MIILI YA WAKENYA 21 WALIOFUNGA HADI KUFARIKI YAFUKULIWA

 

Jeshi la Polisi nchini Kenya wamefukua miili ya watu 21 ambao ni waumini wa kanisa la News International Church, ambao inadaiwa wamefariki dunia kwa njaa baada ya kufuata maelekezo ya mchungaji wao ya kufunga mfululizo.

Mchungaji Paul Makenzie Nthenge ndiye anayedaiwa kuwapa maelekezo hayo waumini wake, ikidaiwa kwamba aliwaambia wakifunga mfululizo, wataenda kuonana ana kwa ana na Yesu.

Tayari mchungaji huyo anashikiliwa na Jeshi la Polisi nchini humo huku taarifa zikieleza kwamba huenda makaburi mengine yakabainika.

Credit: DW

Comments

Popular posts from this blog

HIZI HAPA SMS TAMU ZA KUMTAKIA USIKU MWEMA MPENZI WAKO

SMS na MESEJI 900+ za mapenzi

MIAKA 22 SASA TANGU KUZAMA KWA MELI KUBWA YA MV BUKOBA, TANZANI TUMEJIFUNZA NINI?