Posts

Showing posts from November, 2019

MAANA YA UDHANAISHI: UDHANAISHI KATIKA KAZI ZA KIFASIHI, USHAIRI, RIWAYA, TAMTHILIYA

-maana ya UDHANAISHI -misingi au mihimili ya UDHANAISHI -UDHANAISHI katika ushairi -udhanaishi katika riwaya -udhanaishi katika tamthiliya -Udhanaishi ninini pdf DHANA YA UDHANAISHI Katika kuelezea nadharia hii tutajikita kwanza kangalia maana ya udhanaishi kwa mjibu wa wataalam mbalimbali, waasisi wake kisha mihimili yake na mwisho tutamalizia na uchambuzi wa Riwaya ya “Kichwamaji” kwa kutumia nadharia hii. MAANA YA UDHANAISHI Wataalam mbalimbali wameeleza maana ya udhaishi kama vile; Kimani Njogu na Rocha Chimerah (1999) wanasema “Udhanaishi ni nadharia inayojishughulisha zaidi na dhana ya Maisha” swali la kimsingi katika nadharia hii ni ; Maisha ni nini?. Wadhanaishi huchunguza kwa undani nafasi ya mwanadamu ulimwenguni, pia wanajishughulisha na uchunguzi kuhusu uhuisiano uliopo kati ya binadamu na Mungu. Wamitila, K. W. (2003) Katika Kamusi ya fasihi Istilahi na nadharia amefafanua “Udhanaishi ni dhana inayotumiwa kuelezea falsafa ya kuwako na Maisha. Dhana hii...

Kinachowakwamisha wanamuziki wa kike Tanzania kutamba kimataifa

Image
Baadhi ya wadau wa muziki wamesema ni ukosefu wa ubunifu na uwekezaji mdogo katika kazi wanazofanya.  Pia ushirikiano mdogo na wanamuziki wa nje na kushindwa kutumia mizuri majukwaa ya kimataifa ya mauzo kama Youtube.  Wameshauriwa kujiongeza ili kulifikia soko la kimataifa kama wenzao wa kiume.  Dar es Salaam. Wakati wanamuziki wa kike wa nchi za magharibi mwa Afrika na nje ya bara hilo wakipasua anga la kimataifa kwa kazi za muziki, wenzao wa Tanzania wana kibarua kigumu kuelekea katika anga za kimataifa Hali hiyo inatokana na changamoto mbalimbali ikiwemo ukosefu wa ubunifu wa kutengeneza muziki wenye mvuto unaoweza kugusa idadi kubwa ya watu duniani.  Mathalani, mwanamuziki wa kike wa Nigeria,  Yemi Aladei  ameweza kujipatia umaarufu mkubwa duniani kutokana na muziki wake kugusa maisha ya watu wengi.  Chaneli yake ya Youtube ina wafuasi wasiopungua  milioni 1.1,  Yemi maarufu kama Mama Afrika mwenye miaka 30 ni miongoni m...

UN yatoa mwelekeo kuziba pengo la migawanyiko mtandaoni

Image
Amezitaka nchi kufanya kazi kwa pamoja ili kuziba pengo hilo. Wadau zikiwemo Serikali zimeshauriwa kwenda sambamba na kasi ya teknolojia ya dijitali. Dar es Salaam.  Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Antonio Guterres amesema teknolojia ya dijitali ndiyo inayounda dunia hivi sasa na inakwenda kwa kasi isiyo ya kawaida hivyo kila mtu katika dunia anapaswa kwenda na kasi hiyo ili kufaidika na fursa zinazoambatana nayo. Akizungumza katika kongamano la kimataifa la udhibiti wa masuala ya intaneti Ujerumani jana (Novemba 26, 2019) nchini Ujerumani, Guterres amesema fursa ya upataji wa mtandao wa bure na wazi iko katika hatari kwa sababu hakuna juhudi za pamoja kuondoa mgawanyiko wa kijamii, kiuchumi na kisiasa.  “Lakini hili linaweza kubadilika. Na kuonyesha ni jinsi gani tunaweza kushirikiana mustakabali wa kidijitali kwa pamoja , vyema na kwa matarajio yetu sote,” amesema Guaterres. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na UN, Katibu Mkuu huyo ameonya kuwa, end...

