Posts

Showing posts with the label Makala

UKIWA NA SIFA HIZI LAZIMA UOLEWE!

Image
M OJA  kati ya kilio kikubwa cha mabinti ni kupata wanaume sahihi wa kuwaoa. Ishu si tu kuolewa lakini kupata mume sahihi ni jambo lingine. Wengi wanaishia kukutana na wanaume ‘wasanii’ ambao hawana mpango wa ndoa. Wao wanafurahia maisha ya ujana hadi pale watakapojisikia. Kwa kuwa kiasili mwanaume ndio humfuata mwanamke, fursa ya kuanza kuchagua mke mtarajiwa, mchumba, ‘girlfriend’ huwa inaanza kwa mwanaume. Wazo la kukufanya wewe kuwa rafiki, mchumba na baadaye mke mara nyingi huwa linaanza kwa mwanaume. Hivyo basi utakubaliana na mimi kwamba, kwa kiasi kikubwa mwanaume ndio mwenye ‘funguo’ ya ndoa. Ndiye anayeweza kusema ‘Yes’ au ‘No’. Mara nyingi mwanaume ndiyo mwenye maamuzi ya kusema nioe au nisioe kwa sasa. Ndio mwenye uamuzi wa kusema nioe mwanamke huyu au nisimuoe nitaoa mwingine. Nimuoe huyu kwa sababu ananifaa, nimuache huyu kwa sababu hanifai. Licha ya kuwa mwanaume anaweza kuwa na matatizo yake lakini pamoja na yote hayo, jukumu la kufanya maamuzi huwa linaba...

Hivi Ndivyo Vitu Hatari Vinavyoweza Kuharibu Na Kuvunja Ndoa Ya Wapendanao Katika Familia

Image
WAPENZI wanagombana, ndoa zinavunjika na familia nyingi zipo kwenye msoto kwa sababu ya ubinafsi. Tunazungumza mengi lakini ukweli ni kwamba endapo kila mmoja atafanikiwa kuushinda ubinafasi, upendo utashamiri kila kona. Ubinafsi una matawi mengi. Mtu anaposaliti, maana yake ametekwa na tamaa binafsi. Anashindwa kutambua kwamba yeye ni mpenzi wa mtu, kwa hiyo anatakiwa kulinda penzi la mwenzake. Hajui kama anachokifanya ni dhuluma ya hali ya juu. Ukweli ni kwamba unapoanzisha uhusiano na mtu, maana yake umeamua kumchagua yeye ndiye amiliki penzi lako. Kwa hiyo ukienda kulitoa kwa mwingine, huo ni ubinafsi. Umeingiwa na umimi kwa kuona kwamba unatoa rasilimali za ndani ya mwili wako mwenyewe. Kwa nini ukimfumania mwenzi wako panachimbika? Ni kwa sababu alichokitoa kwa mtu mwingine ni chako, kwa maana hiyo amekutendea dhuluma. Ndiyo maana ukawa na jeuri ya kupigana kwa sababu haki yako imetumika ndivyo sivyo. Hivyo basi, usaliti ni ubinafsi. Umeingiwa na jeuri kwamba una...

HII NDIO HOTUBA YA MWISHO YA HAYATI MUAMMAR GADDAFI

Image
QADAFFI ANAANZA HIVI: "Kwa jina la Mwenyezi Mungu (Allah), Mungu mpaji, na mwenye rehema.... Kwa miaka takribani 40 ama ilikuwa zaidi sikumbuki. Nachokumbuka ni kuwa nilifanya kila nilichoweza kuwapa watu wangu nyumba, hospitali na shule. Na kila walipohisi njaa niliwapa chakula. Niliifanya Benghazi kutoka jangwa kuwa ardhi nzuri ya kilimo. Nilisimama imara dhidi ya Ronald Regan (Rais wa zamani wa Marekani), alipomuua binti yangu niliyemuasili. Alikua anajaribu kuniua mimi lakini akamuua yule binti yatima masikini. Niliwasaidia kaka na dada zangu waafrika fedha kupitia AU. Nilifanya kila nililoweza kuwafanya watu wangu waelewe maana halisi ya demokrasia; ambapo watu wa tabaka la chini niliwapa madaraka. Lakini hawakuridhika. Hata aliyekuwa na nyumba ya vyumba kumi, nguo mpya, na fanicha nzuri, hakuridhika. Alihitaji zaidi. Kwa jinsi walivyokuwa wabinafsi walihitaji zaidi. Hivyo wakawaambia Marekani kuwa wanataka "demokrasia" na "uhuru". Hawakuj...

