Posts

Showing posts with the label AFYA

KUFANYA MAZOEZI KIPINDI CHA UJAUZITO JE NI SALAMA?

Image
1. UMUHIMU WA MAZOEZI KIPINDI CHA UJAUZITO 2. MAZOEZI YA MAMA MJAMZITO 3. JINSI YA KUFANYA MAZOEZI UKIWA NA MIMBA Kufanyaa mazoezi ni jambo ambalo binadamu wengi hulifanya mara kwa mara ikiwa ni mpango wa kimaisha au hulifanya mara moja moja. Mazoezi ni kitendo cha kuushughulisha mwili kwa njia mbalimbali. Mazoezi yaliyojipatia umaarufu ni kama kutembea, kukimbia, kushiriki michezo mbalimbali na hata watu hutumia vifaa maalumu vya mazoezi kuishughulisha miili yao. Hivi karibuni vituo vingi tuu vya mazoezi ambavyo vilikuwa maarufu kwenye nchi zilizoendelea vinaanza pia kuonekana barani Afrika. Mazoezi ni mazuri kwa afya ya mwili na akili. Na pia mazoezi yanahusishwa kabisa kisayansi kwenye jedwali la kupata afya bora. Ikiwa ni kawaida kabisa watu wa umri wowote ule kushiriki katika mazoezi, huwa inazua mjadala mara kwa mara ni kwa namna gani wajawazito wafanye mazoezi. Kwanza kabisa je wanaruhusiwa kisayansi kufanya mazoezi? Waandishi wa Idhaa ya Kiswahili ya DW waliwahi kuya...

TENDE, MAJI ZINAVYOFAA WAKATI WA MFUNGO WA RAMADHANI

Image
V YAKULA  vinavyofaa kuliwa wakati huu wa Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ni vingi, leo tutaanza kuchambua kimoja baada ya kingine, Mbali na Waislamu, uchambuzi huu unawafaa pia wale ambao siyo Waislamu. Chakula kilichozoeleka zaidi kwa futari ni tende. Baada ya kushinda kutwa nzima na Swaumu, kiwango cha sukari ya mwili hupungua na hivyo, kuhitaji kujazilizwa tena. Aina ya kwanza ya sukari itumikayo mwilini na hasahasa ubongoni ni glukosi. Mshuko wa sukari walioupata wale ambao hawakula au kunywa kwa kipindi kirefu, unaweza kusababisha ulegevu wa mwili. Pindi sukari inapoliwa kwa njia ya chakula au kinywaji, viwango vya glukosi ya mwili hujisawazisha vyenyewe na kumfanya mtu aliyefunga asijihisi kuchoka sana na huwa na nuru zaidi ya macho. Ingawaje tende, mara nyingi, si chakula kinachopendelewa sana na watu wenye njaa, lakini ndicho chakula kisicho na mafuta, na ni chanzo madhubuti cha sukari. Nusu ya sukari zitolewazo na tende ni kwa ajili ya glukosi pekee. ...

EPUKA VYAKULA HIVI NDANI YA MWEZI WA RAMADHANI

Image
KUNA aina sita za vyakula na ulaji ambao mfungaji anashauriwa kuepuka ili kulinda afya yake wakati huu wa mfungo wa Ramadhani, vyakula hivyo ni kama ifuatavyo: Vyakula vya kukaanga na vyakula vya mafuta mengi kama chips, sambusa, biriyani, pilau na kadhalika vinafaa kuepukwa kwa sababu vina calories nyingi na virutubisho vichache hivyo kusababisha mlo uwe usio na uwiano. Hii husababisha shibe isiyo na faida na huongeza uchovu wakati wa Ramadhani kwa mfungaji. Pia mfungaji aepuke kula vyakula vilivyo na chumvi nyingi kama achari pickles, sauces, chips na kadhalika kwa sababu chumvi hunyonya maji mwilini. Kutokana na unywaji mchache wa maji ndani ya Ramadhani, utumiaji wa chumvi nyingi unaweza kusababisha upungufu wa maji mwilini, kitaalamu huitwa dehydration na udhaifu wa mwili ndani ya Ramadhani Mfungaji pia aepuke kula vyakula na vinywaji vilivyo na sukari nyingi kama soda, pipi, vinywaji vya kuongeza nguvu n.k. Ingawa vinaweza kukupa nguvu ya haraka lakini vyakula hivi ...

