Posts

NADHARIA ZA VIKOA VYA MAANA

Image
Utangulizi Katika makala hii imegawanyika katika sehemu tatu, utangulizi, kiini na hitimisho. Utangulizi unajumuisha ufafanuzi wa nadharia ya vikoa vya maana, fasili mbalimbali ya vikoa vya maana pamoja na maelezo mafupi kuhusu vikoa vya maana pamoja na sifa za vikoa vya maana, katika kiini maelezo kuhusu umuhimu wa vikoa vya maana na mwisho ni hitimisho Nadharia ya vikoa vya maana imeasisiwa na Mjerumani Jost Strier (1930) akiegemea katika msingi wa kusema kuwa kuna maneno yanayofanana yanaweza kuwekwa pamoja. Mawazo haya ya Strier, Lyons (1970) anadai kuwa hayakuwa mawazo ya Strier bali yalikuwa ni ya Mjerumani mwenzake Von Hambolt. Wataalamu wengine waliokubaliana na mawazo ya Strier ni pamoja na Idsen, Jolls pamoja na Gao na Xu (2013). Hivyo basi, fasili ya vikoa vya maana imetolewa na wataalamu mbalimbali kama ifuatavyo: 1.1 Fasili ya Vikoa vya Maana Resani (2014) anasema vikoa vya maana ni seti au kifungu cha maneno kilicho katika mpangilio fulani, au ni seti ya man...

FASIHI ANDISHI: USHAIRI, TAMTHILIYA, RIWAYA HADITHI FUPI

USHAIRI    Kuna mitazamo ya aina mbili katika kuelezea dhana ya ushairi. kuna wanamapokeo na mamboleo. Hata hivyo kabla ya kuendelea zaidi kuwachambua tuangalie wataalam mbalimbali wanavyofasili dhana hii . Dhana ya ushairi imejadiliwa na wataalamu mbalimbali huku kila mmoja akitoa fasili yake. Baadhi ya wataalam hao ni kama ifuatavyo: MAPOKEO     Mssamba, (2003) akimnukuu Shaban Robert, anasema; “ushairi ni sanaa ya vina inayopambanuliwa kama nyimbo, mashairi na tenzi zaidi ya kuwa na sanaa ya vina ushairi unaufasaha wa maneno machache au muhtasari.”     Mnyampala (1970) anasema kuwa “ushairi ni msingi wa maneno ya hekima tangu kale ndicho kitu kilichobora sana maongozo ya Dunia kwa kutumia maneno ya mkato na lugha nzito yenye kunata iliyopangwa kwa urari wa mizani na vina maalum.”     Amri Abeid (1954:1) anasema kuwa “ushairi au utenzi ni wimbo, hivyo kama shairi haliimbiki halina maana.” Abdulatifu anasema kwamba ushairi ni ule ulio n...

KIONJO CHA RIWAYA: CHRISTINA

Mtunzi info.masshele@gmail.com ..Mle ndani ukimya ulitawala na mazungumzo yaneno moja moja yalikuwa yakiiba nafasi ya ukimya uliokuwopo, kila mtu aliwaza lake, wenye kuhuzunika walihuzunika, walio mhurumia Christina nao walipata mudahuo wa uchungu. Kitanda nacho kiliumia kwa upande wake! Licha ya kubeba mwili dhaifu wa Christina , watu wengine walikaa wakimtazama Christina kwa huruma. Hawa sio wengine bali ndugu wa Christina. .... Mgonjwa, ugonjwa umemlemea kila kiungo ni kizito. Mama Christina anajaribu kumnywesha mgonjwa uji lakini wapi! Uji hauendi umejaa mdomoni kisha unachuruzika unatoka koo halifunguki Ugonjwa umemzidiya. Glory anachukua kitambaa anamfuta mgonjwa jasho lenye harufu kali ya antibiotics, dawa ambazo nazo zilikuwa zimeanza kufika mwisho. Christina anajaribu kuwatazama watu waliokuwa pale , kwanza mama yake lakini hammalizi anaangalia pembeni. Anamtazama Glory naye hammalizi pia anaamua kutazama ukutazama pembeni. Anaona aibu mara hii katika kumalizia mda wak...

