Posts

Showing posts from August, 2019

SIMBA YAUA 3-1 KAGERE HAKAMATIKI AWEKA MBILI

Image
MABINGWA watetezi, Simba SC wameanza vyema msimu mpya wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara baada ya ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya JKT Tanzania jioni ya leo Uwanja wa Uhuru mjini Dar es Salaam. Mshambuliaji wa kimataifa wa Rwanda, Meddi Kagere alikaribia kufunga hat trick katika mechi ya kwanza baada ya kufunga mabao mawili, huku lingine likifungwa na Miraj Athumani ‘Madenge’ aliyerejeshwa kikosini msimu huu. Kocha Mbelgiji, Patrick Aussems leo aliwaanzisha wachezaji wapta, Wabrazil Tairone Santos na Gerson Fraga kucheza pamoja safu ya ulinzi kwa mara ya kwanza tangu wasajiliwe Julai na wakafanya vizuri. Kagere aliye katika msimu wake wa pili Msimbazi tangu asajiliwe kutoka Gor Mahia ya Kenya, alifunga bao la kwanza sekunde ya 20 ya dakika ya kwanza akimalizia pasi ya kiungo Hassan Dilunga kabla ya kufunga la pili dakika ya 59 akimalizia pasi ya kiungo mwingine mzawa, Muzamil Yassin. Kagere alikaribia kukamilisha hat trick dakika ya 65 kama si shuti lake kugonga mwamba – lakini d...

Orodha ya Waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Tano, 2019 Awamu ya Pili

Image
Tangazo: Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Tano, 2019 Awamu ya Pili (Second Selection) Bonyeza hapa kufungua orodha ya  majina

Moto Msitu wa Amazon Brazil Waathiri Bonde la Kongo

Image
MOTO wa Amazon umeanza kusababisha matatizo ya kupumua kwa wananchi wa Brazil, huku Shirika la Kulinda mazingira  Greenpeace  likionya kwamba moto  huo pia unaharibu msitu wa Bonde la Kongo Barani Afrika. Shirika la Kimataifa la Ulinzi wa Mazingira  Greenpeace  limezitaka Serikali za mataifa yaliyo katika Bonde la Kongo kuchukua hatua zaidi kupambana na moto wa msitu wa Afrika ya Kati, katika wakati ambapo ulimwengu umeelekeza macho yake katika moto unaoteketeza msitu wa mvua wa  Amazon  huko  Brazil . Msitu ya Bonde la Kongo sehemu inayofunika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Gabon, Kongo-Brazzaville na Cameroon, msitu  unaoshika nafasi ya pili duniani baada ya msitu wa Amazon. Kama ilivyo kwa msitu wa Amazon, msitu wa bonde la Kongo unachangia kusafisha hewa chafu ya kaboni kwa kiasi kikubwa na ni njia muhimu kwa mujibu wa wataalamu ya kupambana na mabadiliko ya tabia ya nchi.

Ushahidi wa Sura Al Fiil, 105, Ayah ya 1-5, Maingiliano ya Waarabu na jamii za Afrika mashariki na dai la uchotara wa lugha ya kiswahili

Image
Masshele Kiswahili Waliokuja Zamani Kwakuwa Bahari ya Hindi ulikuwa njian rahisi sana ya mawasiliano watu mbalimbali walisafiri katika bahari hii toka karne na karne za zamani kutoka huko walikokuwa mpaka huku.  Yaaminika kuwa karne nyingi kabla ya kuzaliwa Yesu (Isah bin Marium) waashuri (Assyrians) Wafonisi (Phoenicians) wamisri  wakipindi kile cha mafirauni na mayahudi walifika pande mbalimbali za afrika mashariki na kuacha athari zao. Ikiwemo mimea na majengo. Na waarabu nao ntakwambia kuwa walikuwa na fungamano la kale  na ukanda Huu wa Afrika mashariki tangu zama za utukufu wa Ausan ile dola iliyostawi Arabuni  ya kusini nyakati za Marne ya saba kabla ya kusaliwa Masihi. Lakin ndugu mjifunzaji wa historia ya kiswahili kupitia mtandao Huu wa Masshele Swahili, haya yote yangali yakisubiri ithibati ya historia-chimbo (archaeology) Katika makala ya Noor Sharif, mtaalamu wa lugha na Sanaa kuhusu historia ya kiswahili anadai kuwa kulikuwa na uhusian...

