Kamisaa wa Sensa ya Watu na Makazi Nchini, Anne Makinda amesema licha ya mafanikio makubwa yaliyoonekana kwenye kazi ya Sensa la 2022 kuzifikia kaya,  jumla ya makarani kumi walipoteza maisha kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kujiua na kuuawa.


Makinda ametoa ripoti hiyo huko mkoani Manyara wakati alipokutana na Kamati ya Sensa mkoani hapo kwa minajili ya kupokea taarifa ya zoezi la Sensa  ambapo Mkuu wa Mkoa wa Manyara Makongoro Nyerere amesema kwamba zaidi ya kaya 300,000 ziliweza kufikiwa kwenye kazi hiyo.


Credit' Azam Tv