Posts

Showing posts with the label HESLB

Wanafunzi 26,688 kukosa mikopo elimu ya juu 2021-22

Image
Hiyo ni sawa na asilimia 30.1 ya waombaji wote. Serikali yatenga mikopo ya Sh570 bilioni kwa wanafunzi 162,000. Majina ya waliopata mikopo kuwa wazi kabla ya Oktoba 25. Dar es Salaam.   Wakati Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) ikijiandaa kuwapangia wanafunzi wa elimu ya juu mikopo yao mwezi huu, wanafunzi wa 26,688 walioomba mikopo hiyo kwa mwaka 2021/22 hawataweza kupata mikopo hiyo. Mkurugenzi wa Upangaji na Utoaji Mikopo HESLB, Dk Veronica Nyahende amesema majina ya wanafunzi waliopata mikopo wanaotarajia kujiunga na vyuo vikuu mwaka 2021/22 yatatangazwa mapema kabla ya vyuo kufunguliwa kuanzia Oktoba 25 mwaka huu. Hadi kufikia Septemba 30, HESLB ilikuwa imepokea maombi 88,688 na kati ya maombi hayo; 85,706 yalikuwa kamilifu na kutoa siku nne kuanzia Oktoba 4 hadi 7 kwa maombi yenye kasoro kufanyiwa marekebisho.  “Katika uhakiki wa maombi tumebaini waombaji 2,982  fomu zao zina kasoro. Tumetoa muda wa siku nne, na baada ya hatua hiyo kukamilika tutaan...

BODI YA MIKOPO YASITISHA MIKOPO KWA WANAFUNZI WA DIPLOMA

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu,  Abdul-Razaq Badru. Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) inapenda kuutaarifu umma kuwa imesitisha mpango wa kutoa mikopo kwa wanafunzi wanaosoma  stashahada  (Diploma) kuanzia mwaka wa masomo 2018/2019  kama ilivyotangaza awali. Itakumbukwa kuwa tarehe  10 Mei mwaka huu, HESLB ilitoa mwongozo unaosimamia utoaji mikopo kwa mwaka wa masomo  2018/2019 . Mwongozo huo, pamoja na mambo mengine, unaeleza kuwa HESLB itaanza kutoa mikopo kwa wanafunzi wa stashahada na kuwa mwongozo kuhusu utaratibu wa kuomba mikopo hiyo ya wanafunzi wa stashahada ungetolewa baadae. Hatua hii imechukuliwa ili kuhakikisha kuwa kiasi chote cha  TZS 427.5 bilioni zilizotengwa kwa ajili ya mikopo ya wanafunzi kwa mwaka  2018/2019 zinaelekezwa kwa wanafunzi wenye mikopo hivi sasa na waombaji wapya wahitaji ambao wana sifa za kujiunga na kozi za shahada tu ambao ndiyo walengwa wak...

Wasomi’ 122,000 sasa kugaiwa mikopo vyuoni

Image
JUMLA ya wanufaika 122,000 wanatarajia kupata fedha zitakazotolewa na Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) ambayo imefungua dirisha la maombi kwa njia ya mtandao. Kati ya wanafunzi hao, wapya ni 40,000 na wanaoendelea na masomo vyuoni ni zaidi ya wanufaika 80,000. Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB, Dk. Abdul-Razaq Badru, aliyasema hayo jijini Dar es Salaam wakati akizindua rasmi kuanza kupokea maombi ya mikopo jana. Dk. Badru alisema katika wanafunzi wapya, wanawake ni 14,000 sawa na asilimia 35 na wanaume ni 26,000 sawa na asilimia 65. Alisema kwa mwaka huu idadi ya wanufaika wa mikopo imeongezeka ikilinganishwa na mwaka jana ambako walikuwa 33,000. Alisema katika bajeti ya fedha za mikopo kwa mwaka 2018/19 jumla ya Sh. bilioni 427 zimetengwa ili kufanikisha suala hilo. Pia alisema mwaka huu wametanua wigo wa utoaji mikopo ambapo baadhi ya wanafunzi wanaosoma kozi za diploma watanufaika nayo. "Kuna fani chache zinauhitaji mkubwa ambazo ni ualimu wa masomo ya sayansi...

