Posts

Showing posts from March, 2018

TANGA RAHA SEHEMU YA 45

Image
AGE………………18+ WRITER…………EDDAZARIA G.MSULWA ILIPOISHIA Nikabaki nikiwa nipo kimya, kama nimemwagiwa maji ya baridi, swali la kwanza kujiuliza kichwani ni mbinu gani waliyo itumi hadi mimi leo nipo hai.Nikiwa ninaendelea kuliwazia ninalo liwaza nikamuona Olvia Hitler akiwa amesimama nyuma ya Rahma huku macho yake yakimwagikwa na machozi ya damu ENDELEA Nikabaki nikiwa nimeduwaa, pasipo kuzungumza kitu chochote, Olvie akaanza kutingisha kichwa taratibu huku machozi ya damu yakiendelea kumwagika kwa wingi, akauinua mkono wake mmoja na kuanza kuniita taratibu, hapa ndipo nilipoiona mkono wake ukiwa umejaa damu nyingi. “Walipo niambia kwamba umekufa, ikanilazimu kufanya kitu ambacho kingeurudisha uhai wako, kutokana sikuhitaji uweze kupotea kiurahisi maishani mwangu, wakati bado sijaisha nawe vya kutosha” Hata Rahma alicho kizungumza sikukitilia maanani kwa maani macho, na akili yangu zote zilikuwa zipo kwa Olvia aliye simama nyuma ya mke wangu Rahma.Olvia Hitler akaunyan...

Azam waitambia Mtibwa Sugar robo fainali ASFC

Image
Klabu ya soka ya Azam FC ‘Wanarambaramba’ wameitaja timu ya soka ya Mtibwa Sugar kuwa ni timu ngumu licha ya kushuka kiwango katika baadhi ya mechi za ligi kuu ambazo wamecheza hadi hivi sasa. Hayo yameelezwa na afisa habari wa Azam Jaffary Idd Maganga, wakati ambapo Azam inatarajiwa kushuka dimbani kuumana na Mtibwa Sugar katika mchezo wa Robo fainali ya Azam Sports Federations Cup siku ya Machi 31, 2018 katika uwanja wa Azam Complex, jijini Dar es Salaam. “Nitarudia kusema kwamba Mtibwa ni timu nzuri na ni timu ya ushindani, na ni timu ambayo msimu huu ilianza vizuri kwenye ligi lakini kushuka kwao kwenye msimamo wa ligi hakutufanyi sisi kubweteka na kuiona kuwa ni timu ya kawaida,” amesema Maganga. Wachezaji wapo vizuri Aidha Maganga ameendelea kuweka wazi kuwa kurejea kwa wachezaji wao ambao walikuwa kwenye majukumu ya timu ya Taifa kumewasaidia kwa namna moja ama nyingine kuongeza morali ndani ya kikosi. “Wachezaji wapo vizuri, wachezaji ambao wanamejeruhi ni wawili tu ...

IDADI YA VIFO YAONGEZEKA AJALI YA WAKIMBIZI NGARA

Image
Baadhi ya wagonjwa wakiandaliwa kwa safari ya   Bugando Mwanza eneo la Uwanja wa ndege Ruganzo,wilayani    Ngara mkoani Kagera. Basi hilo Eneo la Ajali.   Ajali hiyo imetokea saa 10 jioni    katika mteremko    wenye kona kali wa mlima K9 barabara kuu ya Benaco –Ngara    ambapo Basi lilipoteza mfumo wa breki lenye namba za usajili T 331 DFV aina ya YUTONG Mali ya kampuni ya Lugano (Kampuni ya Mtipa Investment ) ya mkoani Kigoma liligonga Basi T 765 DLD aina ya TATA ambapo lilipoteza uelekeo na kusababisha Vifo na Wengine Kujeruhiwa. Afisa mwandamizi wa Shirika la kuhudumia wakimbizi UNHCR wilayani Ngara Bi. Irene Babu. Idadi ya vifo vya Wakimbizi waliopata ajali kwenye mteremko wenye kona kali wa K9 katika kijiji Kasharazi wilayani Ngara mkoani Kagera, imeongezeka na kufikia 8 baada ya wawili kufariki wakipatiwa matibabu katika Hospitali ya Murugwanza na mmoja katika hospitali ya Nyamiaga. Afisa Mwandamizi wa Shirik...

