Haya Sasa ni Maajabu ya Dunia, Cheki Binti Darasa la 7 Aota Matiti Manne!!!

Haya Sasa ni Maajabu ya Dunia, Cheki Binti Darasa la 7 Aota Matiti Manne!!!

Ukistaajabu ya Musa utayaona ya Firauni! Hivyo ndivyo unavyoweza kusema kufuatia familia moja kukumbwa na mauzauza baada ya watoto wa mama aliyefahamika kwa jina la Hawa Hassan Ngonyani kupatwa na mabadiliko ya maumbile ambapo mmoja ameota matiti na mwingine kuanza kuotwa na uvimbe shingoni.
Hawa anaishi na wanaye watatu maeneo ya Kinzudi Kata ya Goba, jijini Dar ambapo waandishi wetu walifika na kujionea hali halisi ya watoto hao.
Mara baada ya waandishi wetu kufika katika nyumba hiyo, walipokelewa na Hawa aliyeonekana kukata tamaa ya maisha kutokana na jinsi anavyoishi kwa malumbano na mumewe anayedaiwa kuitelekeza familia yake.
Akizungumza na mwandishi wetu nyumbani hapo, Hawa alisema aliolewa ndoa ya mkeka miaka kadhaa iliyopita huku mwanaume akimzalisha ‘fastafasta’.
Alisema mwanaye mwenye umri wa miaka kumi na mbili anayesoma darasa la saba katika Shule ya Msingi Kinzudi, alizaliwa mzima huku akiwa na chuchu mbili tu hadi mwaka jana mwanzoni ndipo alipokumbwa na balaa hilo la kuota chuchu zingine sehemu za juu ya titi za kawaida ambazo hadi sasa zinazidi kukua siku hadi siku.

Comments

Popular posts from this blog

HIZI HAPA SMS TAMU ZA KUMTAKIA USIKU MWEMA MPENZI WAKO

SMS na MESEJI 900+ za mapenzi

MIAKA 22 SASA TANGU KUZAMA KWA MELI KUBWA YA MV BUKOBA, TANZANI TUMEJIFUNZA NINI?