HESLB Yaanza Kupokea Maombi ya Mikopo 2018/2019

Image
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) leo imetangaza kuanza kupokea maombi ya mikopo ya elimu ya juu kwa muda wa miezi miwili na kusisitiza kuwa maombi yote yatapokelewa kwa njia ya mtandao. Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB Bw. Abdul-Razaq Badru (pichani) amesema leo jijini Dar es salaam  wakatik akifungua rasmi kuwa mtandao wa kuwasilisha maombi ya mkopo (www.olas.heslb.go.tz) utakuwa wazi kuanzia Mei 10, 2018 hadi Julai 15, 2018 ili kuwapa fursa wanafunzi wahitaji kuwasilisha maombi yao. “Mwaka jana tulitoa mwezi mmoja, mwaka huu tumetoa muda zaidi ili kuwawezesha kusoma mwongozo kwa makini na kuzingatia maelekezo tunayoyatoa,” amesema Bw. Badru katika mkutano na wanahabari ambapo pia alizungumzia mambo muhimu yaliyomo kwenye mwongozo unaojumuisha sifa na taratibu za utoaji mikopo kwa mwaka 2018/2019. Mwongozo huo unapatikana katika lugha za Kiswahili na Kiingereza kwenye tovuti ya Bodi (www.heslb.go.tz) Mambo muhimu yaliyomo kwenye Mwongozo Mkurugenzi Mten...

Taarifa Kwa Umma Kutoka Bodi ya Mikopo Elimu ya Juu Leo Jumamosi ya Mei 5, 2018

Image
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) inapenda kuwataarifu wananchi kuwa inatarajia kuanza kupokea maombi ya mikopo ya elimu ya juu kwa mwaka wa masomo  2018/2019  kuanzia wiki ya kwanza ya mwezi Mei, 2018 baada ya kukamilishwa kwa maboresho makubwa ya mfumo wa uombaji kwa njia ya mtandao. Maboresho ya mfumo wa maombi Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB Bw. Abdul-Razaq Badru amesema katika taarifa yake ya Aprili 17, 2018 kuwa maombi yote yatapokelewa kwa njia ya mtandao (www.olas.heslb.go.tz) ambao umefanyiwa maboresho na Kituo cha Kompyuta cha Chuo Kikuu cha Dar es salaam (UCC-UDSM). Aidha, Bw. Badru amesema dirisha hilo litafunguliwa sambamba na kutangazwa kwa mwongozo wa kina utakaotoa utaratibu wa kuwasilisha maombi, tarehe ya mwisho ya kuwasilisha maombi, sifa na vigezo vitakavyotumika katika kuchambua na kutoa mikopo kwa mwaka ujao wa masomo unaotarajiwa kuanza mwezi Oktoba, 2018. “Tunawasihi wale wote wanaotarajia kuomba mkopo wa elimu ya juu...

KIGEZO KIPYA UTOAJI WA MIKOPO ELIMU YA JUU 2018/2019

Image
WAKATI serikali ikitangaza kutoa mikopo kwa wanafunzi 123,285 wa elimu ya juu mwaka ujao wa masomo, Bunge limesema kigezo namba moja cha kuzingatiwa wakati wa utoaji wa mikopo hiyo kinapaswa kuwa ufaulu.    Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako, akiwasilisha bungeni mjini hapa jana makadirio ya wizara yake kwa mwaka 2018/19, alisema wanatarajia kutoa mikopo ya jumla ya Sh. bilioni 427 (sawa na fungu la mwaka huu) kwa wanafunzi wa mwaka wa kwanza 40,544 na wanafunzi wanaoendelea na masomo 82,741.  Prof. Ndalichako alisema mikopo na ruzuku kwa wanafunzi wa elimu ya juu itatolewa kwa wenye vigezo vya kupata mikopo na ruzuku hizo.  Hata hivyo, Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo, Hussein Bashe, akiwasilisha bungeni jana maoni ya kamati hiyo kuhusu bajeti ya wizara hiyo, alisema kamati yao inaona kigezo cha ufaulu kinapaswa kupewa kipaumbele cha kwanza katika utoaji wa mikopo hiyo.  “Kamati inashauri serikali kuanzia s...

Taarifa muhimu kwa wanafunzi wa vyuo kutoka Bodi ya Mikopo (HESLB)

Image
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) inawataarifu wanafunzi wanaonufaika na mikopo kuwa  wanatakiwa kuendelea kuingiza taarifa zao kwa njia ya mtandao kupitia http://olas.heslb.go.tz   hadi tarehe 31 Januari, 2018. Wanafunzi wanufaika wanapaswa kufanya yafuatayo: •    Tembelea mtandao wa http://olas.heslb.go.tz •  Fungua kiunganishi cha “Click here to start” kwenye maelezo ya mwanzo ya kukaribisha. •    Weka namba yako ya mtihani ya Kidato cha Nne na mwaka uliofanya mtihani huo, kwa mfano: S0129.0004.2020 •   Weka namba yako ya akaunti ya Benki kama ilivyowasilishwa HESLB au kama inavyoonekana kwenye “signing sheet” •    Ingiza neno jipya la siri na ulithibitishe. •   Baada ya kuthibitisha, ukurasa wa kuweka picha yako “passport size photo” utafunguka. •    Weka picha yako ya rangi katika ukubwa wa 120×150 •    Wanufaika wapya wa mikopo kwa mwaka wa masomo 201...

