Posts

Showing posts with the label Fasihi

TAMTHILIYA LINA UBANI &UHAKIKI

Image
Miongozo ya Lugha na Fasihi MIONGOZO ya Lugha na Fasihi  ni mfululizo uliokusudiwa wanafunzi na watpenzi wa lugha na fasihi ya Kiswahili. Mfululizo huu umebuniwa kutokana na lengo la kuwasaidia wanafunzi wa hjjha na fasihi katika ngazi mbalimbali za taaluma zao, hasa wale wanaojiandaa kwa mitihani ya Taifa. Mfululizo huu utatoa vijitabu ambaVyo vitakuwa vinasaidia kuchambua vitabu vya lugha na fasihi ambavyo vimeteuliwa na Wizara ya Elimu vitumike kuwatahini wanafunzi katika vyuo na sekondari nchini. Kwa hali hiyo, mfululizo huu utajumuisha uchambuzi wa vitabu vilivyochapishwa na Dar es Salaam Umvereity Press (DUP) na vile ambavyo vitakuwa vimechapishwa na mashirika raengine. Uchambuzi wa kila kitabu utazingatia fani na maudhui yanayojitokeza katika kazi hiyo, na mwishoni kuna maswali ambayo yanamwongoza mwanafunzi. Miongozo hii imeandaliwa kwa kuzingatia utaalamu wa hali ya juu ili kurahisisha usomaji wa kitabu kinachohusika. Wanafunzi na wapenzi wa lugha na fasihi...

fasihi simulizi: fasihi ya watoto

  FASIHI SIMULIZI YA WATOTO  Wataalamu wanasemaje kuhusu fasihi simulizi Wamitila  (2003: 44), anaeleza kuwa fasihi simulizi ni dhana inayotumika kurejelea kazi ambazo kimsingi hupokezanwa kwa njia ya masimulizi au kwa mdomo. Anaendelea kueleza kuwa fasihi hii hutumiwa katika jamii kwa njia ya kupashana maarifa inayohusu utamaduni fulani, historia ya jamii, matamanio yao, mtazamo wao na historia yao. Aidha, Njogu (2006: 2) anaeleza kuwa, fasihi simulizi ina ubunifu na uhai wa kipekee wenye kutoa fursa njema ya kuibua nadharia za kijamii, kiuchumi na kisiasa, pia aina hii ya fasihi ni uti wa mgongo wa maendeleo ya binadamu. Kwani ndani yake kuna masimulizi, maigizo, tathmini za mazingira na mahusiano ya kijamii. Kwa ujumla fasihi simulizi ni sanaa inayotumia lugha ya mazungumzo ya ana kwa ana kufikisha ujumbe uliokusudiwa kwa hadhira husika. Lyimo (2014), anaeleza kuwa fasihi ya watoto ni fasihi iliyotungwa ama na watu wazima au watoto wenyewe yenye kutumia lugha na hukusu...

MISINGI YA UCHAMBUZI WA KAZI ZA FASIHI ANDISHI

TAASISI YA ELIMU YA WATU WAZIMA STASHAHADA YA ELIMU YA WATU WAZIMA NA MAFUNZO ENDELEVU KWA MASAFA KIT 06208: MISINGI YA UCHAMBUZI WA KAZI ZA FASIHI ANDISHI                              MASWALI YA PROJEKTI                    OKTOBA 2019 JIBU SWALI MOJA TU Fafanua vipengele vya fani na maudhui katika tamthiliya moja uliyosoma katika kozi (KIT 06208). Chambua vipengele vya kimaudhui vilivyoyojitokeza katika riwaya mbili ulizosoma. Ainisha na fafanua vipengele mbalimbali vya fani na mahudhui vinavyojitokeza katika fungate ya Uhuru.

UTOAJI WA HABARI KWA NJIA YA PODKASTI

Image
Masshele Swahili Chuo- BBC Kupodkasti ni kurikodi mazungumzo yako na kuyaweka katika tovuti. Mteja anaweza kuyasikiliza kwa kutumia komputa au simu ya kisasa. Badala ya kuandika unayotaka kueleza, unaweza piya kuyazungumza na kumfurahisha mteja ambaye sasa ataweza kukusikiliza hata akiwa njiani - kwa kutumia simu. Podkasti ni kama kushughulika na tovuti yako, lakini podkasti unatumia sauti. Kila nakala ni sawa na nakala ya tovuti, itahusu mada fulani. Kama unapotaka kuandika katika tovuti, tafuta pahala/mada fulani; yaani kitu ambacho watu wanataka kujifunza au kujua ambacho hakipo kwengineko. Kumbuka kuwa watu wanaosikiliza podkasti wanatafuta ujuzi/ufundi maalumu na watapenda kuwasikiliza wajuzi wa yale yanayozungumzwa. Podkasti inaweza kuwa ya mtu mmoja tu, yaani wewe watu wawili watu wengi Mtindo huu wa podkasti umesambaa sasa kila pahala. Kuna waandishi wa habari au wasanii ambao wanavutia na wanazungumzwa sana watu wanapokutana. Podkasta maarufu wana...

| HEKAYA ZA LOLIONDO | Babu asisitiza dawa ilifanya kazi [Part 2]

