Posts

Showing posts with the label Chuo cha habari

Uandaaji wa taarifa kwaajili ya tovuti, application, na majukwaa ya mtandani

Image
Masshele Swahili Uchapishaji wa habari mtandaoni kupitia tovuti, app, na majukwaa ya mtandaoni ni miongoni mwa njia maarufu za kutolea habari za kuaminika. Mfano wa tovuti za habari ni Dw kiswahili, BBC Swahili, Cri, Millardayo , fullshangwe, masshele Swahili, mfano wa wa majukwaa ya mtandao yanayotoa habari ni Jamii forum wakati app za habari ni kama vile muungwana app, Millardayo nk Emanuel G,  mwandishi wa mtandao kwa muda mrefu anasema kwamba " Uandaaji wa taarifa kwaajili ya kuchapa katika tovuti au majukwaa ya habari unahitaji umakini mkubwa ili kuendana na matakwa ya msomaji, wakati huo huo ukizingatia uandishi wa kiweledi, ambapo mwandishi unapaswa kuandika kwa mtiririko unaoeleweka, kuzingatia taratibu za kiuandishi na kuhakikisha makosa ya kisarufi na kiuakifishaji ya naepukwa huku ukitumia lugha bora" Hivyo katika kutayarisha habari kwaajili ya tovuti huna budi kuzingatia mambo kadhaa Mambo ya kuzingatia Andaa maudhui bora, yenyewe kuzingatia u kweli,...

Kuandaa utangulizi wa Taarifa ya Redio

Image
Chuo-BBC Angalia habari yoyote kwenye gazeti – kuna kichwa cha habari, mwanzo na habari kamili. Utangulizi wako unatakiwa utimize mambo hayo mawili ya kwanza. Na Neil Churchman Katika chochote ukifanyacho, kamwe usiwachanganye au kuwachosha wasikilizaji. Kuna habari ambazo  zinavutia; zingine zinaweza kukanganya na zisizosisimua. Kazi yako ni kufanya watu waketi, wasikilize na watambue. Utangulizi ndio dirisha la duka letu ambalo tunatumia kumvutia msikilizaji kutamani bidhaa tuliyo nayo, ambayo ni habari. Utakachoweka katika utangulizi Angalia habari yoyote kwenye gazeti – kuna kichwa cha habari, mwanzo na habari kamili. Utangulizi wako unatakiwa utimize mambo hayo mawili ya kwanza. Kwa mfano: Kichwa cha habari: “Kudorora kwa uchumi kwaongeza wizi na ujambazi” Mwanzo wa taarifa: “Kuongezeka kwa visa vya uvunjaji wa nyumba, wizi na wizi wa kutumia visu kwazua wasiwasi kuwa kudorora kwa uchumi kumeanza kuongeza uhalifu” Hayo ndio maelezo unayotakiwa kuwa n...

Jinsi ya kutoa maelezo mbele ya Kamera

Image
Masshele Swahili Chuo-BBC Unaweza kutumia maelezo yako mwenyewe kwenye kamera kuonyesha ukubwa, umuhimu au wakati ambao umepita. Watazamaji wanataka kujua kuwa upo katika eneo ambako jambo linatokea Na wanataka kujua jinsi ilivyo kuwa hapo, kama anavyoeleza, mwandishi wa BBC wa maswala ya sayansi na mazingira David Shukman katika video hii: Njia bora ya kutimiza hilo ni maelezo yako mwenyewe kwenye kamera. Na si hilo tu. Unaweza kutumia maelezo yako mwenyewe kwenye kamera kuonyesha ukubwa, umuhimu au wakati ambao umepita. David anashauri hivi: Chagua jambo fulani muhimu katika taarifa yako ambalo unaweza kulieleza vyema zaidi kwenye kamera. Kwa mfano unaweza kujitumia wewe mwenyewe kuonyesha urefu, kimo au ukubwa wa kitu Fulani Hakikisha unaangalia kamera wakati wote. Kuangalia kando huenda kukawasilisha maana tofauti, kwa hivyo fanya hivyo iwapo tu unataka kuwasilisha ujumbe Fulani Vaa mikrofoni ya redio ili kuepuka kupaaza sauti sana, isipokuwa wakati unata...

