Posts

KUVIMBA KWA MISHIPA YA DAMU WAKATI WA UJAUZITO (VARICOSE VEINS)

Image
Kuvimba kwa mishipa ya damu(Varicose veins) hasa miguuni ni kitu kinachowatokea mama wajawazito walio wengi.Tatizo hili mara nyingi hutokea wakati mimba imekua kubwa kuanzia miezi 8 hadi 9 japo kwa baadhi ya watu hali hii huweza kutokea katika umri mdogo. Mishipa hii huvimba na inaweza kuonekana kwenye ngozi kama Mistari iliyovimba kwenye ngozi isiyoinyooka yenye rangi inaelekea kuwa kama blue. Watu wanopata ujauzito katika umri mkubwa ndio wanakua kwenye hatari kubwa ya kutokewa na hali hii,pia watu wenye uzito kupita kiasi (wanene sana) wanakua kwenye hatari ya kukumbwa na hali hiii. Hizi varicose veins zinatokea sana miguuni,ila zinaweza kutokea maeneo mengine kama kwenye uke na shingo ya kizazi,zinapotokea maeneo haya mama hutokwa na majimaji ukeni yaliyochanganyikana na damu. Varicose veins zinapotokea sehemu ya haja kubwa ndio tunaiita Bawasiri (Haemorrhoids) DALILI ZA TATIZO HILI Mistari myembamba yenye rangi ya blue inayoonekana kwenye ngozi Uvimbe kwenye ngozi ambao...

TATIZO LA WANAWAKE KUOTA NDEVU NA MANYOYA(HIRSUTISM)

Image
 Naam ni jambo la kumshukuru Allah kuiona siku mpya kila siku haijalishi unaumwa ama una magumu unapitia USITAMANI KUFA KWANI KILA TATIZO LINA SULUHISHO LAKE hivyo mshukuru Allah kwa kila kitu katika maisha yako Ama baada ya salam Leo ni vyema tukapata darasa kuhusiana na kichwa cha habari hapo juu HIRSUTISM NI NINI? Ni ugonjwa ambao wanawake hupatwa na mabadiliko ya  kuotwa manyoya sehemu ambazo kikawaida wao hua hawaoti manyoya maeneo hayo mfano ndevu kidevuni, manyoya kifuani, usoni, na mgongoni wakati mwingine manyoya magumu kama ya kiume miguuni na mikononi Kikawaida wingi wa manyoya mwilini mwa binadamu hutegemea sana vimelea vya ukoo husika, kitaalamu kama genetics make up lakini mwanamke anapokua na manyoya mengi kama ya mwanaume hasa ndevu kuna mambo makuu mawili kwamba anaumwa au ukoo wake uko hivyo japokua waathirika wengi wa shida hii ni wagonjwa DALILI ZA HIRSUTISM Kawaida gonjwa wa hirsutism huwa na dalili za kua na manyoya mengi kama nilivyotaja hap...

Msichana ajiua baada ya kukosea kutuma meseji

Image
Binti mmoja nchini Uingereza mwenye umri wa miaka 17, Charlotte Guy, 17, ameamua kujiua baada ya kukosea kutuma meseji na kwenda kwa mpenzi wake badala ya rafiki yake. Charlote ambaye alikuwa akimtumia rafiki yake meseji kwa kutumia snapchat akimwambia kuwa amelala na mwanaume mwengine, alikosea kutuma meseji hiyo na kwenda kwa mpenzi wake Jack Hurst  mwenye umri wa miaka 20. Watu wa karibu wa wawili hao wamesema kwamba baada ya kufanya hivyo alimtumia meseji ya kumuomba radhi Jack na kumuaga ikisema ..”Kwa heri, tafadhali nisamehe, nakupenda, lakini kujua kuwa unanichukia inatosha”. Baada ya hapo Jack alianza kumtafuta kwenye simu mpenzi wake huyo bila mafanikio na kuamua kuita polisi na kwenda chuoni kwao kumtafuta, na kukuta amejinyonga karibu na eneo la chuo alichokuwa akisomea masuala ya afya.

