Posts

Showing posts with the label MWANAMALUNDI

KIFO CHA MWANAMALUNDI , MWANAMALUNDI SEHEMU YA TISA

Hadithi; MWANAMALUNDI Sehemu Ya Tisa  ILIPOISHIA...  "Mwanangu mpenzi, Mungu asifiwe ile shoka nilikuwa sikosi kuiangalia. Ilikuwa ikipanda tu bila kushuka. Ilipofika juu sana ilisimama kwa miaka Saba. Hatimaye nilifanikiwa kuiona ikiteremka, nilijawa na furaha isiyo kifani. Tena iliteremka kasi sana kisha ilitulia kwa muda wa siku moja. Kisha ikaanza kushuka pole pole. Leo asubuhi nilifurahi mara baada ya kufika ulipoiweka. Isiende mbele wala kurudi nyuma na punde nawe ukatokea. Pia yale maziwa uliyoyaacha hayakuganda ila yalitaka kuganda miaka miwili iliyopita. " Aliongea Mama huyo.  Na kweli aliyakuta bado mabichi.  ENDELEA...  Huko Nera alimkuta yule yule Mtemi Masanja. Watu walipomuona Igulu walianza kunong'onezana, hata mwisho tetesi zikamfikia Mtemi, ambaye bila kukawia alimfukuza pale Nera. Hivyo yeye pamoja na familia yake walihama na kuelekea Seke katika Wilaya ya Shinyanga karibu na Mjini Shinyanga.  Huko walimkuta Mtemi Mahizi, ambaye ...

MWANAMALUDI SEHEMU YA -2

Image
Hadithi; MWANAMALUNDI Sehemu Ya Pili Msimuliaji; A. H. Shaban Simu; +255 742 016 407 ILIPOISHIA... Alipokuwa na kufikia makamo ndipo alipoanza kucheza ngoma. Hivyo alipofikia umri wa miaka ishirini aliondoka nyumbani pamoja na vijana wenzake wawili wa pale kijijini kwenda kwa bibi kizee aliyekuwa maarufu sana ili kupata dawa ya 'Samba'. Samba ni dawa ya kisukuma yenye kumfanya mtu apendwe na kuvutia watu. Walipofika waliambiwa wasubiri kwa siku chache. ENDELEA... °MIKIKIMIKIKI. Baada ya siku tatu bibi kizee aliwachukua na kuwapeleka mwituni. Walipofika walianza kutafuta na kuwayawaya huku na huko. Kisha walifika kwenye mti mkubwa na mrefu. Kizee aliwaambia wamngoje kidogo akaokote kuni maana dawa ameikosa kwa hiyo watakuja kuitafuta siku nyingine. Igulu na wenzake waliachwa chini ya mti ule wakiwa hawana la kufanya. Ghafla kifaru alitokea akiwajia mbio na kila mmoja alikimbia kuokoa maisha yake. Igulu akawa katika mkikimkiki wa mbio kutaka kuyaokoa maisha yake,...

MWANAMALUNDI SEHEMU YA 1

Image
MWANAMALUNDI Mtu maarufu katika kabila la wasukuma KUZALIWA. Mwanamalundi alikuwa msukuma. Alizaliwa katika Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza mnamo mwaka 1892. Wazazi wake hawakuwahi kuzaa. Baba yake alikuwa Bugomola na mama yake aliitwa Ngolo. Baba yake alipoona hapati mtoto aliondoka kwenda kwa mganga kuaguliwa. Alipofika aliambiwa; "Mtoto utapata lakini atakapoanza kutembea wewe sharti utaiaga Dunia. Mtoto huyo atakuwa wa kiume na atakuwa na fahari kubwa sana." Bugomola kusikia atapata mwana, tena wa kiume ambaye atapata heshima na kusifiwa nchini pote, furaha aliyokuwa nayo ilikuwa haielezeki. Alipofika nyumbani alimueleza mkewe kinagaubaga alivyoambiwa na mganga huku akichekacheka kama aliyepatwa na kichaa. Siku hiyo alikuwa hatulii. Mara akae hapa mara akae pale. Wakati mwingine alikuwa akitembea huku na huko pale kijijini. Watu walimuona walishangaa kumuona vile, maana siku zote alikuwa ni mpole na mtulivu. Ingawa alikuwa akikumbuka maneno ya mganga kuwa mtoto a...