Posts

Showing posts with the label Matukio

AUDIO | NAVY KENZO - Fella | Download

Image
DOWNLOAD

HABARI MPYA: TUNDU LISSU AMEONDOKA NAIROBI KWENDA UBELGIJI KWA MATIBABU ZAIDI

Image
Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu ametoka Hospitali ya Nairobi nchini Kenya leo Jumamosi asubuhi kwenda nchini Ubeljiji kwa matibabu zaidi ya kuurejesha mwili wake katika hali yake ya kawaida. Lissu ambaye pia ni Rais wa Chama cha Mawakili wa Tanzania (TLS) ataondoka saa 2.30 asubuhi ya leo Jumamosi na Ndege ya Shirika la Kenya akiambatana na mke wake, Alicia. Lissu ametoka hospitalini hapo ikiwa baada ya matibabu aliyoyapata tangu Septemba 7 mwaka jana baada ya kushambuliwa kwa risasi zaidi ya 30 na watu wasiojulikana kwenye makazi yake Dodoma. Mwanasiasa huyo amesindikizwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta na watoto wake pacha, Augustino na Edward, ndugu zake, viongozi na wanachama wa Chadema. "Nawashukuru sana madaktari wa hapa Nairobi na wale wa Dodoma wakiongozwa na Katibu Mkuu (wa wizara ya afya Profesa Mpoki Ulisubisya waliookoa maisha yangu," amesema Lissu kabla ya kupandishwa gari la wagonjwa "Nakwenda Ubelgiji...

KUMRADHI: Tunaomba Radhi kwa kutoa Habari hii isiyo ya kweli

Image
Tunaomba Radhi kwa familia ya mzee kingunge kwa kuandika habari zisizoB sahihi kuhusu Mzee wetu mpendwa mzee Kingunge. Habari za kweli ni hizi.. MTOTO WA MZEE KINGUNGE AKANUSHA TAARIFA ZA KIFO CHA BABA YAKE ZINAZOSAMBAA MITANDAONI.. Mtoto wa mwanasiasa mkongwe Kingunge Ngombae Mwiru,Tonny Ngombale Mwiru amekana taarifa zinazozagaa mitandaoni kuhusu kifo cha baba yake mzee Kingunge Ngombale Mwiru. Tonny amefanya mahojiano na waandishi wa habari jioni ya leo na kuwaeleza kuwa baba yake yuko hospitali akipata matibabu baada ya kung’atwa na mbwa hivyo kupata majeraha Kwenye miguu ambayo ndiyo anayouguza hospitalini kwa sasa. Kuhusu mazishi ya mke wa mwanasiasa huyo ambaye alifariki jana katika hospitali ya Muhimbili Tonny Ngombale Mwiru amesema familia itatoa taarifa mapema kesho baada ya baba yao mzee kingunge kuelezwa na kutoa maelekezo kama baba mzazi na kiongozi wa familia hiyo.

Mvua yaua wanne Manyara

Image
Watu wanne wamefariki dunia Wilayani Kiteto mkoani Manyara baada ya kusombwa na maji yaliyosababishwa na mvua zinazoendelea kunyesha sehemu mbalimbali hapa nchini. Mkuu wa Wilaya ya Kiteto, Tumaini Magessa leo Ijumaa amesema vifo hivyo vimetokea kwenye matukio tofauti katika kata za Matui, Engusero na kijiji cha Ndaleta kata ya Njoro. Magessa amesema tukio la kwanza lilitokea jana Alhamisi jioni kwenye kijiji cha Matui, ambapo watu wawili walisombwa na mafuriko wakati wakielekea nyumbani kwao. Amewataja waliofariki dunia kuwa ni Alhaman Gola (37) mkulima wa Matui na Abuu Juma (27) mkulima wa Kijiji cha Chapakazi. Amesema mtu mwingine Hamis Chilogola (22) alikuwa na wenzake wawili wakielekea Kituo cha Afya Matui kwa ajili ya kutembelea mgonjwa lakini wakiwa njiani walisombwa na maji kwenye korongo wenzake walifanikiwa kuvuka yeye akafa kwa kusombwa na maji. Amesema mtu wa nne kufariki dunia ametambulika kwa jina la Ally Hamis (25) mkazi wa kijiji cha Chilongola ambaye ali...

