Posts

Showing posts from May, 2023

AMUUA BABA YAKE KISHA KUMPIKA KAMA MBOGA

Image
  Mwanaume mmoja kutoka kijiji cha Giankaja, kaunti ya Tharaka Nithi alitiwa mbaroni baada ya kudaiwa kumuua baba yake na kupika sehemu za mwili wake. Mwanamume huyo kwa sasa anazuiliwa katika kituo cha polisi kaunti ya Tharaka Nithi nchini Kenya. Polisi walithibitisha kutokea kwa tukio hilo la kusikitisha wakisema mwathiriwa ambaye ni mzee mwenye umri wa miaka 70, aliripotiwa kutoweka kwa siku tatu. Msako ulifanyika katika kijiji kizima na wakazi wa eneo hilo katika juhudi za kumtafuta mzee huyo. Baada ya saa kadhaa za msako, upekuzi wao uliwaelekeza kwenye mtaro wenye kina kirefu ambapo waliupata mwili wa marehemu ambao tayari ulikuwa umeshaanza kuoza.  Marehemu alikuwa amekatwa kichwa na sehemu za mwili wake kukatwa na miguu yake ikiwa kando ya mwili wake. Walikimbia haraka kwa chifu wa eneo hilo ili kumjulisha kuwa wamempata mtu aliyepotea. Hata hivyo, waliporejea kwenye mtaro, mwili huo haukuonekana. Wakiwa wamechanganyikiwa na jinsi mambo yalivyobadilika, wenyeji hao kat...

ALIYEMPIGA, KUMNG'OA JINO NA KUMTOBOA JICHO MKE WAKE AKAMATWA

Image
  At. Mwandishi wetu Jeshi la Polisi. Jeshi la Polisi mkoani Arusha Mei 27, 2023 limefanikiwa kumtamata mtuhumiwa aitwaye Isack Robertson (45) mkazi wa Sombetini Jijini Arusha kwa tuhuma za kumpiga na kumjeruhi mke wake aitwaye Jackline Mkonyi (38) mkazi wa Sombetini jijini humo. Akitoa taarifa hiyo Mei 28, 2023 Kamanda wa Polisi Mkoani Arusha Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Justine Masejo amesema mtuhumiwa huyo alikamatwa huko katika maeneo ya Himo mkoani Kilimanjaro na wanaendelea kumhoji na pindi upelelezi utakapokamilika jalada litapelekwa ofisi ya Taifa ya Mashtaka kwa hatua zaidi za kisheria. Aidha ametoa onyo kwa baadhi ya watu wachache wanaofanya vitendo vya ukatili katika familia zao ama sehemu nyingine kuacha mara moja kwani hawatasita kuwakamata na kuwachukulia hatua za kisheria. Lakini pia amewaomba wananchi popote walipo wasifumbie macho vitendo viovu na waendelee kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi kwa kuhakikisha wanatoa taarifa za uhalifu na wahalifu katika maeneo...

BIBI BIKRA WA MIAKA 123 ATAFUTA MWANAUME WA KUMUOA

Image
  Bikizee Theresa Nyirakajumba ametoa wito kwa watu kumuunganisha na mwanaume atakayemuoa. Katika video iliyosambazwa kupitia YouTube, ajuza huyo alifichua kuwa hajawahi kuwa na uhusiano na mwanamume yeyote tangu kuzaliwa. Akizungumza na Afrimax English, alisimulia jinsi alivyokataa wachumba kwa sababu alikuwa akimngoja mwanaume kamili ambaye angehisi uhusiano naye. Cha kusikitisha ni kwamba hilo halijawahi kutokea, na sasa, akiwa na umri wa miaka 123, anaomba msaada wa kujipatia mume. Alisema kwenye video hiyo: "Naitwa Theresa Nyirakajumba, sijawahi kuona uchi wa mwanaume. Kwa miaka 123, ninaishi kwa tamaa isiyotimizwa, tumaini potovu na moyo wa ujasiri wa kusubiri kwamba siku moja ataibuka mwanaume na kuikumbatia nafsi yangu.” Maoni ya wanamtandao @chesterphiri7523 aliandika: "Ikiwa "Ubikra" ni mtu, basi Mama huyu ni mmoja. Urefu wa maisha pekee ni zaidi ya furaha ambayo angeweza kupata kutoka kwa mwanadamu. Utukufu kwa Mungu." @francine8905 alitoa maoni: ...