UTOAJI WA HABARI KWA NJIA YA PODKASTI

Image
Masshele Swahili Chuo- BBC Kupodkasti ni kurikodi mazungumzo yako na kuyaweka katika tovuti. Mteja anaweza kuyasikiliza kwa kutumia komputa au simu ya kisasa. Badala ya kuandika unayotaka kueleza, unaweza piya kuyazungumza na kumfurahisha mteja ambaye sasa ataweza kukusikiliza hata akiwa njiani - kwa kutumia simu. Podkasti ni kama kushughulika na tovuti yako, lakini podkasti unatumia sauti. Kila nakala ni sawa na nakala ya tovuti, itahusu mada fulani. Kama unapotaka kuandika katika tovuti, tafuta pahala/mada fulani; yaani kitu ambacho watu wanataka kujifunza au kujua ambacho hakipo kwengineko. Kumbuka kuwa watu wanaosikiliza podkasti wanatafuta ujuzi/ufundi maalumu na watapenda kuwasikiliza wajuzi wa yale yanayozungumzwa. Podkasti inaweza kuwa ya mtu mmoja tu, yaani wewe watu wawili watu wengi Mtindo huu wa podkasti umesambaa sasa kila pahala. Kuna waandishi wa habari au wasanii ambao wanavutia na wanazungumzwa sana watu wanapokutana. Podkasta maarufu wana...

UONGOZAJI NA UTOAJI WA HABARI MITANDAO YA KIJAMII

Image
Masshele Swahili. Mitandao ya kijamii ni sehemu mojawapo ya kutolea habari za uhakika, ambapo huwaza kuenea kwa haraka zaidi. Karibu vituo vyote vya redio na televisheni vinazo kurasa maalumu za kutolea habari katika mitandao ya kijamii, kwa mfano katika mtandao wa kijamii wa facebook utakutana na kurasa kama vile, Azamtv,  EATV, ITV TANZANIA, MASHELE KISWAHILI, CITIZEN RADIO KBC TBC, na kadhalika. Kurasa hizi ni muhimu katika utoleaji wa habari, na mara nyingi huripoti matukio ya yanayotokea kwa muda huo (breaking news) Jinsi ya kuandaa habari katika mtandao  ya kijamii Kwanza nilazima ziwe za u kweli, unapaswa kuepuka utumizi wa maneno mengi( andika kwa ufupi na inayoeleweka)  picha mahususi ni muhimu ili kurahisisha uelewekaji wa tukio, tumia lugha ya staha, epuka kuwajibu vibaya wasomaji maana Mara nyingine huweza kukuudhi, futa comment za matusi kama muda unakuruhusu, Chonde chonde hariri taarifa kabla ya kuiweka kwa umma. Sikiliza wateja wako, ta...

JINSI YA KUWA MENEJA BORA WA STUDIO ENZI HII YA DIGITALI

Image
MASHELE SWAHILI,  CHUO -BBC Namna gani kazi ya meneja wa studio ilivyogeuka tangu kuja vielelezo vya redio na mtandao wa jamii. Hapa tunaangalia uweledi unaohitajiwa. Jukumu la meneja wa studio (SM – Studio Manager) ni uendeshaji wa kifundi wa vipindi vya redio mubashara au vya kurikodi. Na kuhakikisha  vinasikika kwa daraja bora,  na ikiwa vinaendeshwa kwa sauti na kamera, basi daraja bora ya video piya.  Ingawaje kuendesha deski la sauti  ndio bado ni sehemu kubwa ya meneja wa studio, hata hivyo jukumu hilo limepanuka. Na sasa limekuwa pamoja na kusahilisha utoaji matangazo kwenye majukwaa mengi na kidijitali.  Wasikilizaji wanavutiwa  zaidi na redio yenye picha, na kwa hivyo imebidi vipindi vya redio viwafuate waliko.  Mkabala huu mpya wa redio umebadili  majukumu ya timu nzima ya watoaji vipindi. Na hapa tutaangalia meneja wa studio analazimika kuwa na sifa gani.   Tumezungumza na mameneja wa BBC World Se...