Skip to main content

Rais Ruto atoa wito wa kufunguliwa mashtaka kwa mhubiri tata nchini Kenya



Rais wa Kenya William Ruto ametaka kukamatwa na kufunguliwa mashtaka kwa mhubiri mwenye utata Paul Mackenzie ambaye aliwataka wafuasi wake kufunga hadi kufa

Rais amemtaja mhubiri huyo kuwa gaidi. Matamshi yake yanakuja muda mfupi baada ya Polisi kupata mwili mmoja zaidi kutoka kwenye kaburi la pamoja karibu na mji wa pwani wa Malindi. Hii inafikisha 40, idadi ya waliofukuliwa, na idadi ya vifo ikifika 48.

Polisi wameviambia vyombo vya habari kwamba miili miwili zaidi imeonekana na itafukuliwa katika muda mfupi ujao.


Maafisa wakuu wa usalama wakiongozwa na Inspekta Jenerali wa Polisi, Japhet Koome na Mkuu wa Kurugenzi ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai Mohamed Amin wanatarajiwa kujiunga na timu ya wachunguzi katika eneo Shahola palipopatikana makaburi ya kina kifupi

Comments

Popular posts from this blog

HIZI HAPA SMS TAMU ZA KUMTAKIA USIKU MWEMA MPENZI WAKO

SMS na MESEJI 900+ za mapenzi

MIAKA 22 SASA TANGU KUZAMA KWA MELI KUBWA YA MV BUKOBA, TANZANI TUMEJIFUNZA NINI?