Posts

Showing posts from May, 2017

KWA KAULI HII YA HANS POPPE TAYARI WACHEZAJI 10 SIMBA SAFARI IMEWAKUTA

Image
Klabu ya Simba imepanga kuwabakiza wachezaji 15 pekee kati ya 25 iliowasajili msimu uliopita wa Ligi Kuu Bara na Kombe la Shirikisho (FA). Timu hiyo, inataka kukiimarisha kikosi chake kwa ajili ya kujiandaa na michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika (Caf) watakayoshiriki mwakani. Wakati wakipanga kusajili na kuwaacha wachezaji hao, tayari baadhi ya nyota muhimu wa Simba wameshaanza kuaga kwenye timu hiyo akiwemo Abdi Banda ambaye mkataba wake umemalizika, wengine ni Jonas Mkude na Ibrahim Ajibu ambao wanaelezwa kuwa wanaweza kuondoka kwenye timu hiyo. Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe, alisema kuwa bado hawajapokea rasmi ripoti ya Kocha Mkuu wa timu hiyo, Mcameroon, Joseph Omog lakini tayari Kamati ya Utendaji ilikutana kufanya tathmini ya kikosi chao kwa ajili ya usajili. Hans Poppe alisema  katika kikao hicho wameona wachezaji kumi ambao hawana mchango na kupanga kuwaondoa katika mipango yao ya msimu ujao wa ligi na michuano ya...

IMEISHIA MSIMU HUU, SINGIDA YAWANYATIA BARTHEZ, JOSHUA SAFARI YAO YANGA IMEISHIA MSIMU HUU, SINGIDA YAWANYATIA

Image
Kipa mkongwe wa Yanga, Ally Mustapha 'Barthez' na beki wa pembeni wa timu hiyo, Oscar Joshua ni kati ya wachezaji watakaokuwepo kwenye kikosi cha Singida United katika msimu ujao wa Ligi Kuu Bara. Kama hawatakuwa katika kikosi hicho basi safari yao kwa upande wa Yanga itakuwa imeishia hapo. Barthez na Joshua ni kati ya wachezaji ambao hawakuwa na nafasi ya kucheza katika kikosi cha kwanza cha Mzambia, George Lwandamina katika msimu uliopita wa ligi kuu. Wachezaji hao wote bado wana mikataba ya mwaka mmoja wa kuichezea Yanga kwenye msimu ujao wa ligi. Kwa mujibu wa taarifa za ndani wachezaji hao wataondolewa Yanga na kupelekwa Singida inayofundishwa na Kocha Mkuu Mholanzi, Hans Pluijm aliyekuwa anaifundisha timu hiyo kabla ya nafasi yake kuchukuliwa na George Lwandamina. Mtoa taarifa huyo alisema, wachezaji hao walikuwepo kwenye orodha ya wachezaji watakaochwa katika msimu ujao, lakini kutokana na mikataba yao kutomalizika watapelekwa kwa mkopo...

WANAMICHEZO MAARUFU 100 HAWA HAPA, RONALDO ANAONGOZA, LEBRON ANAFUATIA HALAFU MESSI

Image
WANAMICHEZO MAARUFU 100 HAWA HAPA, RONALDO ANAONGOZA, LEBRON ANAFUATIA HALAFU MESSI 1 Cristiano Ronaldo (football) 2 LeBron James (basketball) 3 Lionel Messi (football) 4 Roger Federer (tennis) 5 Phil Mickelson (golf) 6 Neymar (football) 7 Usain Bolt (athletics) 8 Kevin Durant (basketball) 9 Rafael Nadal (tennis) 10 Tiger Woods (golf) 11 Stephen Curry (basketball) 12 Novak Djokovic (tennis)  13 Virat Kohli (cricket) 14 Rory McIlroy (golf) 15 Mahendra Singh Dhoni (cricket) 16 Ronda Rousey (UFC) 17 Jordan Spieth (golf) 18 Kaka (football) 19 Serena Williams (tennis) 20 Kei Nishikori (tennis) 21 Tom Brady (NFL) 22 Gareth Bale (football) 23 Maria Sharapova (tennis) 24 Dwyane Wade (basketball) 25 Conor McGregor (UFC) 26 Zlatan Ibrahimovic (football)  27 James Rodriguez (football) 28 James Harden (basketball) 29 Alexis Sanchez (football) 30 Mesut Ozil (football) 31 Wayne Rooney (football) 32 Andy Murray...

TAASISI YA KUPAMBANA NA RUSHWA -UDSM(CEOAC).YAPATA UONGOZI MPYA.

