Posts

Showing posts from April, 2017

Vyakula vinavyoongoza kwa kuongeza akili kwenye ubongo

Image
Katika mwili wa mwanadamu hakuna kitu chenye umuhimu mkubwa kama ubongo, ubongo ndio ambao humsaidia mwanadamu katika kufanya mambo mbalimbali, hata hivyo inaelezwa ya kwamba ubongo wa mwanadamu ndio humfanya mwanadamu kuonekana hivyo alivyo. Hivyo inaelezwa ya kwamba ili mwanadamu aweze kuongeza akili, katika kufikiri na kutenda mambo mbalimbali anatakiwa kula vyakula vifuatavyo: 1. Mafuta ya samaki. Mafuta ya samaki ni muhimu kwa ubongo na mfumo wa fahamu. Ulaji wa samaki wenye minofu kama sangara na dagaa, utaweza kupata faida hizo kwa sababu aina hii ya samaki ina kiasi kingi cha mafuta ya Omega 3 ambayo huimarisha utendaji kazi na mawasiliano kati ya ubongo na seli za mwili moja kwa moja. 2. Ulaji wa mbegu za maboga. Mbegu za maboga zina kiwango kingi cha madini ya ‘Zinc’ ambayo husadia kuongeza kumbukumbu (memory). Kuna njia nyingi za kula mbegu za maboga, moja wapo ni kuzikaanga na kula kama karanga, ukila kiasi cha kiganja kimoja kwa siku, huweza kusaidia kuweza kuon...

🔴LIVE: Tazama Taarifa ya Habari ya AzamTv leo

Image
Kama ni mpenzi wa kufuatilia taarifa ya habari basi ndo time yako yakuitazama taarifa ya habari ya  April 30 2017  kwani  millardayo.com   na    MASSHELE BLOG TV  inakuunganisha na  Azama TV kutazama taarifa ya habari  LIVE , Bonyeza play hapa chini.

NADHARIA ZA MAANA :MAANA NININI?

Image
NADHARIA ZA MAANA Habwe na Karanja (2007:204), Crystal (1987), Matinde (2012), Ogden na Richards (1923), wanakubaliana kuwa neno maana lina fahiwa nyingi, linaweza kudokeza sababu, kusudi, ishara, urejeleo, maelekezo, ufafanuzi, kufaa na ukweli. Kutokana na ugumu uliopo katika kufafanua maana ya maana, wanaisimu wamefafanua aina kuu mbili za maana ambazo ni maana ya msingi na maana ya ziada. Utetezi wa nadharia hii umesababisha kuibuka kwa nadharia mbalimbali ambazo zinajaribu kueleza maana ya maana kwa kutumia nadharia mbalimbali, ambazo chimbuko lake ni wanaisimu, wanafalsafa, wanamantiki na wanasaikolojia. Nadharia ni mpango wa mawazo uliotungwa ili kuelekeza jinsi ya kufanya au kutekeleza jambo fulani (Mdee na wenzake, 2011). Kwa msingi huo nadharia hubeba mawazo, dhana au maelezo yatolewayo kwa nia au kwa lengo la kueleza hali fulani, chanzo, muundo, utendaji na mwingiliano wa ndani na nje. Sengo (2009:1) anafasili nadharia kuwa ni wazo kuu, fikra kuu, mwongozo mkuu wa mtu, wa...

michakato ya kimofolojia inavyotumika kuunda maneno katika lugha ya kiswahili.

