Posts

Showing posts with the label fonolojia

kanuni za kifonolojia

  Mpaka sasa mjadala umehusu vipashio vya kifonolojia, hususa fonimu na alofoni. Lakini kila mjua-lugha anatambua kuwa watu hawazungumzi kwa kutumia fonimu moja moja. Hata kama tukiweza kuorodhesha fonimu zote za lugha fulani pamoja na alofoni zao, bado tutakuwa hatujajua mfumo wa fonolojia wa lugha hiyo ulivyo. Katika kutumia fbnimu za lugha ili kuunda maneno, na kufanikisha mawasiliano, kuna kanuni za msingi ambazo kila lugha inazifuata. Kanuni ya jumla sana, na ambayo tumekwishaigusia katika kurasa zilizotangulia, ni ile ya  mfuatano  unaoruhusiwa wa fbnimu za lugha fulani; na katika kanuni hii, lugha hutofautiana sana. Katika lugha ya Kiingereza, kwa mfano, vipasuo sighuna /p, t, k/ vinaweza kufuata kikwamizi /s/ lakini vipasuo ghuna /b, d, g/ haviwezi. Hivyo kuna maneno: 28 {spar, star, scar}, lakini hakuna 29 *{sbar, sdar, sgar} Wazungumzaji wa Kiingereza wanajua wazi kuwa maneno ya (29) hayawezi kuwa maneno ya lugha yao kwa sababu hayaruhusiwi na  kanuni za ki...

SIFA MAJUMUI ZA LUGHA KATIKA FONOLOJIA

  UTANGULIZI. Niukweli usiopingika kuwa pamoja na kutofautiana kwa baadhi ya sifa mbalimbali za  lugha zipo sifa majumui ambazo huweza kupatikana katika lugha zaidi ya moja Sifa hizo za lugha huweza kugawanywa katika makundi matatu ambayo ni ,  Sifa majumui halisi za lugha Sifa majumui pana za lugha Sifa majumui tabirifu za lugha. Kwa kuzichanganua zifa hizo nikama ifuatavyo,      SIFA MAJUMUI HALISI ZA LUGHA. Hizi nizile sifa ambazo ni za kawaida na  hupatikana katika lugha zote halisi za binadamu  kwamfano katika lugha zote za binadamu huwa na irabu [a]  katika orodha ya sauti zake , katika utaratibu wa lugha zote asilia za binadamu huwa na utaratibu wa irabu na konsonanti,  ingawa kwa habari ya idadi ya irabu na konsonanti huweza kutofautiana baina ya lugha moja na nyingine. Vilevile katika lugha zote za asilia  irabu na konsonati hupangiliwa katika silabi. SIFA MAJUMUI ZA LUGHA PANA. Hizi ni zile sifa ambazo hupatikana katika lu...

sifa majumui za lugha ; taja sifa majumui za lugha

SIFA MAJUMUI ZA LUGHA KATIKA FONOLOJIA Katika sehemu iliyopita tumesema kwamba lengo kuu la fonolojia ni kujaribu kuziweka wazi baadhi ya sifa majumui   zinazojitokeza katika lugha asilia. Maelezo hayo yamejengeka kwenye mantiki kwamba pamoja na ukweli kuwa kunatofauti za wazi   zinazojitokeza   klatika fonolojia ya mifumo mbalimbali ya lugha asilia, bado kuna tofauti fulani ambazo zinaelezwa kuchangiwa lugha zote na lugha zote asilia ndizo zijulikanazo katika taaluma ya fonolojia kama SIFA MAJUMUI ZA LUGHA.   -           KUNA AINA KUU TATU ZA SIFA MAJUMUI ZA LUGHA. Ambazo ni sifa majumui halisi za lugha, sifa majumui pana za lugha, na sifa majumui tabirifu za lugha.   SIFA MAJUMUI   HALISI ZA   LUGHA-   Ni zile sifa za kiisimu ambazo ni zakawaida katika lugha zopte za kibinadamu . mfano katika lugha zote kuna irabu a’ na nikwaidsa katika lugha zote kuwa na utaratibu wa konsonanti na irabu i...

tofauti za kifonolojia

   Mifumo Tofauti ya Fonolojia Tumesisitiza tokea mwanzo kuwa kila lugha inachagua baadhi tu ya sauti zinazoweza kutolewa na viungo-sauti vya mwanadamu. Na hata ikitokea kuwa kiuchunguzi lugha mbili zinatumia sauti zinazofanana, (yaani zenye sifa sawa za kifonetiki), zinaweza kutofautiana katika jinsi sauti hizo zinavyotumika katika lugha hizo. Kwa biyo ni kawaida kutarajia kuwa lugha zitakuwa na mifumo tofauti ya fonolojia. Hapa, isieleweke kuwa tunasisitiza mno tofauti kuliko mfanano. Ikiwa msisitizo unajitokeza, ni kwa tahadhari tu, kwa sababu hata wachunguzi (wanaisimu) wanaathiriwa na mazoea. Kwa mfano, ikiwa mchunguzi amezoea tofauti fulani katika sauti za lugha yake, ni rahisi kufikia hitimisbo la haraka akikuta sauti zinazofanana na za lugha yake katika lugha anayocbunguza, kwa sababu atakuwa anahusisha sauti za lugha hiyo na zile za lugha yake mwenyewe. Anaweza kuona mfanano mahali ambapo pana tofauti, au kuweka tofauti mahali ambapo hapahusiki. Na hili sijambo la kus...