Nyakiiru Kibi pdf-2
Fasilu ya Tatu
Taswira
615
Habari ilienea
Watu wakaisikia
Kawamara wametua
Vijana wa kuvutia.
Habari ilienea
Watu wakaisikia
Kawamara wametua
Vijana wa kuvutia.
616
Wana mioyo ya wema
Wanagawa bure nyama
Na adabu na heshima
Na nguo wamevalia.
Wana mioyo ya wema
Wanagawa bure nyama
Na adabu na heshima
Na nguo wamevalia.
617
Kwa kasi ilisambaa
Habari ikazagaa
Watu wakaja manria
Wageni kuangalia.
Kwa kasi ilisambaa
Habari ikazagaa
Watu wakaja manria
Wageni kuangalia.
618
Habari ikasaflri
Hadi katika kasiri
Ya Omukama amiri
Ntumwa akaisikia.
Habari ikasaflri
Hadi katika kasiri
Ya Omukama amiri
Ntumwa akaisikia.
619
Akataka sulutani
Waitwe mara wageni
Kuwahoji atamani
Ajue walichojia.
Akataka sulutani
Waitwe mara wageni
Kuwahoji atamani
Ajue walichojia.
620
Akapelekwa tarishi
Mwenye mbio mtumishi
Aupeleke utashi
Wa mkuu wa jamia.
Akapelekwa tarishi
Mwenye mbio mtumishi
Aupeleke utashi
Wa mkuu wa jamia.
621
Mithili ya mbayuwayu
Akenda mjumbe huyu
Anahema kama kuyu
Kwa mbio kuzidmua.
Mithili ya mbayuwayu
Akenda mjumbe huyu
Anahema kama kuyu
Kwa mbio kuzidmua.
622
Kwake Nyakiru mgeni
Kabisha kangia ndani
Akisha subalherini
Amri kaitongoa.
Kwake Nyakiru mgeni
Kabisha kangia ndani
Akisha subalherini
Amri kaitongoa.
623
“Mtukufu Omukama
Simba anayenguruma
Mume wa waume wema
Wageni awamkia.
“Mtukufu Omukama
Simba anayenguruma
Mume wa waume wema
Wageni awamkia.
624
“Mtukufu wajamala
Anasema halahala
Leo msende kulala
Kabula ya kumwendea.
“Mtukufu wajamala
Anasema halahala
Leo msende kulala
Kabula ya kumwendea.
625
“Mtukufu utashiwe
Leo mfike mpewe
Atakayo muambiwe
Na kisha mtarejea.”
“Mtukufu utashiwe
Leo mfike mpewe
Atakayo muambiwe
Na kisha mtarejea.”
626
Akaridhi muungwana
“Twashukuru maulana
Tu watumwa wake bwana
Wito twauitikia.”
Akaridhi muungwana
“Twashukuru maulana
Tu watumwa wake bwana
Wito twauitikia.”
627
Kamwita Kanyamaishwa
Kumwarifu alopashwa
Kuwa wameamrishwa
Kigarama kwelemea.
Kamwita Kanyamaishwa
Kumwarifu alopashwa
Kuwa wameamrishwa
Kigarama kwelemea.
628
Wakawaita wenzao
Kuwapa ujumbe huo
Wafanye maandalio
Ikuluni kwelekea.
Wakawaita wenzao
Kuwapa ujumbe huo
Wafanye maandalio
Ikuluni kwelekea.
629
Wakavalia vizuri
Ngozi zisizo dosari
Wakisha kuwa tayari
Safari wakabandua.
Wakavalia vizuri
Ngozi zisizo dosari
Wakisha kuwa tayari
Safari wakabandua.
630
Wakaenda kishujaa
Silaha zang'aang'aa
Kigarama wakangia
Mukama kawapokea.
Wakaenda kishujaa
Silaha zang'aang'aa
Kigarama wakangia
Mukama kawapokea.
Taswira
631
“Wapi mlikotokea
Wapi mnakokwendea
Kazi gani mwafanyia
Kujua natamania.”
“Wapi mlikotokea
Wapi mnakokwendea
Kazi gani mwafanyia
Kujua natamania.”
632
Wakamjibu vijana
“Twasikia maulana
Nasi tu radhi kunena
Yote kukutobolea.
Wakamjibu vijana
“Twasikia maulana
Nasi tu radhi kunena
Yote kukutobolea.
633
“Sisi, ewe Mtukufu
Tu wawindaji hafifu
Nasaba zetu dhaifu
Tu wanyonge twazagaa.
“Sisi, ewe Mtukufu
Tu wawindaji hafifu
Nasaba zetu dhaifu
Tu wanyonge twazagaa.
634
“Twazagaa e Jalali
Karibuni hata mbali
Tukitafuta fadhili”
Nyakiru akatongoa.
“Twazagaa e Jalali
Karibuni hata mbali
Tukitafuta fadhili”
Nyakiru akatongoa.
635
“Kibumbiro ni nyumbani
Kiziba sisi wageni
Bali tunayo imani
Simba utatujalia.
“Kibumbiro ni nyumbani
Kiziba sisi wageni
Bali tunayo imani
Simba utatujalia.
636
“Kuwinda ni kazi yetu
Toka utotoni mwetu
Kuivinjari misitu
Ndiyo ya kwetu tabia.
“Kuwinda ni kazi yetu
Toka utotoni mwetu
Kuivinjari misitu
Ndiyo ya kwetu tabia.
637
“Twajua kila mnyama
Kila ndege mwenye nyama
Na misimu ya kuhama
Ya madege twaijua.
“Twajua kila mnyama
Kila ndege mwenye nyama
Na misimu ya kuhama
Ya madege twaijua.
638
“Twajua misitu gani
Husitawisha kongoni
Kuro, swala hata nyani
Makazi yao twajua.
“Twajua misitu gani
Husitawisha kongoni
Kuro, swala hata nyani
Makazi yao twajua.
639
“Twajua kila kiumbe
Toka kwa simba kabambe
Hadi kwa fisi mzembe
Mahiri wa kudoea.
“Twajua kila kiumbe
Toka kwa simba kabambe
Hadi kwa fisi mzembe
Mahiri wa kudoea.
640
“Tunajua tamu nyama
Hutoka yupi mnyama
Na nyama ngumu kuuma
Mnyama gani hutoa.
“Tunajua tamu nyama
Hutoka yupi mnyama
Na nyama ngumu kuuma
Mnyama gani hutoa.
641
“Tu mafundi wa kuvuta
Kila aina ya nyuta
Pia mapanga kufuta
Na mikuki kuinua.
“Tu mafundi wa kuvuta
Kila aina ya nyuta
Pia mapanga kufuta
Na mikuki kuinua.
