Posts

KUKOJOA KITANDANI/NOCTURNAL ENURESIS

Image
  Kukojoa kitandani ni moja ya matatizo yanayowakumba watoto wengi ambao wamefikia umri wa kuweza kudhibiti haja ndogo. Tatizo hili  pia liko miongoni mwa watu wazima wachache. Kukojoa kitandani ni moja kati ya mambo ambayo yanaweza kumfanya mtoto asifanye vizuri kimasomo na kukosa kujiamini mbele ya wenzake. Kwa wazazi wenye watoto wenye tatizo hili ambao umri wao ni chini ya miaka saba wasiumize kichwa kwani watoto wanakuwa bado wanajifunza kudhibiti haja ndogo. Kukojoa kitandani kunawapata sana watoto wa kiume kuliko wa kike. Kwa watu wazima tatizo la kukojoa kitandani linasababisha matatizo kwenye jamii ikiwemo wachumba kuachana na baadhi ya ndoa kuvunjika kwa ajili ya kukosa uvumilivu na uelewa kuwa tatizo hili si makusudi ya muhusika na kuwa anahitaji kutiwa moyo na kusaidiwa. Kama tatizo litaendelea baada ya miaka saba basi mzazi anaweza kuanza kutafuta tiba ya tatizo. Tiba ni pamoja na kubadili mfumo wa maisha, kumfundisha mtoto namna ya kudhibiti haja ndog...

Dhima za fasihi linganishi

Fasihi linganishi ni ule ulinganishaji wa kazi mbili za kifasihi kutoka kwa mwandishi mmoja au kazi ya Jamii moja na nyingine. Ulinganishaji huu huhusu pia kulinganisha fani nyinginezo. Aisha ulinganishaji huweza kuongozwa na misingi ya ulinganishaji kama vile Historia Utamaduni Itikadi Falsafa Maswala ya kijinsia Dhamira Fani na kadhalika Ulinganishaji wa kazi za fasihi huweza kuwa na dhima zifuatazo -Kujua utamaduni, historian falsafa za Jamii nyinginezo -kuweza kuzigawa kazi za kifasihi katika makundi ya kitaifa, kiafrika. na kiulimwengu -Kujua ubora na udhaifu wa fasihi yako -Kujua mwego wa mwandishi -Kujifunza mbinu Mpya za uandishi -Kukuza taaluma ya tafsiri -Kujua chimbuko na maingiliano ya Jamii. www.masshele.blogspot.com

Mitazamo kuhusu fasihi simulizi ya Kiafrika

Dhana ya fasihi simulizi kwa mujibu wa Mlokozi (1996), ni fasihi inayotungwa au kubuniwa kichwani na kuwasilishwa kwa hadhira kwa njia ya mdomo na vitendo bila kutumia maandishi. Hivyo fasihi simulizi inafungamana na muktadha au mazingira fulani ya kijamii na kutawaliwa na mwingiliano wa mambo kama vile fanani, hadhira, fani, tukio, mahali pamoja na wakati wa utendaji. Ni aina ya fasihi ambayo hutumia mdomo katika kuumbwa, kuwasilishwa na kusambazwa kwa wasikilizaji na watumiaji wake (Balisidya, 1983). Fasili hizi zinasisitiza kwamba fasihi simulizi inategemea uwepo wa fanani, hadhira, jukwaa na mada. Hivyo kwa ujumla, tunaweza kusema kuwa fasihi simulizi ni sanaa inayotumia lugha kisanaa ili kufikisha ujumbe kwa hadhira iliyokusudiwa kwa njia ya mdomo au masimulizi. Nadharia ya fasihi simulizi ni mawazo yanayotoa mwongozo kuhusu mwelekeo wa jambo fulani katika fasihi simulizi. Kwa kufanya hivyo, nadharia hizo zimeweza kuleta mabadiliko katika nadharia asilia zilizokuwe...