GOOD NEWS KWA WATUMIAJI WASIMU TCRA YAPUNGUZA GHARAMA ZA KUPIGA SIMU

Image
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), yashusha gharama za kupiga simu kutoka shilingi 26.96 kwa dakika moja hadi shilingi 15.60 kuanzia 2018. Mkurugenzi wa TCRA James Kaliba amesema kuwa gharama hizo zitaendelea kupungua kadiri miaka inavyozidi kwenda kama ambavyo imeanishwa hapa. Gharama za mwingiliano zitakazotozwa kwa dakika na mwaka kwenye mabano ni Sh15.60 (Januari Mosi, 2018), Sh10.40 (2019), Sh5.20 (2020), Sh2.60 (2021) na Sh2.00 (2022). Viwango hivyo vimepungua kulinganisha na miaka mitano iliyopita ambayo gharama zake za mwingiliano zilizokuwa zikitozwa kwa dakika na mwaka wake kwenye mabano ilikuwa Sh34.92 (2013), Sh32.40 (2014), 30.58 (2015), Sh28.57 (2016) na Sh26.96 (2017). Hata hivyo amesema kuwa kampuni za simu zimekuwa na kigugumizi kukubaliana na viwango hivyo na kuingia mikataba ya mwingiliano kwa sababu ya masilahi ya kibiashara hivyo TCRA ililazimika kuingilia kati na kuvipangia kwa kufuata utaratibu kama ilivyoainishwa katika sheria namba 12 y...

Agizo la Waziri Nchemba kama huna kitambulisho cha utaifa

Image
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dk. Mwigulu Nchemba amewataka wananchi wa Tanzania kujiandikisha kupata kitambulisho cha Taifa kwani si zoezi la hiari na kwamba ni lazima kwa mtanzania aliyeko ndani ya mipaka ya nchi ili kutambuliwa. Amesema hayo akizindua zoezi la kujiandikisha kupata kitambulisho  cha Taifa na kugawa vitambulisho katika Mkoa wa Ruvuma na kukagua zoezi hilo linaendaje kwa mikoa ya Nyanda za Kusini hasa iliyoko mipakani mwa nchi. Waziri Nchemba amewataka wananchi waache mazoea ya kutafuta kutambuliwa mpaka wanapokuwa na shida hasa za kutaka hati ya kusafiria au migogoro ya ardhi pale anapoambiwa yeye si raia wa Tanzania. Mh. Nchemba amewagiza viongozi wa wilaya na vijiji kutokuunganisha zoezi la kuandikisha wananchi kupata vitambulisho vya uraia na zoezi lingine lolote akitolea mfano baadhi ya viongozi kuchangisha fedha za kijiji kwa kuwaambia kuwa hutopata kitambulisho mpaka utakapo lipa fedha unazo daiwa na kijiji. "Hili zoezi...

UMEIPATA HII YA WEMA NA RC MAKONDA LEO?

Image
Mwigizaji  Wema Sepetu  bado anazo headlines za baada ya kurudi CCM ambapo leo kaendelea kuandika ya moyoni kuhusu uhusiano wake na Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam  Paul Makonda . Maneno yake aliyoyatoa leo ni haya >>> “Sikukufahamu vyema mpaka nilipokuchukia, na sasa nilipokutana na wewe nashukuru Mungu nimekupata maana hata kila wingu jeusi huwa na rangi ya fedha”

