image
Kwa kawaida wanyama hurahisisha maisha ya wanadamu kwakuwa walinzi wetu, chakula chetu na usafiri wetu lakini kuna baadhi ya wanyama na ndege walioweza kujiwekea heshima duniani hasa  kwenye sekta maalum za kijeshi na wameweza kupata nafasi za juu jeshini.  1: Sir Nils Olav Nils Olav  ni ndege aina ya  Penguin alipewa cheo mara ya kwanza mwaka 1972  na kuwekwa  kwenye timu ya walinzi wa mfalme  Harald V Loudon  wa  Norway kwa sasa Sir  Nils Olav  ni  Brigedia anapewa heshima zote za kijeshi ikiwemo kupigiwa saluti na kukagua jeshi. 2: Treo Ni mbwa aliyetumikia jeshi la  Uingereza kuanzia mwaka 2001 mpaka 2015 ,  Trio ana medali zisizopungua 63, alipewa medali hizo baada ya kufaya kazi kubwa ya kutegua mabomu na kutambua mahali mabomu yalipo fichwa. 3:   William of Orange. William  ni njiwa aliyekuwa mwanajeshi wa jeshi la Uingereza mwenye namba  MI14,  mwaka 1944  William  alip...

ISIMU JAMII

ISIMUJAMII NA ISIMU “Isimujamii na Isimu kama taaluma mbili, hutofautiana lakini kimsingi hukamilishana.” Taaluma ya isimujamii ilianza huko Marekani katika miaka ya 50 na 60. Ilianza na wanasosiolojia kama vile Fishman (1971) na wanaanthropolojia kama vile Del Hymes (1972) na wengine ni wanaisimu kama vile akina Labov William (1972), Gumperz (1972) na Bright William (1965). Wataalamu hawa walitaka kujua tofauti za tamaduni ngeni huko Marekani ambapo kulikuwepo na wamarekani wenye asili ya kiafrika na wamarekani wahindi (wahindi wekundu). Hivyo walitaka kuzifahamu tamaduni hizo ngeni ili waweze kuzifanyia kazi katika elimu. Na hapo ndipo isimujamii ilipoanza Mekacha (2000). Katika kufasili isimujamii Msanjila na wenzake (2011) wanasema kwamba, wataalamu mbalimbali wa lugha wanakubaliana kimsingi kwamba isimujamii ni taaluma inayoshughulika na uchunguzi unaolenga kufafanua uhusiano uliopo kati ya isimu na jamii. (kwa mfano Trudgill 1983; Hudson 1985 na Mekacha 2000). Msa...

SEMANTIKI NA TAALUMA NYINGINE

Semantiki na Taaluma nyingine UHUSIANO WA SEMANTIKI NA TAALUMA NYINGINE Makala haya yatashughulikia semantiki na taaluma zingine zinazokaribiana nazo kama semiolojia, leksikolojia, leksikografia na pragmantiki kwa kuangalia ufanano na utofauti wake na mwisho hitimisho. Semantiki ni taaluma katika isimu ambayo hushughulikia maana ya maumbo au sentensi katika lugha. Taaluma hii ilianza enzi za Aristotle na Plato ambao walizingatia zaidi sifa za maana, katika kipindi hicho walitaka kujua sifa na tabia za maana. Leech (1981) anasema “ wakati fonolojia, mofolojia, na sintaksia ni taaluma zinazohusu matamshi, maumbo, na miundo, semantiki inaangalia maana ya matamshi, maumbo na miundo katika lugha. Anaendelea kusema, maana ni sehemu ya umilisi na ufahamu wa lugha, kujifunza lugha ni kukubaliiana na maana za vipengele vyote vilivyopo katika lugha” Massamba (2004:75) anafasili dhana ya semantiki kuwa ni taaluma ya isimu inayojishughulisha na uchunguzi na uchambuzi wa maana za maneno na tungo ...