642
“Japo tu watu hafifu
Sio watu wenye hofu
Japo sio watukufu
Uungwana twaujua.
“Japo tu watu hafifu
Sio watu wenye hofu
Japo sio watukufu
Uungwana twaujua.
643
“Tumezurura kutosha
Kadka yetu maisha
Twapenda kubahatisha
Maisha yalotulia.
“Tumezurura kutosha
Kadka yetu maisha
Twapenda kubahatisha
Maisha yalotulia.
644
“Kwa fadhilazo mwadhamu
Tu radhi kuishi humu
Tufanye masitakimu
Na kuwa zako raia.
“Kwa fadhilazo mwadhamu
Tu radhi kuishi humu
Tufanye masitakimu
Na kuwa zako raia.
645
“Tu radhi kutumikishwa
Tu radhi kuamrishwa
Hili litahakikishwa
Muda ukitupatia.
“Tu radhi kutumikishwa
Tu radhi kuamrishwa
Hili litahakikishwa
Muda ukitupatia.
646
“Sisi na wetu vijana
Tuko radhi kupigana
Ili kudumisha jina
La enzi yako murua.
“Sisi na wetu vijana
Tuko radhi kupigana
Ili kudumisha jina
La enzi yako murua.
647
“Hatuogopi adui
Katika dunia hii
Madhali bado tu hai
Huna cha kukihofia.
“Hatuogopi adui
Katika dunia hii
Madhali bado tu hai
Huna cha kukihofia.
648
“Vita ni chakula chetu
Damu ni kinywaji chetu
Adui zako ni zetu
Wajapo watatujua.
“Vita ni chakula chetu
Damu ni kinywaji chetu
Adui zako ni zetu
Wajapo watatujua.
649
“Nchi hii ya Kiziba
Ni nchi yenye haiba
Wana bahati Baziba
Humu wanaolowea.
“Nchi hii ya Kiziba
Ni nchi yenye haiba
Wana bahati Baziba
Humu wanaolowea.
650
“Una bahad Mukama
Kutawala nchi njema
Yenye maziwa na nyama
Kama hii twakwambia.
“Una bahad Mukama
Kutawala nchi njema
Yenye maziwa na nyama
Kama hii twakwambia.
651
“Kwa kuwa twaitamani
Tu radhi kuiauni
Ukikiri masikani
Yetu hapa kujengea.”
“Kwa kuwa twaitamani
Tu radhi kuiauni
Ukikiri masikani
Yetu hapa kujengea.”
652
Akiyasikiya haya
Mukama kafurahiya
Kaona siyo wabaya
Hawa wawinda shujaa.
Akiyasikiya haya
Mukama kafurahiya
Kaona siyo wabaya
Hawa wawinda shujaa.
653
Kakuna upara wake
Na ndevu na mvi zake
Kasugua bongo zake
Kaona watamfaa.
Kakuna upara wake
Na ndevu na mvi zake
Kasugua bongo zake
Kaona watamfaa.
654
Kaona watamfaa
Wataja mpigania
Nchini akiridhia
Kuwaruhusu kukaa.
Kaona watamfaa
Wataja mpigania
Nchini akiridhia
Kuwaruhusu kukaa.
655
Watoto wake wachanga
Wanaonyesha ujinga
Wataogopa mapanga
Hapo watakapokua.
Watoto wake wachanga
Wanaonyesha ujinga
Wataogopa mapanga
Hapo watakapokua.
656
Watakaposhika enzi
Watahitaji walinzi
Wapepezi na wakanzi
Ili kuwahudumia.
Watakaposhika enzi
Watahitaji walinzi
Wapepezi na wakanzi
Ili kuwahudumia.
657
Kwani uzee balaa
Kaona unamtwaa
Ujana wamuambaa
Yazimika yake taa.
Kwani uzee balaa
Kaona unamtwaa
Ujana wamuambaa
Yazimika yake taa.
658
Na hivyo akatamka
“Ombi limekubalika
Mwaweza kujenga maka
Kizibani kulowea.
Na hivyo akatamka
“Ombi limekubalika
Mwaweza kujenga maka
Kizibani kulowea.
659
“Nawapenda wanaume
Wenye nyoyo za kiume
Na maungo ya kidume
Kuja kunitumikia.
“Nawapenda wanaume
Wenye nyoyo za kiume
Na maungo ya kidume
Kuja kunitumikia.
660
“Napenda waume bora
Wasochelea madhara
Walo tayari kukera
Adui kuniulia.
“Napenda waume bora
Wasochelea madhara
Walo tayari kukera
Adui kuniulia.
661
“Mnaweza kwendelea
Makazi kujijengea
Kibali nimekitoa
Hamna cha kuhofia.”
“Mnaweza kwendelea
Makazi kujijengea
Kibali nimekitoa
Hamna cha kuhofia.”
Taswira
662
Wakamshukuru sana
Hilo alipolinena
Na kuhakikisha tena
Kuwa watamfalia.
Wakamshukuru sana
Hilo alipolinena
Na kuhakikisha tena
Kuwa watamfalia.
663
Kwa furaha wakatoka
Waongea na kucheka
Kwani wamekubalika
Kadka nchi kukaa.
Kwa furaha wakatoka
Waongea na kucheka
Kwani wamekubalika
Kadka nchi kukaa.
664
Wakirudi majumbani
Wakaweleza wandani
Mambo yote Kikaleni
Ambavyo yamewendea.
Wakirudi majumbani
Wakaweleza wandani
Mambo yote Kikaleni
Ambavyo yamewendea.
665
Pia wakawaambia
“Wake zetuni sikia
Mnaweza kupania
Mashamba kujilimia.
Pia wakawaambia
“Wake zetuni sikia
Mnaweza kupania
Mashamba kujilimia.
666
“Kama wanawake wote
Mabibi nchini popote
Mlime, maji mchote
Hamna cha kuhofia.
“Kama wanawake wote
Mabibi nchini popote
Mlime, maji mchote
Hamna cha kuhofia.
667
“Udongo mwanze kuchimba
Tupandikize migomba
Mpalilie mashamba
Na ndizi kujichumia.
“Udongo mwanze kuchimba
Tupandikize migomba
Mpalilie mashamba
Na ndizi kujichumia.
668
“Utapofika msimu
Wa maharage matamu
Mpande ili kukimu
Wa'me zenu na jamaa.
“Utapofika msimu
Wa maharage matamu
Mpande ili kukimu
Wa'me zenu na jamaa.
669
“Sisi waume vijana
Kuwinda hatutakana
Tutazidi kupambana
Na nyang'au wa dunia.