HESLB UPDATE: Bodi ya Mikopo yatangaza vita kwa Wanafunzi waliokiuka sheria

Image
  Dar es Salaam. Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetangaza kiama kwa wanufaika119,497 nchini kote ambao wamekiuka sheria iliyoanzisha bodi hiyo kwa kutoanza kurejesha mikopo yenye thamani ya Sh 285 bilioni waliokopeshwa tangu mwaka 1994/1995 na mikopo yao imeiva lakini hawajaanza kurejesha. Taarifa iliyotolewa leo Jumatano imeeleza kuwa itaanza kuwasaka wanufaika hao kuwanzia Jumatatu, Januari 8, 2018. Imeeleza kuwa inatarajia kuanza kufanya ukaguzi kwa waajiri mbalimbali nchini kote ili kubaini kama katika orodha za waajiriwa wao (payrolls) kuna wanufaika wa mikopo ambao hawajaanza kurejesha. Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB, Abdul-Razaq Badru amesema Jumatano kuwa msako huo utafanywa kwa miezi mitatu kuanzia wiki ijayo Jumatatu, Januari 8, 2018. Badru ametoa kauli hiyo wakati akitoa tathmini ya utekelezaji wa majukumu ya Bodi ya Mikopo kwa nusu ya mwaka wa fedha wa 2017/2018 uliomalizika Desemba 31, 2017. Akifafanua zaidi, Badru amesemaingawa kila mw...

HESLB UPDATE: MAELEZO YABODI YA MIKOPO KWA WADAIWA AMBAO BADO HAWAJAAJIRIWA

Image
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imewataka wanufaika wote wa mikopo ambao wanadaiwa na hawajaajiriwa bado, wafike katika ofisi za bodi hiyo zilizoko katika maeneo mbalimbali nchini ama kuwasiliana nao, ili wapewe maelekezo na utaratibu maalum wa namna ya kulipa mikopo yao. Akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za Bodi ya Mikopo zilizoko Mwenge, Jijini Dar es Salaam, mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa elimu ya Juu (HESLB), Abdul-Razaq Badru ametoa wito kwa wale ambao bado hawajaanza kurejesha mikopo yao, hata kama bado hawajapata ajira maalumu, wafike katika ofisi za bodi maeneo mbalimbali nchini ili kupewa maelekezo na utaratibu wa namna ya kuanza kurejesja mikopo hiyo. “Tunatoa wito kwa wale ambao kwa sababu fulani fulani walikuwa hawajaanza kulipa, walipe na wanakaribishwa kwenye ofisi zetu. Hata wale ambao hawako kwenye ajira maalum kuna utaratibu maalum tumewatengenezea. Wanaweza kuwasiliana na sisi katika mawasiliano yetu ...

Waziri Ndalichako atoa tamko kwa wanafunzi wa elimu ya juu

Image
  Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako amesema wizara yake imejipanga kikamilifu kuhakikisha kila mwanafunzi anayenufaika na mkopo wa elimu ya juu, anarejesha mkopo wake. Dk Ndalichako alitoa kauli hiyo juzi wakati akifanya mahojiano katika kipindi cha Tunatekeleza kinachorushwa na TBC 1. Alisema Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu nchini (HESLB) ilianza kutoa mikopo kwa wanafunzi mwaka wa fedha 1994/1995. Wakati Rais John Magufuli alipoingia madarakani mwaka 2015, fedha zilizokuwa zimerejeshwa ni Sh bilioni 75.9, lakini baada ya mwaka mmoja tangu awepo madarakani wamekusanyaSh bilioni 211. Ndalichako aliongeza kuwa katika mwaka wa fedha 2016/2017, bodi ilikusanya Sh bilioni 116, hivyo ukilinganisha na fedha zilizokusanywa katika mwaka mmoja wa fedha ni zaidi ya fedha zilizokuwa zimekusanywa katika miaka 10 tangu kuanzishwa kwa bodi ya mikopo. Aidha, alisema kabla ya serikali ya Rais Magufuli kuingia madarakani, HESLB walikuwa...