Penzi shubiri :2

Image
MTUNZI: JOSEPH SHALUWA ILIPOISHIA JANA... Baada ya kufanya mipango yote kwa siri, tuliamua tukapumzike Marangu Mtoni, twende huko siku ya week-end tukafurahie maisha! Kila nikiufikiria uzuri wa Linna nazidi kuchanganyikiwa, siyo siri Linna ni mrembo jamani! Tamaa ya mapenzi ilinizidi, mshawasha wa mapenzi ukanipanda nikaamua kumweleza hisia zilizoko katikati ya moyo wangu. Mwanzo niliogopa, lakini nijipa moyo nikamweleza. Cha ajabu sasa, wala hakukataa, alikuwa maharage ya Mbeya! Maji mara moja! Akadai eti alikuwa ananipenda mimi tu na alikuwa na Shams kwa sababu ya kitu kimoja tu; pesa! Si vinginevyo. Mh! Jamani nyie!!! SASA ENDELEA... KWANZA tulienda kushangaa maporomoko ya maji kwenye milima iliyokuwa jirani na hoteli tuliyofikia. Tulipata upepo na hewa safi ya mlima Kilimanjaro. Kaubaridi ka eneo hilo kalikuwa si mchezo! Baada ya hapo tukaingia maeneo ya chini kabisa ya maporomoko ya maji yale, ambapo kulikuwa na vijito vidogovidogo. Tukaanza kuchezea maji ambayo yalikuwa baridi ka...

Zitto :NECTA hawana rekodi ya Albert Bashite wala Paul Makonda

Image
Zitto: NECTA Limesema hawana rekodi ya Albert Bashite wala Paul Makonda Tumejulishwa kwenye Kamati kuwa NECTA hawana rekodi ya Albert Bashite wala Paul Makonda. Yani wote hawapo kwenye kanzidata ya Baraza la Mitihani. Kwamba Tanzania haijawahi kuwa na wanafunzi wenye majina hayo NECTA itaweka wazi uhakiki wa vyeti vya Elimu ya Watumishi wa Umma wote tarehe 30 April, 2017 

OKWI BADO NI HATARI ANGALIA ALICHO WAFANYA HAWA WAFARANSA

Image
KAMA ulidhani kiwango cha Emmanuel Okwi kimeshuka baada ya kusota sana benchi kwenye klabu ya Sonderjyske ya Denmark basi unajidanganya, nyota huyo aliyerejea Uganda na kujiunga na SC Villa ‘Jogoo’ yuko bado yuko juu na hashikiki kwa kutupia nyavuni. Katika michezo sita tu aliyoichezea Villa, Okwi ametupia mabao saba huku akitisha kwenye timu ya taifa ya Uganda ‘The Cranes’ alikokabidhiwa kitambaa cha unahodha pia. Katika mchezo wa hisani kati ya Cranes na Jeshi la Ufaransa uliopigwa Jumamosi iliyopita Okwi alizidi kuuthibitishia umma juu ya uwezo wake pale alipopachika bao moja na kusaidia kupatikana kwa jingine katika ushindi wa mabao 3-1 walioupata. Hizi hapa ni picha zinazoonyesha jinsi alivyosababisha penati iliyosaidia kupatikana kwa bao la kwanza lililofungwa na Geofrey Sserunkuma kabla yeye mwenyewe hajatupia la pili akiwa ndani ya sita na Martin Kizza kufunga kitabu cha mabao kwa upande wa Cranes kwa penati

Nadharia ya upokezi/ mwitiko wa msomaji

NADHARIA YA UPOKEZI/MWITIKIO WA MSOMAJI NADHARIA YA UPOKEZI/MWITIKIO WA MSOMAJI Malengo ya kazi hii ni: (a)        Kueleza maana ya nadharia ya upokezi. (b)        Kueleza historia fupi ya nadharia hii pamoja na kuwataja waasisi wa nadharia hii. (c)        Kueleza mihimili ya nadharia hii. I.          UTANGULIZI Nadharia inayoshughulikia upokeaji wa matini za fasihi inahusiana na ulimbwende na mitazamo ya kisaikolojia.  Kimapokeo, msomaji huwa na mawazo kuhusu matini anayopitia.  Kutokana na tajriba ya usomaji, msomaji hupata hisi maalum.  Uteuzi na upokeaji wa sanaa hushirikishwa sana na hisi kwa mujibu imani na nadharia za kilimbwende. Ulimbwende ni mwelekeo wa kusimulia ambapo wahusika walikuwa mashujaa na wenye nguvu za ajabu na ambao walikuwa wanajeshi.  HISTORIA FUPI YA NADHARIA YA UPOKEZI NA WAASISI WA NADHARIA             YENYEWE ...