Makala ya mediaeval Evidence for Swahili ya G.s.p.Freeman- Grenville na D.Phil , F.R.N.S

Image
Masshele swahili ASILI YA KISWAHILI: FREEMAN GENVILLE KATIKA “MEDIEVAL EVIDENCES FOR SWAHILI” Kwanza tutaangalia nini maana ya neno asili, pia tutaeleza kwa ufupi mitazamo mbalimbali kuhusu asili ya lugha ya Kiswahili, halafu tutaangalia kwa undani kiini cha mada yetu kwa kuchanganua vyema mawazo ya Freeman Grenville katika makala yake inayoitwa ‘Medieval Evidences for Swahili’ pia tutaonesha ubora pamoja na udhaifu wake na mwisho tutatoa hitimisho. Neno asili kwa mujibu wa Massamba na wenzake (1999:3) ni jinsi kitu au jambo lilivyotokea au lilivyoanza. Fasili hii ni nzuri na inajitosheleza kwa maana kwamba jambo au kitu kinaweza kutokea kibahati kama ilivyo katika lugha au linaweza kuanzishwa. Hivyo basi asili ya lugha ya kiswahili bado ni mjadala mrefu ambapo wataalamu mbalimbali wanahitilafiana juu ya asili au chimbuko la lugha ya kiswahili. Wapo wanaokinasibisha kiswahili na kiarabu kwa kutumia kigezo cha msamiati na dini ya kiislamu. Wengine wanashikilia kiswahili ni ...

Maendeleo yq kiswahili, Asili na historia ya lugha ya kiswahili

Image
Masshele Kiswahili -Asili ya kiswahili Asili ni chimbuko au namna kitu kinavuoanza. Kwa hiyo Asili ya kiswahili ni namna kiswahili kilivyoanza. Katika kuangalia historia hii kunanadharia mbalimbali zinazoelezea chimbukoa na asili ya lugha hii. -Kiswahili ni kiarabu Wapo wataalamu wanaodai lugha hii asili yake ni kiarabu. Na mkazo wao upo kuwa kiswahili kinayo maneno mengi ya kiarabu. Vile vile asili ya neno kiswahili linatokana na neno la kiarabu sahil lenye maana ya pwani. Hata hivyo hoja hii haina nguvu kutokana na kuwa kiswahili hakina maneno ya kiarabu pekeyake na kuwa ni tabia ya lugha kuazima maneno kutoka katika lugha nyingine. Chunguza etimolojia ya maneno  yafuatayo, Shule, bibo, skuli, na chai. 2. Kiswahili ni lugha chotara (pijini na kreoli) Mtazamo huu unaona kuwa kiswahili kimetokana na muunganiko wa waarabu na wabantu. Kwa mujibu wa profesa Noor Sharif, katika makala kiswahili kinawenyewe alitetea ukrioli wa kiswahili. Aisha somo hili litajadiliwa kw...

SWAHILI IDIOM, NAHAU ZA KISWAHILI NA MAANA

Kumpa mtu ukweli wake                  =>  Kumwambia mtu wazi [to be transparent] Pua kukaribiana kushikana na uso     =>  Kukunja uso kwa hasira [to express anger] Sina hali                                            => Sijiwezi  [I am helpless (mostly when talking about love)] Kupiga uvivu                                     => Kukaa tu bila kazi [abject laziness] Kupiga kubwa              ...