Msanii Bi Cheka Afariki Dunia

Image
Msanii wa Muziki Nchini Tanzania Cheka Hija Mzee Maarufu zaidi Bi Cheka amefariki dunia mchana wa Leo Novemba 28,2019 katika Hospitali ya Mloganzila. Kifo cha msanii huyo mkongwe kimethibitishwa na mtoto wake wa kiume, Adam Juma, ambaye amesema kuwa mama yake alikuwa akisumbuliwa na tatizo la moyo. Familia ya marehemu inaendelea na mipango ya mazishi ambayo itaitangaza. Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi

Nafasi za Kazi Baobab Secondary School, Office Secretaries

Image
Position: Office Secretary (02 posts) Qualifications: A Diploma in Secretarial Course. The candidates must have excellent Computer skills in Microsoft Office with at least two (02) years’ experience in a similar position in the reputable Institution. In both positions, the salary is negotiable, depending on the candidate’s qualifications and experience. Interested candidates should send their applications attached with CV and relevant Certificates to: The Principal Baobab Secondary School P.O. Box 35692, Dar es salaam Or through email: headmaster@baobab.ac.tz or deputyheadmasterac@baobab.ac.tz To reach him not later than 13th December, 2019.

Akamatwa na Kadi 23 za Benki Tofauti, Azisokomezea Ukeni

Image
 JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linamshikilia  Bi Halima Juma  (23) Mkazi wa Chalinze kwa tuhuma za wizi wa fedha kwenye mashine za kutolea fedha (ATM). Kwa mujibu wa taarifa ya Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa, picha halisi ni kama ifuatavyo: Mnamo tarehe 25/10/2019 katika Kituo cha Polisi Mbagala Maturubai, mzee Ernest Mika Sakala, ambaye ni Ofisa Mwandamizi Mstaafu wa Jeshi la Polisi alitoa ripoti kwamba tarehe 23/10/2011 majira ya 10:00hrs alibadilishiwa kadi yake ya benki ya CRDB na kupewa ya mtu mwingine bila yeye mwenyewe kufahamu, wakati alipokwenda kutoa fedha kwa wakala wa benki hiyo ambaye anaendesha biashara yake maeneo ya Dar Live Mbagala Zakhem. Kwamba siku mbili baadaye aligundua kuwa kadi ya benki aliyo nayo siyo yake, na alipokwenda kufuatilia benki ya CRDB Mbagala siku ya tarehe 25/10/2019 aligundua kuibiwa kwa fedha kutoka kwenye account yake kiasi cha tzs. 10,000,000/=. Fedha hizo zilitolewa...

Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete Kupokea Madaktari Bingwa Kutoka China

Image

ATHARI ZA MWANGA WA BLUE KIAFYA.

Image
Naposema mwanga wa blue wengi watafikiria ule mwanga unaotoka kwenye taa za blue,Ila sio huo naouzungumzia hapa. Mwanga tunaoona kutokea kwenye jua,taa,simu nk inakuwa ni muunganiko wa mawimbi ya umeme-sumaku (electro magnetic waves). Mawimbi haya yanaposafiri huzalisha nguvu. Mawimbi yakiwa mafupi ndo huzalisha nguvu nyingi zaidi na mwanga wenye mawimbi marefu unakuwa na nguvu kidogo. Kila urefu wa mawimbi unawakilishwa na rangi na hapo ndipo tunapata makundi mbali mbali mfano X ray,gamma rays, ultra violet rays. Katika aina za mawimbi hayo ya mwanga macho yanaweza kuona baadhi (visible light). Mwanga wa blue (blue light) mawimbi yake ni mafupi (short wave length) kwa hiyo unazalisha nguvu kubwa. Kuwa katika mwanga wa blue kwa muda mrefu ina madhara kiafya hasa kwenye macho na mfumo wa usingizi (circadian rythm) VYANZO VYA MWANGA WA BLUE. mwanga wa blue upo kila sehemu. Mwanga wa jua unakuwa pia na mwanga wa blue ndani yake. Vyanzo vingine ni TV,simu,...

Nafasi Mpya Za Kazi Tume Ya Taifa Ya Uchaguzi-NEC

Image

Treni ya abiria Dar – Moshi Kuanza Desemba, nauli zatajwa

Image
Ikiwa tunaelekea sikukuu za mwisho wa mwaka 2019, abiria wa Kanda ya Kaskazini watakuwa na kicheko kwao baada ya treni ya abiria kutoka Dar es Salaam kwenda Moshi itaanza Desemba. Tayari Shirika la Reli Tanzania (TRC) limetoa tangazo la kuanza kwa usafiri huo na kuthibitishwa na Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi, Isaac Kamwele. Waziri Kamwele amesema kama Serikali imefurahi kufikia hatua hiyo ukizingatia treni hiyo ilikuwa ianze tangu Septemba 2019. Hata hivyo, amesema kutokana na changamoto za kunyesha mvua na kusababisha baadhi ya miundombinu ikiwemo ya reli kuharibika katika ukanda huo wa Kaskazini ndio maana kukawepo na uchelewaji wa kuanza kwake. “Sasa ile tabia ya wafanyabiashara pale stendi ya ubungo kulangua abiria tiketi wakati watu wakienda kula sikukuu na ndugu zao itakoma, kwani hata mimi ilishanikuta na kama Serikali tulikuwa tunahangaika kutafuta njia ya kukomesha vitendo hivyo na ujio wa treni hii ya abiria utasaidia,” amesema Kuhusu nau...