“Sisi waume vijana
Kuwinda hatutakana
Tutazidi kupambana
Na nyang'au wa dunia.
670
“Tutazidisha usasi
Wa nyama bila kiasi
Tujiletee nemsi
Na kuwalisha raia.
“Tutazidisha usasi
Wa nyama bila kiasi
Tujiletee nemsi
Na kuwalisha raia.
671
“Pia tutajizoeza
Mishale kuipaaza
Na panga kuzipepeza
Na mikuki kurushia.
“Pia tutajizoeza
Mishale kuipaaza
Na panga kuzipepeza
Na mikuki kurushia.
672
“Tufanye jeshi la nguvu
La wachache wa mabavu
Kuja kufuta maovu
Ambayo yamezagaa.”
“Tufanye jeshi la nguvu
La wachache wa mabavu
Kuja kufuta maovu
Ambayo yamezagaa.”
673
Na kwa kwandalia hili
Mwendo hawakubadili
Raha hawakukubali
Tabu walivumilia.
Na kwa kwandalia hili
Mwendo hawakubadili
Raha hawakukubali
Tabu walivumilia.
674
Waendelea kuuwa
Wanyama wanaoliwa
Na nyama yao kugawa
Kwa wakulima raia.
Waendelea kuuwa
Wanyama wanaoliwa
Na nyama yao kugawa
Kwa wakulima raia.
675
Wauwapo kwa upanga
Nyama mmoja mjinga
Hukata na kumchonga
Watu wakawagawia.
Wauwapo kwa upanga
Nyama mmoja mjinga
Hukata na kumchonga
Watu wakawagawia.
676
Hivyo wakajulikana
Kwa wazee na vijana
Watumwa na waungwana
Wote wakawasifia.
Hivyo wakajulikana
Kwa wazee na vijana
Watumwa na waungwana
Wote wakawasifia.
677
Wakasema “Hawa watu
Ni kama wazazi wetu
Bahad kwa nchi yetu
Kuwa wameijilia.
Wakasema “Hawa watu
Ni kama wazazi wetu
Bahad kwa nchi yetu
Kuwa wameijilia.
678
“Hawa kwetu walishaji
Matumbo washibishaji
Wagawi si wafujaji
Mengi wastahilia.”
“Hawa kwetu walishaji
Matumbo washibishaji
Wagawi si wafujaji
Mengi wastahilia.”
679
Nyama ikawa nchini
Kama ndizi za shambani
Watu wakawa rahani
Kwa nyama kuwazidia.
Nyama ikawa nchini
Kama ndizi za shambani
Watu wakawa rahani
Kwa nyama kuwazidia.
680
Mifugo haWakuchinja
Nyama yao kuionja
Ng'ombe mazizi wavunja
Jinsi walivyozidia.
Mifugo haWakuchinja
Nyama yao kuionja
Ng'ombe mazizi wavunja
Jinsi walivyozidia.
681
Watu wakatajinka
Maziwa yakafurika
Nyama zikamiminika
Nchini zikaenea.
Watu wakatajinka
Maziwa yakafurika
Nyama zikamiminika
Nchini zikaenea.
682
Ukanong'ozana umma
“Wameileta neema
Hawa wawindaji wema
Mizimu wawape dia.
Ukanong'ozana umma
“Wameileta neema
Hawa wawindaji wema
Mizimu wawape dia.
683
“Nyamuhanga wabariki
Waondokane na dhiki
Wape mali kwa malaki
Waitawale dunia.
“Nyamuhanga wabariki
Waondokane na dhiki
Wape mali kwa malaki
Waitawale dunia.
684
“Wape faraja Mugasha
Uwaepushe rabusha
Nyakalembe wa maisha
Uwaepushe na njaa.
“Wape faraja Mugasha
Uwaepushe rabusha
Nyakalembe wa maisha
Uwaepushe na njaa.
685
“Irungu wape salama
Washinde kila mnyama
Tuzidi kula minyama
Miungu twawalilia.”
“Irungu wape salama
Washinde kila mnyama
Tuzidi kula minyama
Miungu twawalilia.”
686
Na huu wote wakad
Mutalala ameketi
Nyumbani kama hayati
Akila ha kujinywea.
Na huu wote wakad
Mutalala ameketi
Nyumbani kama hayati
Akila ha kujinywea.
687
Kachutama kama nguu
Ashindwa kwinuka juu
Au kwinua mguu
Unene wamzidia.
Kachutama kama nguu
Ashindwa kwinuka juu
Au kwinua mguu
Unene wamzidia.
688
Unene wamzidia
Kama kameza dunia
Na bado ajipakia
Vyakula kwa magunia.
Unene wamzidia
Kama kameza dunia
Na bado ajipakia
Vyakula kwa magunia.
689
Ulezi vyungu na vyungu
Na matoke kwa mikungu
Vitamu hata vichungu
Kinywanimwe hupotea.
Ulezi vyungu na vyungu
Na matoke kwa mikungu
Vitamu hata vichungu
Kinywanimwe hupotea.
690
Maziwa yenye shahamu
Maji yenye chumvi tamu
Mapombe nayo dawamu
Huyanywa akibugia.
Maziwa yenye shahamu
Maji yenye chumvi tamu
Mapombe nayo dawamu
Huyanywa akibugia.
691
Dunia ina mizungu
Imewazua wazungu
Na Mutalala mwenzangu
Yu mzungu nakwambia.
Dunia ina mizungu
Imewazua wazungu
Na Mutalala mwenzangu
Yu mzungu nakwambia.
692
Mzungu hawezi shiba
Japo angemeza mamba!
Nguruwe katika shamba
Zimwi kadka dunia.
Mzungu hawezi shiba
Japo angemeza mamba!
Nguruwe katika shamba
Zimwi kadka dunia.
693
Akisha kula bahau
Ngoma aliisahau
Ameshapata nafuu
Ya tumbo kujijazia.
Akisha kula bahau
Ngoma aliisahau
Ameshapata nafuu
Ya tumbo kujijazia.
694
Nafuu amesha pata
Kitambi kimeshaota
Kwani kuanza matata
Goma shinda kuwania?
Nafuu amesha pata
Kitambi kimeshaota
Kwani kuanza matata
Goma shinda kuwania?
695
Hajui kushika panga
Wala ngao kujikinga
Vita kwake ni ujinga
Kwani kuvifuatia?
Hajui kushika panga
Wala ngao kujikinga
Vita kwake ni ujinga
Kwani kuvifuatia?
696
Ndivyo alivyoamini
Mutalala ugenini
Na hii yake imani
Vema alishikilia.
Ndivyo alivyoamini
Mutalala ugenini
Na hii yake imani
Vema alishikilia.
