Posts

MOTIFU YA SAFARI ,

Image
MOTIFU YA SAFARI By Glory mushy MOTIFU YA SAFARI NA MSAKO KAMA MWEGA MKUU WA DHAMIRA KATIKA “MARIMBA YA MAJALIWA” “Marimba ya Majaliwa ni hadithi iloyoandikwa na Edwini Semzaba mwaka (2008) ambayo inaelezea kuhusiana na marimba ya Majaliwa iliyopotea. Mwandishi ameonyesha jinsi Majaliwa alivyokuwa anatafuta marimba yake mpaka akaipata. Majaliwa alisafiri kwa kutumia njia mbalimbali kama vile ungo, fagio, na maumbo ya samaki akizunguka Tanzania nzima akisaka marimba ya nyuzi ishirini (20). Alianza Mafia, akaenda Zanzibar, Tanga, Moshi na Arusha, Iringa, Mwanza, Kigoma, na miji mingine mingi. Na Kongoti bingwa wa Taifa wa Marimba akimchenga kila mara huku akinga’nga’nia Marimba ya Majaliwa ili amzuie kushinda na ashinde yeye na bila Marimba yenye nyuzi ishirini (20) hakuna ushindi. Katika mada hii tutaanza kuelezea maana ya fasihi, fasihi ya watoto, na maana ya motifu, na maaana ya dhamira. Kisha katika kiini cha swali letu tutachambua motifu mbalimbali...

MIX BREAKING: Rais Magufuli kateua Mkuu mpya wa Majeshi Tanzania anaechukua nafasi ya Mwamunyange

Image
Inatokea IKULU Dar es salaam ambapo Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli amefanya utauzi wa Mkuu mpya wa majeshi ya ulinzi na usalama Tanzania kama inavyosomeka kwenye hii taarifa hapa chini. Aliyeteuliwa kuchukua nafasi ya Davis Mwamunyange ni Venance S. Mabeyo ambapo pamoja na kuteuliwakuwa mkuu wa majeshi ya ulinzi Tanzania Mabeyo amepandishwa cheo na kuwa Jenerali. Jenerali Venance anachukua nafasi ya Jenerali Davis Mwamunyange ambaye amestaafu ambapo kitu kingine cha kufahamu ni kwamba Rais Magufuli amemteua Meja Jenerali James M. Mwakibolwa kuwa Mnadhimu mkuu wa majeshi ya ulinzi Tanzania. Pamoja na kuteuliwa kuwa Mnadhimu mkuu wa Majeshi ya ulinzi Tanzania, Meja Jenerali James Mwakibolwa amepandishwa cheo na kuwa Luteni Jenerali ambapo anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Jenerali Venance aliyeteuliwa kuwa mkuu wa majeshi. Uteuzi huu unaanza mara moja ambapo tarehe ya kuapishwa itatangazwa baadae.

Nafasi za kazi Maabara

Image
Serikali inatarajia kuajiri Fundi Sanifu wa Maabara ya Shule Daraja la II. Ajira hii ni kwa Fundi Sanifu wa Maabara ya Shule waliohitimu kati ya mwaka 2013 - 2015. Hivyo, wenye sifa stahiki na wanaotaka kuajiriwa Serikalini, wanatangaziwa kuwasilisha nakala za vyeti vyao vya: Elimu ya Sekondari (Kidato cha nne na / au Sita); Taaluma ya Fundi Sanifu wa Maabara ya Shule na Cheti cha kuzaliwa kwa ajili ya uhakiki. Aidha, mwombaji aambatishe nakala ya wasifu binafsi (CV) ya Elimu, Taaluma na Uzoefu. Mwombaji aainishe majina yake matatu kwa kirefu na usahihi. Mwombaji ambaye katika vyeti vyake vya Elimu na Taaluma havina jina la tatu, akamilishe taratibu za kisheria kuongeza jina la tatu na kuwasilisha kiapo stahiki pamoja na maombi yake. Nyaraka zote ziwasilishwe kwa barua pepe ifuatayo: apa@moe.go.tz SIFA ZA MWOMBAJI Mwombaji awe na cheti cha Kidato cha IV au Kidato cha VI katika masomo ya Sayansi na waliofuzu Mafunzo ya Laboratory Technology au Laboratory Science and Technology katika ...