Huu ndio utajiri wa MILLARD AYO

Image
Huu ndio utajiri wa millard Ayo

TAIFA STAARS VS BOTSWANA FT 2- 0

Image

Nape alivyo tishiwa na bastola tukio zima lipo hapa

Image

Maneno ya NAPE mchana huu

Image

Maneno ya Zitto kabwe baada ya uteuzi wa raisi magufuli leo

Image
Baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dr. John Pombe Magufuli march 23, 2017   kufanya mabadiliko madogo kwenye baraza la Mawaziri ambapo sehemu ya mabadiliko hayo ni kamteua Waziri mpya wa Habari, Sanaa, Utamaduni na michezo. Sasa basi leo mbunge wa Kigoma mjini Zitto Kabwe kupitia ukurasa wake wa twitter ameyaandika haya>>> Nimezungumza na mbunge wa Mchinga Nape kuthibitisha kuwa Ni Kweli ameondolewa kwenye Uwaziri. Nape ni Shujaa wa kizazi chetu’ Zitto Kabwe Ruyagwa  ✔ @zittokabwe Nimezungumza na mbunge wa Mchinga @Nnauye_Nape  na kuthibitisha kuwa Ni Kweli ameondolewa kwenye Uwaziri. Nape ni Shujaa wa kizazi chetu 9:05 AM - 23 Mar 2017    

Alicho andika NAPE NAWIE baada ya taarifa kutoka ikulu

Image
Alichokiandika Nape Nnauye baada ya taarifa kutoka ikulu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dr. John Pombe Magufuli amefanya mabadiliko madogo kwenye baraza la Mawaziri ambapo sehemu ya mabadiliko hayo ni kumteua Waziri mpya wa Habari, Sanaa, Utamaduni na michezo… na taarifa kamili ndio hii hapa chini kutoka  IKULU . Aliyekuwa Waziri wa Habari Nape Nnauye ameandika kupitia account yake ya Twitter ‘Ndugu zangu naomba TUTULIE! LEO mchana nitakutana na Wanahabari na tutalizungumza hili. Nitawaambia saa na mahali, kwasasa naomba TUTULIE!’

UMEMSIKIA SAMATA ALIVYO SEMA KUHUSU KOLOMIJE ?

Image
Mtanzania  Mbwana Samatta  tayari yupo Dar es Salaam  kwa ajili ya maandalizi ya michezo ya kimataifa ya kirafiki iliyo katika kalenda ya  FIFA  ambapo  Tanzania itachezwa jumamosi ya March 25 na March 28 ikianza na  Botswana  na baadae Burundi . Samatta  ambaye ndio nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania  Taifa Stars  jioni ya March 22 2017 kupitia ukurasa wake wa twitter amejaribu kutoa wazo na kuuliza swali kwa watu wake kuwa  “Nina wazo kwa nini Dar isibadirishwe jina ikaitwa Kolomije kwani tutapungikiwanini @himid23mao  @IdrisSultan @jotitanzania   @makivic08 @Ulimwengu11 “ Swali la  Samatta  limechukuliwa kama utani tu kutokana na jina la kijiji cha Kolomije  kilichopo  Mwanza  kimekuwa maarufu kutokana na kutajwa mara kwa mara hivi karibuni katika mitandao ya kijamii.