Wanafunzi 2,679 Wapata Mikopo Baada ya Kukata Rufaa

Image
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) leo (Disemba 5, 2017) imetangaza orodha yenye wanafunzi 2,679 ambao wamepata mikopo ya elimu ya juu yenye thamani ya TZS 9.6 bilioni kufuatia kukamilika kwa uchambuzi wa rufaa zilizowasilishwa. Kati ya wanafunzi hao 1,847 ni wa mwaka wa kwanza ambao mikopo yao ina thamani ya TZS 6.84 bilioni. Wengine 832 ni wale wanaoendelea na masomo lakini hawakuwa na mikopo katika miaka iliyopita. Wanafunzi hao wanaoendelea na masomo wamepata mikopo yenye thamani ya TZS 2.76 bilioni. Akizungumza na wanahabari leo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB Abdul-Razaq Badru amesema orodha ya wanafunzi hao na fedha zao zimetumwa katika vyuo walipo wanafunzi hao hivi sasa “Hatua hii inafanya jumla ya wanafunzi wa mwaka wa kwanza kuwa wamepangiwa mikopo yenye thamani ya zaidi ya TZS 108 bilioni kwa mwaka wa masomo 2017/2018 hadi sasa”, amesema Badru na kufafanua kuwa Serikali imetenga jumla ya TZS 427.54 bilioni kwa aji...

HSLB :HAYAHAPA MAJINA YA WANAFUNZI WENGINE 1,775 WA MWAKA WA KWANZA WAPATA MIKOPO

Image
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) leo imetangaza orodha ya Awamu ya Nne  yenye wanafunzi  1,775  wa Mwaka wa Kwanza waliofanikiwa kupata mikopo na hivyo kufanya jumla ya wanafunzi wa mwaka wa kwanza waliopangiwa mikopo hadi sasa kufikia  31,353.  Katika  Awamu ya Kwanza , wanafunzi  10,196  wa mwaka wa kwanza walipangiwa mikopo,  Awamu ya Pili (11,481)  na  Awamu ya Tatu (7,901) . Orodha hiyo ya Awamu ya Nne inapatikana <<< hapa >>>>> .  Aidha, orodha hii inapatikana katika tovuti ya Bodi ( www.heslb.go.tz ) na imeshatumwa kwa vyuo husika ili kuwawezesha wanafunzi kufanya usajili na kuendelea na masomo. Kiasi cha  shilingi 427.54 bilioni  zimetengwa kwa ajili ya mikopo ya wanafunzi kwa mwaka  2017/2018  na kati ya fedha hizo shilingi 108.8 bilioni  ni kwa ajili ya wanafunzi wa mwaka wa kwanza. Tayari Serikali imeshatoa  shilingi   147...

HESLB : Wanavyuo waja juu tena kuhusu mikopo, wasema wanachokitaka (+video)

Image
Ishu ya mkopo kwa Wanafunzi wa elimu ya juu Tanzania bado ipo kwenye headlines ambapo leo Jumamosi November 11 2017 Mtandao wa Wanafunzi Tanzania umezungumza kwa dakika zaidi ya 30 kutoa dukuduku lao. Sisi hatuna ukorofi wala mgogoro na Serikali, bodi wala Wizara na tunatambua jitihada zinazofanywa na Serikali kuitoa elimu yetu sehemu moja kuipeleka kwenye hatua nyingine lakini bado kuna changamoto ambazo tunatakiwa kuzisema. “Juzi Bungeni Waziri  Profesa Ndalichako baada ya kuulizwa kuhusu mikopo ya elimu ya juu tunamshukuru alijibu kuhusu udahili na usajili vyuoni lakini kuna swala ambalo mpaka anamaliza hakulitolea ufafanuzi wowote, mpaka anamaliza hakuna jibu lolote ambalo lilienda kwa Wanafunzi sisi tuliokosa mkopo hatma yetu ni nini?” “ Wanafunzi elfu 31 waliokosa mkopo hatma yao haisemwi, Mkurugenzi tu anaamka inasemekana hawa Wanafunzi wamekosa mikopo kwa kukosa vigezo………….. sio kweli, tatizo sio vigezo…. tatizo ni bajeti iliyotengwa ni ndogo “ ...

