Posts

Showing posts from July, 2017

MCHELE WA PLASTIKI’ BALAA UPYA!

Image
Magunia ya mchele. KWA siku kadhaa sasa tangu kuibuka kwa taharuki nchini juu ya uwepo wa mchele wa bandia almaarufu mchele wa plastiki huku mamlaka za serikali zikikanusha ishu hiyo, lakini kadiri siku zinavyosonga, jambo hilo limekuwa likiibua balaa upya. Mapema wiki hii, mwanamke mmoja aliyejukana kwa jina la Zuwena Mapunda, mkazi wa Kimara-Baruti jijini Dar alizua timbwili zito na la aina yake baada ya kudai kuuziwa mchele unaodaiwa kuwa ni wa plastiki. Zuwena aliuziwa  mchele  huo na mfanyabishara aliyetajwa kwa jina moja la Kijagwa. Akizungumza na Amani mbele ya duka la nafaka la Kijagwa lililopo Kimara-Baruti, Dar huku kukiwa na umati uliotaka kuushuhudia mchele huo baada ya kuwepo kwa madai hayo kwa muda mrefu, Zuwena alisema kuwa, alinunua mchele huo kwenye duka hilo kwa ajili ya chakula cha familia. Zuwena alisema kuwa, baada ya kuupika kwa muda mrefu bila kuiva ndipo alipouchunguza kwa kuufinyanga na kuudunda chini ambapo alishangaa kuona unadund...

NEW VIDEO : kutoka kwa Rich Mavoko ft Fid Q ‘Sheri’

Image
Angalia kisha acha comment yako ili Rich na Fid q wakipita humu wakutane na comment yako  Pia usiache kumshirikisha mwingine kama hii ngoma ya  ‘Sheri’  ya  Rich Mavoko  aliyomshirikisha Legend  Fid Q .  Dondosha comment yako whatsapp kwa kuandika neno M'  MUZIKI  ktk +255766605392  

Umeiona simba mpya? Hadi raha

Image
Text M sport to  +255766605392 STRAIKA Mghana, Nicholas Gyan, kutoka Ebusua Dwarfs, amekamilisha orodha ya nyota wapya waliosajiliwa ndani ya Simba kwa ajili ya msimu mpya wa mashindano. Mabosi wa timu hiyo wameweka bayana kikosi chao kipya cha Wekundu wa Msimbazi ambacho kwa sasa kipo Afrika Kusini kikijiandaa na msimu huo mpya ambapo Simba itacheza Ligi Kuu Bara na Kombe la Shiriisho Afrika. Mghana huyo aliyetupia kambani mabao 11 katika Ligi Kuu Ghana, ndiye mchezaji anayetajwa kukamilisha idadi ya waliosajiliwa Msimbazi kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hanspoppe. Hanspoppe aliwataja nyota wengine 11 ambao dili zao zimekamilika huku akidai kwamba bado hawapo katika nafasi nzuri ya kumtangaza kipa, Aish Manula, kuwa ni mchezaji wao halali. Bosi huyo aliwataja wachezaji ambao tayari mambo yao yamekamilika kuwa ni makipa Said Mohammed ‘Nduda’ na Emmanuel Mseja, mabeki Yusuf Mlipili, Salim Mbonde, Erasto Nyoni, Ally Shomar...

Taarifa muhimu kutoka Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ)

Image
Meja Jenerali Simon Mumwi ambaye ni Mkuu wa Mipango na Maendeleo wa JWTZ akizungumza na Waandishi wa habari. JESHI la Ulinzi laWananchi wa Tanzania leo limetoa taarifa kwa vyombo vya habari juu ya maadhimisho ya Siku ya Mashujaa yanayotarajiwa kufanyika Julai 25 mwaka huu. Maadhimisho hayo kama ilivyo desturi ya nchi hutoa fursa ya kuwakumbuka mashujaa wa Tanzania waliotoa maisha yao kwa ajili ya kupigania nchi yetu.

Watu Wenye Sifa Hii Ndiyo Wanaofanikiwa

Image
  Linapokuja swala la mafanikio zipo sifa na mambo mengi ambayo yanakuwa yanatajwa katika kumfikisha mtu ili aweze kufanikiwa. Mambo au sifa  hizo huwa ni za msingi sana kwa kila mtu ili kufikia mafanikio. Hata hivyo pamoja na sifa hizo,  ipo sifa moja muhimu sana ambayo kwa mtafuta mafanikio kama unayo ni lazima utafanikiwa. Sifa hii  muhimu ya kimafanikio ambayo nataka kuiongelea hapa ni uvumilivu wako katika kuelekea mafanikio. Unaweza ukawa unajituma kweli, una nidhamu binafsi na unafanya juhudi za kuwekeza kila wakati, lakini ukikosa uvumilivu hasa pale unapokutana na changamoto au pale unaposubiri mafanikio yako makubwa huwezi kufanikiwa. Uvumilivu ni kitu cha muhimu sana kama umeamua kuishi maisha ya ndoto zako. Inabidi uvumilie  hali ngumu unazokutana nazo, inabidi uvumilie kuishi wakati mwingine chini ya kipato ili kutimiza malengo ya ndoto zako. Kuna kitu najua unataka kujiuliza nitavumilia mpaka lini, mbona maisha yangu naona kama m...

