IMG_4131
Baadhi ya wagonjwa wakiandaliwa kwa safari ya Bugando Mwanza eneo la Uwanja wa ndege Ruganzo,wilayani  Ngara mkoani Kagera.
29831194_1813052908734611_1275003936_o
Basi hilo Eneo la Ajali.

 Ajali hiyo imetokea saa 10 jioni  katika mteremko  wenye kona kali wa mlima K9 barabara kuu ya Benaco –Ngara  ambapo Basi lilipoteza mfumo wa breki lenye namba za usajili T 331 DFV aina ya YUTONG Mali ya kampuni ya Lugano (Kampuni ya Mtipa Investment ) ya mkoani Kigoma liligonga Basi T 765 DLD aina ya TATA ambapo lilipoteza uelekeo na kusababisha Vifo na Wengine Kujeruhiwa.
IMG_4060
Afisa mwandamizi wa Shirika la kuhudumia wakimbizi UNHCR wilayani Ngara Bi. Irene Babu.

Idadi ya vifo vya Wakimbizi waliopata ajali kwenye mteremko wenye kona kali wa K9 katika kijiji Kasharazi wilayani Ngara mkoani Kagera, imeongezeka na kufikia 8 baada ya wawili kufariki wakipatiwa matibabu katika Hospitali ya Murugwanza na mmoja katika hospitali ya Nyamiaga.

Afisa Mwandamizi wa Shirika la kuhudumia Wakimbizi UNHCR wilayani Ngara Bi. Irene Babuamesema kati ya hao Nane waliopoteza maisha, Sita ni Wakimbizi na Watanzania ni wawili ambapo kati ya hao Watanzania, mmoja mkazi wa Kasharazi aliyekuwa akiendesha baiskeli ambaye basi lilimwangukia na mwingine alikuwa Mfanyakazi wa Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM).
IMG_4168
Majeruhi wote waliopata rufaa wamekwishasafirishwa kwa ndege ya UNHCR kwenda hospitali ya Bugando kupitia uwanja wa ndege wa Ruganzo uliopo wilayani Ngara
kagera-4
Mganga Mkuu wa Hospitali ya Murugwanza ya Wilayani NgaraDr. Remmy Andrew amesema katika Hospitali hiyo alipokea Majeruhi 65 kati yao 30 ni Wanawake na 35 ni Wanaume na kwamba waliotibiwa na kuruhusiwa ni 40 na waliopatiwa rufaa kwenda Hospitali ya Bugando ni 7

Aidha Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Nyamiaga Dr. Simon Kyamwenge amesema Hospitali hiyo ilipokea Majeruhi 31 kati yao Wanaume ni 24 na Wanawake 7 na kwamba mpaka sasa ameruhusiwa mtu mmoja pekee.

Pia Dr. Kyamwenge amesema Majeruhi 12 wenye hali mbaya wamepewa rufaa ya kupelekwa katika Hospitali ya Bugando Jijini Mwanza kwa matibabu zaidi.