Image

| HEKAYA ZA LOLIONDO | Tiba ya Babu wa Loliondo [Part 1]

Image

Wanawake katika fasihi ya kiswahili (Womens in Swahili literature)

Fasihi ya kiswahili ni zile kazi za kiufundi na kisanaa zilizo andikwa au kusemwa  zitumiazo lugha ya kiswahili, utamaduni wa mswahili au pengine mtunzi kuwa mswahili, na zinazowahusu waswahili, kwa lengo la kufikisha ujumbe fulani. Tunazo kazi kadhaa za kifasihi kama vilie  -Nyimbo -Ushairi -Riwaya -Tamthiliya -Hadithi -Utenzi -Tendi -Methali -Vitendawili -Nyambi -Matangazo ya biashara( kwa mujibu wangu) N.k. Je mwanamke anatazamwa vipi katika fasihi ya kiswahili? Wanawake wamekuwa wakifasiliwa kwa namna tofauti tofauti katika kazi za kifasihi, hasa kulingana na mtunzi Wa kazi hiyo na Jamii anayotoka. Mathalani, ukichunguza kazi za E. Mbogo hasa zile za Malkia Bibi titi Mohammed, Morani na Watoto wa mama ntilie utagundua kuwa Emanuel mbogo anamtazama mwanamke tofauti na watunzi wengine wanavyomtazama kama vile, P.Muhando katika kazi za Nguzo mama, Pambo, na ile ya Tambueni haki zenu. Kazi za kifasihi zinazomsawiri mwanamke kichany...

Dhima za fasihi linganishi

Fasihi linganishi ni ule ulinganishaji wa kazi mbili za kifasihi kutoka kwa mwandishi mmoja au kazi ya Jamii moja na nyingine. Ulinganishaji huu huhusu pia kulinganisha fani nyinginezo. Aisha ulinganishaji huweza kuongozwa na misingi ya ulinganishaji kama vile Historia Utamaduni Itikadi Falsafa Maswala ya kijinsia Dhamira Fani na kadhalika Ulinganishaji wa kazi za fasihi huweza kuwa na dhima zifuatazo -Kujua utamaduni, historian falsafa za Jamii nyinginezo -kuweza kuzigawa kazi za kifasihi katika makundi ya kitaifa, kiafrika. na kiulimwengu -Kujua ubora na udhaifu wa fasihi yako -Kujua mwego wa mwandishi -Kujifunza mbinu Mpya za uandishi -Kukuza taaluma ya tafsiri -Kujua chimbuko na maingiliano ya Jamii. www.masshele.blogspot.com

Mitazamo kuhusu fasihi simulizi ya Kiafrika

Dhana ya fasihi simulizi kwa mujibu wa Mlokozi (1996), ni fasihi inayotungwa au kubuniwa kichwani na kuwasilishwa kwa hadhira kwa njia ya mdomo na vitendo bila kutumia maandishi. Hivyo fasihi simulizi inafungamana na muktadha au mazingira fulani ya kijamii na kutawaliwa na mwingiliano wa mambo kama vile fanani, hadhira, fani, tukio, mahali pamoja na wakati wa utendaji. Ni aina ya fasihi ambayo hutumia mdomo katika kuumbwa, kuwasilishwa na kusambazwa kwa wasikilizaji na watumiaji wake (Balisidya, 1983). Fasili hizi zinasisitiza kwamba fasihi simulizi inategemea uwepo wa fanani, hadhira, jukwaa na mada. Hivyo kwa ujumla, tunaweza kusema kuwa fasihi simulizi ni sanaa inayotumia lugha kisanaa ili kufikisha ujumbe kwa hadhira iliyokusudiwa kwa njia ya mdomo au masimulizi. Nadharia ya fasihi simulizi ni mawazo yanayotoa mwongozo kuhusu mwelekeo wa jambo fulani katika fasihi simulizi. Kwa kufanya hivyo, nadharia hizo zimeweza kuleta mabadiliko katika nadharia asilia zilizokuwe...

UHAKIKI TAMTHILIYA YA FUMO LIYONGO

IKISIRI Haya ni masimulizi ya kitendi yaliyowekwa katika umbo la tamthiliya, ambapo mwandishi wa tamthiliya hii Emmanuel Mbogo  amechota visa na matukio kutoka katika utendi wa Fumo Liyongo na kuweka ubunifu wake.  Katika tamthiliya hii mwandishi anamtumia mhusika Fumo Liongo kama shujaa wa kitendi, katika kumuelezea Fumo Liongo mwandishi anagawa visa vyake katika vitendo vitano na kila kitendo kina maonesho mbalimbali. Katika kitendo cha kwanza (onesho ni mji wa Pate) mwandishi anaanza kwa kuwaonesha wananchi wa Pate wakienda kumlaki Liongo baada ya kurudi kutoka vitani ambako aliweza kumshinda adui yake Sango Vere. Liongo anapokelewa kwa shangwe na watu wa Pate na kuhutubia umati akiwapa hali halisi ilivyokuwa katika uwanja wa kivita. Katika onesho la pili tunamuona mfalme na waziri kiongozi wakipanga mikakati ya kumuua Liongo. Matukio ya kitendo cha pili yanaanzia  katika mji wa Fumo Liongo ambapo tunamuona Fumo Liongo akiwa na mama yake ...