Rais Samia afanya mabadiliko ya viongozi leo

Image
  Rais Samia Suluhu Hassan, amefanya mabadiliko madogo ya baadhi ya wakuu wa mikoa, uteuzi wa mkuu wa mkoa, uhamisho wa wakuu wa mikoa na uteuzi wa mkuu wa wilaya. Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Zuhura Yunus imeeleza kuwa Rais Samia amemteua Said Mtanda kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara, akichukua nafasi ya Meja Jenerali Suleiman Mzee ambaye atapangiwa majukumu mengine. Queen Sendinga aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, amehamishiwa kwenda kuwa Mkuu wa Mkoa wa Manyara, akichukua nafasi ya Makongoro Nyerere aliyehamishiwa Rukwa. Pia amemteua Kenani Kihongosi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Urambo, akichukua nafasi ya Mtanda aliyeteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara. Taarifa imeongeza kuwa uhamisho na uteuzi huo unaanza mara moja.  

MNADA WA CHAI KUANZA DAR ES SALAAM

Image
  WAZIRI wa Kilimo, Hussein Bashe amesema kuwa mnada wa Chai unatarajiwa kuanza mwezi Juni mwaka huu ambapo mara baada ya kuanza hakuna mtu atakayeruhusiwa kuuza chai nje ya mipaka ya Tanzania. Bashe ameyasema hayo Mei 21,2023 jijini Dodoma wakati wa maadhimisho ya siku ya Chai Dunaini kitaifa na kusema kuwa awali mnada huo ulikua uanze mwezi Desemba. Amesema kuwa Chai yote ya Tanzania ni lazima ipite kwenye mnada na wanunuzi wa ndani watanunua chai mnadani hata kama wana mikataba ya manunuzi. Bashe amesema ambaye hatataka kupitisha chai mnadani hakuna kupewa kibali cha kusafirisha chai kwenda nje. Aidha Waziri Bashe amezitaka kampuni zinazonunua chai kutoka kwa wakulima hapa nchini kuhakikisha wanawalipa wakulima hao kwa wakati kwani si vyema kwa wanunuzi kuchukua majani ya chai kutoka kwa mkulima halafu hawawalipi. . “Nina data hapa, kuna kampuni inadaiwa malipo ya pili toka mwaka 2018 haijawalipa wakulima sasa nimemuagiza DG kuanzia sasa ataanza kuwapiga faini. Hiyo ni haki ya w...

KIPINDUPINDU KITISHO KIPYA

Image
  Baada ya miaka mingi ya kupungua, ugonjwa wa kipindupindu sasa unarejea kwa kishindo ukilenga nchi zilizo hatarini zaidi duniani.   Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani ( WHO ) na lile la kuhudumia watoto duniani (UNICEF) yanasema nchi nyingi zaidi hivi sasa zinakabiliwa na milipuko, huku idadi ya wagonjwa ikiripotiwa ikiwa ni kubwa kuliko miaka 10 iliyopita. “Janga la kipindupindu linaua maskini zaidi mbele ya macho yetu,” amesema Jérôme Pfaffmann Zambruni, Mkuu wa kitengo cha  UNICEF  kinachohusika na Dharura ya Afya Umma.  Takwimu za WHO zinaeleza kuwa hadi Mei mwaka jana, nchi 15 ziliripoti kuwa na wagonjwa wa kipindupindu, lakini hadi katikati ya mwezi huu wa Mei, tayari kuna nchi 24 zinazoripoti kuwa na ugonjwa huo idadi inaweza kuongezeka zaidi. “Licha ya maendeleo yaliyopatikana miongo iliyopita katika mbinu za kudhibiti kipindupindu bado tuko hatarini kurudi nyuma,” amesema Henry Gray, Meneja wa WHO akihusika na hatua dhidi ya kipindupindu...

MAYELE AIPELEKA YANGA FAINALI

Image
  KLABU ya Yanga Sc imefanikiwa kutinga fainali Kombe la Shirikisho la Azam mara baada ya kuichapa Singida Big Stars 1-0 kwenye mchezo ambao ulipigwa kwenye dimba la Liti mkoani Singida. Yanga Sc iliweza kuwapa nafasi wachezaji wengi ambao mara nyingi wamekuwa hawaanzi kwenye mechi akiwemo Mauya, Doumbia, Mzize na mlinda lango Metacha Mnata. Katika mchezo huo ambayo ilikuwa ya aina yake, timu zote zilitengeneza nafasi za magoli kipindi cha kwanza bila mafanikio, hivyo kwenda mapumziko matokeo yakiwa 0-0. Yanga ilifanya mabadiliko kadhaa kwa baadhi ya wachezaji, wakaingia Fiston Mayele, Tuisila Kisinda, Dikson Job pamoja na Musonda mabadiliko hayo yalizaa natunda kwani Yanga ilianza kulisakama lango la wapinzani na kufanikiwa kupata bao kupitia kwa mshambuliaji wao hatari Fiston Kalala Mayele na matokeo kuwa 1-0. Yanga Sc inaenda fainali ambapo inaenda kukutana na Azam Fc ambao walitinga hatua hiyo mara baada ya kuwaondoa Simba Sc. Mechi hiyo ya Fainali itechezwa katika dimba la Mkw...