Giroud to Chelsea?

Image
Chelsea has now turned attention towards Arsenal striker Olivier Giroud. Why the need for a new striker? Antonio Conte is scouring the transfer market to find a second choice striker ahead of Michy Batshuayi. The Belgian has fallen out of favour with Conte and is also being linked with multiple European clubs. Batshuayi has racked up a decent tally of 10 goals in 24 appearances this season but still cannot pick up second string minutes in the cup competitions. Alvaro Morata’s arrival to the Stamford Bridge has faced a shaky period in recent weeks. The Spaniard’s £58m price tag looked like a bargain when he started off the season in scintillating form netting the ball 9 times in the early stages of the campaign. But the tide has shifted and so has Morata’s run of form with the former Galactico missing out on clear-cut opportunities. While the fans at the Bridge are venting over their displeasure with the number nine, Conte is trying to find a replacement or at least a support f...

Kovacic to Man United?

Image
Manchester United is weighing up a move to bring Real Madrid midfielder Mateo Kovacic to Old Trafford. The Croatian international has fallen down the pecking order under Zinedine Zidane at the Bernabeu, and Jose Mourinho eyes up a potential bid for the 23-year-old. Why move? Kovacic has been restricted to just six appearances in the top-flight this season- starting just once - as he is forced to compete with the likes of Luka Modric, Toni Kroos, Casemiro and Isco. It is believed that he is desperate for first team chances, and is willing to leave the La Liga champions for regular football. Mourinho is understood to have identified the 38-cap international as a possible replacement for the retiring Michael Carrick, while Marouane Fellaini has just six months left on his deal.

KINGEREZA KINADUMAZA UBUNIFU NA UFANISI KATIKA TAIFA HILI.

Image
Makala Na: Jumaa H Heshima Sitoanza kwa salamu kama ilivyo kawaida ya kile kiitwacho ustaarabu wa Waswahili. Kimsingi hakuna ustaarabu wa Waswahili. Ustaarabu ni wa Waarabu ila tunazo amali tulizozisaliti kwa kuzinasibisha na Uarabu. Basi ya nini kuzibebesha amali zetu adhimu majina yanayozinyima Uafrika wake? Tutafute jina sahihi kuzirejelea amali hizi. Hasira za makala haya ni juu ya athari za "ukoloni lugha'' unavyonyonya na kufifisha ubunifu wa vijana wasomi wa taifa hili pendwa, Tanzania. Sote tunafahamu kuwa Kiswahili ni lugha ya taifa hili, Tanzania. Mwanazuoni mmoja katika kongamano la Kiswahili pale Chuo Kikuu cha Dar es Salaam aliuliza  swali; ``je, Kiswahili ni lugha ya taifa kikatiba au kimazoea?'' Ukumbi mzima ulitumbua macho pasi na kujibu. Sababu hakuna andiko lolote lile kwenye katiba wala sheria yoyote ile nchini humu inayoeleza na kuelekeza kuwa lugha yetu ya taifa  ni Kiswahili. Hii ni lugha ya taifa kimazoea ni si kimaan...

Umeme kukosekana Mbagala, Kurasini, Bandari

Image
  Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) limesema njia ya kusafirisha nishati hiyo ya Ilala -Kurasini itazimwa kwa muda kupisha matengenezo ya dharura. Taarifa ya Tanesco iliyotolewa leo Jumamosi Januari 27,2018 kwa wateja wa Mbagala, Kurasini na Bandari imesema njia hiyo itazimwa kwa muda wa saa tatu kuanzia saa nne asubuhi. Maeneo yatakayo athirika yametajwa kuwa ni yote ya Mbagala, Kurasini na Bandari. Tanesco imewatahadharisha wananchi kutoshika waya uliokatika.