Binti akata Nyeti za baba yake na kuziondoa

 

Mwanamke anayefahamika kwa jina Grace Kihumba(30) mkazi wa Wang'ing'ombe mkoani Njombe anayedaiwa kuwa na matatizo ya akili anashikiliwa na jeshi la polisi kwa kumshambulia baba yake mdogo akiwa usingizini na kisha kuzikata sehemu za siri na kuziondoa.



Baada ya kukamatwa na kufanyiwa mahojiano na maofisa wa jeshi la polisi mwanamke huyo amesema amefanya hivyo kutokana na kukasirishwa na kitendo cha wanafamilia kuendelea kusherekea wakati yeye anaendelea kuumwa licha ya kutoa hela za matibabu kwa mzee huyo ambaye anadaiwa kuwa ni mtaalamu wa tiba asilia,kama ambavyo Kamanda wa jeshi la polisi mkowa Njombe Hamis Issa alivyobainisha wakati akizungumza na Waandishi wa Habari.


Katika tukio jingine Kamanda Issa amesema jeshi hilo linamshikilia kijana anayefahamika kwa jina la Baraka Alfonce mkazi wa kitongoji cha Kimbila Ludewa mjini kwa tuhuma za kuhusika kumkata kiganja cha mkono bosi wake baada ya kutomlipa fedha kiasi cha elfu 65

Comments

Popular posts from this blog

HIZI HAPA SMS TAMU ZA KUMTAKIA USIKU MWEMA MPENZI WAKO

SMS na MESEJI 900+ za mapenzi

MIAKA 22 SASA TANGU KUZAMA KWA MELI KUBWA YA MV BUKOBA, TANZANI TUMEJIFUNZA NINI?