697
Wenzake aliwacheka
Kuona wanatumika
Misuli yajisimika
Matumbo yawabonyea.
Wenzake aliwacheka
Kuona wanatumika
Misuli yajisimika
Matumbo yawabonyea.
698
“Maisha ni kula sana
Na kunywa kulewa sana
Na kujizalia wana
Na mwishowe kujifia.
“Maisha ni kula sana
Na kunywa kulewa sana
Na kujizalia wana
Na mwishowe kujifia.
699
“Kamwe si kutangatanga
Kama nzige kwenye anga
Bila makazi kujenga
Na tumbo kujilelea.”
“Kamwe si kutangatanga
Kama nzige kwenye anga
Bila makazi kujenga
Na tumbo kujilelea.”
700
Ndivyo alivyowambia
Mutalala asojaa
Na sasa twamuachia
Yake tumeyasikia.
Ndivyo alivyowambia
Mutalala asojaa
Na sasa twamuachia
Yake tumeyasikia.
701
Yake tumeyasikia
Sasa tuzidi kujua
Nyama za wale shujaa
Nini zilichokizaa.
Yake tumeyasikia
Sasa tuzidi kujua
Nyama za wale shujaa
Nini zilichokizaa.
702
Kwanza na itambulike
Ile Ngoma ya makeke
Kachwankizi Ngoma pweke
Nyakiru aliitwaa.
Kwanza na itambulike
Ile Ngoma ya makeke
Kachwankizi Ngoma pweke
Nyakiru aliitwaa.
703
Nyumbani kaisetiri
Aitunza kwa hadhari
Kuigusa ni hatari
Japo uwe Malikia.
Nyumbani kaisetiri
Aitunza kwa hadhari
Kuigusa ni hatari
Japo uwe Malikia.
704
Kachwankizi imetua
Hapo imejiketia
Kwa saburi yangojea
Siku yake ya kung'aa.
Kachwankizi imetua
Hapo imejiketia
Kwa saburi yangojea
Siku yake ya kung'aa.
705
Sasa basi siku moja
Asubuhi ilikuja
Habari yenye faraja
Watu kuwaamkia.
Sasa basi siku moja
Asubuhi ilikuja
Habari yenye faraja
Watu kuwaamkia.
706
Ikaingia habari
Mapema alifajiri
Habari kweli ya heri
“Senene wameingia.
Ikaingia habari
Mapema alifajiri
Habari kweli ya heri
“Senene wameingia.
707
“Senene wameingia
Mithili wingu la mvua
Kwa wingi wamezidia
Enyi Baziba sikia.
“Senene wameingia
Mithili wingu la mvua
Kwa wingi wamezidia
Enyi Baziba sikia.
708
“Enyi Baziba wafane
Enyi walaji senene
Tokeni nje muone
Alichotuangushia.
“Enyi Baziba wafane
Enyi walaji senene
Tokeni nje muone
Alichotuangushia.
709
“Alichotuangushia
Mugasha mwenye kujua
Asiyeogopa jua
Mweusi mleta mvua.
“Alichotuangushia
Mugasha mwenye kujua
Asiyeogopa jua
Mweusi mleta mvua.
710
“Tokeni nje mabibi
Wanaume hawashibi
Leo hadi magharibi
Wajazie magunia.
“Tokeni nje mabibi
Wanaume hawashibi
Leo hadi magharibi
Wajazie magunia.
711
“Tokeni nje madume
Uzembe wenu ukome
Senene muwaandame
Jioni watajendea.
“Tokeni nje madume
Uzembe wenu ukome
Senene muwaandame
Jioni watajendea.
712
“Tokeni nje watwana
Na mihi yenu vijana
Lete senene kwa bwana
Sulutani kujilia.
“Tokeni nje watwana
Na mihi yenu vijana
Lete senene kwa bwana
Sulutani kujilia.
713
“Tokeni nje watoto
Acheni zenu topito
Kuna mlo motomoto
Washika na kujilia!”
“Tokeni nje watoto
Acheni zenu topito
Kuna mlo motomoto
Washika na kujilia!”
714
Na watu wakaondoka
Kila hirimu na rika
Senene kwenda kusaka
Katika zogo la mvua.
Na watu wakaondoka
Kila hirimu na rika
Senene kwenda kusaka
Katika zogo la mvua.
715
Watu wakajifunika
Milumba yenye viraka
Na ngozi wakajivika
Manyuriyu kuyazuia.
Watu wakajifunika
Milumba yenye viraka
Na ngozi wakajivika
Manyuriyu kuyazuia.
716
Na maji yakaanguka
Kwa ghadhabu ya kizuka
Aridhi ikafurika
Mifuo yakachimbua.
Na maji yakaanguka
Kwa ghadhabu ya kizuka
Aridhi ikafurika
Mifuo yakachimbua.
717
Meme zinamemetuka
Radi nazo zapasuka
Nchi inatetemeka
Kama ukufi sikia!
Meme zinamemetuka
Radi nazo zapasuka
Nchi inatetemeka
Kama ukufi sikia!
718
Wasijali binadamu
Wenye shauku na hamu
Kupata senene tamu
Tumboni kujitilia.
Wasijali binadamu
Wenye shauku na hamu
Kupata senene tamu
Tumboni kujitilia.
719
Wakajitoma sharini
Kwa ari iso kifani
Na kuyalaza majani
Senene kujishikia.
Wakajitoma sharini
Kwa ari iso kifani
Na kuyalaza majani
Senene kujishikia.
720
Senene bila vitimbi
Wakaangnka kiwimbi
Wimbi baada ya wimbi
Watu wakajizolea.
Senene bila vitimbi
Wakaangnka kiwimbi
Wimbi baada ya wimbi
Watu wakajizolea.
721
Senene kawa senene
Kila mahali senene
Kushoto kwako senene
Mbele nyuma na kulia!
Senene kawa senene
Kila mahali senene
Kushoto kwako senene
Mbele nyuma na kulia!
722
Kichwani pako senene
Nyayoni pako senene
Nguoni mwako senene
Senene wakazagaa!
Kichwani pako senene
Nyayoni pako senene
Nguoni mwako senene
Senene wakazagaa!
723
Katika nyasi senene
Kadka miche senene
Na mitini ni senene
Senene wakaenea.
Katika nyasi senene
Kadka miche senene
Na mitini ni senene
Senene wakaenea.
724
Senene kwenye mashamba
Senene kwenye miamba
Kwenye mapaa ya nyumba
Senene wakatambaa!
Senene kwenye mashamba
Senene kwenye miamba
Kwenye mapaa ya nyumba
Senene wakatambaa!
725
Senene miti kishika
Matawi yanavunjika
Matunda yanaanguka
Na mashina kupembea!