Image
TAASISI YA KUPAMBANA NA RUSHWA -UDSM(CEOAC).YAPATA UONGOZI MPYA.            Taasisi ya kuzuia na kupambana rushwa chuo kikuu cha Daresaalam yaani "combined Efforts Organization against corruption"(CEOAC-UDSM), tarehe 28/05/2017,imefanya uchaguzi wake na kupata viongozi wake katika nafasi ya Raisi ,makamu, ukatibu, muweka hazina,kama inavyoeleza katika katiba yao ambapo uraisi alishinda Abdul Omar Nondo, na umakam alishinda Veronika Kipingu, katibu mrisho Rashidi, P.R.O Gikaro Bernard na bulahya maiko, system admin. Benedictor eliji, Mhasibu, masaka Omary. Akiongea na MASSHELE BLOG , Abdul Nondo, raisi mteule alishukuru uongozi uliopita kwa kutua mzigo wa majukumu kwao na akaahidi, kufanya Kazi na uongozi wake kikamilifu, " nashukuru uongozi uliopita ni muda sasa kufanya taasisi hii kukua ndani na nje ya jumuiya yetu ya chuo,sababu lengo kubwa ni kuwa na jamii itakayotambua umuhimu wao katika mapambano ya rushwa, jamii itakayokasirishwa juu ya...

HII NDIO SIMBA MPYA

Image
Share this on WhatsApp NA ZAITUNI KIBWANA, SIKU chache baada ya Simba kubeba Kombe la FA na kukata tiketi ya kushiriki michuano ya kimataifa mwakani, timu hiyo imepanga kuboresha kikosi chao kwenye maeneo kadhaa. Tayari Wekundu wa Msimbazi hao wana uhakika wa kushiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika, huku tiketi ya Ligi ya Mabingwa ikienda kwa mabingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga. Kutokana na hilo, Simba wamepanga kuingia sokoni kununua wachezaji ambao wataweza kuwa na timu imara itakayoweza kuhimili mikikimikiki ya michuano ya kimataifa. Tayari nafasi kadhaa zimeanza kutajwa kufanyiwa marekebisho, ikiwamo eneo la ulinzi, kiungo mwenye nguvu na safu ya ushambuliaji. Nyota wanaotajwa kuingia kwenye kikosi hicho msimu ujao ni kipa Aishi Manula aliyemaliza mkataba wake Azam ambaye atachukua nafasi ya Mghana Daniel Agyei anayetajwa kuwa mbioni kuondoka Msimbazi. Wachezaji wengine ambao wapo kwenye hesabu za Simba, ni kiungo mkabaji wa Mbao FC, Yu...

BREAKING: Mzee aliyechora Nembo ya Taifa amefariki Dunia

Image
Taarifa zilizonifikia kutoka Hospitali ya Muhimbili zinasema mzee Francis Kanyasu maarufu kama Ngosha, ambaye amehusika kwenye kuchora Nembo ya Taifa Tanzania, amefariki dunia akiwa kwenye matibabu hospitalini hapo. Kwa mujibu wa taarifa inaelezwa kuwa May 29, 2017 hali ya mzee huyo ilibadilika ghafla na madaktari walijitahidi kadri ya uwezo wao kuweza kunusuru maisha yake lakini ilishindikana na akafariki duniani saa 2 usiku. Mwili wa mzee huyo upo chumba cha kuhifadhia maiti hospitalini hapo ambapo unasubiri mamlaka husika kutoa maelekezo zaidi. VIDEO: Ulipitwa na maamuzi ya serikali kuhusu aliyechora Nembo ya Serikali? Tazama hapa chini. VIDEO: Ilikupita hii kauli ya familia nyingine kuhusu mtu sahihi aliyechora Nembo ya Taifa? Bonyeza play kutazama. +255766605392 Findings comment yako wasap

KIKOSI BORA CHA LIGI KUU BARA FIRST ELEVEN

Image
KIKOSI BORA CHA LIGI KUU BARA 2016-17 1. Aishi Manula 2. Salum Kimenya 3. Mohamed Hussein 4. Mohamed Yakubu-Azam 5. Method Mwanjale 6. Kenny Ally-Mbeya City 7. Simon Msuva-Yanga 8. Haruna Niyonzima 9. Abdulrahman Musa 10. Mbaraka Yusuf 11. Shiza Kichuya

