Posts

Showing posts with the label TP-Mwalimu

ANDALIO LA SOMO

Image
Andalio la somo ni utaratibu au mpangilio wa hatua za kufundishia unaotayarishwa na mwalimu kwa kipindi husika na kwa darasa fulani. Siku zote Andalio la Somo ndio dira ya kumuongoza mwalimu wakati wa kufundisha kwake. UMUHIMU WA ANDALIO LA SOMO          Huonesha wazi malemgo ambayo mwalimu anatarajia yafikiwe na mwanafunzi wake katika kipindi          Ni muongozo wa kufuata hatua kwa hatua mwalimu anapofundisha darasani          Humuonesha mwalimu sehemu za somo za kuuliza maswali, kutumia zana au kuhusisha wanafunzi katika vitendo. SIFA ZA MALENGO MAHSUSI YA SOMO A)    Kipindi kimoja lazima kisiwe na malengo mengi          Kila lengo kuu liandikwe kwa mtindo unaoonesha jambo watakaloweza kufanya wanafunzi na linaweza kuthibitishwa au kubainika.     ...

UMUHIMU WA MWALIMU KUFAHAMU SHERIA

Image
Kufanya Kilicho Sahihi Sheria ni nini? Sheria ni masharti yanayowekwa katika nchi ili kutoa mwongozo wa jinsi ya kufanya mambo kwa usahihi. Sheria lazima zifuatwe na watu wote, na anayevunja sheria huadhibiwa. Kanuni ni nini? Kanuni ni maagizo kwa ajili ya asasi kubwa ya umma, zinazoongoza kufanya mambo yaliyo sahihi. Kanuni hizi mara nyingi zinafafanua sheria za nchi. Taratibu ni nini? Taratibu ni maelekezo yanayotolewa kwa idara zote za serikali ili kuelekeza kufanya mambo yaliyo sahihi. 1. Mwalimu ni nani katika mazingira yetu ya Tanzania? Neno  “mwalimu”  limetafsiriwa kwenye ‘Kamusi ya Kiswahili Sanifu’ TUKI (1981) kwenye ukurasa wa 201 kuwa ni “mtu afundishaye elimu au maarifa Fulani, au mtu anayeonesha wengine”. Katika Sheria ya Elimu, (sura ya 353 R.E.2002), neon ‘mwalimu’ limepewa maana kwenye fungu la 2 (1) kuwa ni “mtu yeyote aliyesajiliwa kama mwalimu chini ya sheria hii.” Na fungu la (46) la sheria hii, linaonesha kuwa baada ya ...

VIFAA VYA MTAALA

Image
Mtaala una vifaa vyake maalumu ambavyo vinatakiwa vitumike kwa usahihi ili kutekeleza mtaala kwa ufaninsi. Vifaa hivyo ni; Muhtasari Vitabu vya kiada Kiongozi cha mwalimu Kitabu cha mwalimu  na Rejea. MATAYARISHO YA UFUNDISHAJI Mtayarisho ya ufundishaji ni ile hali ya mwalimu kuandaa zana na vifaa muhimu kwa ajili ya kufundishia na kujifunzia UMUHIMU WA MATAYARISHO YA UFUNDISHAJI Kazi ya kufundisha ni kazi ya kitaalamu hivyo inahitaji maandalizi wakati wote. Hivyo basi mwalimu anapaswa kufanya maandalizi ya kutosha kabla ya kuingia darasani kufundisha na kwa mantiki hiyo mwalimu analazimika kujiandaa ili kuepuka matatizo yafuatayo wakati wa kufundisha na kujifunza. Kukosa mtiririko unaofaa wa ufundisahaji Kufundisha kwa kubahatisha au kubabaisha Kuchosha wanafunzi katika kujifunza Uwezekano wa kupotosha maudhui Kushindwa kutunza muda Kushindwa kukidhi matarajio ya somo na ya wanafunzi Kujiamini au kutojiamini kusiko na misingi dhahiri ...

MBINU ZA KUFUNDISHIA

 Uchaguzi bora wa Mbinu na Njia za Kufundishia Ni Jumla ya vitendo vya maandalizi ya somo linalokusudiwa, matumizi ya vifaa vya kufundishia na kujifunzia, vitendo vya mwanafunzi katika harakati za kujifunza na jukumu la Mwalimu kinadharia na vitendo katika ufundishaji na ujifunzaji. Maana ya Mbinu za Kufundishia Ni mwongozo mbalimbali atumiao Mwalimu darasani wakati wa kuwasilisha somo alilioliandaa kwa wanafunzi wake. Mwalimu anapashwa kuaamua kwa kuchagua kwa makini Njia na Mbinu bora za kufundishia ili wanafunzi wake waweze kujifunza kwa ufanisi. Misingi ya kuchagua njia na mbinu ni kuzingatia mambo yafuatayo:- Maudhui ya somo. Mwalimu lazima azingatie hali ya somo, maarifa na stadi anayopaswa kujenga mwanafunzi. Hali  na umri wa wanafunzi wako. Mwalimu lazima azingatie umri wa wanafunzi, kukomaa au kutokomaa kwa akili za wanafunzi na mazingira yao ya nyumbani na ya shuleni. Malengo ya somo. Bainisha mambo ambayo wanafunzi wak...

Zana za Kujifunzia na Kufundishia

Image
Mwalimu yeyote anapaswa kujifunza utengenezaji na matumizi ya zana, kwani ni nyenzo muhimu sana katika kazi ya kufundisha na kujifunza. Nini maana ya Zana za Kujifunzia na Kufundishia? “Zana ni kitu chochote kinachopangwa na kutumika katika kuinua kiwango cha elimu”. Je, mwalimu anaweza kuwa Zana? NDIYO ,  Mwalimu pamoja na vifaa vingine anaweza kuwa zana kwa sababu vifaa vya kufundishia pamoja na mwalimu vimepangwa na kutayarishwa kwa madhumuni ya kuboresha tendo la kujifunza na kufundisha. Je, unadhani Mwanafunzi anaweza kujifunza pasi kuwa na Mwalimu? NDIYO , Mwanafunzi anaweza kujifunza kwa kutumia zana pekee bila ya mwalimu (Resource-based learning) lakini mwalimu atashindwa kufundisha bila ya mwanafunzi ingawa anazo zana za kufundishia. JIPIME Mwalimu anaposimama mbele ya darasa na zana zake, Je, madhumuni na lengo lake ni kuinua kiwango cha wanafunzi kujifunza au kuinua kiwango chake cha kufundisha? KUMBUKA Lengo hasa la kutumia zana kati...