MALIMWENGU :.MAMA AJIFUNGUA MAPACHA WAWILI WENYE BABA TOFAUTI

Image
Katika hali ya kushangaza huko nchini Uganda, wanaume wawili na watu wengine wamejikuta kwenye mshangao baada ya kukuta wote wawili ni baba wazazi wa watoto wawili mapacha. Inaelezwa kuwa wanaume hao waliingia kwenye mgogoro siku za hivi karibuni kila mtu aking’ang’ania kuwa baba mzazi wa mapacha hao, na ndipo walipoamua kwenda hospitali ili kupima kipimo cha DNA. Hatahivyo matokea ya daktari yalionesha kuwa wanaume hao wote wawili ni baba halali wa mtoto mmoja wa mapacha hao, yaani kila mmoja ana mtoto mmoja kati ya mapacha hao. Inaeelezwa kuwa wanaume hao Joseph Baseka Sengendo, 25, na Patrick Ssegane, 30, wamezaa na Rashida Nakabugo, ambapo Sengendo anatajwa kuwa mume wa ndoa wa mwanamke huyo. Wanaume hao wanasemekana kuwa ni ndugu.

MAMBO SASA, SILAHA ILIYO MUUA AKWILINA BADO HAIJAJULIKANA TUNAENDELEA NA UCHUNGUZI

Image
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum jijni Dar es salaam, Lazaro Mambosasa, ameelezea hatua inayoendelea kuchukuliwa juu ya askari polisi sita waliokuwa wameshikiliwa kutokana na kifo cha mwanafunzi wa NIT Akwilina Akwilin, aliyeuawa kwa risasi mapema mwaka huu Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jijini Dar es salaam, Kamanda Mambosasa amesema polisi hao bado wapo kwenye uchunguzi kubaini ni nani anahusika, kwani mpaka sasa hakuna ushahidi wa moja kwa moja wa kuweza kumbaini. “Wale walipokamatwa tulieleza bayana kwamba upelelezi unafanyika ili kujua ni nani ambaye ametenda kosa lile, bado suala la upelezi linaendelea. "Yapo maelekezo yaliyotolewa ambayo tunaendelea kufuatilia ili kuja kubaini,  ikumbukwe silaha moja ambayo haijajulikana ni ipi ndio ilikwenda ikamgusa Akwilina , lakini kama ulivyojua askari walikuwa ni wengi lakini pia kulikuwa hakuna ushahidi kwamba yupi aliyekuwa ametenda hivyo, kwa hiyo uchunguzi bado unaendelea”, amesema Kamnda Mam...

WABUNGE SITA WAPATA AJALI MMOJA ALAZWA ICU

Image
Wabunge sita wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wamepata ajali ya gari jana usiku Machi 29, 2018 mkoani Morogoro wakati wakitokea Dodoma kuelekea Dar es Salaam. Baada ya kutokea ajali hiyo saa 2 usiku katika barabara kuu ya Morogoro-Dodoma eneo la Bwawani, wabunge hao waliumia maeneo mbalimbali ya miili yao na kukimbizwa hospitali ya Mkoa wa Morogoro. Wabunge hao ambao wote ni kutoka Zanzibar ni Haji Ameir Haji (Makunduchi), Khamis Ali Vuai (Mkwajuni), Bhagwanji Maganlal Meisuria (Chwaka), Makame Mashaka Foum (Kijini), Juma Othman Hija (Tumbatu). Mganga mfawidhi hospitali ya rufaa Mkoa wa Morogoro, Dk Rita Lyamuya amesema majeruhi hao walipokelewa saa 3 usiku na kupatiwa huduma za awali. "Jana tumepokea majeruhi sita walioumia sehemu mbalimbali na mmoja wao alilazimika kulazwa chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi wa karibu (ICU) lakini hali yake inaendelea vizuri,” amesema. “Leo asubuhi tayari tumewapa rufaa kwenda hospitali ya Taifa Muhimbili...

NJIA ZA UZAZI WA MPANGO,FAIDA NA HASARA ZAKE

Image
Hakuna kitu kizuri duniani kama mtoto, kuwa na mtoto wako ni kitu kizuri sana. Ila ni muhimu sana mtoto akija wakati muafaka na muda muafaka sio inakuwa surprise… Yes kuna surprise nzuri, ila surprise ya mimba wakati una kichanga cha miezi sita, duh! Hiyo ni balaa. Kwa nini ukumbwe na balaa wakati kuna njia rahisi ya kujipanga. Inafahamika zaidi kama nyota ya kijani, kwa ufupi ni uzazi wa mpango, hii inahusu walio kwenye ndoa na wasio kwenye ndoa, walianza kuzaa na ambao bado hawajaanza. Lazima wote tujipange, mtoto wa kwanza aje lini, wa pili aje lini na namba ya mwisho ni ngapi? Ni rahisi ukizijua njia za uzazi wa mpango! Njia za uzazi wa mpango ni nini?? Njia za uzazi wa mpango ni njia zinazopelekea kuchelewa, kutoa muda au kuzuia mimba. Kuna njia nyingi ambazo ni kwa wanawake na nyingine ni  kwa wanaume. Kwa ujumla kuna njia za aina mbili, barrier methods aka vizuizi na hormonal methods. Tofauti kubwa kati ya barrie methods na hormonal methods ni jinsi zinav...

