Posts

Showing posts with the label fonimu

maana ya fonimu pdf

Image
  dhana ya fonimu Fonimu ni nini TUKI (1990:45) wanasema fonimu ni kipashio kidogo kabisa cha kifonolojia kinachobadili maana. Hyman (1975:59) yeye anasema fonimu ni kipashio kidogo kabisa cha sauti kinachoweza kutofautisha maneno yenye maana tofauti. Mfano: ‘bata’ kuwa ‘pata’. Fonimu inawakilishwa katika maandishi kwa kutumia alfabeti za kifonetiki katika mabano mshazali / /. 2.1.1 Historia ya Fonimu Dhana ya fonimu ina historia ndefu sana ambayo ilitokana na nadharia ya wanamuundo inayoitwa “nadharia ya fonimu”. Katika kuitalii historia hii tunaanza na asili ya istilahi ‘fonimu’ na kisha tutaangalia ‘nadharia yenyewe ya fonimu’. Kwa miaka mingi dhana ya fonimu ilikuwa katika akili za wanaisimu wa wakati huo lakini istilahi yenyewe iliundwa baadaye sana. Hata hivyo, wanaisimu wanatofautiana juu ya nani alianzisha istilahi hiyo na au kuipa fonimu dhana inayot6umika hivi leo. Jones (1957) anasema istilahi hiyo iliundwa na Baudouin de Courtenay. Robins (1967) naye anaunga mkono mawaz...

NADHARIA YA FONIMU

 NADHARIA YA FONIMU UTANGULIZI, Dhana ya fonimu inahistoria ndefu sana. Na ilitokana na nadharia ya wanamuundo iliyojulikana kama nadharia ya fonimu. Asili ya istilahi fonimu.  Ingawa inawezekana kuwa dhana ya fonimu ilikuwamo katika mawazo ya wanaisimu na wanafilolojia wa zama hizo kwa miaka mingi  lakini istilahi yake iliundwa baadaye kabisa kama asemavyo Maasamba. Kwamujibu wa Jones (1957)  istilahi hii iliundwa na Baudouin de Courtenay, madai hayo ya Jones yanaungwa mkono na  Robins (1967:204) ambaye anaeleza kwamba katika kitabu chake cha theory of Phonemes  (yaelekea hii ni tafsiri ya baadaye) ambaco kimechapishwa  mwaka 1884 ambacho de Courtenay alitumia neno la Ki-Rus fonema kama istilahi, Hata hivyo Firth (1957:1) anasema kwamba inaelekea de Courtenay aliliazima istilahi hiyo fonema kwa manafunzi wake Kruszewiski ambayo aliitumia katika insha yake  iliyokuwa na mada  ya “ athari za mkazo  katika ubadilishanaji wa irabu  kat...

kubainisha fonimu

  Jambo moja ambalo limejitokeza katika yale tuliyoyasema kuhusu uanishaji wa fbnimu na alofbni ni umuhimu wa mfanano wa sifa za kifonetiki kati ya sauti tulizotolea mifano. Kwa mfano, tumeona kuwa sauti [t] na [d] zinatofautiana katika sifa moja tu, ya  ughuna,  zinachangia sifa za mahali pa kutamkia (zote ni za ufizi), na namna ya utamkaji (zote ni vipasuo). Hali kadhalika [t] na [th] zinatofautiana katika sifa moja tu, ya  mpwnuo;  zinachangia sifa za mahali pa kutamkia (zote ni za ufizi), na namna za utamkaji (zote ni vipasuo, na zote ni sigbuna). Katika kuchunguza mifumo-sauti ya lugha mbalimbali, mfanano wa kifonetiki kati ya sauti ni muhimu sana, kwa vile mahusiano yote ya kifonolojia, kanuni, pamoja na minyumbuo yote, kama tutakavyoona, yanaegemea katika sifa hii. Katika kuainisba sauti za lugha ili kugundua zipi ni fonimu za lugha biyo pamoja na alofoni zao, umuhimu huwekwa katika kuangalia uhusiano uliopo kati ya makundi ya sauti kufuatana na mahali pa...

fonimu na alofoni pdf

  Hapojuu tumetofautisha kati ya sauti-msingi na zile ambazo si za msingi.  Sauti-msingi  ni zile ambazo wazungumzaji wanaziona kuwa zinatenganisha maneno ya lugha yao, tofauti na zile ambazo, ingawa wanaweza kuzitamka wakipenda, hawazioni kuwa zina umuhimu katika kuunda maneno ya lugha yao. Hizi sauti-msingi huitwa  fonimu . Katika sura iliyotangulia tumesema kuwa sauti yoyote inayotolewa na viungo-sauti vya mwanadamu inaitwa  foni,  na tukaangalia jinsi foni zinavyochunguzwa na kupewa sit’a zao za kifonetiki, bila kujali zinatokea katika lugha gani, au zinatymika vipi. Lakini foni zikishachukuliwa na kutumiwa katika lugha fulani kuunda na kutofautisha maneno ya lugha hiyo, zinaingia katlka utaratibu wa mfumo-sauti wa lugha hiyo na kuwa fonimu za lugha hiyo. Hivyo, wakati ambapo foni ni vitamkwa halisi vinavyoweza kupimwa kiuchunguzi (yaani kifonetiki), fonimu ni vipashio vya mwanafonolojia vinavyomwezesha kujadili mfumo-sauti wa lugha maalumu. Katika mifa...