Posts

Showing posts with the label Chaurembo

Jinsi Asali, Sukari, Maziwa, na Limao vinavyoweza kuleta mng`ao mpya katika sura yako

Image
Usafi wa  uso ni moja ya mambo muhimu sana kwa mwanamke au mwanaume yeyote  yule ambaye anapenda kuwa nadhifu na mwenye mvuto. Kumbuka “reception  ndio kila kitu “. Unapokutana na mtu sura yako na mwonekano wa sura yako ndio kitu cha kwanza kinachomtambulisha kwamba wewe ni nani  na upo kwenye hali gani. Kuna njia nyingi za kuufanya uso wako uvutie na kupendeza. Leo tutaongelea zaidi jinsi ya kusafisha uso kwa njia ya asili.  Mie hupenda kutumia njia ya asili sababu ni rahisi kupata vifaa na ni nafuu . Pia mtu anaweza kufanya kwa mazingira yoyote yale. Na matumizi ya vitu vya asili kwenye mwili husaidia kupunguza sumu mwilini kwani kutumia vipodozi vyenye kemikali husababisha miili yetu kujaaa sumu. Njia ya asili ya kusafisha na kupendezesha mwili ninayokueleza leo inahitaji vitu vikuu vinne : asali, sukari, maziwa, na limao. Haijalishi aina gani ya ngozi unayo , njia hii ya asili inaweza kutumika kwa aina yoyote ile ya ngozi iwe ngozi yenye mafuta au ngozi kavu...

Matumizi ya ndizi katika urembo

Image
    Mbali na kulika, ndizi zina manufaa mengine, hasa katika urembo wa ngozi. Ndizi zina virutubisho muhimu vinavyoboresha ngozi. Ndizi pia zina aina tatu za sukari zinazojulikana kama ‘sucrose’, ‘fructose’ na ‘glucose’. Hakikisha unanawa uso wako mara tatu kwa siku. Unapofanya hivyo unaondoa uchafu. Ndizi pia husaidia kuzuia chunusi. Hakikisha unanawa uso kwa sabuni ambayo inaendana na ngozi yako. Ikiwa ngozi yako ni ya mafuta, hakikisha unatumia sabuni ambayo itakuacha ukiwa mkavu na kama ngozi yako ina ukavu, jioshe na sabuni itakayokufanya uwe na unyevu. Kulainisha ngozi Changanya asali na ndizi moja iliyopondwa na upake kwenye uso na shingo. Nawa uso kwa maji ya fufutende baada ya muda wa nusu saa. Fanya hivi angalau mara moja kwa wiki. Kung'arisha uso Ndizi huwa na Vitamin C ambayo husaidia kuiweka ngozi kuonekana iking'aa. Kwenye ndizi iliyopondwa, ongeza vijiko viwili vidogo vya juisi ya limau na upake kwa uso na shingo. Osha kwa maji ya fufutende baada ya dakika 20. N...

Mambo 8 mwanamke anapaswa kufanya kabla ya kufunga ndoa

Image
    Kufanya mambo haya kutakupatia maarifa na kukufanya uwe na uwezo wa kufanya uamuzi bora zaidi maishani. Ni jukumu lako kama binti asiye katika uhusiano kufanya mambo mazuri zaidi maishani kabla ya kufunga ndoa. Kufanya vitu hivi kutakusaidia kuwa mwerevu zaidi na kujua mambo unayo na usiyo paswa kufanya. Soma makala yetu ya mambo ambayo mwanamke anapaswa kufanya kabla ya kuingia katika ndoa! 1. Jifunze jinsi ya kupika Tofauti na imani za watu kuwa kila mwanamke anapaswa kujua kupika ili ampikie bwana yake, kujifunza kupika kwa mwanamke kuna umuhimu tofauti. Ukiwa peke yako bila mchumba, una wakati mwingi, kwa hivyo katika wakati huu, utaweza kujipikia vyakula vinavyo kufurahisha zaidi. Pia, unapo pata wageni utaweza kuwa burudisha na ustadi wako wa mapishi. 2. Fanya vitu vinavyo kupendeza katika wakati wako wa ziada Unapokuwa peke yako, una wakati mwingi wa mapumziko, ni vyema kufahamu vitu unavyo vipendelea, katika wakati huu, utaweza kuvifanya badala ya kubaki kwenye nyu...