KILA MWANAUME MWENYE UMRI WA MIAKA 40+ YUPO KWENYE HATARI YA KUPATA UGONJWA WA TEZI DUME.

Image
PROSTATE GLAND (TEZI DUME). Ni sehemu mojawapo ya mfumo wa uzazi wa kiume.Tezi hii ipo mbele kidogo ya puru (rectum) na chini kidogo ya kibofu cha mkojo. Tezi dume inauzunguka mrija unaounganisha kibofu cha mkojo na uume (urethra). Ina umbo la yai,ina ukubwa wa kawaida japo ukubwa huongezeka kadri umri unavyoongezeka. Mojawapo ya kazi za tezi dume ni kutoa majimaji yanayochanganyika na mbegu za kiume (sperms) wakati wa kilele cha tendo la kujamiiana(sex). Mchanganyiko huu wa mbegu pamoja na majimaji hayo hufanya shahawa (semen). Aidha majimaji hayo husaidia kuzipa mbegu za kiume nguvu ya kusafiri kwenye uke mpaka kufikia kwenye mirija ya fallopian tayari kwa utungisho na yai la kike. Vilevile husaidia kupunguza hali ya kitindikali iliyopo katika uke, ambayo kama isiporekebishwa, huweza kuua mbegu nyingi za kiume na kufanya utungisho kuwa wa tabu. SEHEMU KUU ZA TEZI DUME. 1.PERIPHERAL ZONE(SEHEMU YA NJE) ~Hii ni sehemu ya nje ya tezi ambayo madakari wengi hutumia hii tezi kuba...

MAMA MWENYE VVU ANAZAAJE MTOTO ASIYE NA VVU?

Image
Mama mwenye vvu anaweza kuzaa mtoto asiye na vvu endapo njia zote zinazoweza kumweka mtoto katika hatari ya kupata maambukizi zitazuiwa. Ni vyema tukatambua kuwa mtoto anaweza kupata maambukizi toka kwa mama katika njia tatu muhimu.Njia hizo ni pamoja na mtoto anapokuwa tumboni,wakati wa kuzaliwa na wakati wa kunyonya maziwa ya mama.Hatari zaidi ni pale mama anapokuwa na idadi kubwa ya vvu katika damu na akawa anaugua mara kwa mara.Kwa jinsi hii usalama wa mtoto tumboni unakuwa ni mdogo na anaweza akapata maambukizi akiwa tumboni hasa pale mfuko wa uzazi unapokuwa dhaifu kiasi cha kuruhusu damu ya mama ichanganyike na ile ya mtoto.Maambukizi ya mama kwenda kwa kwa mtoto kwa njia hii ni kwa kiasi kidogo tu.Endapo kiasi cha vvu katika damu ya dawa ya kumkinga mtoto,hali ya mama itakuwa nzuri na uwezekano wa mtoto kupata maambukizi kwa njia hii huwa mdogo. Wakati wa kuzaliwa mtoto anaweza kupata maambukizi toka kwa mama kama atapata michubuko mwilini mwake na mama akaw...

NUFAIKA KWA KUJIUNGA NA KAMPUNK AIM GLOBAL

Image

Haya ndiyo maneno yakishujaa ya MWLM JULIUS NYERERE

Image

Kama hukuwahi kufika mount KILIMANJARO mtu wangu huu ndio uzuri wake

Image

USIPITWE NA HII MTU WANGU KITU KINAITWA Kibao cha mpenzi

Image

SAMATTA AANDIKA HISTORIA MBELE YA ROONEY, AIFUNGA EVERTON

Image
KRC Genk vs Everton. Mtanzania Mbwana Samatta ameandika historia ya kuwa Mtanzania aliyeweza kufunga bao dhidi ya timu ya Everton ambayo inashiriki Ligi Kuu ya England baada ya kufanya hivyo katika mchezo wa kirafiki akiwa ndani ya jezi ya KRC Genk. Samatta ambaye amekabidhiwa jezi namba tisa hivi karibuni katika kikosi hicho, amefanikiwa kuifungia timu yake hiyo bao katika dakika ya 55 katika mchezo uliomalizika kwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Everton ambao walikuwa na staa wao, Wayne Rooney. Bao la Samatta lilipatikana baada ya kupigwa pasi zaidi ya saba kuanzia kwa kipa wa Genk hadi mpira ulipomfikia Samatta ambaye alimalizia kwa kupiga shuti kali. Mchezo huo uliochezwa Jumamosi hii nchini Ubelgiji ni maalum kwa ajili ya kujiandaa na msimu wa 2017/18 kwa timu zote mbili. Bao la Everton lilifungwa na Rooney katika dakika ya 45. Samatta amekuwa na mwendelezo mzuri katika mechi za maandalizi ambapo wiki iliyopita pia alifunga bao moja katika sare ya mabao 3...

