Posts

Showing posts with the label WANAWAKE KUMEKUCHA

Jinsi ya kukabiliana na mambo yanayozuia wasichana kuwa wabunifu Tanzania

Image
  Ni pamoja na kuondia vikwazo vya kitamaduni na wasichana waanze waamke na kujitoa. Wadau watakiwa kuwa mstari wa mbele kutoa taarifa sahihi kwa wasichana. Pia wametakiwa kutatua changamoto za jamii yao.  Kilimanjaro.  Licha ya juhudi mbalimbali za Serikali na wadau wa maendeleo kuwawezesha wasichana wengi kuingia katika fani ya sayansi, bado wanakabiliwa na changamoto mbalimbali zinazowakwamisha kuwa wabunifu.  Changamoto hizo zikiwemo za mifumo na utamaduni zinawazuia wasichana kuonyesha uwezo na kutoa suluhu za teknolojia zitakazosaidia kuboresha maisha ya jamii.  Mei 21 mwaka huu wadau wa ubunifu walikusanyika mkoani Kilimanjaro ili kujadili changamoto zinazokwamisha ubunifu miongoni mwa wasichana na namna ya kuwasaidia kujikwamua na wakatumia ubunifu huo kutoa suluhu zitakazosaidia kuboresha maisha ya jamii.  Mwanzilishi mwenza wa jamii ya wadau wa ubunifu ya Startup Grind Kilimanjaro, Dorcas Mgogwe amesema ubunifu miongoni mwa wasichana upo chini kut...

Kinachowakwamisha wanamuziki wa kike Tanzania kutamba kimataifa

Image
Baadhi ya wadau wa muziki wamesema ni ukosefu wa ubunifu na uwekezaji mdogo katika kazi wanazofanya.  Pia ushirikiano mdogo na wanamuziki wa nje na kushindwa kutumia mizuri majukwaa ya kimataifa ya mauzo kama Youtube.  Wameshauriwa kujiongeza ili kulifikia soko la kimataifa kama wenzao wa kiume.  Dar es Salaam. Wakati wanamuziki wa kike wa nchi za magharibi mwa Afrika na nje ya bara hilo wakipasua anga la kimataifa kwa kazi za muziki, wenzao wa Tanzania wana kibarua kigumu kuelekea katika anga za kimataifa Hali hiyo inatokana na changamoto mbalimbali ikiwemo ukosefu wa ubunifu wa kutengeneza muziki wenye mvuto unaoweza kugusa idadi kubwa ya watu duniani.  Mathalani, mwanamuziki wa kike wa Nigeria,  Yemi Aladei  ameweza kujipatia umaarufu mkubwa duniani kutokana na muziki wake kugusa maisha ya watu wengi.  Chaneli yake ya Youtube ina wafuasi wasiopungua  milioni 1.1,  Yemi maarufu kama Mama Afrika mwenye miaka 30 ni miongoni m...

Kutana na mwanadada wa miaka 26 anayeongoza taasisi ya kuwainua wasichana kiuchumi Tanzania

Image
Lydia akiwa katika masomo yake ya elimu ya juu katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Udsm), yeye na wenzake  waliamua kuanza kuwasaidia wasichana kwa kuendesha warsha pamoja na matamasha yaliyolenga kuelimisha na kumuunga mkono mwanamke kwa ujumla. Picha | Mtandao . Ni mhitimu wa chuo kikuu anayeongoza taasisi ya ‘Her Initiative’ inayofanya kazi kwa lengo la kumkomboa mtoto wa kike dhidi ya ukatili wa kijinsia. Alikuwa na ndoto ya kuwasaidia wanawake tangu akiwa shule ya msingi. Utoaji wa elimu kwa wasichana, kuwasaidia kuanzisha miradi ya kiuchumi ni njia zinazotumiwa na taasisi hiyo. Dar es Salaam.  Wakati Serikali ikiendelea na mikakati ya kuzuia na kukomesha ukatili wa kjinsia kwa wasichana, baadhi ya taasisi nao wanatumia mbinu mbalimbali ili kuhakikisha mtoto wa kike anakuwa huru ili kutimiza ndoto zake ikiwemo kuelimika na kupata fursa za kiuchumi. Lakini wapo wanawake ambao hawasubiri kufanyiwa kila kitu, bali wanachukua hatua kuwasaidia wasichana wali...