Takukuru yajitosa Bodi ya Mikopo

Image
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) inafanya uchunguzi dhidi ya vigogo na maofisa wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) wanaotuhumiwa kutafuna mabilioni ya shilingi kutokana na mbinu mbalimbali ikiwamo ya kujilipa posho ya ukarimu, imefahamika. Agosti 31, mwaka jana, wakati Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) ikipitia taarifa za fedha za bodi hiyo kwa mwaka 2014/15, ilibainika imetumia Sh. bilioni 15 kwa shughuli za uendeshaji huku kiasi kikubwa kikiwa posho. Kutokana na 'madudu' hayo, kamati hiyo iliitaka bodi kupunguza matumizi yasiyo ya lazima na kuhakikisha ulipaji wa posho unazingatia sheria na miongozo ya serikali. Kabla ya kupitiwa kwa taarifa za fedha za bodi hiyo na PAC Februari 16, mwaka jana, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako, alitangaza kusitisha mkataba wa ajira wa aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB, George Nyatega, pamoja na kuwasimamisha kazi wakur...

Bodi ya mikopo kufungua dirisha la kukata rufaa kwa wanafunzi waliokosa mikopo

Image
  Mkurugenzi wa Bodi ya mikopo ya elimu ya juu (HESLB), Abdul Razaq Badru amesema kuwa bodi hiyo itafungua dirisha la kukata rufaa kwa wanafunzi waliokosa mikopo ili waweze kupata haki yao. Ameyasema hayo leo jijini Dar es salaam wakati akifafanua vigezo na sifa za mwanafunzi kupata mkopo baada ya kuwepo kwa kasoro kadhaa kwa baadhi ya waombaji katika awamu ya kwanza ya wanafunzi wa mwaka wa kwanza. “Kwa wale wenye changamoto ndogo ndogo labda walikosea, tutatangaza dirisha la kukata rufaa mapema wiki ijayo na tutashughulikia watakaokamilisha vigezo watapata mkopo lakini wanatakiwa kuzingatia maelekezo tutakayoyatoa,” amesema Badru Hata hivyo, mkurugenzi amesema katika majina ya waombaji waliyoyapokea na kuthibitishwa na TCU kwamba yamepata vyuo na wakayapitia wakajiridhisha hayana kasoro kwenye uombaji, tayari wanafunzi 29,578 wameshapata mkopo na wameanza masomo ambapo kiasi cha shilingi bilioni 96 zimetumwa vyuoni

MAJIBU YABODI YAMIKOPO BAADA YAWANAFUNZI KUKUSANYIKA OFISINI MWAO

Image
Saa chache baada ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Vyuo Vikuu kukusanyika katika Ofisi za Bodi ya Mikopo wakidai kupewa mkopo kwa kudai kuwa wana na vigezo stahiki, Bodi ya mikopo imezungumzia suala hilo. Meneja Mawasiliano wa bodi hiyo Omega Ngoli, ameeleza kuwa mpaka sasa wamekwisha toa mikopo kwa wanafunzi 29, 500 katika awamu ya kwanza na pesa hizo zimeshapelekwa vyuoni na awamu nyingine ya majina ya wanufaikaji wa mikopo hiyo itatolewa hivi karibuni. Ameeleza pia kufikia Ijumaa November 10, 2017 Bodi hiyo ifungua dirisha la rufaa na hivyo wanafunzi ambao wanaona hawajatendewa haki watakata rufaa hiyo.

HESLB: WANAFUNZI ELIMU YAJUU AMBAO HAWAJAPANGIWA MIKOPO WAANDAMANA HADI BODI YAMIKOPO DAR

Image
Baadhi ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na vyuo vya elimu ya juu wamekwenda ofisi za Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) kushinikiza wapewe mikopo ili wafanye usajili kwa mwaka wa masomo 2017/18. Wanafunzi hao wamekusanyika leo Jumatatu Novemba 6,2017 katika ofisi za HESLB zilizoko Mwenge jijini Dar es Salaam, hivyo kusababisha askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) kufika eneo hilo. Baadhi ya wanafunzi waliangua vilio walipozungumzia tabu wanazopata kutokana na majina yao kutoonekana katika orodha ya wanaopata mikopo. Soma: HESLB yatoa orodha ya wanafunzi waliopangiwa mikopo Mwanafunzi, Nillan Liunga amesema hajui hatima yake kwa kuwa fedha alizonazo zinakaribia kwisha na hana ndugu jijini Dar es Salaam. "Maisha yenyewe naishi ya kuungaunga nimetoka Mbeya nimefikia gesti. Sina wazazi, nimesoma kwa shida licha ya kuwa na vigezo vyote vya kupewa mkopo mpaka sasa sijui nini hatima yangu," amesema Liunga. Wanafunzi hao wameta...