KINGEREZA KINADUMAZA UBUNIFU NA UFANISI KATIKA TAIFA HILI.

Image
Makala Na: Jumaa H Heshima Sitoanza kwa salamu kama ilivyo kawaida ya kile kiitwacho ustaarabu wa Waswahili. Kimsingi hakuna ustaarabu wa Waswahili. Ustaarabu ni wa Waarabu ila tunazo amali tulizozisaliti kwa kuzinasibisha na Uarabu. Basi ya nini kuzibebesha amali zetu adhimu majina yanayozinyima Uafrika wake? Tutafute jina sahihi kuzirejelea amali hizi. Hasira za makala haya ni juu ya athari za "ukoloni lugha'' unavyonyonya na kufifisha ubunifu wa vijana wasomi wa taifa hili pendwa, Tanzania. Sote tunafahamu kuwa Kiswahili ni lugha ya taifa hili, Tanzania. Mwanazuoni mmoja katika kongamano la Kiswahili pale Chuo Kikuu cha Dar es Salaam aliuliza  swali; ``je, Kiswahili ni lugha ya taifa kikatiba au kimazoea?'' Ukumbi mzima ulitumbua macho pasi na kujibu. Sababu hakuna andiko lolote lile kwenye katiba wala sheria yoyote ile nchini humu inayoeleza na kuelekeza kuwa lugha yetu ya taifa  ni Kiswahili. Hii ni lugha ya taifa kimazoea ni si kimaan...

KIFUNGO HURU CHA AJIRA

Image
Na: Jumaa H heshima Kifungo kwa maana ya kawaida kabisa ni hali ya kuzuia mtu au kiumbe katika mazingira fulani na kukiwekea mipaka kufika baadhi ya maeneo au kufanya baadhi ya mambo. Neno huru linaashiria hali ya kuamua kufanya jambo mtu alitakalo bila vizuizi. Dhana ya uhuru ni tata kidogo, katika jamii yoyote ile uhuru huwa na mipaka. Mfano kila mtu anao uhuru wa kuvaa nguo aitakayo kwa namna apendavyo ila tu nguo hiyo isioneshe tupu zake. Pia kuna uhuru wa kuongea unalolitaka ila sio kumtukana mtu au kumdhalilisha na kumvua utu wake. Utata uko hapa kwenye kuamua unalolitaka na kisha kuwepo kwa mipaka. Ajira kwa mujibu wa Kamusi ya Karne ya 21 ni kazi ya kulipwa mshara. Maana hii inatuacha na swali juu ya ajira binafsi (self emloyment). Je, muajiriwa analipwa mshahara na nani? Tunaweza kujiridhisha kuwa katika hali hiyo mfanyakazi huyo analipwa mshahara na kazi hiyo anayoifanya na isipomlipa anavyotaka basi ataiacha kama ilivyo kawaida kwa waajiriwa wengine. ...

TAMTHILIA

Image
UANDISHI WA TAMTHILIA Tamthilia ni nini? Tamthilia ni utanzu ambao hutegemea mazungumzo na uigizaji ili kuwasilisha ujumbe wake. Huu ni utanzu ambao huandikwa kwa mtindo wa mazungumzo ya wahusika (Wamitila, 2007). Nkwera (h.t) anaelezea kuwa tamthilia ni: “ Tamthilia ni mchezo wa kuigiza au utungo wa kisanaa ambao huweka wazo fulani katika matendo na mazungumzo ” (Nkwera, h.t) AINA ZA TAMTHILIA Kwa mujibu wa Aristotle, kuna aina mbili za tamthilia. Aina ya kwanza ni tanzia na nyingine ni ramsa. Tanzia ni nini? Tanzia ni kinyume cha ramsa kwa maana kuwa hutumika kuonesha kuanguka na kushindwa kwa mhusika maarufu, mbabe, au shujaa atokaye katika tabaka la juu yaani mtu wa nasaba bora (Mutembei, 2005 katika mihadhara ya SW 234). Kama ilivyo kwa ramsa, tanzia ilianzia katika miviga ya kidini, katika sherehe ya kumhusu Dionisius. Wachezaji na Waigizaji walivalia na kuonekana kama mbuzi wakiimba nyimbo zilizohusu anguko la shujaa (Mutembei, 2...