INASIKITISHA: Aishi bila ulimi kwa zaidi ya miaka mitano “nimeuza kila kitu kwenda India”(+video)

Image
Salim Mohamed mkazi wa Tuangoma DSM, anaishi bila ulimi kwa takribani miaka kadhaa sasa, Salim anasumbuliwa na kansa ambayo ilianza kama kipele mdomoni lakini kila baada ya muda kiliongezeka ukubwa na alipoenda Hospitali akaambiwa aende India. Japo ilikuwa ni kwa mbinde kutokana na hali ya kiuchumi lakini Salim alifanikiwa kwenda India na alikatwa ulimi na kuwekewa nyama iliyotolewa kwenye paja lakini baada ya kurejea Tanzania nyama ile nayo imeisha na sasa hana ulimi kabisa, limebakia shimo tu mdomoni. Bonyeza hapa chini kutazama mwanzo mwisho. credit AyoTv

AUDIO | Chemical - Najiskia | Download

Image
DOWNLOAD

Kuishi na mwenza siyo rahisi jipange!

Image
J UMAMOSI  nyingine tunakutana kwenye darasa la mahusiano. Maisha yetu hayawezi kwenda bila ya kuhusiana, lazima tushirikiane, tusaidizane katika mambo mbalimbali na mwisho wa siku tunatengeneza uhusiano mzuri.   Waswahili wanakuambia ili maisha ya mahusiano yawe mazuri lazima uwe na mtu sahihi ambaye atakuwa pamoja na wewe katika shida na raha. Atakayejua thamani yako wakati ambao upo na hata pale utakapokuwa haupo. Ndiyo maana leo ninakuja na mada kama inavyojieleza hapo juu. Kuwa na mahusiano ni jambo moja lakini kuwa na mahusiano yenye afya ni jambo lingine na ndiyo maana tunashuhudia watu wengi sana wanaingia na kutoka kwenye uhusiano. Hii inatokana na baadhi ya watu kutopenda kubeba udhaifu wa mwingine. Mtu anapokutana na mtu ambaye atamkwaza kidogo tu, akili yake inamu-ambia aingie mitini. Haoni sababu ya kubeba tatizo fulani kichwani kwake kwa muda mrefu. Ndugu zangu lazima tuelewe kwamba kwenye maisha ya uhusiano wanakutana watu wawili ambao wamekuwa...

VIDEO | Goodluck Gozbert - Nibadilishe

Image

AUDIO | Goodluck Gozbert - Nibadilishe | Download

Image
DOWNLOAD

UDSM MAIN CUMPUS, MUCE, DUCE, 2019/2020 MAJINA YOTE HAYA HAPA

Wote waliochaguliwa kujiunga na chuo kikuu cha Dar es salaam na cumpus zake zote majina haya HAPA

WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM KOZI MBALIMBALI 2019/2020

Image
Bofya HAPA KUPAKUA MAJINA

Familia Yapinga Mahakamani Wosia wa Mengi, Mazito Yaibuka!

Image
FAMILIA ya aliyekuwa Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP Limited, Marehemu Dkt. Reginald Mengi imewasilisha pingamizi katika Mahakama Kuu, ikipinga wosia wa Mengi aliouandika kabla ya kifo chake ukiwa na maelekezo ya mgao wa mirathi na mali za zake. Katika pingamizi hilo ambalo limetolewa na mdogo wa marehemu Mengi, Benjamin Mengi baada ya tangazo kutoka kwenye gazeti la Daily News la Julai 30, 2019, na wosia huo kuwasilishwa mahakamani hapo, Benjamin amedai kwamba, wakati kaka yake, Dkt. Mengi akiandika wosia huo alikuwa amechanganyikiwa. Kesi kiyo ya mirathi namba 39, ya mwaka 2019 imepangwa kusikilizwa Septemba 16, 2019 na Jaji Josi Myambina. Upande wa pingamizi unaongozwa na Wakili Nikael Tenga huku upande wa usimamizi wa mirathi ukiongozwa na wakili Elisa Msuya. Aidha, Makama hiyo imewaamuru waliowasilisha pingamizi hilo kuwasilisha ushahidi Mahakamani hapo kabla ya Agosti 28, mwaka huu. Katika wosia aliouandika Dkt. Mengi Agosti 17, 2017 umewataja wasimami...