Azam yaibuka na App inayoweza kukomboa wafanyabiashara.

Image
Inandoa usumbufu wa usafiri na ulazima wa kufunga duka Haitoi huduma za Azam pekeyake kwani bidhaa za makampuni mengine zinapatikana Gharama za manunuzi zinajumuisha kodi na huduma ya risiti inapatikana Dar es Salaam . Mara nyingi kufanya manunuzi ya jumla kwaajili ya dukani imeikuwa  ni pasua kichwa kwa mfanya biashara yeyote ikiwemo usafiri au hata kulazimika kufunga duka tu ili kuifuata bidhaa hiyo. Praxeda Mathias ni mhasibu kwenye hoteli ya Nothern Breeze Dar es Salaam. Yeye amesema katika kufanya manunuzi ya vitu vya jikoni vikiwemo unga, sukari na mafuta, inamlazimu kutenga muda walau mara moja kwa wiki ili kufanya manunuzi ya moja kwa moja. Endapo vitu vikiisha kabla ya siku iliyopangwa, basi huwa anapata changamoto kwani anatumia pesa ya ziada kwenye usafiri na muda mwingine inasababisha baadhi ya vitu kupatikana kwa uchache vikiwemo vyakula.. Changamoto anazokutana nazo Mathias huenda zinawakumba wafanya biashara mbalimbali  hata hivyo, huenda suluhi...

Mkapa Aweka Wazi Rostam Aziz alivyochangia kuanzishwa NHIF

Image
Rais mstaafu, Benjamin Mkapa ameweka wazi kuwa uamuzi wa kuwa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), ni mpango ulioasisiwa na mfanyabiashara maarufu nchini Rostam Aziz. Katika kitabu chake cha ‘My Life, My Purpose’ alichokizindua wiki iliyopita jijiji Dar es Salaam, Mkapa ameeleza alijifunza mpango huo wakati mfanyabiashara huyo alipokuwa Mbunge wa Jimbo la Igunga alikouasisi mwaka 1996 kabla ya kutangazwa rasmi kuwa wa kitaifa. “Njia nyingine ya moja kwa moja ya kuwasaidia masikini ni kupitia Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), ambao umejitolea kuzipatia familia hizo bima za afya. “Nilijifunza kuhusu mpango huu kutoka kwa Rostam Aziz, Mbunge na mmoja kati ya wafanyabiashara wakubwa waliofanikiwa. “Mwaka 1996 alianzisha mpango wa bima ya afya kwa wananchi wake wa Jimbo la Igunga kwa kiwango kidogo cha fedha ya Sh 10,000 ambacho kilisaidia familia yenye watoto wanne kutumia bima hiyo kwa kipindi cha mwaka mzima. Tuliamua kuutangaza mpangohuu kitaifa,” ameeleza...

MAJIGAMBO KATIKA NYIMBO ZA KIZAZI KIPYA, BONGO FLEVA NA HIP POP

SANAA YA MAJIGAMBO KATIKA NYIMBO ZA KIZAZI KIPYA Kwa hakika sanaa ya majigambo yaijapotea Barani Afrika, isipokuwa imebadilika tu kulingana na maendeleo ya Sayansi na Teknolojia. Katika kujadili mada hii, kwanza tutaanza kufafanua dhana ya majigambo kwa kuwatumia wataalamu mbalimbali huku tukitoa maana yetu kutokana na mawazo ya wataalamu hao, pia tutaelezea kwa ufupi kuhusu chimbuko la muziki wa kizazi kipya, kisha tutaingia katika kiini cha mada tajwa kwa kuonesha jinsi gani majigambo yalivyojitokeza katika nyimbo mbili za kizazi kipya ambapo tumetumia wimbo wa msanii Prof Jay “Ndiyo mzee” na wimbo wa Sugu “Sugu”. Kisha hitimisho. Kwa mijibu wa Simiyu (2011), majigambo ni maigizo yanayotoa mwanya kwa wahusika kujisifu kwa sababu ya matendo fulani ya kishujaa au mafanikio katika nyanja fulani za maisha. Mulokozi (1996), vivugo (majigambo) ni ghani la kujisifia. Kwa kawaida hutungwa na kughanwa na muhusika mwenyewe. Kivugo hutungwa kwa ufundi mkubwa kwa kutumia mb...