Posts

Showing posts with the label Historia

DOLA YA WACHAGGA MIAKA MICHACHE KABLA YA UHURU.

Image
Wakati wazungu wanagawana bara la Afrika, walipokuja walikuta baadhi ya maeneo kuna tawala zenye nguvu, zilizokua na mfumo rasmi wa uongozi. Wao waliziita tawala za jadi (Chiefdoms). Moja ya tawala iliyokua na nguvu katika ukanda huu wa Afrika Mashariki ni dola ya wachagga (Chagga state). Zilikuwepo nyingine zenye nguvu kama Himaya ya Sultani wa Zanzibar, Dola ya Buganda, Nyamwezi, Ngoni, Haya, Hutu, Tutsi, Hehe, etc. Dola ya wachagga imetamalaki eneo la pembezoni mwa mlima Kilimanjaro kuanzia maeneo ya Rongai hadi Siha. Eneo hili lilikua na mtawala mkuu mmoja (aliyeitwa Mangi Mkuu). Huyu alikua kama Rais ama Mfalme wa jamii hiyo. Chini yake walikuwepo watawala wakuu wawakilishi wa majimbo. Hawa waliitwa 'Mangi Waitori'. Chini yao walikuwepo watawala wa wa maeneo madogo, hawa waliitwa Mangi kama vile Mangi Meli wa Old Moshi, Mangi Sina wa Kibosho, Mangi Salakana wa Useri etc. Kwa mfano eneo kama Rombo lilikuwa na Mangi wengi. Alikuwepo Mangi wa Keni, Mangi wa Masha...

KAMWE HAITASAHULIKA 25 DECEMBER 1914

Image
Kuna matukio ndani ya dunia hii ni magumu kusahulika kwa vizazi na vizazi. Ni ngumu kwa waingereza kumsahau Diego Maradona na goli lake la mkono robo fainali kombe la dunia mwaka 1986. Yapo mengi sana ya kukumbukwa ambayo yanarithishwa  kwa vizazi na vizazi ili kumbukumbu isipotee. Ijumaa ya tarehe 25 December 1914 katika maadhimisho ya siku kuu ya Christmas, miezi mitano tu baada ya mtutu wa vita vya kwanza vya dunia kuwaka, dunia ilishuhudia tukio la ajabu ambalo mpaka leo limebaki historia ya pekee katika uga wa soka , diplomasia, kijeshi na masuala ya haki za kibinaadamu. Vikosi vya majeshi ya Uingereza toka Bataliani namba mbili ya London Rifle Brigade vilikutana na vikosi vya Ujerumani kwenye eneo lisiloshikiliwa na upande wowote kivita ( noman's land ) na kusheherekea siku kuu ya Christmas kwa kuimba nyimbo za Christmas na kucheza mpira pamoja. Mtandao wa CIA Book of facts unaielezea kirefu vita hii. Tukio hili ambalo kwenye kumbukumbu kidunia linajulikana kama ...

KUHUSU FURSA ZA KISWAHILI KATIKA NCHI ZA KIGENI, NA DR ANNE JABET KUTOKA CHUO KIKUU CHA VIRGINIA MAREKANI

Image
Dr Anne Jabet Chuo kikuu cha Virginia USA Katika mahojiano mafupi yaliyo fanyika kwa njia ya barua pepe kati ya masheleblog na mkufunzi huyo kutoka chuo kikuu cha Virginia Marekani  amabaye pia ni mjumbe wa CHAUKIDU,  katika mahojiano yaliyo husu fursa mbalimbali katika lugha ya kiswahili katika nchi za kigeni Dk A. Jabet aliithibitishia mashelebog uwepo wa fursa mbalimbali za ajira  na za kimasomo katika nchi za kigeni kwa wasomi wa lugha ya kiswahili Aidha alipo ulizwa kuhusu upatikanaji wa fursa hizo alijibu kuwa fursa hizo hutolewa, Na mhitaji hupaswa kuzitafuta katika mitandao hasa mtambo tafutizi wa Google. Je unaomba fursa za kazi au za kusoma uzamifu? inabidi kuangalia nafasi za kazi mtandaoni kisha kuomba kazi, kunazo kazi mbalimbali hasa za kufunza Kiswahili-umejaribu kuomba nafasi ya fulbright teaching assistant? kama ni nafasi ya kusima inabidi kijaza fomu kupitia idara unayotaka kusomea. natumaini nimejibu swali lako ndug mwandishi. Hayo nd...