Image
Mofolojia ni taaluma inayoshughulikia vipashio vya lugha na mpangilio wake katika uundaji wa maneno. Vipashio hivyo vya lugha huitwa mofimu (Rubanza, 1996). Mofolojia ni tawi la taaluma ya isimu ambalo huchunguza maumbo ya maneno na hususani: maumbo ya mofimu. (Mathews, 1974) Hartman (1972) anasema kuwa mofolojia ni tawi la sarufi ambalo hushughuliia na uchunguzi na uchambuzi wa maumbo, fani na aina zao maneno yalivyo sasa pamoja na histori zao. Mofolojia huchunguza mofimu na alomofu zake fulani na jinsi ambavyo hukaa pamoja kuunda maneno mbalimbali katika lugha zinamotumika (Richard na wenzake 1985). Kwa ujumla, mofolojia ni tawi la isimu ambalo huchunguza maneno ya lugha fulani na aina zake za maneno hasa upande wa upangaji wa mofimu mbalimbali zitumikazo kwa ajili ya kuunda maneno. Pia wana taalamu mbalimbali wamefasili maana ya maneno kwa mitazamo mabalimbali kama ifuatavyo. Tuki, (1970) Neno ni mkusanyiko wa sauti ambazo huweza kutamukika na kuandikwa kwa pa...

Video :Alicho Sema magufuli kuhusu Watumishi wasio na vyeti

Image
Umesikia alicho Sema magufuli kuhusu wale watumishi wasio na vyeti. Kila kitu kipo hapa mtu wangu tembelea blogu yako kila siku upate kila hitaji

Yanga yamtema Ngoma

Image
Yanga yamtema Ngoma   Thursday, April 27, 2017   Klabu ya soka ya Yanga SC inapenda kutoa taarifa juu ya safari yake kuelekea Mwanza katika mechi ya nusu fainali ya kombe la Azam Sport Confedaration cup. Msafara wa wachezaji,benchi la ufundi na viongozi utaondoka saa 11 jioni na ndege ya shirika la ndege la ATC. Wachezaji watakaoondoka ni... Makipa: Deogratius Munishi, Beno Kakolanya na Ally Mustapha. Nafasi ya ulinzi ni ; Nadir Haroub,Vicent Andrew, Oscar Joshua , Juma Abdul , Mwinyi Haji, Hassan Kessy na Kelvin Yondani.  Viungo: Thabani Kamusoko, Haruna Niyonzima, Deusi Kaseke,Said Makapu, Juma Mahadhi, Saimoni Msuva, Geofrey Mwashuiya na Emmanuel Martin. Washambuliaji: Amissi Tambwe , Matheo Antony na Obrey Chirwa. Wachezaji watakaoukosa mchezo huo kwa sababu mbalimbali ni:  Malimi Busungu,Vincent Bossou na Donald  Ngoma Imetolewa na idara ya habari na mawasiliano;  Young Africans SC 27/04/2017 ...

Upinzani Kenya yamtaja atakayeshindana na Rais Kenyatta kwenye Uchaguzi Mkuu

Image
Upinzani Kenya yamtaja atakayeshindana na Rais Kenyatta kwenye Uchaguzi Mkuu   Thursday, April 27, 2017   Muungano wa Vyama vya Upinzani nchi Kenya NASA umemtangaza mwanasiasa mkongwe nchini humo Raila Odinga kuwa mgombea wa nafasi ya Urais wa nchini kwenye Uchaguzi Mkuu utakaofanyika August 8 mwaka huu. Aidha, NASA imemtangaza Kalonzo Musokya kuwa mgombea-mwenza

