Posts

Showing posts with the label UTAFITI

MAAJABU YA PENSELI USIYO YAJUA KUHUSU KALAMU HII YA RISASI

Image
Naomba Penseli NA MWANDISHI WETU NCHINI UINGEREZA HAIGHARIMU pesa nyingi, inaanza kufanya kazi mara moja, na haina uzito mkubwa. Inaweza kuwekwa mfukoni vizuri. Haitumii umeme, haivuji, na alama zake zinaweza kufutwa. Watoto huitumia wanapojifunza kuandika, wachoraji huitumia kuchora picha za kupendeza, na wengi wetu huitumia kuandika habari fupi-fupi. Naam, kifaa hicho chenye bei rahisi na kinachotumiwa sana ulimwenguni ni penseli. Penseli ilivumbuliwa bila kutarajiwa katika maeneo ya vijijini huko Uingereza. Acheni tuwasimulie jinsi ilivyogunduliwa na kutengenezwa. Risasi Nyeusi Katika karne ya 16, mabonge ya kitu fulani cheusi yaligunduliwa chini ya kilima cha Borrowdale, kwenye bonde la Wilaya ya Lake kaskazini mwa Uingereza. Ingawa madini hayo yalifanana na makaa ya mawe, hayangeweza kuungua; nayo yaliacha alama nyeusi inayong’aa iliyoweza kufutwa. Kwa kuwa kitu hicho kingebaki kwenye vidole mtu alipokigusa, watu walifunika mabonge ya kitu hicho kwa ngozi y...

Hivi ni Vyakula Vinavyoongeza Nguvu na Akili katika Ubongo wa Mwanadamu

Image
Kuna wakati unaona wazi ubongo wako umechoka au ufanisi wake umepungua tofauti na zamani. Au sababu tu ya kazi na misongamano mingi unajikuta kichwa kimechoka kufanya kazi. Hakuna dawa yoyote hospitalini inayoweza kukurudishia nguvu zako za ubongo. Dawa nyingi za kizungu za kuongeza nguvu za ubongo zina madhara makubwa baadaye katika mwili. Kila mmoja wetu anapatwa na tatizo hili la kuhisi kushuka kwa nguvu za ubongo wake. Takwimu zinaonyesha baada ya miaka 85 uwezekano wako wa kupata ugonjwa wa kupoteza kumbukumbu huongezeka kwa asilimia 50. Hivyo ni wazi tunahitaji kujiwekea mazoea na tabia ya kula vyakula na kuishi namna ambazo zitakuwa zikiendelea kuupa nguvu ubongo kila siku. Hapa nimekuandalia orodha ya haraka haraka ya vyakula hivyo, pia uhakikishe unapata usingizi wa kutosha kila siku: Mafuta ya zeituni Mafuta ya nazi. Samaki. Binzari Mayai Korosho Mazoezi ya viungo Broccoli Parachichi Mvinyo mwekundu SpinachiLozi (Almonds) Mbegu za mabogaKitunguu s...

UTAFITI: Maziwa ya Ng’ombe husaidia watoto kuwa warefu

Image
Utafiti mpya uliofanywa na madaktari bingwa wa Hospitali ya  St. Michael’s Toronto,  Canada  umegundua kuwa watoto wanaokunywa maziwa ya ng’ombe huwa warefu ukilinganisha na watoto wanaokunywa maziwa ya wanyama wengine au wasiokunywa kabisa. Utafiti uliohusisha zaidi ya watoto 5,034 wenye umri wa miaka mitatu hadi sita ulibaini zaidi ya 50% ya watoto waliokunywa maziwa ya mbuzi na wanyama wengine walionekana wafupi ukilinganisha na watoto waliokunywa maziwa ya ng’ombe. Kwa mujibu wa utafiti huo, maziwa ya ng’ombe yanasaidia ukuaji wa watoto hasa wanaoanza kutambaa kutokana na viritubisho vya  calcium,  vitamin D  na protein  nyingi vinavyopatikana ukilinganisha na maziwa ya wanyama wengine.  KARIBU TENA MASSHELE BLOG BLOG YAKO

Siri ya kufaulu mtihani: Mmea wa Rosemary husaidia kukumbuka mambo 4 Mei 2017

Image
Hivi ni viunganisho vya nje na vitafungua katika dirisha mpya Mshirikishe mwenzako Haki miliki ya picha GETTY IMAGES Watafiti nchini Uingereza wamesema huenda harufu ya mmea wa rosemary ikawa na uwezo wa kusaidia mtu kukumbuka mambo. Mmea huyo, ambao huwa na maua ya rangi ya nyeupe, waridi, zambarau au samawati, sana hutumiwa kama kiungo kwenye chakula, vinywaji au mchuzi. Utafiti ulibaini kwamba wanafunzi waliokuwa kwenye chumba kilichopulizwa harufu ya rosemary, iliyokuwa kwenye mafuta, walikuwa na uwezo wa kukumbuka mambo kwa asilimia 5 hadi 7 zaidi kuliko wanafunzi ambao hawanusa harufu hiyo. Mark Moss kutoka Chuo Kikuu cha Northumbria anasema matokeo ya kutumia mmea huyo yalikuwa sawa pia kwa watu wazima.   . Dkt Moss alisema utafiti huo unaonekana kutilia mkazo itikadi kuhusu uwezo wa mmea huo. Amesema kwa miaka mingi, mmea huyo umehusishwa na uwezo wa kukumbuka mambo. : TANGAZO JE  WEWE NI MTANZANIA NA UNGEPENDA KUNUFAIKA KUPITIA E...