Kwa mujibu wa Neil Fraistal (1985), wanafafanua kuwa kitabu ni makala iliyoandikwa  kisanaa na makala hii inaweza kuzalishwa na mtu yoyote yule mwenye uwezo wa kufanya hivyo. Tunaona fasili hii inajikita katika swala la sanaa na kufanya kitabu kiwe kipana zaidi kwani swala la sanaa ni pan asana na mtaalamu huyu hafafanui ni sanaa ipi.

Halikadhalika, TUKI (2014), wanafasili kitabu ni maandishi yaliyowekwa pamoja katika kurasa zilizoandikwa kwa mkono au zilizopigwa chapa na kupangwa kwa utaratibu maalumu na kutiwa jalada. Tunaona fasili hii inajikita katika kurasa kuelezea maana ya kitabu huku haiweki wazi utaratibu maalumu ambao kitabu inabidi kiwe nao.

Pia Kamusi pevu ya Kiswahili (2016) wakifafanua maana ya kitabu wanaeleza kuwa  ni kurasa zenye maandishi zilizofungwa pamoja kwa utaratibu. Pia fasili hii inajikita katika kuelezea utaratibu maalumu na kurasa lakini pia haiweki wazi huo utaratibu maalumu ni upi.

Kwa mujibu wa Oxford Advanced Leaners Dictionary (2012), wanafafanua kuwa kitabu ni jumla ya karatasi zilizochapwa ambazo zimewekwa kwa pamoja ndani ya jalada ambazo zinaweza kusomwa. Fasili hii inajikita katika kuelezea kuwa kitabu lazima kiwe kwenye jalada na kuwa kwenye mfumo wa karatasi.

Collins na Thesaurus (2018), wanafafanua kuwa kitabu ni idadi ya vipande vya karatasi vyenye maneno yaliyochapishwa juu yake ambayo yanaunganishwa pamoja na kuwekwa ndani ya jalada gumu. Pia fasili hii inajikita katika kuelezea kuwa kitabu huwa kwenye vipande vya karatasi na huwekwa kwenye jalada.

UNESCO katika (Business Dictionary), wanaeleza kuwa Kitabu ni chapisho lolote lenye kurasa 48 au zaidi. Tunaona fasili hii inajikita katika idadi ya kurasa katika kuelezea maana ya kitabu huku ikisisitiza kitabu kuanza na kurasa 48 na kuendelea.

Kwa ujumla kutokana na fasili za wataalamu hao tunaweza kufasili dhana ya kitabu kuwa ni mkusanyiko wa mawazo, maarifa yaliyowekwa pamoja katika utaratibu maalumu na kuhifadhiwa kwa njia mbalimbali kama vile maandishi katika nakala ngumu au laini na njia ya sauti.

Hivyo kutokana na fasili mbalimbali za wataalamu mbalimbali nilizozipitia, naona kuwa uchangamani katika dhana ya kitabu unatokana na mambo mbalimbali ambayo kutokana na fasili za wataalamu yamejitokeza kama ifuatavyo;

Uchangamani wa kitabu unaletelezwa na namna ya uhifadhi. Katika fasili za wataalamu mbalimbali tunaona wataalamu wanatofautiana na kukinzana kuhusu kitabu kinapaswa kihifadhiwe wapi. mathalani kwa mujibu wa kamusi Pevu (keshatajwa) wanasema kitabu ni kile kilichotiwa jalada, halikadhalika Collins (keshatajwa) anaunga mkono na kudai kuwa kitabu lazima kiwe kwenye jalada. Katika swala la uhifadhi kitabu kinawezwa kuhifadhiwa kwa namna mbalimbali na bado kikawa kitabu kama vile njia ya sauti, nakala laini na nakala ngumu na njia ya sidii na kaseti. 

Dhana ya kitabu ni changamani kutokana na idadi ya kurasa. Mathalani UNESCO wanadai kuwa kitabu ni kile kinachoanzia kurasa 48 na kuandelea, hivyo kama kuna kitabu ambachokina kurasa pungufu ya 48 sio kitabu. Fauka ya hayo kuna vitavu vya watoto ambavyo huwa vina kurasa chache pungufu ya 48 na pia wataalamu wengine hawahusishi idadi ya kurasa katika kufasili dhana ya kitabu hivyo kuleta uchangamani kuhusu dhana ya kitabu.

Dhana ya kitabu ni changamani kutokana na suala la umbo la kitabu. Suala la umbo la kitabu ni lipi limeleta utata na kuchanganya wataalamu mbalimbali. Hii ni kutokana na kushindwa kujua umbo la kitabu ni lipi, mathalani umbo la kitabu ni mstatili, bapa, pembe tatu au duara. Suala la umbo pia limesababisha dhana ya kitabu kutoeleweka miongoni mwa watu mbalimbali.

Dhana ya kitabu ni changamani kutokana na suala la muonekano wa kitabu. Mathalani Oxford Advanced Learner (washatajwa) wanadai kuwa kitabu huwa kipo kwenye muonekano wa karatasi zilizochapwa na kuwa ndani ya jarada. Pia TUKI (washatajwa) wanaona kuwa kitabu huwa kwenye muonekano wa karatasi zilizoandikwa kwa mkono. Hivyo tunaona kuwa kitabu kinaweza kuwa katika muonekano tofautitofauti kama vile kuwa katika nakala ngumu, nakala laini na kadhalika.

Dhana ya kitabu ni changamani kutokana na suala la sura za kitabu. Mathalani kitabu kinatakiwa kiwe na sura ngapi? Lakini pia kuna baadhi ya waandishi huandika kitabu bila ya kuzingatia sura za kitabu. Suala la sura za kitabu husababisha pia dhana ya kitabu kuwa na utata miongoni mwa wataalamu.

Pia dhana ya kitabu ni changamani kutokana na suala la ukubwa wa kitabu. Mathalani kitabu kinatakiwa kiwe na ukubwa upi na maandishi ya kwenye kitabu yanatakiwa yatumie fonti yenye ukubwa upi. Wapo wataalamu wanaoamni kuwa kitabu kinatakiwa kiwe kikubwa, wastani au hata kidogo hivyo kuleta changamoto katika dhana ya kitabu.

Kwa ujumla ili kuweza kuondoa uchangamani katika dhana ya kitabu inabidi tuweke wazi vitu vya msingi ambavyo vinatakiwa viwepo kwenye kitabu ili dhana ya kitabu ikamilike. Mathalani kitabu kinabidi kiwe na sehemu za kitabu kama vile, jarada la mbele, jarada la mbele ndani, nusu anuani, anuani, ukurasa wa haki miliki, tabaruku, dibaji, yaliyomo, matini, bibiliografia, sherehe, faharasa, jarada la nyuma ndani na nje. Kwa kufanya hivyo kunaweza kuondoa utata juu ya dhana ya kitabu. Pia kutoa elimu kwa waandishi, wachapishaji na wachapaji kuhusu uandishi mzuri wa kitabu na mambo kadha wa kadha ambayo wanatakiwa kuzingatia katika uandishi wa kitabu.

Mapitio mbalimbali

 Collins na Thesaurus. (2018). English Dictionary Complete and Unbrigde: Third edition. 

Faistal, N. na Flanders, J.(1985). Textual Scholarship: Cambridge University Press.

                              Publisher
Kamusi Pevu ya Kiswahili (2016). Nairobi: Vide – muwa publisher Limited.
Oxford Advanced Learners Dictionary. (2012). Oxford University Press Elt.
TUKI (2014). Kamusi ya Kiswahili Sanifu. TUKI: Dar es Salaam.
UNESCO.