Posts

Showing posts from November, 2018

PICHA 6 MUONEKANO WA MAKTABA YA KISASA UDSM

Image
Majengo mbalimbali ya Maktaba ya Kisasa ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambayo imefunguliwa jana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli. Maktaba hio ina uwezo wa kuchukua Wanafunzi 2100 kwa wakati mmoja na uwezo wa kuhifadhi vitabu 800,000 

MBABANE LAZIMA AFE LEO

Image
Ofisa habari wa timu ya Simba, Haji Manara amesema kuwa mashabiki na watanzania wote kwa ujumla waungane leo kuishangilia timu ya Simba itakapocheza na Mbabane Swallows kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika. Manara amesema wamejipanga kuhakikisha wana wapa furaha watanzania na mashabiki na kocha ameahidi kufanya makubwa pamoja na wachezaji na kitashushwa kikosi makini. "Tunajua kazi kubwa ambayo tunatakiwa kufanya na tutasimamia kwa vitendo hasa mashindano haya ya kimataifa, mashabiki watupe sapoti na tuweze kupeperusha bendera ya taifa. "Mbinu ambazo kocha mkuu Patrick Aussems amezipanga ni kubwa na ameahidi ushindi nyumbani ili tuweze kupenya hatua ijayo, wachezaji wana morali kubwa watafanya kweli," alisema.

The MEDIA HISTORY IN TANZANIA HISTORIA YA VYOMBO VYA HABARI TANZANIA

Ingia kwenye link kuona na kupakua https://docdro.id/c3wTqsa

Ngoma ya asili ya wachagga

Image
WACHAGGA NA NGOMA YAO HII YA JADI/ASILI!!! Ni ngoma ya kabila la Wachagga kutoka katika Wilaya ya Arusha wakicheza ngoma ya Jadi/asili.....

Askofu wa Jimbo Katoliki la Bukoba Ataka Mashoga Wasitengwe

Image
Askofu wa Jimbo Katoliki la Bukoba mkoani Kagera, Desiderius Rwoma amekemea vitendo vya ushoga na kutaka wanaofanya dhambi hiyo wasitengwe na kubaguliwa badala yake wasaidiwe na kuonyeshwa ubaya wa wanachofanya. Amesema kumvumilia mkosefu yeyote haina maana ya kumuunga mkono na kuwa ushoga ni dhambi na laana na watu wenye tabia hiyo wanahitaji msaada wa matibabu na huduma za kisaikolojia. Katika mahubiri yake leo katika siku ya wanaume wa Jimbo Katoliki kwenye kanisa la Bikra Maria Mama wa Huruma, Askofu Rwoma ametaka uwepo wa sheria za kudhibiti vitendo vya ushoga

Changamoto za tafsiri ya Kiswahili kwenye Google

  05:18 06:51 Je, unautegemea mtandao wa Google kufanya tafsiri kutoka lugha moja ya kigeni kuja kwenye Kiswahili? Unauamini kiasi gani? Dk. Hadija Jilala wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania anazungumza na Mohammed Khelef kwenye wasaa huu wa Kiswahili Kina Wenyewe juu ya changamoto za tafsiri ya Google kwa watumiaji wa Kiswahili.

HISTORIA YA BIBI TITI MOHAMED

Image
Bibi Titi Mohamed Historia ya Bibi titi mohamed -mwanamke shujaa na mwanaharakati wa ukombozi wa Tanganyika BIBI Titi Mohammed alizaliwa juni mwaka 1926 ,Dar es salaam, katika harakati zake za kuwakomboa wanawake ,Bibi Titi alikaririwa siku moja akisema; " Dhumuni langu kubwa ni kuhakikisha naamsha akili za wanawake waliolala na kubadilisha fikra na mitazamo yao na kuwaaminisha kwamba Uhuru wa Tanganyika utapatikana kama wanawake watajitambua". Kumbukumbu pekee tulinayo ya Mwanaharakati huyu katika taifa letu ni mtaa na Barabara ya Bibi Titi iliyopo Dar es salaam, Kihistoria Bibi Titi Mohammed aliingia katika siasa kwa kushawishiwa na Schneider Plantan ,akapewa kadi namba 16 ,na mumewe bwana Boi Selemani alipewa kadi namba 15.( Bibi Titi Mohammed aliolewa akiwa na umri wa miaka 13) Alikuwa muasisi wa Umoja wa wanawake Tanganyika (UWT) uliokuja kuundwa rasmi Mwaka 1963, wakati wa harakati za kupigania Uhuru alisimamia vikundi vya muziki kama vile " ...