EXCLUSSIVE: Babu Seya kuachiwa Huru

Image
EXCLUSSIVE: Babu Seya kuachiwa Huru   Thursday, April 27, 2017   Tumaini jipya! Mtoto wa kiume wa mfungwa anayetumikia kifungo cha maisha jela, Nguza Viking ‘Babu Seya’, Mbangu Nguza ameibuka na kusema kuwa, mwaka 2017 ndiyo wa mwisho kwa baba yake na mdogo wake, Johnson Nguza ‘Papii Kocha’ kuendelea kutumikia kifungo chao cha maisha jela. Akizungumza katika mahojiano maalum na Gazeti Amani mwanzoni mwa wiki hii, Mbangu alisema kuwa, turufu ya mwisho ya hukumu ya ndugu hao ipo kwenye mikono ya Mahakama ya Haki za Binadamu Afrika (AfCPHR) yenye makazi yake jijini Arusha ambayo kimsingi vikao vitatu vya awali vimeshakaa na kubaini kuwa, hukumu ya Babu Seya na Papii ilikuwa na kasoro. “Unajua watu hawafahamu, kule ambako hukumu ya mzee na bwana mdogo (Papii), ilipelekwa kuna hatua. Kwanza kabisa, wale majaji wanatoka nchi mbalimbali, kwa hiyo siyo kwamba wanakwenda tu Arusha na kupitia hukumu, hapana. “Kilichofanyika ni kwamba, kuna watu walikaa mar...

Man United kuikabili Man City bila Pogba, bila Zlatan, bila Rojo.

Image
Man United kuikabili Man City bila Pogba, bila Zlatan, bila Rojo. Sahau kuhusu majeraha ya Smalling na Phill Jones waliyoyapata wakati wa kambi ya timu ya taifa ya Uingereza lakini majeruhi ndani ya United wanazidi kumiminika. Tayari Zlatan Ibrahimovich yuko nchini Marekani kwa ajili ya upasuaji baada ya kuumia katika mchezo wa ligi ya Europa dhidi ya klabu ya Ubelgiji ya Anderlchelt. Marcos Rojo naye aliumia katika mchezo huo wa Europa lakini kuna jipya, Paul Pogba hatakuwepo katika mchezo mkubwa kwa Manchester dhidi ya majirani zao City. Taarifa kutoka ndani ya klabu hiyo zinasema majeruhi aliyopata Pogba katika mchezo wa ligi kuu dhidi ya Burnley utamfanya asiwepo katika Manchester Derby. Jose Mourinho amesema kutokuwepo kwa Pogba hakuwaumizi sana na wanaamini atarudi siku nyingine na kwa sababu hayupo inabidi wapambane na walichonacho. Mechi kati ya United na City ni ngumu sana na inavuta hisia za wengi lakini pia klabu hizo mbili zinapigana vikumbo kuingia top four ya li...

Meli kubwa ya kijasusi ya Urusi yazama Uturuki

Image
Meli kubwa ya kijasusi ya Urusi yazama Uturuki Meli ya kijasusi ya Urusi imezama baharini katika pwani ya Uturuki baada ya kugongana na meli ya kubeba mizigo, maafisa wa uchukuzi wa baharini wa Uturuki wamesema. Wote waliokuwa kwenye meli hiyo wameokolewa. Urusi awali ilikuwa imethibitisha kwamba meli ya Liman, ambayo ni sehemu ya kundi la meli za taifa hilo katika Bahari Nyeusi ilikuwa imepatwa na hitilafu na kwamba juhudi za kuizuia kuzama zilikuwa zinaendelea. Chanzo cha kugongana kwa meli hizo hakijabainika lakini kulikuwa na ukungu mwingi eneo hilo. Meli hiyo ya kijasusi iligonga meli yenye bendera ya Togo ambayo ilikuwa ikisafirisha mizigo, vyombo vya habari Uturuki vinasema. Waziri mkuu wa Uturuki Binali Yildirim amezungumza na mwenzake wa Urusi Dmitry Medvedev, na kumueleza masikitiko na huzuni yake kutokana na ajali hiyo, duru katika afisi ya waziri mkuu huyo wa Uturuki zimenukuliwa na shirika la habari la Reuters. Kundi la Meli za Urusi Bahari Nyeusi (BSF) hupitia m...

