Umeme kukosekana Mbagala, Kurasini, Bandari

Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) limesema njia ya kusafirisha nishati hiyo ya Ilala -Kurasini itazimwa kwa muda kupisha matengenezo ya dharura.

Taarifa ya Tanesco iliyotolewa leo Jumamosi Januari 27,2018 kwa wateja wa Mbagala, Kurasini na Bandari imesema njia hiyo itazimwa kwa muda wa saa tatu kuanzia saa nne asubuhi.

Maeneo yatakayo athirika yametajwa kuwa ni yote ya Mbagala, Kurasini na Bandari.

Tanesco imewatahadharisha wananchi kutoshika waya uliokatika.

Popular posts from this blog

HIZI HAPA SMS TAMU ZA KUMTAKIA USIKU MWEMA MPENZI WAKO

SMS na MESEJI 900+ za mapenzi

MIAKA 22 SASA TANGU KUZAMA KWA MELI KUBWA YA MV BUKOBA, TANZANI TUMEJIFUNZA NINI?