Posts

Showing posts from September, 2017

Mbinu za Kupata Mtaji wa Biashara

Image
Watu wengi wanatamani kumiliki biashara siku moja na huenda wana mipango mizuri juu ya bishara zao. Mipango hii inaweza ikawa vichwani tu au mingine katika maadishi lakini inapofika wakati wa utekelezaji wa mipango hii ukosefu wa mtaji wa biashara hiyo ni kipingamizi kwa wengi. Lakini kuna jinsi kadhaa ambazo zinaweza kusaidia upatikanaji wa mitaji kwajili ya biashara.  Aina Za Mitaji Kuna aina mbili ya mitaji kwaajili ya biashara au uwekezaji wa aina yoyote. Mtaji wa Mkopo Mtaji wa Mmiliki  Mtaji wa Mkopo unakuwezesha kukopa toka kwa taasisi za fedha au mtu binafsi wakiwemo ndugu ,jamaa na marafiki na kuhitajika kulipa katika kipindi maalumu ikiwa pamoja na riba au bila riba. Aina hii ya mtaji inakuwezesha kufanya biashara lakini ni lazima uwe makini katika utunzaji wa fedha zako na uzalishaji wake kwani mwishowe utahitajika kurudisha fedha zote pamoja na riba pengine kila mwezi.  Mtaji wa Mmiliki ni mtaji toka kwa mtu au kampuni ambayo inahitaji kuwa...

Teknolojia: Roketi kuanza kusafirisha abiria duniani

Image
Teknolojia mpya inayotengenezwa na mwanateknolojia na mfanyabiashara maarufu Elon Musk inategemewa kuweza usafiri kutoka mji mmoja kwenda mwingine kwa kutumia roketi kwa dakika chache tu. Moja kati ya safari hizo imetajwa kuwa ni ile ya kutoka London Uingereza hadi New York Marekani kwa kutumia dakika 29 tu. Musk ameeleza pia kuwa kufikia mwaka 2024, ataanza kuwasafirisha watu hadi sayari ya Mars na Kampuni yake ya SpaceX itaanza kujenga meli za kipekee zitakazofanikisha mambo haya ifikapo mwaka ujao.

Diamond kaweka rekodi East Africa ndani ya saa 16

Image
Diamond amevunja rekodi ya Alikiba ambaye alikuwa msanii wa kwanza East Africa kupata views milioni moja kwa saa chache, So Diamond anakuwa msanii wa kwanza Easta Africa video yake kupata views milioni 1 Youtube chini ya masaa 20 toka iachiwe YouTube .

KWIKWI HUSABABISHWA NA NINI? |FAHAMU JINSI YA KUZUIA KWIKWI

Image
Baada ya kusoma makala inayohusu kijana mmoja aliyesumbuliwa na kwikwi kwa zaidi ya miaka miwili na nusu, na baadaye kutibiwa tatizo hilo kwa kufanyiwa upasuaji wa ubongo na kutolewa tezi, nimeamua leo nizungumzie kwikwi. Kwiki ni kitendo kisichozuilika ambacho hutokana na kusinyaa kwa kuta za kiwambo cha moyo au diaphragm. Kwa kawaida kwikwi ni kitendo kinachojirudia rudia mara nyingi. Sauti ya 'hic' inayotokea wakati unapokuwa na kwikwi husababishwa na kidaka tonge (epiglottis)  ambacho hufunga haraka wakati hewa inapoingia kwenye koo. Kupiga kwikwi kwa kawaida hakuna maumivu lakini mara nyingine husumbua hasa inapoendelea kwa muda mrefu. Kwikwi ya kawaida huweza kutulizwa kwa kunywa maji, lakini wakati mwingine kufanya hivyo hakusaidii. Zifutazo ni sababu zinazoweza kukuletea kwikwi 1. Kula kwa haraka. 2. Kula chakula cha moto na kunywa maji baridi baada yake. 3. Kulia au kukasirika. 4. Kula chakula chenye viungo vingi au pilipili. 5. Kula chakula cha moto ...

MATATIZO YA KIAFYA KWA WATOTO NA JINSI YA KUKABILIANA NAYO.

Image
Wakati mwingine, pamoja na juhudi zetu nzuri za kuzuia magonjwa, watoto huugua. Ugonjwa kwa mtoto unaweza kuzidi au kuongezeka haraka. Ni muhimu kugundua dalili za ugonjwa mapema na kuushughulikia mara moja.   Dalili za hatari Mtoto mwenye dalili mojawapo zifuatazo anahitaji matibabu haraka na uangalizi wakati wote. Akipatiwa huduma, anaweza taratibu kupata nafuu. Kama ana dalili zifuatazo zaidi ya moja, au iwapo dalili yoyote itazidi kuwa mbaya, mtoto yu hatarini:   Kupungukiwa na maji mwilini.  Kukosa mkojo, mdomo kukauka, au utosi kwenye kichwa cha mtoto kubonyea ndani ni dalili za kupungukiwa na maji mwilini-tatizo linalotishia uhai wa mtoto. Angalia chini -sehemu ya kupungukiwa na maji.   Mashambulio. Mashambulio ya ghafla kwa mtoto ambayo hujumuisha kupoteza fahamu na kurusha maungo ya mwili au kutetemeka- kawaida huambatana na homa kali.   Ulegevu mwilini. Udhaifu na uchovu wa mara kwa mara mwilini siyo hali ya kawaida na wa...