maajabu ya temple of appolo na watu kutoka dunia nyingine

Image

Malkia wa Sheba: na safari yake ya kutafuta hekima

Image
Licha ya kuwa chimbuko lake bado linashindaniwa, Malkia wa Sheba – anaejulikana pia kwa jina la Makeda – ni jina muhimu kwa Waethiopia. Kwa wengi ni alama ya uzuri, upendo, amani, na mtu aliyependa kutafuta elimu na maarifa. Lakini kwa Waethiopia, Malkia wa Sheba kwao ni kila kitu. Kukutana kwake na Mfalme Sulemani miaka 3,000 iliyopita, ni jambo la kihistoria. Hii hapa hadithi yake. Malkia wa Sheba aliishi lini?  Anaaminika aliishi zaidi ya miaka elfu tatu iliyopita. Malkia wa Sheba anajulikana kwa lipi?  Kufuatia kiu chake cha kupata maarifa, malikia huyu anasemekana alimtembelea mfalme Sulemani wa Israel aliyekuwa na hekima nyingi mjini Jerusalem. Historia iliyoandikwa inadokeza kuwa malkia huyu alimzalia mfalme Sulemani mwana wa kiume ambaye alikuja kuwa mfalme wa kwanza wa Ethiopia wa utawala wa Kisulemani. Tunajuaje kuhusu kuishi kwake?  Tukio hilo la Jerusalem lilinakiliwa katika nyaraka mbali mbali ikiwemo bibilia ya Kiyahudi, Quran ambamo Malk...

MFAHAMU YAA ASANTEWAA MWANAMKE SHUJAA ALIYEKUWA MALKIA WA ASHANTI

Image
Alizaliwa mwaka 1863 katika mji wa Besease katika jamii ya Ashanti yenye dhahabu nyingi, Ghana ya sasa, magharibi mwa Afrika. Kaka yake Nana Akwasi Afrane alikuwa ndiye Edweso (kiongozi, au chifu) wa milki ya Ashanti wakati huo. Nana Yaa Asantewaa akiwa bado binti alijishughulisha sana na kilimo.  Kaka yake (chifu Akwasi) alipokuwa Edweso (kiongozi) alituma askari wake kwenda mapiganoni dhidi ya wakoloni. Baadae aliwekwa kizuizini na wakoloni katika visiwa vya Ushelisheli pamoja na mfalme Prempeh I. Akiwa kizuizini, Nana Akwasi Afrane alimteua dada yake NANA YAA ASANTEWAA kuwa malkia wa milki ya Asante.  Mwaka 1899 gavana wa wakoloni Waingereza Frederick Hodgson aliitisha mkutano mjini Kumasi ili kulazimisha apewe kiti kilichotengenezwa kwa dhahabu tupu ambacho ni alama takatifu ya Ashanti ambapo askari wa kikoloni walishindwa kukipata kiti hicho, hii ni baada ya kufikiri kwamba ugumu wa kuwatawala Waashanti ungeisha baada ya kupata kiti hicho cha dhahabu. Nan...

VIDEO Shujaa Mekatilili Wa Menza Mwanamke Shujaa Kutoka Giriama

Image
 Karibu ndugu msomaji leo nimekuletea mwanamke shujaa kutoka makabila ya mijikenda kabila  lenye muunganiko wa makabila kenda ya kenya ambayo ni Wadigo Wachonyi Wakambe Waduruma Wakauma Waribe Warabai Wajibana Wagiryama . Wadigo wako kusini kabisa  wakiingia hadi Tanzania.( Kwamujibu wa profesa Noor shariff katika makala ya DW, 'kiswahili kinawenyewe' kabila la Wagiryama ndilo kabila kubwa zaidi la kibantu) Shujaa mekatilili anatoka katika kundi la wagiriama na ndiye aliyewaongoza wagiriama kupigana na wakoloni katika kipindi cha ukoloni wa mwingereza. Mwanamke huyu anaheshimiwa zaidi katika kabila la wagiriama kama kiongozi wa kitamaduni na sherehe ya kumuenzi mama huyu aliyeletea sifa kabila la giriama hufanyika kila mwaka maeneo ya Kisii kule kenya bofya video hii kutazama             kukuletea makala haya ni mtaalamu wa sanaa, lugha na utamaduni, pamoja na lugha na TEHAMA +255766605392