Zijue mascara na namna ya kupaka

Image
  Unapochagua mascara kuna mambo muhimu ya kuzingatia kulingana na lengo lako unalotaka kutimiza. Unatakiwa kujua unataka kope zionekane ndefu( lengthenning), zionekane zimejaa/nene (thickenning), zisishikane na je ukinawa na maji mascara itoke au laa (water proof). Wengi tunanunua tu mascara kwa wamachinga nk bila kujua itafanya nini mradi ukipaka kope zinaonekana. Ya Kurefusha kope( lengthenning) Hii kibrashi chake kina vinyweleo vingi ili ifikishe mascara vizuri kwenye kope hasa katika ncha za kope, Urefu wa kope hutengenezwa na namna mascara inavofika vizuri kwenye ncha (tips) za kope. Unapopaka mascara katika kope hakikisha ncha za kope umezifikia vizuri. Unaweza usibandike kope za bandia lakini mascara ikakubeba ukaonekana na kope ndefu. Ya kujaza kope (thickener) Hii huwa na kibrashi ambacho ni rahisi kufikisha mascara katika shina la kope zako kuzipa ujazo. Na pia unaweza kuzifanya zijae kwa kuziviringisha katika brashi yako. Hakikisha imeandikwa Volume/ thickener: mara nyi...

Njia bora na asili ya kukuza nywele zako pasipo na gharama kubwa

Image
  Kwa wale ambao tuna nywele asilia a.k.a natural hair, tayari tunafahamu changamoto kadhaa tunazokumbana nazo. Kwa wale mnaofikiria kuanza kuwa na nywele asilia, karibuni sana tuendelee kujuzana namna ya kutunza nywele zetu kama tulivyopewa na Mungu. Katika mada ya leo,nitakwenda kuzungumzia vitu vya kuzingatia ili kuikuza nywele yako asilia kwa haraka zaidi. Je,unazifahamu nywele zako vizuri? Una nywele za aina gani? Zina tabia gani? Zinataka nini? 1. Kuzikubali kama zilivyo na kuzipenda. Utasikia ..hiki kipilipili changu ni steelwire ya kimataifa, ..hakitikisiki hata upepo wa dunia yote ungevumia pande hizi. Mwingine oh.. nywele zangu kama miti ya mibuyu kichwani…hazishikiki.Tatizo ni kwamba hamjafahamiana vizuri yani wewe na nywele zako.  Hata mimi niligombana nazo sana huko nyuma kabla ya kuzielewa vizuri hivyo jambo la msingi la kuzingatia katika nywele zako ni kujenga mahusiano mazuri tu na nywele zako ,zielewe, ukifikia hapo utaanza kuzipatia hata hazitaku...

MAUMIVU WAKATI WA HEDHI (DYSMENORRHEA)

Image
Menstrual cramps ni maumivu ya kukakamaa kwa misuli ya eneo la chini ya tumbo. Wanawake wengi hupata maumivu haya kabla kidogo au wakati wakiwa kwenye siku zao. Kwa baadhi ya wanawake, maumivu haya huwa ni ya kuwakosesha raha. Kwa wengine, huwa ni makubwa kiasi cha kuwafanya washindwe kuendelea na shughuli zao za kila siku kwa siku kadahaa kila mwezi. Primary dysmenorrhea  ni maumivu ya wakati wa hedhi ambayo hujirudiarudia kila mwezi na ambayo hayatokani na magonjwa mengine ya mwili. Maumivu haya ya wakati wa hedhi ambayo hayana sababu za kueleweka, hupungua kadri mwanamke anavyozidi kuwa na umri mkubwa na mara nyingi hupungua sana mara baada ya kuzaa. Secondary dysmenorrhea  ni maumivu ya wakati wa siku za mwanamke ambayo yanatokana na dosari katika viungo vya uzazi vya mwanamke, kama endometriosis, adenomysis, uterine fibroids au maambukizi ya wadudu. . Maumivu ya kukakamaa kwa misuli sehemu ya chini ya tumbo yanayoweza kuwa makali . Kichwa kizito na maumivu...