Senene miti kishika
Matawi yanavunjika
Matunda yanaanguka
Na mashina kupembea!
Taswira
726
Nyumba wakiikalia
Hubonyeza lake paa
Na ndani wakiingia
Nyumba wanairarua!
Nyumba wakiikalia
Hubonyeza lake paa
Na ndani wakiingia
Nyumba wanairarua!
727
Ndivyo walivyoanguka
Hao senene wa mwaka
Wakazidisha mpaka
Jinsi walivyoenea.
Ndivyo walivyoanguka
Hao senene wa mwaka
Wakazidisha mpaka
Jinsi walivyoenea.
728
Kabula ya siku hio
Senene kwa wingi huo
Hawajakumbana nao
Kiziba kuangukia.
Kabula ya siku hio
Senene kwa wingi huo
Hawajakumbana nao
Kiziba kuangukia.
729
Pia tangu siku hio
Watu wanakiri leo
Senene wengi ja hao
Katu hawajatokea.
Pia tangu siku hio
Watu wanakiri leo
Senene wengi ja hao
Katu hawajatokea.
730
Ntumwa katika nyumbaye
Kuona senene naye
Katamani ajiliye
Utamu kufaidia.
Ntumwa katika nyumbaye
Kuona senene naye
Katamani ajiliye
Utamu kufaidia.
731
Kaamuru watumwaze
Wazanaze na wakeze
Nao wakajitokeze
Senene kumletea.
Kaamuru watumwaze
Wazanaze na wakeze
Nao wakajitokeze
Senene kumletea.
732
Kaamuru watu wote
Ikuluni mwake mwote
Wapigwe mvua watote
Senene kumshikia.
Kaamuru watu wote
Ikuluni mwake mwote
Wapigwe mvua watote
Senene kumshikia.
733
Wakampinga wahenga
Wakamba: “Twahofu janga
Utabaki bila kinga
Sote tukikuachia.”
Wakampinga wahenga
Wakamba: “Twahofu janga
Utabaki bila kinga
Sote tukikuachia.”
734
Akasema bila hofu
“Enyi viumbe dhaifu
Mukama ni mtukufu
Siye mfungwa sikia!
Akasema bila hofu
“Enyi viumbe dhaifu
Mukama ni mtukufu
Siye mfungwa sikia!
735
“Hahitaji asikari
Daima kumsetiri
Kama kwamba yu kauri
Wezi watamvamia.
“Hahitaji asikari
Daima kumsetiri
Kama kwamba yu kauri
Wezi watamvamia.
736
“Semeni yu wapi mtu
Ambaye angethubutu
Kuja Ikuluni mwetu
Mukama kushambulia?
“Semeni yu wapi mtu
Ambaye angethubutu
Kuja Ikuluni mwetu
Mukama kushambulia?
737
“Nendeni enyi wavivu
Toa hapa upumbavu
Lete senene wabivu
Ninataka kujilia.
“Nendeni enyi wavivu
Toa hapa upumbavu
Lete senene wabivu
Ninataka kujilia.
738
“Senene waliofana
Wa matumbo yalotuna
Na vichwa vilivyonona
Ndio ninahitajia.
“Senene waliofana
Wa matumbo yalotuna
Na vichwa vilivyonona
Ndio ninahitajia.
739
“Bali si yenu maneno
Na rangi ya yenu meno
Nendeni kwenye mavuno
Wazee mlopumbaa!”
“Bali si yenu maneno
Na rangi ya yenu meno
Nendeni kwenye mavuno
Wazee mlopumbaa!”
740
Wakaondoka wahenga
Nyuso zimejiviringa
Kuona kawasimanga
Bwana wao kawashua.
Wakaondoka wahenga
Nyuso zimejiviringa
Kuona kawasimanga
Bwana wao kawashua.
741
Katika tufani kali
Manyunyu yenye ukali
Vipara vikahimili
Senene kufuatia.
Katika tufani kali
Manyunyu yenye ukali
Vipara vikahimili
Senene kufuatia.
742
Mukama kabaki hali
Na vijakazi wawili
Vikongwe viso amali
Vyangojea kujifia.
Mukama kabaki hali
Na vijakazi wawili
Vikongwe viso amali
Vyangojea kujifia.
743
Na radi zikapasuka
Dhoruba ikacharuka
Na mvua ikaanguka
Nchi ikaogelea!
Na radi zikapasuka
Dhoruba ikacharuka
Na mvua ikaanguka
Nchi ikaogelea!
744
Nchi ikazamiana
Watu wakaloweana
Senene wafurikana
Kama nyasi wakajaa!
Nchi ikazamiana
Watu wakaloweana
Senene wafurikana
Kama nyasi wakajaa!
745
Na mvua ikawa mvua
Tufani ikazidia
Radi zikajilipua
Na mbingu zikaungua!
Na mvua ikawa mvua
Tufani ikazidia
Radi zikajilipua
Na mbingu zikaungua!
746
Kama panga la maud
Umeme wafuma nti
Na kufyeka katikati
Anga lote kwa sawia!
Kama panga la maud
Umeme wafuma nti
Na kufyeka katikati
Anga lote kwa sawia!
747
Na senene wajibwaga
Mabwawani na kuoga
Tayari kufanywa mboga
Watu kuwatowelea.
Na senene wajibwaga
Mabwawani na kuoga
Tayari kufanywa mboga
Watu kuwatowelea.
748
Watavunjwa zao mbawa
Na miguu kung'olewa
Na pembe kuchopolewa
Na hawatajitetea.
Watavunjwa zao mbawa
Na miguu kung'olewa
Na pembe kuchopolewa
Na hawatajitetea.
749
Watakongolewa wengi
Watiwe kwenye mitungi
Na kuchemshwa kwa wingi
Hadi wamejiivia.
Watakongolewa wengi
Watiwe kwenye mitungi
Na kuchemshwa kwa wingi
Hadi wamejiivia.
750
Wengine watabugiwa
Chunguni wakitolewa
Na wengine watatiwa
Moshini kukaukia.
Wengine watabugiwa
Chunguni wakitolewa
Na wengine watatiwa
Moshini kukaukia.
751
Wakazidia senene
Wanono wenye unene
Kutimia saa nne
Bado tu wanatokea!
Wakazidia senene
Wanono wenye unene
Kutimia saa nne
Bado tu wanatokea!
752
Na watu wakawapata
Kwa wingi wakawachota
Mihi yote ikaputa
Ikajaa kuzidia.
Na watu wakawapata
Kwa wingi wakawachota
Mihi yote ikaputa
Ikajaa kuzidia.