LUGHA KIENZO YA KAMUSI NA FAIDA ZAKE

Karibu katika makala haya ambayo tutatalii maana ya lugha kienzo ya kamusi. Mtunga kamusi anapoazimia kutunga kamusi, anakabiliwa na maswali kadhaa. Miongoni mwayo ni 1. Leksimu zipi ziteuliwe kuwa vidahizo. 2. Taarifa gani zitolewe kwa kila kitomeo ili kukidhi haja ya watumiaji Wa kamusi na 3.  Taarifa hizo zielezwe vipi ili msomaji aweze kuziona na kuzielewa. Maana ya lugha kienzo. Lugha kienzo kama asemavyo Bwege (1995) ni lugha au mtindo utumikao kufasili au kueleza leksimu za lugha. Kwa ufupi lugha kienzo ni lugha inayotumika kuifafanua na kuifasili lugha. Lugha kama chombo cha mawasiliano imekuwa ikitumiwa kuelezea maarifa, na mambo mbalimbali. Kwamfano lugha hutumiwa kueleza na kufafanua dhana anuwai za hesabu, sayansi, uchumi, ufundi, fasihi nk. Dhima ya lugha kienzo kwa mujibu Wa Bwege ni kueleza lugha kwa ufasaha, utoshevu, kwa muktasari na uwazi ili kumwezesha mtumiaji, kupata na kuelewa mara moja kile anacho kifafanua bila kuchosha akili. Kamusi kama kita...

HABARI: MABWENI SHULE YA WASICHANA ASHIRA YANATEKETEA KWA MOTO

Image
Picha kutoka eneo la tukio Mabweni ya shule ya sekondari ya Wasichana Ashira iliyopo Marangu mkoani Kilimanjaro yameteketea kwa moto, Mkuu Wa mkoa wa Kilimanjaro Bi Annie Mgwira, amedhibitiksha kutokea kwa tukio hilo lililotoke majira ya asubuhi na amesema tayari askari wa Zimamoto walitumwa eneo la tukio Taarifa zaidi zitakujia hivi punde.

Tangazo la nafasi za kazi 645 toka shirika la Umeme Tanzania-TANESCO

Image
Tangazo la nafasi za kazi 645 toka shirika la Umeme Tanzania-TANESCO 1. 53 Customer Service Representatives/Radio Telephone Operators. ...Jobs at Tanzania Electric Supply Company (TANESCO) 2.  14 Customer Relations Officers (Ossc &District) Jobs at Tanzania Electric Supply Company (TANESCO)   3.  12 Record Management Assistants Jobs at Tanzania Electric Supply Company (TANESCO) 4.  Human Resources Officer Job at Tanzania Electric Supply Company (TANESCO)   5. 5 Stores Attendants Jobs at Tanzania Electric Supply Company (TANESCO) 6. 1 2 Stores/Supplies Assistants Jobs at Tanzania Electric Supply Company (TANESCO)   7. 3 Assistant Supplies (Stores) Officers Jobs at Tanzania Electric Supply Company (TANESCO)    8. 20 Accounts Assistants Jobs at Tanzania Electric Supply Company (TANESCO)  9. 31 Electrical Technicians Jobs at Tanzania Electric Supply Company (TANESCO)    10.  318 Artisans Jobs ...

UCHAGUZI WA CHAUKIDU 2019 TAARIFA ZA WALIO KUWA WAGOMBEA WA NAFASI ZA UONGOZI

Image
RAIS Dk. Dainess Maganda  ni mkurugenzi wa kitengo cha lugha, tamaduni na fasihi za Kiafrika katika chuo kikuu cha Georgia. Nimekuwa mwalimu wa Kiswahili kwa zaidi ya miaka kumi. Nimekitumikia chama hiki katika nyanja mbalimbali miaka iliyopita, kama mwana bodi na mweka hazina. Ninajivunia lugha yangu ya Kiswahili. Naamini kwamba lugha ya Kiswahili ni ya muhimu sana na nimechukua jukumu la kuitangaza lugha hii na utamaduni wake kwa kutumia fasihi, utafiti, kupeleka wanafunzi Tanzania na pia nimeanzisha miradi ya ufundishaji wa Kiswahili kwa wazee na watoto kama huduma katika jamii mbalimbali zilizoko katika mji ninaoishi. Nimefanikiwa kutunukiwa tuzo kadhaa za ufundishaji ikiwepo na tuzo ya ufundishaji bora katika chuo hiki mwaka jana (2018). Naamini kwamba sisi sote tuliopewa zawadi hii ya kujua lugha ya Kiswahili tuna jukumu la kujivunia lugha yetu na kuwafanya wengine waipende na kuithamini. Ingawa nilizaliwa Tanzania, kwa sasa ninaishi na familia yangu katika mji wa Athe...