Posts

Showing posts with the label Fumanizi

FUMANIZI

Image
  *FUMANIZI* (Sehemu ya III) *©Mwafrika Merinyo* Fatima hakuelewa chanzo cha maradhi haya yaliyomsibu Himid na hakutaka hata kujua. Alishamuuliza mumewe kama amewaona matabibu na jibu la mumewe likawa kwamba wataalam wamemweleza kuwa hana tatizo, ni hali ya kupita tu. Na sasa Fatima hakujali kuhusu hali ya Himid, kwani alikwishaona kuwa hapa ndoa haiwezi kuwepo. Alishawasiliana na bi mkubwa Salama, mke wa kwanza wa Himid, kuulizia kuhusu shida hii ya mume wao. Naye Salama akakiri kuwa kuna tatizo, ila kwa mawazo ya bi Salama Himid haelekei kujishughulisha na tiba yoyote. Mwaka wa pili baada ya mchezo wa vidole kuanza, Fatima alichoka, akihisi kuwa anajitesa bila sababu. Kuomba talaka akahofia kuwa angeonekana mkorofi, kwa kuwa wenzake wawili walikuwa wanaendelea kuvumilia. Lakini kwa umri wake wa miaka arobaini na uzao wa mtoto mmoja tu, akajihisi mhitaji sana na asiye na msaada. Katika hali ile, na katika kuwa na maelewano ya kirafiki kati yake na Rama, mmoja wa wateja wake wa bia...

FUMANIZI

Image
  *FUMANIZI* (SEHEMU YA II) *©Mwafrika Merinyo* Hulka yake ilimwepusha ugomvi na mapigano kati yake na Rama. Tena hakumjua yule jamaa kwa jina wala kwa wasifu, seuze kipimo cha nguvu zake. Kidudumtu wake alimwambia tu kwamba kuna mtu, tena mtu mzima mwenziye, aliyekuwa anatia mkono katika sahani yake ya ugali na kusokota matonge makubwa kumzidi. Mwanzoni hakutaka kuamini. Kidudumtu akakoleza moto na kumwambia aje siku ya Jumanne kufumania, kwani mwizi wake alikuwa na tabia ya kuja kuchonga na kula nanasi siku za jumanne. Jambo hili kwanza lilimfadhaisha. Kisha likamtia hasira. Akaweka nia na kuingia mjini Uswazini siku ya Jumatatu kwa jahazi la jioni kutoka Chanjali. Akalala kwa jamaa yake na siku ya Jumanne akazuga mitaa ya mbali mpaka pale alipoletewa taarifa kuwa tayari nyegere analipua mashuzi mzingani na keshaanza kubugia asali. Himid akatoka huko atokako kwa hasira na wahaka kwenda kumfumania mkewe Fatima. Baada ya kushindwa kupambana na mgoni wake, sasa alijikuta pia anaishi...

FUMANIZI

Image
  *FUMANIZI* (Hadithi fupi) *©Mwafrika Merinyo* Himid aligonga mlango mara ya kwanza. Akagonga mara ya pili. Mara ya tatu akalazimika kusindikiza na mwito: “Hodi!” Mwili ulimtetema kwa fukuto la hisia mchanganyiko. Hasira, uchungu, wivu, maumivu, wahaka. Alijua kilichokuwa kinaendelea ndani, kwani kaja kwa taarifa za kidudumtu na bila kumpa taarifa mkewe Fatima. Kaletwa na wahka, kabebwa na roho ya kisasi japo hakujipanga atakavyolipiza, kasukumwa na mshawasha wa kuadhibu bila kujua aina ya adhabu wala utekelezaji wake utakavyokuwa.  Ndani, Fatima na Rama walikuwa ngomani. Walikuwa wamekolea mchezoni, kila mmoja akikwea mlima kutoka upande wake, wamekaribia kukutana kileleni. Kitanda kilikuwa kinaonewa, la kinaadhibiwa. Pumzi zao zilikuwa zikipishana mithili ya fuo za msana chuma. Palikuwa hapatoshi. Na katika patashika ile ya “Njoo basi! Nipishe nipite miye kwanza! Utaniua! . . .” ndipo hodi tatu  zilipogongwa kwa mfululizo mlangoni. Ilikuwa adhuhuri, jua limeuacha tu ut...