Best of Diamond Platnumz Dj Mixtape (Greatest Hits)

Image
Mixtape Title :  Best of Diamond Platnumz Dj Mix Type : Tanzania  Bongo Flava Mixtape Description : This is  comupilation  Dj Mixtape of one Tanzania  best bongo flava artist  Diamond Platnumz,  best of Diamond Platnumz  mixtape is available  for download,  Mix contains of  popular Diamond  Platnumz Mp3 songs. He has had several  hit songs including  “Number One” which he  featured Nigerian artist Davido.  Diamond won numerous  awards at Channel O and  the HiPipo Music Awards.  Download and enjoy best of wasafi bongo mix download Diamond Platnumz Mixtape Number One by Diamond Platnumz Wangu by Diamond Platnumz Hallelujah by Diamond Platnumz Amanda by Diamond Platnumz Jibebe by Diamond Platnumz African Beauty by Diamond Platnumz Marry You by Diamond Platnumz Baila by Diamond Platnumz Poporopipo by Diam...

M-PESA MASTERCARD INAVYOWEZA KUBADILI BIASHARA YAKO

Image
-Unaweza kununua bidhaa yeyote mtandaoni ikiwa mahala popote ulimwenguni kwa kupitia M-pesa -Inakupatia card number pamoja na security code utakazo zitumia kufanya malipo mtandaoni -Utaweza kuweka fedha katika kadi yako na kufanya miamala kadiri upendavyo -Ni rahisi kutumia Hujambo ndugu msomaji,  Karibu tuangazie namna muunganiko wa mpesa na MasterCard unavyo weza kuinufaisha biashara yako. Maendeleo ya kiteknolojia ni ahueni katika nyanja zote, na hii sekta ya biashara haijaachwa nyuma katika suala hilo. Kupitia Mpesa master card unaweza kulipia na kutangaza bidhaa yako katika mitandao yenye wafikiaji wengi kama vile Facebook na Instagram hivyo itakuongezea Wateja wengi na wapya kutoka sehemu mbalimbali. Vilevile inakuwezesha kununua bidhaa mbalimbali kutoka maduka ya mtandaoni  ambayo yanapokea malipo ya MasterCard. Sio hivyo tu bali unaweza kupokea malipo ya bidhaa zako kupitia program hii rahisi. Licha ya hayo program hii ni rahisi sana kutumia, kama ili...

UGONJWA WA EBOLA

Image
  Ebora ni moja kati ya virusi 30 vinavyoweza kusababisha homa ya kutokwa na damu. Genusi ya kirusi cha ebola kwa sasa bado kimegawanyika katika makundi matano ambayo ni: Sudan Ebolavirus, Zaire eboravirus, taiforest(ivory coast) eboravirus, Reston ebora virus na bundibugyo Ebolavirus. Mlipuko wa ugonjwa wa kirusi cha Ebolavirus mwaka 2014 huko afrika magharibi ilihusisha kirusi cha Zaire Ebolavirus, ulikuwa mlipuko mkubwa sana katika historia ya ugonjwa huu duniani. NI vema kuangalia magonjwa ya milipuko kabla hujaenda baadhi ya nchi ili kujua hali ya usalama katika nchi hizo nazoenda Shirika la Chakula na madawa la Us food  lilipitisha vipimo viwili vya haraka kwa ajili utambuzi wa kirusi huyu kwenye damu na mkojo kwa mda wa saa moja tu kwenye baadhi ya hospitali na kuzipa uwezo wa kupima kipimo hicho, pia kipimo cha pili ni kile ambacho damu au mkojo hupimwa kwenye maabara maalumu na majibu hutoka kati ya masa...

Vipengele vya uhakiki wa ushairi

Shairi ni tungo ya kinudhumu inayoweza kuimbika au isiimbike yenye lengo Fulani miongoni mwa kazi za kifasihi kama vile, kufikisha ujumbe Fulani, kuonya, kuburudisha n.k. shairi nilazima liwe na mguzo wa moyo. Tunazo aina mbili za ushairi, ushairi ule unaofuata urari wa vina na mizani na ule ushairi ambao unazingatia au kutozingatia urari wa vina na mizani. Kimajina tunaweza kuita ushairi wa kimapokeo na ushairi wa kisasa. Vipengele. i . Muundo ii. Mtindo iii. Lugha iv. Usambamba v. Rithimu Vi. Mchomozo