TUNACHOJIFUNZA MAUAJI YA KIMBARI RWANDA – SEHEMU YA-02

Image
WATANZANIA wengi hawajui nini kilisaba-bisha mauaji ya kimbari ya nchini Rwanda yaliyosababisha mamia ya watu kuuawa mwaka 1994. Naamini kama wakisoma makala haya watajifunza kitu na kuona umuhimu wa mshikamano na amani tulionayo na faida yake. Endelea: Kuna baadhi ya wasomaji hawajui nini maana ya mauaji ya kimbari. Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa mwaka 1948, ibara ya 2, unafafanua kuwa mauaji ya kimbari ni: “Tendo lolote kati ya yale yafuatayo linalofanyika kwa nia ya kuharibu kikamilifu au katika sehemu, kikundi cha kitaifa, kikabila, kirangi au cha kidini, kama vile mauaji ya watu wa kikundi hicho; kusababisha athari, kubwa upande wa mwili au wa akili kwa watu wa kikundi hicho…” Wiki iliyopita tulisema Jeshi la Uganda mwaka huo wa 1994 yalipotokea muaji hayo ya kutisha ya kimbari Rwanda lilikuwa eneo la Mto Kagera ili kuhakikisha kuwa taharuki iliyozuka baada ya maelfu ya miili hii kuonekana haigeuki na kuvuruga amani katika eneo hili. Lakini pia jeshi lilikuwa hapa...

MAAFA YA MV BUKOBA , TANZANIA TUMEJIFUNZA NINI? SEHEMU YA -01

Image
KILA KIFO NA SIKU YAKE Kila binadamu atakufa, lakini kila kifo kina siku yake. Nyaisa Simango, katika makala haya  ana tudhihirishia hivyo. Vinginevyo ni vipi mtu anaweza kuelezea alivyo nusurika wakati mamia ya wenzake walio kuwa katika meli moja walishindwa kujiokoa. Ilikuwa sio siku yake. Ziwa victoria limekuwepo kwa karne na karne, watu wanaoishi kuzunguka ziwa hilo wamekuwa wakijishughulisha na shughuli mbalimbali. Kuvumbuliwa kwa Ngalawa, Jahazi, Boti, na meli  kumewezesha kazi za usafirishaji kuwa rahisi. Bila shaka Simango alipo itwa na mkuu wake wakazi na kuarifiwa kuwa itabidi aende Bukoba  kumpeleka mfungwa kusikiliza rufaa ya kesi yake alifurahi kwani angeweza kuona mandhari nzuri njiani.  Ijapokuwa yeye anatoka katika nmkoa unao pakana na ziwa  bado angefurahia kula samaki.  Nakwavile hakuwahi kufika bukoba, safari ingempa fursa nzuri ya kutalii mjini huko, na pia baada ya kumfikisha mfungwa huko alikotumwa na yeye angepata fursa nzuri...

TUNACHOJIFUNZA MAUAJI YA KIMBARI RWANDA – SEHEMU YA 01

Image
WATANZANIA wengi hawajui nini kilisababisha mauaji ya  Kimbari ya nchini Rwanda  yaliyosababisha maelfu ya watu kuuawa. Naamini msomaji wa makala haya atajifunza kitu na kuona umuhimu wa mshikamano na amani tulionao hapa nchini. Tafadhali tuwe pamoja. Mauaji ya Kimbari ya Rwanda ni mgogoro ambao vyombo vya habari vya  Magharibi  vimekuwa vikiuzungumzia kama kisa na mateso makubwa waliyoyapata watu, lakini wakati huo huo vinakwepa kulipa nafasi suala la kuzungumzia wahusika halisi wa kutokea mauaji hayo ya kutisha. Leo tutaanza kwa kuangalia wasababishaji wa mauaji ya  Kimbari yaliyotokea katika nchi hiyo ya katikati mwa Afrika, nchi isiyo na bahari ( Land locked Country ) na ambayo imezungukwa kila upande na nchi nyingine Tanzania ikiwemo. Historia inaonesha kuwa mwaka 1918, Ubelgiji  iliivamia nchi hiyo na kuanza kuifanya koloni lake na kuikalia kwa mabavu. Kabla ya hapo ilijulikana kwa jina la Rwanda-Urundi wakati ilipokuwa ndani ya makolo...