UMESIKIA HIKI ALICHOAMBIWA RAIS MAGUFULI,? A ---Z. IPO HAPA

Image
                      Abdul Omar Nondo.                                         *PONGEZI KWA MH.RAISI JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI* Na  *Abdul Omar Nondo*.  Napenda kumpongeza Mh.Raisi kwa hatua alizochukua, na kwa namna alivyokasirishwa juu ya mapato makubwa ambayo tumekuwa tukiyapoteza.  Kampuni ya ACACIA ,ni kampuni ya uingereza ambayo viongozi wake wakuu ni *kelvin Dushnisky* Kama m/kiti,Bradly Gordon Kama *CEO* na imeanza kuwekeza tangu mwaka 1999,ikitambulika Kama BARRICKS GOLD COOPERATION LTD.kabla ya kubadilishwa jina tarehe 27.november 2014. ndio ikaitwa ACACIA ikimiliki mgodi wa Buzwagi na Bulyanhulu, baadaye north Mara,na tulawaki. hii ndio kampuni ya kimataifa ambayo imekuwa ikisafirisha mchanga tangu 1999. Hivyo basi kwa ripoti ya kamati hiyo iliundwa kuchunguza kiwango cha madin...

TAARIFA KUHUSU ORODHA YA MAJINA YA WANAFUNZI KIDATO CHA SITA WANAOJIUNGA NA JKT KWA MUJIBU 2017

Wanafunzi wa kidato cha sita waliohitimu mwaka huu May 2017 takribani 14,747 sawa na asilimia 23.2%, wamepangiwa katika vituo mbalimbali vya Jeshi kati ya wahitimu 63,623, wanatakiwa kufika kambini kuanzia 25-30 May.  Taarifa imetolewa na Mkuu wa JKT  Akiongea na ITV amesema Orodha ya waliochaguliwa katika kambi mbalimbali yanapatikana katika tovuti yao ya JKT.  www.jkt.go.tz Source: ITV (Habari

UGONJWA WA KUKOJOA DAMU (HAEMATURIA)

Image
HAEMATURIA  ni ugonjwa wa kukojoa damu ambapo kwenye mkojo kunakuwepo chembechembe za damu nyekundu (Red blood cells). Kukojoa damu ni dalili ya kuonyesha kuwa mtu anayekojoa ana magonjwa katika mfumo wa mkojo kama vile magonjwa ya kichocho au magonjwa mengine yanayoshambulia kibofu cha mkojo au kwenye figo. SABABU Magonjwa yanayoshambulia mfumo wa mkojo kama vile UTI, magonjwa ya zinaa hasa kwa wanawake, vijidudu kama staphylococcus saprophyticus, mawe kwenye figo (kidney stone) kuvimba kwa tezi zinazozalisha manii kwa wanaume ambao umri  umeenda yaani wazee. Sababu nyingine ni kama kupata ajali na kuumia sehemu za mfumo wa mkojo (trauma), kupata magonjwa kama kansa  ya kibofu cha mkojo, hii hutokea  mara nyingi hasa  vijijini  ambapo watu wanacheza au kuogelea kwenye madimbwi ya maji yasiyotembea. Sababu zingine  ni mtu kuugua magonjwa ya sickle cell anemia na magonjwa mengine  ya figo kama vile nephotic syndrome na mengine mengi...

ENDOMETRIOSIS NI UGONJWA GANI?| FAHAMU ZAIDI KUHUSU UGONJWA WA ENDOMETRIOSIS

Image
Ukuta wa ndani wa kifuko cha uzazi unaitwa endometrium. Ukuta huu hujengeka na kubomoka kila mwezi na kusababisha hedhi kwa wanawake. Kujengeka na kubomoka kwa ukuta huu wa ndani wa kifuko cha uzazi kunasababishwa na mabadiliko ya kiasi cha hormoni za uzazi mwilini. Endometriosis ni ugonjwa unaosababishwa na uwepo wa tishu zinayofanana na ukuta wa ndani wa kifuko cha uzazi (endometrium) sehemu nyingine kwenye mwili. Mara nyingi tishu hizi huota kwenye sehemu ya chini ya tumbo (pelvis) karibu na ovari, kifuko cha uzazi, kibofu cha mkojo na njia ya haja kubwa. Kama ilivyo kwa ukuta wa ndani wa kifuko cha uzazi (endometrium), tishu hizi zinazopatikana nje ya kifuko cha uzazi pia hujengeka na kubomoka kutokana na mzunguko wa hedhi. Kwa sababu hii, hata dalili za uwepo wa ugonjwa wa endometriosis hufuatana na mzunguko wa hedhi. Kitu kinachosababisha ugonjwa huu hakifahamiki kwa uhakika lakini inaaminika kuwa kiasi kidogo cha damu kinachoingia tumboni wakati wa hedhi kupitia mirija...