Queen: Msichana aliyebuni tovuti kuwasaidia vijana mafundi

Image
Vyuo vinakataa maombi yake, kisa amepata daraja la tatu hivyo hana sifa ya kusoma elimu ya juu. Ameona isiwe tabu. Maarifa yake ya masomo ya Kemia , Fizikia na Biolojia aliyosomea kidato cha tano na sita, ameamua kuyahamishia katika uhalisia maishani. Sasa ameamua kuwa mjasiriamali akishirikiana na mafundi kutoa huduma kwa watu mbalimbali. Ni Queen Mtega (20) msichana anayeamini katika uthubutu. Amebuni tovuti yake ya FundiPopote, akilenga kutoa huduma za ufundi kwa wananchi na kuondoa dhana ya watu kuwaona mafundi kama watu wasio na thamani. Wazo la FundiPopote “Sikuwahi kuwaza kuwa nitajikita katika masuala ya ufundi kwani awali niliwaza kujikita katika mazingira, lakini nilishindwa kutokana na changamoto mbalimbali,”anasema. Baada ya kumaliza kidato cha sita Queen alichaguliwa kwenda kushiriki mafunzo ya jeshi, lakini baada ya kurejea kutoka jeshini siku moja alikwenda kumtembelea rafiki yake. Aliomba maji ya baridi, akaletewa ya moto. Mama wa rafiki y...

Mfahamu mwanamke nguli anayehubiri teknolojia ya Blockchain Tanzania

Image
Ni mmoja wa wanawake wa kwanza nchini ambaye amechukua kozi ya umahiri kwenye teknolojia hiyo inayokua kwa kasi duniani. Kwa sasa amejikita katika kugawa maarifa kuhakikisha wanawake wenzie na Watanzania wote wanachangamkia fursa za teknolojia hiyo. Amesema blockchain itaondoa upigaji katika utoaji wa huduma mbalimbali za kijamii kikiwemo kilimo. Dhana ya kutokufanya kazi nyingine unapoajiriwa inazidi kupungua kwa baadhi ya watu walioona fursa zinazoweza kumsaidia kujiongezea kipato zaidi kupitia teknolojia. Hii ni kwa sababu matumizi ya teknolojia hayahitaji uwe katika eneo hilo moja kwa moja bali unaweza kufanya vitu vingine kupitia fursa zilizopo mtandaoni. Sandra Chogo (42), ambaye ameajiriwa kama mkaguzi wa mahesabu, aliona fursa nyingine kwenye masuala ya mfumo wa ‘Blockchain’ na kuamua kuchangamkia fursa hiyo ya teknolojia inayokua kwa kasi zaidi duniani. Kwa kifupi blockchain ni teknolojia ya mfumo unaomruhusu mtu kutuma au kuhifadhi vitu vyake z...

Kutana na Aneth David mwanasayansi anayechipukia Tanzania

Image
Kwa sasa anafanya utafiti wa kina wa viumbe vidogo vidogo kwenye udongo utakaosaidia kuongeza tija katika sekta ya kilimo nchini. Ni mmoja ya wanawake ambao wanahitajika katika kuhakikisha wanakuwa mifano kwa kizazi cha sasa juu ya dhana ya ugumu wa masomo ya sayansi. Dar es Salaam. Imekuwa ikiaminika kuwa watoto wa kike wengi wanaogopa masomo ya sayansi na kukukimbilia kuchagua masomo ya biashara au sanaa kwa kuwa ndiyo rahisi kuyasoma na hata baadaye kutoka kimaisha.  Hata hivyo, ukweli ni kwamba kuna wanawake wamefanya mengi katika ugunduzi wa vitu mbalimbali duniani baada ya kusoma vema na kuipenda sayansi. Wao na sayansi, sayansi na wao tangu wakiwa wadogo na wanafanya vizuri  hadi sasa kuliko hata wanaume.  Miongoni mwao ni binti wa Kitanzania, Aneth David (29), Mhadhiri msaidizi katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) na mwanafunzi Shahada ya Uzamivu (PhD) aliyejikita kufanya utafiti wa namna viumbe vidogo vidogo vilivyo kwen...