Ashikiliwa na Polisi kwa kuvua viatu vinavyonuka

Image
  Mwanaume mmoja jijini New Dehli nchini India amekamatwa na polisi kwa kosa la kuvua viatu vinavyotoa harufu mbaya kwenye basi la usafiri wa umma kwa kusababisha vurugu kwa abiria waliokuwa kwenye usafiri huo. Mwanaume huyo aliyetambulika kwa jina Prakash Kumar (27) inaelezwa kuwa baada ya kuvua viatu hivyo abiria wenzake walianza kumshambulia kwa maneno wakimtaka ashuke kwenye gari lakini alikataa ndipo wakamuamuru dereva apeleke gari kwenye kituo cha polisi. Gari hilo lililokuwa kwenye safari kutoka mjini Himachal Pradesh kuelekea jijini New Dehli lilimshusha kwenye kituo cha Polisi cha Bharwain nje kidogo ya Himachal ambako polisi walimzuia asiendelee na safari. “Tulimkamata Kumar baada ya kuletwa na Basi akivuruga amani kwenye Basi. “amesema Sanjeev Gandhi Kamanda wa polisi mjini Himachal Pradesh. Gazeti la Hindustan Times la nchini India limeeleza kuwa bwana Kumar aliambiwa avitupe viatu vyake nje ya gari lakini alikataa kwa kudai kuwa vilikuwa havitoi haru...

DR LOUIS SHIKA MIMI SIO MBABAISHAJI AONESHA KAMPUNI YAKE MTANDAONI

Image
Bado jina la  Dr. Luis Shika  lipo kwenye vichwa vya habari na ni baada ya kuachiwa kwa dhamana na Polisi Dar es salaam jana ambapo alikamatwa wiki iliyopita kwa kuharibu mnada, mnada ambao alijinadi kununua nyumba za Bilioni 2 kumbe hana pesa mfuko katika mahojiano baada ya kup ata nafasi ya kumtembelea Dr. Luis Shika nyumbani kwake Tabata na kuwaambia Watanzania ambao hawaamini kwamba anamiliki Kampuni huko Russia kwamba yeye sio Mbabaishaji….  jionee mwenyewe kwenye hii video hapa chini VIDEO:kwahisani ya Ayo TV Masshele Blog

USIYO YAJUA KUHUSU TAJIRI MTATA ALIYE LETA GUMZO NYUMBA ZA LUGUMI , YADAIWA NIMSUKUMA WA SIMIYU.......

Image
Wakati maswali mengi yakijitokeza kuhusiana na Dk. Louis Shika, ambaye aliibuka mshindi katika mnada wa nyumba za kifahari za Said Lugumi zilizoko Mbweni JKT na Upanga jijini Dar es Salaam kwa thamani ya jumla ya Sh. bilioni 3.3, imebainika kuwa anaishi katika chumba kimoja cha kupanga. Imebainika kuwa Dk. Shika anakaa kwenye nyumba hiyo iliyopo Mtaa wa Amani kwa kipindi cha takribani mwaka mmoja sasa na kodi anayolipa kwa mwezi ni takribani Sh. 50,000. Aidha, baadhi ya majirani zake wamemuelezea kuwa ni mtu asiye na makeke, huku baadhi wakidai kuwa aliwahi kuwaahidi wauza mihogo ya kukaanga walio jirani na mahala anapoishi kuwa atawaunganishia kupata mikopo nafuu ili wakuze biashara zao, lakini bila ya kuwatajia taasisi atakayowaunganisha nao. Inadaiwa kuwa vilevile, kwa baadhi ya watu hufahamika kwa jina la ‘profesa’. Dk. Shika alijipatia umaarufu katikati ya wiki baada ya kuibuka mshindi katika mnada wa nyumba za kifahari za Lugumi, kwa kununua nyumba moja ya M...