SIMBA WAIPIGIA MAGOTI AZAM FC KWA MANULA

Image
Kipa wa Azam FC, Aishi Manula.  UONGOZI  wa Klabu ya  Simba , umeipigia magoti  Azam FC  imruhusu  Aishi Manula aweze kushiriki mazoezi na klabu hiyo mapema kwa kuwa bado ana  mkataba  wa mwezi mmoja na timu hiyo. Inadaiwa kuwa Manula ameshamalizana na  Simba  kwa mkataba wa miaka miwili lakini hataweza kutangazwa rasmi kuwa mchezaji wa timu hiyo kwa kuwa bado mkataba wake na  Azam FC  haujamalizika. Taarifa ambazo MASHELE BLOG imezipata ni kuwa uongozi wa Simba umeiomba  Azam FC  kumruhusu Manula mapema ili akafanye mazoezi na kikosi hicho kilichopo Afrika Kusini  ili kuepuka kesi kama ilivyokuwa kwa  Hassan Kessy alivyokwenda  Yanga . Ulipotafutwa uongozi wa  Azam FC kuzungumzia suala hilo ulisema kwa upande wao wanatambua kuwa Manula ni mchezaji wao hadi pale atakapomaliza mkataba na si vinginevyo. “Manula  bado ni mchezaji wetu hadi atakapomaliza mkataba wake, pia ye...

List ya vyuo na website zake zipo hapa

Image
Click hapa chini NECTA RESULT& LOAN BOARD TANZANIA, KENYA, UGANDA, USA, S.A ,NIGERIA: List of tanzania university website : 1.    Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam (UDSM)         …………..         https://www.udsm.ac.tz 2.    Chuo Kikuu huria cha Tanzania (OUT)  ...

Polisi yauwa Wawili Kibiti

Image
Jeshi la Polisi limefanikiwa kuwaua watu wawili wanaosadikiwa kuwa ni miongoni mwa wahalifu wanaoendesha mauaji katika Kibiti na maeneo mengine ya Pwani. Watu hao ni pamoja Abdallah Ally Ngande Makeo ambaye alikuwa anatafutwa na Jeshi la Polisi kwa muda mrefu kutokana na kushiriki kwake katika matukio ya mauaji maeneo ya Ikwiriri, Kibiti pamoja na uvamizi wa kituo cha Polisi Ikwiriri. Akielezea tukio hilo, Mkuu wa Operesheni Maalum za Jeshi la Polisi, Naibu Kamishna wa Polisi, Liberatus Sabas alisema kuwa tukio hilo lilitokea mnamo tarehe 19, julai, 2017 saa mbili usiku katika eneo la Utende kata ya Ikwiriri, wilaya Rufiji Kanda Maalum ya Polisi Rufiji. “Askari Polisi wa doria waliwatilia mashaka watu wanaokadiliwa kuwa watano ambapo walianza kuwafutilia ndipo walianza kukimbia huku wakiwashambulia askari kwa risasi, askari nao kwa ujasiri walijibu mashambulizi na kufanikiwa kuwajeruhi wahalifu wawili miongonio mwao ambao baadaye walifariki wakipelekwa Hospitali ya Taif...

Matumizi 5 Ya Coke Yanayothibitisha Kwamba Si Sahihi Kwa Matumizi Ya Binadamu

Image
Coca-Cola ni kinywaji maarufu na kinajulikana sehemu nyingi sana duniani. Kuna maswali mengi ya kujiuliza juu ya unywaji wa kinywaji hiki kwa binadamu,kama ni sahihi kwa matumizi ya binadamu au la,au unywaji wa kinywaji hiki una madhara kwa baadae au la, nauliza hivi kwa sababu pH yake ipo juu kuliko hata ya asidi ya kwenye betri. Taasisi ya moyo,mapafu na damu walidhamini utafiti ufanywe kwa mtu mmoja mmoja ambae anatumia japo soda moja kwa siku. Walikutwa na uwezekano wa asilimia 44 ya kupata magonjwa yanayohusiana na mishipa ya moyo na aina ya pili ya kisukari kwa mda wa miaka minne Utafiti ulifanywa kwa watu zaidi ya 2400 ya vijana,ambapo watu 1600 walikuwa hawana dalili zozote za metabolic syndrome ,na baada ya miaka minne nao wakawa na uwezekano wa kupata magonjwa ya moyo na kisukari. Watu wanaopendelea kutumia soda kila siku wanaweza kupata matatizo ya; 1.uwezekano wa kupata shinikizo la damu 2.asilimia 25 walikuwa na uwezekano wa kupata kisukar...