753
Na kila mtu Kanyigo
Mkubwa hata mdogo
Alikusanya mzigo
Wa senene kujilia.
Na kila mtu Kanyigo
Mkubwa hata mdogo
Alikusanya mzigo
Wa senene kujilia.
754
Na bado walendelea
Senene kuzoazoa
Furusa wakitambua
Haiwezi kurejea.
Na bado walendelea
Senene kuzoazoa
Furusa wakitambua
Haiwezi kurejea.
755
Hata Mutalala naye
Bila kujali haliye
Alichukua fimboye
Tufanini kuingia.
Hata Mutalala naye
Bila kujali haliye
Alichukua fimboye
Tufanini kuingia.
756
Akichupa kama chura
Kitumboche chamkera
Senene kiteka nyara
Aliowafumania.
Akichupa kama chura
Kitumboche chamkera
Senene kiteka nyara
Aliowafumania.
757
Aliwashika mikia
Meno wasije mtia
Wakimuuma hulia
Kisha akawaachia.
Aliwashika mikia
Meno wasije mtia
Wakimuuma hulia
Kisha akawaachia.
758
Hatima aliwashinda
Vichwa alipowaponda
Akaweza kuyapinda
Meno yao ya udhia.
Hatima aliwashinda
Vichwa alipowaponda
Akaweza kuyapinda
Meno yao ya udhia.
759
Watu wote kijijini
Walitoka majumbani
Hapakubakia ndani
Ila waliougua.
Watu wote kijijini
Walitoka majumbani
Hapakubakia ndani
Ila waliougua.
760
Ila waliougua
Na wachache mashujaa
Ambao walibakia
Mipango kujipangia.
Ila waliougua
Na wachache mashujaa
Ambao walibakia
Mipango kujipangia.
761
Wakitengeza mipango
Ya kuingia ulingo
Kwa mikuki na magongo
Himaya kujitwalia.
Wakitengeza mipango
Ya kuingia ulingo
Kwa mikuki na magongo
Himaya kujitwalia.
762
Siku hii waliona
Kaileta Maulana
Kuwawezesha kukana
Wanaowasujudia.
Siku hii waliona
Kaileta Maulana
Kuwawezesha kukana
Wanaowasujudia.
763
Imeletwa na Mizimu
Kuwafanya mahakimu
Juu ya hii kaumu
Isiyo na mtetea.
Imeletwa na Mizimu
Kuwafanya mahakimu
Juu ya hii kaumu
Isiyo na mtetea.
764
Hivyo walitafakari
Kwa hamu tena kwa siri
Vipi wapate fahari
Ile waliyoijia.
Hivyo walitafakari
Kwa hamu tena kwa siri
Vipi wapate fahari
Ile waliyoijia.
765
Na wakisha kuamua
Silaha walichukua
Na kutoka kishujaa
Kigarama kwelekea.
Na wakisha kuamua
Silaha walichukua
Na kutoka kishujaa
Kigarama kwelekea.
766
Na mvua ilifuliza
Manyunyu kuyanyunyiza
Na pepo zilipuliza
Kwa shari ya kuzidia.
Na mvua ilifuliza
Manyunyu kuyanyunyiza
Na pepo zilipuliza
Kwa shari ya kuzidia.
767
Senene wakianguka
Tokajuu kwa Mahoka
Juu, chini, wafurika
Mawindo ya kujiua.
Senene wakianguka
Tokajuu kwa Mahoka
Juu, chini, wafurika
Mawindo ya kujiua.
768
Walikwenda kwa harara
Bila hata kudorora
Waenda kujipa kura
Kwa mikuki na jambia.
Walikwenda kwa harara
Bila hata kudorora
Waenda kujipa kura
Kwa mikuki na jambia.
769
Senene walifuata
Nyuma yao kuwaita
Waende kuwakamata
Wao hawakusikia.
Senene walifuata
Nyuma yao kuwaita
Waende kuwakamata
Wao hawakusikia.
770
Manyunyu yakiwatosa
Pepo zikiwapapasa
Senene wakiwagusa
Wao wanaendelea.
Manyunyu yakiwatosa
Pepo zikiwapapasa
Senene wakiwagusa
Wao wanaendelea.
771
Watu wakiwatazama
Huwafikiria wema
“Hawa wawinda wa nyama
Senene wafuatia.”
Watu wakiwatazama
Huwafikiria wema
“Hawa wawinda wa nyama
Senene wafuatia.”
772
Nao wakasonga mbele
Bila kujali kelele
Ambazo ziwazingile
Za dhoruba na ghasia.
Nao wakasonga mbele
Bila kujali kelele
Ambazo ziwazingile
Za dhoruba na ghasia.
773
Walikwenda kwa shauku
Kwanyoyoza dukuduku
Kukabili lao juku
Walilojiamulia.
Walikwenda kwa shauku
Kwanyoyoza dukuduku
Kukabili lao juku
Walilojiamulia.
774
Mavazi yalilowana
Baridi iliwabana
Upepo uliwakuna
Bila wao kutambua.
Mavazi yalilowana
Baridi iliwabana
Upepo uliwakuna
Bila wao kutambua.
775
Wakaenda, wakaenda
Kilima wakakipanda
Bila taabu na shida
Ikulu wakelemea.
Wakaenda, wakaenda
Kilima wakakipanda
Bila taabu na shida
Ikulu wakelemea.
776
Hapo njia ili pweke
Walikuwa wao peke
Raia wasioneke
Senene wajishikia.
Hapo njia ili pweke
Walikuwa wao peke
Raia wasioneke
Senene wajishikia.
777
Na radi zinarindima
Na dhoruba inavuma
Na baridi imeuma
Na inamwagika mvua.
Na radi zinarindima
Na dhoruba inavuma
Na baridi imeuma
Na inamwagika mvua.
778
Bali hawa wasijali
Waenda kwa nyoyo kali
Na nyuso zenye uvuli
Wa tamaa ya kuua.
Bali hawa wasijali
Waenda kwa nyoyo kali
Na nyuso zenye uvuli
Wa tamaa ya kuua.
779
Walipofika langoni
Langoni pa sulutani
Wakaingilia ndani
Wawili si kuzidia.
Walipofika langoni
Langoni pa sulutani
Wakaingilia ndani
Wawili si kuzidia.
780
Nyakiru aliingia
Na Kanyamaishwa pia
Na kumi si kupungua
Langoni wakabakia.
Nyakiru aliingia
Na Kanyamaishwa pia
Na kumi si kupungua
Langoni wakabakia.
781
Wakajiendea ndani
Na tazama sulutani
Yupo pale sebuleni
Salama kajikalia.
Wakajiendea ndani
Na tazama sulutani
Yupo pale sebuleni
Salama kajikalia.