wizara ya mambo ya nje yasisitiza Hakuna maandamano April 26

Image
Kumekuwa na taarifa kwenye mitandao ya kijamii zinazosambazwa na watu wasioitakia mema nchi, zinazotishia usalama wa raia na mali zao. Taarifa hizo zimewatia hofu baadhi ya raia wa kigeni na wanadiplomasia wanaofanya kazi na kuishi hapa nchini. Taarifa hizo zimekuwa zikidai kuwa kutakuwa na maandamano yatakayofanyika tarehe 26 Aprili 2018 na zinawaonya raia wa kigeni wasiende Zanzibar katika kipindi cha Sikukuu ya Pasaka na sherehe za Muungano kwa sababu za kiusalama. Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki inawahakikishia wanadiplomasia na raia wote wa kigeni wanaofanya kazi na kuishi nchini na wananchi kwa ujumla kuwa, waendelee na shughuli zao ikiwemo kusafari kutoka eneo moja kwenda jingine bila ya hofu yeyote kwa kuwa hakuna dalili zozote za uvunjifu wa amani, usalama na utulivu wa nchi.Vyombo vya usalama vipo makini vinatekeleza majukumu yake ipasavyo kuhakikisha kuwa matukio yote ya uhalifu yanadhibitiwa kabla ya kuleta madhara kwa umma....

AJALI YA BASI YAUA WATANO KAGERA

Image
Watu watano wamekufa na wengine kadhaa kujeruhiwa baada ya basi moja kati ya manane yaliyokuwa yakisafirisha wakimbizi kutoka kambi ya Nduta wilayani Kibondo mkoani Kigoma kuelekea nchini Burundi kupinduka. Ajali hiyo imetokea leo Machi 29,2018 katika Kijiji cha Kasharazi wilayani Ngara mkoani Kagera saa 10:00 jioni. Taarifa zinasema ajali imetokea eneo la K9 lenye mteremko na kona kali baada ya kupata hitilafu ya mfumo wa breki na kisha kuligonga lingine lililokuwa mbele na baadaye kupinduka. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Agustino Olomi akizungumzia ajali hiyo amesema miili ya waliofariki dunia bado haijatambuliwa pamoja na idadi ya majeruhi. Amesema waliofariki dunia ni wanawake watatu na wanaume wawili. Kati yao yupo mkazi wa Kasharazi aliyekuwa akiendesha baiskeli ambaye basi lilimwangukia. Mmoja kati ya madereva waliokuwa katika msafara huo, Raymond Revocatus amesema kila basi lilikuwa na wastani wa abiria 65. Baadhi ya majeruhi wamepelekwa k...

TANGA RAHA SEHEMU YA 44

Image
AGE………………18+ WRITER…………EDDAZARIA G.MSULWA ILIPOISHIA “Asante sana mke wangu” Nilizungumza huku nikimvuta karibu Rahma, na akakilaza kifua kichwa chake juu ya kifua changu “Ila mume wangu, ninasiri moja kubwa sana katika maisha yetu, ambayo inanisumbua sana kwenye kipindi chote cha maisha yangu” “SIRI.....!!, Siri gani?” ENDELEA “Nitakuambia tu mume wangu, subiri kwanza watu waondoke” “Hapana, naomba uniambie mke wangu” “Nitakuambia tu mume wangu, nakuomba uwe mvumilivu.Ngoja kwanza nikazungumza na hao watu nje, alafu nitarudi kukuambia” Nikamtazama Rahma kwa macho makali ya kumchunguza, akayakwepesha macho yake katika kunitazama usoni.Akanipiga busu la shavu na akatoka nje, nikajilaza kitandani huku amani ikiwa imenitoweka kwani sijui ni siri gani ambayo Rahma anataka kuniambia.Nikasikia kelele za watu wakishangilia kwa furaha, sikujua ni kitu gani ambacho Rahma alizungumza hadi kuwafanya watu kushangilia kwa furaha namna hii.Nikanyanyuka kitandani na kuanz...