UKIFANYA HAYA MAMBO MATANO NILAZIMA UFANIKIWE KATIKA MAISHA

Image
Unaweza ukawa upo kwenye hali ya kulalamika maisha yako ni magumu na unashangaa kwa nini hufanikiwi katika maisha yako kama jinsi unavyotaka wewe. Hali hii inaweza ikawa inakuumiza pengine kila ukiangalia rafiki zako ama maisha ya wengine yanavyozidi kuwa mazuri, wakati wewe upo katika hali ngumu. Na pengine umekuwa ukijiuliza nini siri kubwa  ya mafanikio yao ambayo wanaitumia ambayo wewe huna. Kutokana na hali hiyo umekuwa ukijilaumu kujilaumu na kujiuliza kwanini nyingi ambazo hazina majibu. Kitu usichokijua watu hawa huwa wanatumia mbinu Fulani kufanikiwa. Kawaida, katika maisha kama ulivyomchezo wa miguu, au michezo mingine mara nyingi huwa zipo mbinu za kufanikisha kile tunachokifanya. Mbinu hizi huweza kutambulika kama sheria, kanuni, au siri lakini zote hulenga kukufanikisha kama unataka mafanikio ya kweli. Mbinu hizi zinapotumiwa kwa bahati mbaya au nzuri huwa hazifanyi ubaguzi zinamwendea yoyote na kuleta matunda unayoyataka. Hata kama ikitokea umezitumia ...

Mambo 5 Ya Kuzingatia, Kama Wewe Ni Mjasiriamali Unayetaka Mafanikio Makubwa

Image
Mafanikio ni kitu cha lazima sana katika safari ya mjasiriamali. Uwe mjasiriamali mdogo, wa kati au mkubwa kwa vyovyote vile  unahitaji mafanikio. Lakini ili kufanikiwa na kufikia mafanikio hayo,  yapo mambo ya msingi ambayo unatakiwa kuyazingatia. Mambo hayo ni kama haya yafuatayo:- 1. Kujiwekea malengo. Ukiwa kama mjasiriamali unayetakiwa kufikia mafanikio makubwa, suala la kujiwekea malengo ni lazima kwako. Unapokuwa na malengo yanakuwa yanakupa mwelekeo sahihi wa kupata kile unachokitaka. Hiki ni kitu ambacho unahitaji kukizingatia sana kwani ni nguzo kubwa ya kufikia mafanikio makubwa. 2. Kujitoa Mhanga(Take Risks) Hakuna mafanikio makubwa utakayoyapata bila kujitoa mhanga. Wajasirimali wote wakubwa ni watu wa kujitoa mhanga sana. Wanakuwa wako tayari kutoa kitu chochote ilimradi wafikie malengo yao. Kitu cha kuzingatia hata kwako wewe unalazimika kujitoa mhanga na kulipia gharama ili kufikia mafanikio makubwa. 3. Kutokuogopa Kushindwa. Wengi wetu tumefun...

SABABU KWANINI JERUSALEM NI MJI MTAKATIFU

Image
Haki miliki ya picha AFP Image caption Maeneo matakatifu ya kidini Jerusalem Kumekuwa na mzozo wa muda mrefu kuhusu udhibiti wa mji wa Jerusalem kati ya Waisraeli na Wapalestina. Mji huo kwa sasa huwa umegawanywa mara mbili, Jerusalem Mashariki na Jerusalem Magharibi. Jerusalem ya Magharibi hutazamwa na Israel kama mji wake mkuu nayo Jerusalem Mashariki hutazamwa kuwa mji mkuu wa taifa la Wapalestina (litakapoundwa), ingawa eneo hilo bado kwa kiwango kikubwa limetawaliwa na Israel tangu vita vya 1967. Tangu wakati wa vita hivyo, Israel imejengwa nyumba za walowezi wa Kiyahudi takriban 200,000 ambao huishi Jerusalem Mashariki, hatua iliyoshutumiwa na jamii ya kimataifa. Eneo hilo huishi Wapalestina takriban 370,000. Israel ilitangaza 1980 Jerusalem yote kuwa mji wake mkuu wa milele, lakini nchi nyingi duniani hazikubali azimio hilo. Hivyo basi, balozi za nchi za kigeni katika Israel ziko nje ya Jerusalem, katika mji wa Tel Aviv. Mzozo huo umefufuliwa tena kutokana na ha...