782
Katika enzi kazama
Ametarama kikama
Buni kavu anauma
Kwa raha ametulia.
Katika enzi kazama
Ametarama kikama
Buni kavu anauma
Kwa raha ametulia.
783
Kakaa kama chuguu
Katulia kama nguu
Mikono hadi miguu
Vikuku amevalia.
Kakaa kama chuguu
Katulia kama nguu
Mikono hadi miguu
Vikuku amevalia.
784
Tumbole laning'inia
Ja boga lilokomaa
Ungedhani malikia
Ataka kujifungua.
Tumbole laning'inia
Ja boga lilokomaa
Ungedhani malikia
Ataka kujifungua.
785
Na vijakazi viwili
Vikongwe roho na mwili
Mukama vimekabili
Bwabwaja vyambwatia.
Na vijakazi viwili
Vikongwe roho na mwili
Mukama vimekabili
Bwabwaja vyambwatia.
786
Akiwaona vijana
Sulutani akanena
“Karibuni wangu wana
Ili tupate ongea.
Akiwaona vijana
Sulutani akanena
“Karibuni wangu wana
Ili tupate ongea.
787
“Nimechoka na ukiwa
Kinywa sijakifunguwa
Vijakazi wangu hawa
Hawajui kuongea.
“Nimechoka na ukiwa
Kinywa sijakifunguwa
Vijakazi wangu hawa
Hawajui kuongea.
788
“Na wala siwalaumu
Ukabwela nao sumu
Wangakuwa na adhamu
Kusema wangalijua.
“Na wala siwalaumu
Ukabwela nao sumu
Wangakuwa na adhamu
Kusema wangalijua.
789
“Na maajuza kunena
Vilevile siyo sana
Meno vinywani hawana
Ni fizi zimebakia.
“Na maajuza kunena
Vilevile siyo sana
Meno vinywani hawana
Ni fizi zimebakia.
790
“Ni mkiwa mtawala
Anapokaa mahala
Patovu pa kabaila
Wawezao kuongea.
“Ni mkiwa mtawala
Anapokaa mahala
Patovu pa kabaila
Wawezao kuongea.
791
“Hivyo ninyi karibuni
Ijapo mu watu duni
Kujalisi ninadhani
Mwaweza kujaribia.”
“Hivyo ninyi karibuni
Ijapo mu watu duni
Kujalisi ninadhani
Mwaweza kujaribia.”
792
Na mmoja mjakazi
Macho yake machunguzi
Aliyakodoa wazi
Kwake Kanyamaishua.
Na mmoja mjakazi
Macho yake machunguzi
Aliyakodoa wazi
Kwake Kanyamaishua.
793
Kwake macho alikaza
Bila kope kupepeza
Kana kwamba anawaza
Huyu wapi katokea.
Kwake macho alikaza
Bila kope kupepeza
Kana kwamba anawaza
Huyu wapi katokea.
794
Akatamka Nyakiru
“Ni mwema wako udhuru
Nasi tunakushukuru
Udhuru kuutongoa.
Akatamka Nyakiru
“Ni mwema wako udhuru
Nasi tunakushukuru
Udhuru kuutongoa.
795
“Bali sisi e dubwana
Hatuji kwa kupatana
Bali twaja kwa hiana
Mauti tumechukua!”
“Bali sisi e dubwana
Hatuji kwa kupatana
Bali twaja kwa hiana
Mauti tumechukua!”
796
Vijakazi kusikia
Vilio wakaangua
Mmoja macho katia
Kwake Kanyamaishua.
Vijakazi kusikia
Vilio wakaangua
Mmoja macho katia
Kwake Kanyamaishua.
797
Na Mukama akakaa
Amepigwa na butaa
Sauti hakuitoa
Macho aliwakazia.
Na Mukama akakaa
Amepigwa na butaa
Sauti hakuitoa
Macho aliwakazia.
798
Nyakiru akaongeza
“Hatuji kukutukuza
Tunakuja kukukuza
Enziyo kukuambua.
Nyakiru akaongeza
“Hatuji kukutukuza
Tunakuja kukukuza
Enziyo kukuambua.
799
“Tunakuja kwa kisasi
Tunakuja kwa maasi
Ili kutakasa nsi
Ambayo umechafua.
“Tunakuja kwa kisasi
Tunakuja kwa maasi
Ili kutakasa nsi
Ambayo umechafua.
800
“Twaja kukupatiliza
Kwa nguvu zake Muweza
Ukiona unaweza
Waweza kujiokoa!”
“Twaja kukupatiliza
Kwa nguvu zake Muweza
Ukiona unaweza
Waweza kujiokoa!”
801
Na hapo Mukama Ntumwa
Tumbo akanza kuumwa
“Mbwa! Wana wa watumwa
Akili zimewapaa!
Na hapo Mukama Ntumwa
Tumbo akanza kuumwa
“Mbwa! Wana wa watumwa
Akili zimewapaa!
802
“Akili zimewapaa
Bila nyinyi kuelewa
Mwanena msichojua
Mwaja moto kuchezea!
“Akili zimewapaa
Bila nyinyi kuelewa
Mwanena msichojua
Mwaja moto kuchezea!
803
“Watoto mnazo ndwele
Bongonimwenu zitele
Kuthubutu kama vile
Mukama kumtishia!
“Watoto mnazo ndwele
Bongonimwenu zitele
Kuthubutu kama vile
Mukama kumtishia!
804
“Ntumwa katu si kabwela
Ntumwamtu kabaila
Kuguswa na mtu fala
Hilo halitatokea!
“Ntumwa katu si kabwela
Ntumwamtu kabaila
Kuguswa na mtu fala
Hilo halitatokea!
805
“Mngali wana wachanga
Mmezidiwa ujinga
Akili imewachenga
Nadhari imepungua.
“Mngali wana wachanga
Mmezidiwa ujinga
Akili imewachenga
Nadhari imepungua.
806
“Angalia, angalia
Kuwaonya narudia
Haliwezi kutokea
Mnalolidhamiria!”
“Angalia, angalia
Kuwaonya narudia
Haliwezi kutokea
Mnalolidhamiria!”
807
Nyakiru akatongowa
“Litatokea na kuwa!”
Na papo akainuwa
Mkuki na kumtia!
Nyakiru akatongowa
“Litatokea na kuwa!”
Na papo akainuwa
Mkuki na kumtia!
808
Akamfuma mkuki
Ukaingia kwa maki
Mambo yakawa mkiki
Mukama kamrukia!
Akamfuma mkuki
Ukaingia kwa maki
Mambo yakawa mkiki
Mukama kamrukia!
