Posts

Showing posts with the label MAGAZETI

MAANA YA UREJESHAJI PDF

TUKI (1990) wanasema urejeshaji ni tendo la kuweka kiwakilishi ambacho huweza kutumiwa kupatanisha kishazi kinachojirejea na kukivumisha kikundi nomino hicho. Yaani kishazi rejeshi kinafanya kazi ya kuvumisha Nomino katika kikundi nomino hicho. Tungo rejeshi ni tungo tegemezi ambayo hutegemezwa kwenye kundi nomino. Wengine wanasema ni uhusianishaji wa maneno kisarufi ambapo tungo rejeshi hurejelea kwenye neno kuu (kisabiki) la kifungu chote. Kuna uhusisano wa moja kwa moja kati ya kile kinachoelezwa katika tungo rejeshi na kile kisabiki kinachorejelewa. Ili kuwa na kishazi bebwa katika sentensi moja inayotokana na sentensi mbili, kishazi kimoja hakina budi kupachikwa ndani ya kishazi kingine yaani kubebwa na kishazi kingine. Hii ni sawa na kusema kuwa kishazi kimoja kinashushwa hadhi na kukipachika ndani ya sentensi nyingine baada ya KN cha sentensi husika. Kishazi rejeshi ni sentensi iliyoshushwa hadhi na kufanya kazi ya KN (ndani ya KN). Mwalimu anaasoma kitabu Kitabu ni kizu...

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumamosi ya January 12

Image

VIDONDA VYA TUMBO,

Image
Vidonda vya tumbo (Peptic Ulcers) ni ugonjwa unaompata mtu ambapo kunatokea vijitundu au michubuko katika kuta za ndani za viungo vya mfumo wa uyeyushaji chakula. Michubuko hiyo huweza kutokea katika eneo la mfuko wa tumbo, katika duodenum au katika eneo la koo. Inakadiriwa kuwa asilimia 5 hadi 10 ya watu hupatwa na ugonjwa huu angalau mara moja katika maisha yao. Huu ni ugonjwa ambao unaweza kumrudia mtu baada ya kupona endapo chanzo chake hakikudhibitiwa. Kama ugonjwa huu utamrudia mgonjwa , mtu huyu atakuwa amejiweka kwenye hatari kubwa ya kupata madhara makubwa zaidi kama kutokwa na damu au kutokea tundu kubwa katika kuta za mfuko wa tumbo.   Chanzo Cha Vidonda Vya Tumbo Bacteria:  Chanzo kikubwa cha ugonjwa wa vidonda vya tumbo ni bacteria waitwao Helicobacter pylori (H. pylori). Bacteria hawa huenezwa kwa kula chakula na kunywa maji. Katika mwili wa binadamu bacteria hawa wapo katika mate na katika ute unatanda juu ya ...

Azam waapa kuitungua Tanzania Prisons

Image
Kocha msaidizi wa Timu ya Azam Idd Seleman Cheche amesema kuwa wapo tayari kuwavaa 'wajelajela' Tanzania Prisons watakapokutana nao katika mchezo wa ligi utakaofanyika Jumapili ya tarehe 21 Januari, 2018 kwenye uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya. Akizungumza na mtandao wa Azam Fc Cheche amesema kuwa wamerekebisha makosa madogo waliyoyafanya dhidi ya Timu ya Majimaji na kuwa wanatarajia ushindi.  "Plan yetu Jumapili ni kuhakikisha tunapambana kadri ya uwezo wetu ili kupata matokeo, tumeangalia kitu gani kilitukwanza tukijumuisha na uchovu na tutaangalia jinsi ya kurekebisha ili tusirudie makosa", amesema Cheche. Cheche amewataja Tanzania Prisons kuwa timu nzuri ambayo watahitaji umakini mkubwa ili kuwashinda. Timu nzuri "Tanzania Prisons ni wazuri wanapambana lakini tutatumia udhaifu wao ili tuwaangamize na tuhakikishe tunapata alamu tatu muhimu", ameongeza Cheche. Mabingwa hao wa Kombe la Mapinduzi mwaka 2018, tayari wapo Jijini Mbeya ambapo wanaen...

Kikosi cha Simba Vs Ndanda, Djuma afanya mabadiliko makubwa

Image
Kocha Mrundi Masoud Djuma amefanya mabadiliko makubwa katika kikosi cha Simba SC ambacho kitacheza na Ndanda FC katika muendelezo wa ligi kuu soka Tanzania Bara. Katika mabadiliko hayo Kocha Djuma amewaanzisha kiungo Mohamed Ibrahim 'MO' pamoja na kinda Paul Bukaba ambaye atacheza katika nafasi ya ulinzi. Aidha Pacha wawili Jonas Mkude pamoja na James Kotei kwa pamoja wameanza huku safu ya ushambuliaji ikipambwa na mkongwe John Bocco pamoja na Juma Luizio. Wanaoanza:  Aishi Manula, Paul Bukaba, Erasto Nyoni, James Kotei, Juuko Murshid, Jonas Mkude , Shiza Kichuya, Mzamiru Yassin, John Bocco, Juma Luizio na Mohamed Ibrahim Akiba : Emanuel Mseja, Hussein Mohamed, Jamal Mwambeleko, Yusuph Mlipili, Said Ndemla, Nicholas Gyan na Moses Kitandu. Mchezo huo unatarajiwa kufanyika katika Dimba la Nangwanda Sijaona mkoani Mtwara kuanzia majira ya saa 10:00 jioni.

Tanzania magazine's on December 29/2017

Image

Today magazine's from Tanzania on December 28/2017

Image