Wakorea Kusini: Hatutaki Marekani iweke ngao yake ya makombora nchini kwetu

Image
Wakorea Kusini: Hatutaki Marekani iweke ngao yake ya makombora nchini kwetu Raia wa Korea Kusini wamefanya maandamano kulalamikia uamuzi wa serikali wa kukubali kuweka ngao ya makombora ya THAAD katika ardhi ya nchi hiyo. Maandamano hayo yameshuhudiwa katika kaunti ya Seongju, kusini mashariki mwa Korea Kusini ambapo waandamanaji hao wameunda mnyororo wa mshikano wa watu wenye urefu wa kilometa mbili na mita 600, kuonyesha upinzani wao juu ya uamuzi wa Marekani wa kuweka ngao hiyo ya makombora katika mji huo. Washiriki wa mnyororo huo wa mshikano wa watu, sambamba na kutoa nara za kupinga hatua hiyo ya Washington, wamelalamikia uamuzi wa serikali ya Seoul ya kuridhia kuwekwa ngao hiyo karibu na makazi ya raia. Ngao ya makombora ya THAAD Maandamano hayo ya sasa ya kupinga uwekaji ngao ya makombora ya THAAD  kwa kimombo "Terminal High Altitude Area Defense" ambayo imetajwa kuwa na madhara mbalimbali ya kimwili na kwa kilimo, yameifanya serikali ya Ko...

KWA NINI HUPASWI KUPUUZIA KIKOHOZI

Image
KWA NINI HUPASWI KUPUUZIA KIKOHOZI Kukohoa ni njia inayotumiwa na mwili ili kuhakikisha kwamba njia au mfumo wa upumuaji katika mwili wako unakuwa salama, na hii ni kwa kuhakikisha kwamba vitu kama vumbi, bacteria au kitu chochote kile kisichokuwa salama, basi hakipati nafasi ya kukudhuru wewe kupitia njia ya upumuaji. Pamoja na kikohozi kuwa njia ya mwili kujilinda, bado unapaswa kuchukua hatua za kupata matibabu zaidi endapo tatizo hili litakuwa endelevu hata zaidi ya wiki moja baada ya kutumia njia tofauti tofauti za kujitibu au kutumia dawa rahisi zinazopatikana katika mazingira ya nyumbani (mfano tangawizi au kitunguu saumu). Mpenzi msomaji, wewe binafsi unafahamu tatizo la kikohozi unalipa uzito gani, ila ningependa kukufahamisha baadhi ya madhara ambayo huweza kumpata mtu endapo atapuuzia tatizo hili: Kwanza kabisa utakubaliana na mimi kwamba, endapo mtu anakohoa, basi inamuwia vigumu kuyanyoosha maelezo yake au hawezi kuongea katika mtiririko wa maneno ulio ...

Haya Sasa ni Maajabu ya Dunia, Cheki Binti Darasa la 7 Aota Matiti Manne!!!

Image
Haya Sasa ni Maajabu ya Dunia, Cheki Binti Darasa la 7 Aota Matiti Manne!!! April 27, 2017   Hussein S. Omary Ukistaajabu ya Musa utayaona ya Firauni! Hivyo ndivyo unavyoweza kusema kufuatia familia moja kukumbwa na mauzauza baada ya watoto wa mama aliyefahamika kwa jina la Hawa Hassan Ngonyani kupatwa na mabadiliko ya maumbile ambapo mmoja ameota matiti na mwingine kuanza kuotwa na uvimbe shingoni. Hawa anaishi na wanaye watatu maeneo ya Kinzudi Kata ya Goba, jijini Dar ambapo waandishi wetu walifika na kujionea hali halisi ya watoto hao. Mara baada ya waandishi wetu kufika katika nyumba hiyo, walipokelewa na Hawa aliyeonekana kukata tamaa ya maisha kutokana na jinsi anavyoishi kwa malumbano na mumewe anayedaiwa kuitelekeza familia yake. Akizungumza na mwandishi wetu nyumbani hapo, Hawa alisema aliolewa ndoa ya mkeka miaka kadhaa iliyopita huku mwanaume akimzalisha ‘fastafasta’. Alisema mwanaye mwenye umri wa miaka kumi na mbili anayesoma darasa la saba katika Shule...