VIDEO: Rais Magufuli akiwa nyumbani kwao Chato ,

Image
Mara nyingi tunapomtazama Rais Magufuli huwa anakua kwenye sura ya kazi akiwa kwenye ziara au kwenye hotuba ila leo tumeonyeshwa upande wake mwingine, kakaa juu ya mkeka akipiga stori na Mama yake mzazi (kushoto) na Dada yake Monica (kulia) mtazame kwenye hapa chini

Mtandao wa WhatsApp Waruhusu Kufuta Ujumbe

Image
  Ilishawahi kukutokea kutuma ujumbe, picha au video au documenti yeyote kwa mtu usiyemkusudia kwa bahati mbaya kupitia programu ya WhatsApp? kama huwa unapatwa na matatizo hayo sahau kabisa kwani tayari programu hiyo imeshaongeza sehemu ya kufuta jumbe hizo. WhatsApp is rolling out the Delete for Everyone (Recall) feature for all users! 🎉https://t.co/3bnbgxtPvU — WABetaInfo (@WABetaInfo) October 26, 2017 WhatsApp tayari imezindua huduma hiyo ambayo imeongezwa kwenye programu kwa jina ‘Delete For Everyone’ ambapo mtumaji wa ujumbe, picha au video atachagua kufuta kwake au kwa mtu aliyemtumia kimakosa. Kwa sasa huduma hiyo inapatikana kwa watumiaji wote wa iOS na Android kama bado basi cha kufanya update programu yako ya WhatsApp ili uanze kutumia. Hii inakuwa hatua nyingine ya maboresho ya programu hiyo baada ya kutangaza kuongeza sehemu ya Live Chart  ndani ya mwaka huu. Mwanzoni mwa mwezi Agosti mwaka huu WhatsApp Inc walitangaza kuwa wataleta mabadiliko makub...

900 wasimamishwa shule, kisa binti mmoja

Image
KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida, karibu wanafunzi 900 wa Shule ya Sekondari Kabale katika Manispaa ya Kabala nchini Uganda wamesimamishwa masomo kutokana na vurugu kubwa zilizoibuka shuleni hapo, chanzo kikielezwa ni kumgombea kimapenzi binti mmoja ambaye pia ni mwanafunzi shuleni hapo. Wanafunzi hao waliibua vurugu kubwa na kuanza kupigana mchana wa Ijumaa iliyopita shuleni hapo. Inaelezwa kuwa, mwanafunzi wa kidato cha sita aliomba kuwa na uhusiano na binti ambaye alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanafunzi mwingine wa kidato cha nne. Kutokana na kuvuja kwa taarifa hizo, makundi mawili ya wavulana hao yaliibua uhasama ulioishia kupigana. Ugomvi huo haukuishia kwa wanafunzi tu, waliharibu pia mali za shule na hata za majirani wanaoishi karibu na shule hiyo. Kutokana na hali hiyo, jeshi la Polisi lililazimika kuingilia kati kutuliza ghasia kwa kutumia mabomu ya machozi na silaha nyingine kutawanya wanafunzi hao. Kaimu Ofisa anayeshughulikia usalama wilayani Kabale, ...

Kiongozi wa Catalonia aliyefutwa "aenda Ubelgiji"

Image
  Rais wa Catalonia aliyefutwa Carles Puigdemont ameenda nchini Ubelgiji, wakili wake aliye chini humo anasema. Wakili huyo Paul Bekaert, hakuzungumzia ripoti kuwa Bw. Puigdemont anajiandaa kuomba kupewa hifadhi. Mwendesha mashtaka nchini Uhispania ametaka mashataka ya uasi kufunguliwa dhidi yake na viongozi wengine ya kura ya maoni iliyopogwa marufuku. Serikali ya Uhispania ilichukua udhibiti kamili wa Catalonia siku ya Jumatatu, kuchukua mahala pa viongozi waliofutwa. Ilifuta utawala wa eneo hilo na kuitisha uchaguguzi mpya baada ya Bw Puigdemont na serikali yake kujitangazia uhuru wiki iliyopita. Wakili huyo wa Ubelgiji Paul Bekaert alisema kuwa Bw. Puigdemont kwa sasa yuko mji mkuu wa Ubelgiji Brussels. Mbona Puigdemont akaenda Ubelgiji? Uhispania ilikuwa imekumbwa na mzozo wa kikatiba tangu kura ya maoni iliyopangwa na serikali ya Bw. Puigdemont, ilipoandaliwa tarehe mosi Oktoba kinyume na amri ya mahakama iliyoamua kuwa kura hiyo ilikuwa kinyume na katiba. Serik...