MAREKANI KUISAIDIA UKRAINE NDEGE ZA KIVITA

Image
  Marekani imesema itawaruhusu washirika wake wa Magharibi kuipatia Ukraine ndege za kivita za hali ya juu, zikiwemo za F-16 zilizotengenezwa Marekani, katika kuimarisha zaidi Kyiv. Mshauri wa Usalama wa Kitaifa Jake Sullivan alisema Rais Joe Biden “aliwajulisha wenzake wa G7” juu ya uamuzi huo katika mkutano wa kilele wa umoja huo huko Japan siku ya Ijumaa. Wanajeshi wa Marekani pia watawapa mafunzo marubani wa Ukraine kutumia ndege hizo, Bw Sullivan alisema. Ukraine kwa muda mrefu imekuwa ikitafuta ndege za teknolojia ya juu na Rais Volodymyr Zelensky alipongeza hatua hiyo kama “uamuzi wa kihistoria”. Marekani inapaswa kuidhinisha kisheria uuzaji upya wa vifaa vilivyonunuliwa na washirika na hatua hiyo itasafisha njia kwa mataifa mengine kutuma hifadhi zao zilizopo za F-16 kwa Ukraine. “Katika kipindi cha miezi michache iliyopita, sisi na washirika wetu tumezingatia sana kuipa Ukraine silaha zenye kutumia mifumo na mafunzo inayohitaji kufanya operesheni za kushambulia msimu huu,”...

MIAKA 22 SASA TANGU KUZAMA KWA MELI KUBWA YA MV BUKOBA, TANZANI TUMEJIFUNZA NINI?

Image
MAAFA YA MV BUKOBA  KILA KIFO NA SIKU YAKE May 21 kila mwaka tunakumbuka maafa ya MV BUKOBA 😿 Kila binadamu atakufa, lakini kila kifo kina siku yake. Nyaisa Simango, katika makala haya  ana tudhihirishia hivyo. Vinginevyo ni vipi mtu anaweza kuelezea alivyo nusurika wakati mamia ya wenzake walio kuwa katika meli moja walishindwa kujiokoa. Ilikuwa sio siku yake. Ziwa victoria limekuwepo kwa karne na karne, watu wanaoishi kuzunguka ziwa hilo wamekuwa wakijishughulisha na shughuli mbalimbali. Kuvumbuliwa kwa Ngalawa, Jahazi, Boti, na meli  kumewezesha kazi za usafirishaji kuwa rahisi. Bila shaka Simango alipo itwa na mkuu wake wakazi na kuarifiwa kuwa itabidi aende Bukoba  kumpeleka mfungwa kusikiliza rufaa ya kesi yake alifurahi kwani angeweza kuona mandhari nzuri njiani.  Ijapokuwa yeye anatoka katika nmkoa unao pakana na ziwa  bado angefurahia kula samaki.  Nakwavile hakuwahi kufika bukoba, safari ingempa fursa nzuri ya kutalii mjini...

SMS na MESEJI 900+ za mapenzi

Image
  SMS 1000 za kubembeza, mapenzi na mahaba Najiuliza kila leo hivi ni mimi tu kimeo katika dunia hii ya leo maana kila leo nayempata huishia kunipa ahadi kila leo, mpenzi kila siku waniaidi mara nitakupa leo mara kabla ya machweo, hivi ni lini utanipa jibu la uhakika nakunipa mapenzi ya uhakika nipate farijika? Nakupenda mpenzi .  Hakika mtoto umeumbika mithili ya malaika japo mbinguni sijafika lakini nauhakika kwa kila mwanaume aliyeumbika na kukamilika akikuona lazima udenda utamtoka, naomba japo yako dakika nipate kukueleza moyoni yaliyonifika kwani siwezi tena kuficha jinsi navyokupenda, nakupenda amini kwako nimefika!  Nimezunguka pande zote za Tanzania macho nikiangaza kumsaka mrembo wakumkabidhi yangu nafsi na kulila tunda lake kwa nafasi huku nikimpa mahaba yangu ya dhati na sikuwahi kuhisi kama wewe ndiye ungeiteka yangu nafsi, nakupenda sweetie. Sijui nikuekleza namna gani uelewe yaliyionijaa moyoni kwani k...