Shocking news !!!!

Image
Murder in school kenya Shocking News; Pupil Beaten To Death For Failing To Read English.  A ten year old girl has died after she was allegedly beaten in school by the deputy headteacher and some pupils for not being able to read loudly an

Wadau waendelea kuonesha masikitiko baada ya mwanafunzi huyu kufukuzwa katika chuo kikuu cha Dar es salaam

Image
BY Erick Mwakikato Imeniuma sana,Imeniumiza Na kunisikitisha hii Taharifa..!! Sina Mengi Ya Kuandika Ila Naimani MUNGU yuko pamoja nawe atakusimamia na kukupigania....Akuna Kiumbe Chenye Nguvu ya Mamlaka Chini ya Jua Kuzidi MUNGU . USIFE MOYO MKUU Alphonce Lusako ...Usichoke Pambania Unachokiamini....Utashinda!!!! Utashinda!!! Utashinda!!! By Davis Betram Nabii Jr !Making a great changes can be a scary but not scary as to regret. What we want to see in Tanzania, creating a fair and just Government for the future generation to be in safe place. My comrade my brother Mpambanaji Alphonce Lusako be strong due to the situation you face now but God he knows what we want for our Country and he will bless in our movements always. At whatever cost needed but for the Fair and Just future Tanzania (Tanzanian) we must fight💪💪 From your young comrade and brother Tsnp coordinator in Ruvuma, Mbeya, Iringa and Njombe Davis Betram Akwangajikason By Ndeke Wa Ndeke Najua unajiamini na kuamini maono y...

KITENDO CHA KUFUKUZWA KWA MWANAFUNZI HUYU WA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM CHAENDELEA KULAANIWA KILA KONA

Image
Alphonce Lusako kwaheri mpambanaji. Ulifukuzwa mwaka 2011 ukiwa mwaka wa 3, Kwa kutambua umuhimu wa elimu ukaamua kurudi chuo kuendelea na masomo yako kwa kuanza mwaka wa kwanza sheria 2016, lakini leo baada ya kutoka kwenye mtihani umekutana na barua ikikutaka uondoke chuo haraka kwa sababu kuwa ulisajiliwa kimakosa. Inauma sana lakini ndio gharama halisi ya harakati za kujitoa kwajili ya wengine. ALUTA CONTINUA  BY Malisa GJ Nimesikitika kupata habari za Ndugu.Alphonce Lusako mwanafunzi wa UDSM aliyefukuzwa mara mbili chuoni hapo. Mwaka 2011 akiwa mwaka wa 3, (ambao ni mwaka wa mwisho wa masomo) alifukuzwa chuoni hapo kwa madai ya kuchochea mgomo. Kwa maelezo niliyopata ni kuwa hoja zake zilikua mbili. Mosi TCU inadahili wanafunzi hewa, pili Bodu ya mikopo inafanya ubadhirifu wa pesa za wanafunzi. Madai haya yakaonekana ni uchochezi na akafukuzwa chuo akiwa mwaka wa mwisho. Akakaa mtaani miaka 6, bila kupewa barua ya kumuita tena chuoni. Mwaka jana akaamua kuomba tena naf...

Hii ndio timu mpya ya Okwi kwa sasa

Image
Mshambuliaji Emmanuel Arnold Okwi amejiunga na klabu yake ya zamani ya SC Villa ya nchini kwao Uganda baada ya kuachana na klabu ya Denmark SønderjyskE. Mshambuliaji huyo aliyeanza kucheza soka katika klabu hiyo ya Villa anarudi kwa mkataba mfupi ambapo atacheza kwenye klabu hiyo maarufu kama Jogoos mpaka mwisho wa msimu. “Ni dili ambalo limeshakamilika”, Alisema Mkurugenzi Mkuu wa klabu hiyo ya Villa, Ivan Kakembo Okwi ambaye aliachana na Villa kujiunga na Simba mwaka 2010 ataungana na wachezaji wengine wapya klabuni hapo ambao ni Sulaiman Luzige, Arthur Arakaza na Farouk Musisi. Emanuel Okwi