UTAFITI : KUMPA MTOTO CHINI YA MWAKA JUISI ZA VIWANDANI UNAMWEKA KWENYE HATARI YA KUPATA PUMU

Image
Utafiti mpya unaonesha ya kwamba watoto wanaokunywa juisi au ambao mama zao walikunywa vitu vyenye sukari kipindi cha ujauzito wapo kwenye hatari kubwa ya kuugua ugonjwa wa Pumu Wajawazito ambao walikunywa soda na vinywaji vyenye sukari (sugary beverages) wana asilimia 70 ya kuzaa watoto ambao baadae watapata ugonjwa wa Pumu Matokeo ya utafiti kutoka Chuo Kikuu cha Harvard nchini Marekani yameonyesha ya kwamba, watoto wanaokunywa vinywaji vyenye sukari au juisi (artificial juice) na ambao mama zao walikunywa soda kipindi cha ujauzito wao wapo kwenye hatari kubwa ya kupata ugonjwa wa Pumu. Watoto ambao waligundulika kuwa na kiwango kikubwa cha sukari aina ya fructose (ambayo hupatikana kwenye juisi au soda) kwenye milo yao kipindi cha ukuaji, walikuwa kwenye hatari ya asilimia 79 kupata ugonjwa wa Pumu ukilinganisha na watoto ambao hunywa vinywaji vyenye sukari kwa nadra au wale watoto ambao hawanywi kabisa vinywaji hivyo. Kina mama ambao walitumia vinywaji vyenye sukari a...

JINSI YA KUPATA MTOTO WA KIUME NA WAKIKE

Image
Katika urutubishaji yai la mwanamke linabeba chromosome X yani XX. Na mbegu ya mwanaume inabeba chromosome XY. Chromosome X kutoka kwa mwanamke ikikutana na Y kutoka kwa mwanaume mtoto wa kiume hupatikana. Chromosome X kutoka kwa mwanamke ikikutana na X kutoka kwa mwanaume mtoto wa kike hupatikana Fahamu sifa za chromosomes X na Y za mwanaume. Ili uweze kufanikiwa kuchagua mtoto wa kiume au wa kike lazima ujue sifa za chromosomes hizi zinazoamua jinsia ya mtoto. Sifa za chromosomes Y • Zina spidi  kubwa sana kwahiyo kama yai lipo tayari zenyewe  zitawahi kwenda kurutubisha • Zina maisha mafupi sana kulinganisha na X Sifa za chromosomes X • Zina spidi ndogo sana • Zina maisha marefu kulinganisha na Y Baada ya kujua sifa za chromosome ambazo ndo zinatusaidia kuamua jinsia twende moja kwa moja kwenye jinsi ya kupata mtoto wa jinsia unayotaka Mambo ya kuzingatia katika suala la kuamua jinsia ya mtoto amtakaye: • Lazima mwanamke ajue mzunguko wake (menstrual cycle)siku ya...

CHUNUSI , JINSI YA KUZUIA NA MATIBABU

Image
Chunusi ni ugonjwa wa ngozi unaowapata watu wa mataifa yote na wa umri wote. Ugonjwa uliozoeleka zaidi ni ule unaowapata vijana wakiwa kwenye umri wa balehe. Zaidi ya asilimia 70 ya vijana wa umri huu hupata chunusi. Chunusi huwapata vile vile watu wenye umri mkubwa na, vichanga wengine hupata chunusi kutokana na mama zao kuwarithisha homoni kabla tu ya kuzaliwa. Ukurasa huu utajadili chanzo cha chunusi katika mwili wa binadamu, aina za chunusi na hatua zinazoweza kuchuliwa ili kuepukana na chunusi. Katika mwili wa binadamu, chunusi huonekana zaidi maeneo ya usoni, mgongoni, kifuani, mabegani na shingoni. Kutegemeana na uwingi wa chunusi hizo, mwathirika huweza kunyanyasika kimawazo na kupata makovu juu ya ngozi yake. Kuna dawa za kutibu chunusi ingawa ni ugonjwa unaoweza kujirudiarudia. Chunusi huondoka polepole sana na wakati mwingine chunusi mpya huanza kujitokeza kabla nyingine kupona kabisa. Ni ugonjwa unaotakiwa kupewa tiba ya mapema ili kuepuka kupata madhara ya kudu...

FAHAMU ZAIDI KUHUSU KUHARIBIKA KWA MIMBA (ABORTIONS)

Image
Tatizo la mimba kutoka au kutolewa ni jambo ambalo limewakumba kina mama wengi walio katika umri wa kuzaa. Aidha mijadala kuhusu kuhalalishwa au kuendelea kuharamishwa kwa utoaji mimba ni jambo linalochukua nafasi ya mazungumzo ya kila siku katika maisha yetu. Kwa baadhi ya nchi, suala la utoaji mimba ni jambo lililohalallshwa kisheria ingawa kwa nchi kama Tanzania, suala hili halijahalalishwa isipokuwa tu pale panapokuwa na sababu za kitabibu zinazolazimisha kufanya hivyo. Nini maana ya mimba kutoka? Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), utokaji mimba (abortion) hutokea pale ambapo kiumbe (mimba) kilicho chini ya wiki 22 kinapotoka kwa sababu moja ama nyingine, au kinapotolewa kwa njia yeyote ile. Aidha shirika la Afya limekwenda mbali zaidi na kutoa maana nyingine ya utokaji mimba kuwa ni pale mtoto (kiumbe) anapozaliwa akiwa na uzito wa chini ya gram 500. Aidha baadhi ya matabibu hupendelea kutumia neno 'abortion' kumaanisha kitendo cha utoaji wa mi...