Raisi magufuli ateuwa waziri mpya wa Habari ,sanaa utamaduni na michezo

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dr. John Pombe Magufuli amefanya mabadiliko madogo kwenye baraza la Mawaziri ambapo sehemu ya mabadiliko hayo ni kumteua Waziri mpya wa Habari, Sanaa, Utamaduni na michezo… na taarifa kamili ndio hii hapa chini kutoka  IKULU .

Kaburi alilozikwa yesu lafunguliwa tena Israel

Image
Chumba kidogo kinachofunika kaburi ambako inaaminika Yesu Kristo alizikwa kimefunguliwa rasmi tena baada ya kufanyiwa ukarabati kwa miezi tisa katika Kanisa la Kaburi la Yesu Kristo katika maeneo ya mji wa zamani wa Jerusalem kilikuwa kimekuwa dhaifu sana kiufundi. Aidha, kilikuwa limebadilika rangi na kuwa karibu rangi nyeusi kutokana na masizi ya mishumaa mingi ambayo huwashwa eneo hilo. Kanisa takatifu lafunguliwa Israel Mji wa kale sana wagunduliwa Misri Mzozo kati ya madhehebu matatu ambayo kwa pamoja husimamia kanisa hilo - Kanisa la Kiothodoksi la Ugiriki, Kanisa la Kiarmenia na Kanisa Katoliki la Kirumi - ulichelewesha ukarabati huo kwa miongo mingi. Antonia Moropoulou, aliyesimamia ukarabati, amesema chumba hicho sasa kimepata tena rangi yake asili inayokaribia hudhurungi. Chumba hicho kilifanyiwa ukarabati

Nadharia ya Ufeminism

NADHARIA YA UFEMINISM SWALI:   Malengo ya nadharia ya ufeministi yamejitokeza kukinzana na maisha halisi ya mwanamke wa kiafrika.      Jadili Nadharia ya Ufeministi imefasiliwa na wataalamu mbalimbali kama vile:     Wamitila (2003:253), hii ni nadharia ambayo imewekewa msingi na msukumo mkubwa pamoja na nia ya kupigania ukombozi wa mwanamke kutokana na pingu za kiutamaduni, kidini, kijamii, kisiasa na kiuchumi. Hii ni nadharia ambayo inasaili na kudadisi itikadi ya kiume ambayo imekuwepo katika jamii kwa kipindi kirefu. Kudadisi pia fasiri za kiume za fasihi pamoja na mikabala ya kiubabedume. Ntarangwi (2004:45), ni nadharia ambayo inajaribu kukiuka mitazamo ya kiume ambayo yaelekea inatumiwa sana katika jamii. Mukobwa M. nadharia ya ufeministi imetokana na mkondo na harakati za kutetea haki za wanawake ulimwenguni na imejikita katika imani ya usawa wa kijinsia, kijamii, kisiasa na kiuchumi. Kwa jumla, nadharia ya ufeministi...

Nadharia ya Ufeminism

NADHARIA YA UFEMINISM SWALI:   Malengo ya nadharia ya ufeministi yamejitokeza kukinzana na maisha halisi ya mwanamke wa kiafrika.      Jadili Nadharia ya Ufeministi imefasiliwa na wataalamu mbalimbali kama vile:     Wamitila (2003:253), hii ni nadharia ambayo imewekewa msingi na msukumo mkubwa pamoja na nia ya kupigania ukombozi wa mwanamke kutokana na pingu za kiutamaduni, kidini, kijamii, kisiasa na kiuchumi. Hii ni nadharia ambayo inasaili na kudadisi itikadi ya kiume ambayo imekuwepo katika jamii kwa kipindi kirefu. Kudadisi pia fasiri za kiume za fasihi pamoja na mikabala ya kiubabedume. Ntarangwi (2004:45), ni nadharia ambayo inajaribu kukiuka mitazamo ya kiume ambayo yaelekea inatumiwa sana katika jamii. Mukobwa M. nadharia ya ufeministi imetokana na mkondo na harakati za kutetea haki za wanawake ulimwenguni na imejikita katika imani ya usawa wa kijinsia, kijamii, kisiasa na kiuchumi. Kwa jumla, nadharia ya ufeministi...