Polisi: Mhitimu wa SUA Aliyeuawa, Alivutwa Shingo


Jeshi la Polisi mkoa wa Morogoro linamshikilia mtu mmoja kwa mahojiano kufuatia kifo cha mhitimu wa Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA), Magreth Mashue, na kusema kwamba uchunguzi wa awali wa daktari umebaini kwamba shingo ya marehemu ilivutwa.

 

Taarifa hiyo imetolewa na Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai mkoa wa Morogoro Ralph Meela, na kusema kwamba waliyemkamata ni mwanachuo mwenzake aliyekuwa akiishi naye.

 

Imeelezwa kwamba Magreth alipotea Desemba 14 hadi Desemba 18 mwili wake ulipopatikana katika mashamba ya chuo hicho.

Comments

Popular posts from this blog

HIZI HAPA SMS TAMU ZA KUMTAKIA USIKU MWEMA MPENZI WAKO

SMS na MESEJI 900+ za mapenzi

MIAKA 22 SASA TANGU KUZAMA KWA MELI KUBWA YA MV BUKOBA, TANZANI TUMEJIFUNZA NINI?