MAAJABU YA ASALI KATIKA UREMBO WAKO

Image
Utashangaa sana kwamba asali ndiyo hasa kitu kitamu ambacho kwa miaka mingi watu wamekuwa wakikifananisha na raha. Hii inatokana na ukweli kwamba asali inachukua nafasi ya pekee katika dunia ya mwanadamu. Nafasi hii ya pekee imo katika mambo mengi mpaka mwenye tiba kwa kaaida asali dawa ya kukabiliana na vitu vingi pamoja na vimelea. Pamoja na kuwa na antiseptic pia ina moisturizer na pia ina antioxidants na inasaidia kukabiliana na uzee. Uwepo wa kiwango kikubwa cha sukari katika asali kunaipatia uwezo wa dawa na ndiyo maana kwa miaka maelfu imesaidia watu kutibu vidonda. Mtaalam mmoja wa ngozi mwenye makazi yake mjini New York City ambaye pia ni daktari, Amy Wechsler anasema hali ya kunyunyurika iliyonayo asali na inayonasa inafanya kuwa kinga imara katika kidonda ambacho kinahitaji kisiingiliwe n vimelea na kutoa mazingira ya kuponya, hivyo asali ni bomba kwa tiba.   Pamoja na tiba asali ni moisturize babu kubwa kwa ajili ya sura na mwili pia. Asali ni dawa y...

Jinsi ya kuifanya ngozi yako kuwa nzuri kwakutumia vitu vya asili

Image
Uzuri wa ngozi sio rangi tu bali ni muonekano wa ngozi yenyewe kwamba ina afya na mng'ao unaoashiria afya njema. Leo tushirikishane jinsi ya kufanya facial treatment kwa kutumia vitu vya jikoni kama kiini cha yai,machicha ya nazi,tango na limao.Treatment hii inaweza kufanyika Mara moja kwa wiki au kila baada ya wiki mbili, unaweza kufanya hata mara moja kwa mwezi ukipata nafasi kama unakuwa busy sana lkn matokeo mazuri utayashuhudia. JINSI YA KUFANYA Andaa maji masafi yenye joto kiasi unachomudu ktk ngozi yako, osha uso wako kwa hayo maji safi . Kama una ngozi kavu au ya kati chukua kipande cha tango kidogo na upake yale maji yake usoni, kwa wenye ngozi ya mafuta unaweza kutumia kipande cha limao kwa kupaka maji yake. Chukua pamba au kitambaa laini na futa maji ya matunda usoni kwa mtindo wa kusafisha taratibu usoni. Chukua machicha ya nazi na Anza kuusugua uso  na shingoni taratibu Mpaka uridhike uso wote umepitiwa na machicha yako hasa unapoona unang'aa kwa mafuta ...

ASALI KWA UREMBO WA SURA NA NYWELE

Image
Tumia Asali katika Urembo wa Nywele na Ngozi yako Asali hutumika kulainisha Ngozi Asali ina asili ya kuvuta unyevu kutoka kwenye hewa na kuipa ngozi uwezo wa kuhifadhi unyevu hivyo ni faida kwa mtu mwenye ngozi kavu. Jinsi ya kuandaa Chukua asali mbichi kijiko kimoja cha chai kisha paka usoni, kaa nayo kwa dakika 15 hadi 20 kisha safisha uso wako. Asali katika kusafisha ngozi, kutibu na kuzuia chunusi Kutokana na uwezo wa asali katika kuua bacteria na kuvuta uchafu katika matundu ya ngozi asali itakusaidia kutatua tatizo la chunusi. Jinsi ya Kuandaa Chukua asali mbichi Kijiko kimoja cha chakula changanya na mafuta ya nazi vijiko viwili changanya mchanganyiko uwe mlaini kisha paka usoni huku ukisugua taratibu kwa kufanya kama viduara huku ukiepuka kufikisha machoni. ukimaliza kusugua uso na mchanganyiko wako osha uso wako. Jinsi ya kuandaa kama kisafisha ngozi, exfoliator Changanya kijiko kimoja asali na kijiko kimoja baking soda. tumia mchanganyiko huu kusugua ngozi yako. ...