Simba Yashinda dhidi ya Vipers huko Uganda

 


NA EMMANUEL MBATILO

KLABU ya Simba imefanikiwa kuondoka na alama tatu ugenini baada ya kufanikiwa kuichapa Vipers ya nchini Uganda 1-0, na kufanikiwa kushika nafasi ya tatu kwenye kundi akiwa amecheza mechi tatu.

Katika mchezo huo muhimu ambao Simba Sc alihitaji kupata ushindi ili aweze kupata matumaini katika kuwania nafasi mbili za juu na kuweza kutinga robo fainali kwenye michuano hiyo ya Klabu Bingwa Afrika inayoendelea.

Simba Sc ilifanikiwa kupata bao la mapema kipindi cha kwanza kupitia kwa beki wao kisiki Inonga Baka na kuiwezesha timu yake kuibuka na ushindi wa bao 1-0.

Comments

Popular posts from this blog

HIZI HAPA SMS TAMU ZA KUMTAKIA USIKU MWEMA MPENZI WAKO

SMS na MESEJI 900+ za mapenzi

MIAKA 22 SASA TANGU KUZAMA KWA MELI KUBWA YA MV BUKOBA, TANZANI TUMEJIFUNZA NINI?