809
Kanyamaishwa tazama
Naye pia kamfuma
Mkuki ukamzama
Na Ntumwa akaugua.
Kanyamaishwa tazama
Naye pia kamfuma
Mkuki ukamzama
Na Ntumwa akaugua.
810
Akajiuma vidole
Na kupaaza kelele
“Ninakufa wangu ole
Vitwana vimeniua!”
Akajiuma vidole
Na kupaaza kelele
“Ninakufa wangu ole
Vitwana vimeniua!”
811
Na Ntumwa akageuka
Kitamtn kimetoboka
Damu zampukutika
Akataka kukimbia.
Na Ntumwa akageuka
Kitamtn kimetoboka
Damu zampukutika
Akataka kukimbia.
812
Asiweze kaanguka
Hali amefadhaika
Macho yamemkodoka
Adui yamwangalia.
Asiweze kaanguka
Hali amefadhaika
Macho yamemkodoka
Adui yamwangalia.
813
Macho akayakodoa
Kwake Kanyamaishua
Kisha akayashushia
Shingoni pake sikia.
Macho akayakodoa
Kwake Kanyamaishua
Kisha akayashushia
Shingoni pake sikia.
814
Palepale kayakaza
Wala hakuyapepeza
Hirizi aichunguza
Kwani ameitambua!
Palepale kayakaza
Wala hakuyapepeza
Hirizi aichunguza
Kwani ameitambua!
815
Hirizi ni ya ukoo
Mwana wake siku hio
Walipomtoa kwao
Ali amejivalia.
Hirizi ni ya ukoo
Mwana wake siku hio
Walipomtoa kwao
Ali amejivalia.
816
Zamani hirizi hiyo
Mwanawe katupwa nayo
Na sasa karudi nayo
Ni leo ayangalia.
Zamani hirizi hiyo
Mwanawe katupwa nayo
Na sasa karudi nayo
Ni leo ayangalia.
Taswira
817
Na hili alipoona
Kajua huyu ni mwana
Mwana wake wa laana
Kashiriki kumuua!
Na hili alipoona
Kajua huyu ni mwana
Mwana wake wa laana
Kashiriki kumuua!
818
Kamba kwa sauti chungu
“Enyi vijakazi wangu
Elezeni ulimwengu
Mwanangu ameniua!”
Kamba kwa sauti chungu
“Enyi vijakazi wangu
Elezeni ulimwengu
Mwanangu ameniua!”
819
Na hapo akaanguka
Rohoye ikamtoka
Machoye yakafumbika
Na shingo likalegea.
Na hapo akaanguka
Rohoye ikamtoka
Machoye yakafumbika
Na shingo likalegea.
820
Nao vijakazi hao
Wakatoka mbio mbio
Wakalia “Yoo! Yoo!
Mukama wamemuua!”
Nao vijakazi hao
Wakatoka mbio mbio
Wakalia “Yoo! Yoo!
Mukama wamemuua!”
821
Na wale wakaingia
Nje waliobakia
Wakakuta analia
Kanyamaishwa sikia.
Na wale wakaingia
Nje waliobakia
Wakakuta analia
Kanyamaishwa sikia.
822
Kanyamaishwa kasema
“Moyo wangu una homa
Sikutenda jambo jema
Mtima waniambia.
Kanyamaishwa kasema
“Moyo wangu una homa
Sikutenda jambo jema
Mtima waniambia.
823
“Maneno nimesikia
Hayati akitongoa
Ati mwana kamuua
Mwana aliyemzaa!
“Maneno nimesikia
Hayati akitongoa
Ati mwana kamuua
Mwana aliyemzaa!
824
“Babangu simfahamu
Mamangu simfahamu
Walakini nafahamu
Kiziba nilitokea.
“Babangu simfahamu
Mamangu simfahamu
Walakini nafahamu
Kiziba nilitokea.
825
“Na hii hirizi yangu
Tangu utotoni mwangu
Havaa shingoni mwangu
Sijapata kuitoa.
“Na hii hirizi yangu
Tangu utotoni mwangu
Havaa shingoni mwangu
Sijapata kuitoa.
826
“Na mama alinambia
Yule aliyenilea
'Hirizi uliyovaa
Si ya kabwela tambua!'
“Na mama alinambia
Yule aliyenilea
'Hirizi uliyovaa
Si ya kabwela tambua!'
827
“Nikitazama usoni
Mwake huyu sulutani
Ninaanza kuamini
Yale niliyoambiwa.
“Nikitazama usoni
Mwake huyu sulutani
Ninaanza kuamini
Yale niliyoambiwa.
828
“Nimekufuru hakika
Nimekosea Mahoka
O! Niliyelaanika
Sisitahili afua!”
“Nimekufuru hakika
Nimekosea Mahoka
O! Niliyelaanika
Sisitahili afua!”
829
Nyakiiru kampoza
“Kaka wacha kujisoza
Vipi kosa lakuliza
Usilolikusudia?
Nyakiiru kampoza
“Kaka wacha kujisoza
Vipi kosa lakuliza
Usilolikusudia?
830
“Na wala huna hakika
Kwamba aliyotamka
Mfu yamethibitika
Ni kweli mia kwa mia.
“Na wala huna hakika
Kwamba aliyotamka
Mfu yamethibitika
Ni kweli mia kwa mia.
831
“Tulia tutauliza
Wazee na maajuza
Mambo yote kueleza
Kabula ya kuamua.
“Tulia tutauliza
Wazee na maajuza
Mambo yote kueleza
Kabula ya kuamua.
832
“Mengl tumesha yatenda
Kukoma hapa ni shida
Tutafululiza kwenda
Hadi mwisho kufikia.”
“Mengl tumesha yatenda
Kukoma hapa ni shida
Tutafululiza kwenda
Hadi mwisho kufikia.”
833
Na vijana kawambia
Maiti kumuinua
Waende kumfukia
Kaburini kumtia.
Na vijana kawambia
Maiti kumuinua
Waende kumfukia
Kaburini kumtia.
834
Ndivyo alivyofariki
Huyu dhalimu wa haki
Akilia kwenye dhiki
Hana wa kumtetea.
Ndivyo alivyofariki
Huyu dhalimu wa haki
Akilia kwenye dhiki
Hana wa kumtetea.
835
Ndivyo alivyofanki
Akaiacha miliki
Akaacha halaiki
Aliyoiatamia.
Ndivyo alivyofanki
Akaiacha miliki
Akaacha halaiki
Aliyoiatamia.
836
Ndivyo alivyofariki
Akenda bila rafiki
Kwenenda akadiriki
Kusiko na kurejea.
Ndivyo alivyofariki
Akenda bila rafiki
Kwenenda akadiriki
Kusiko na kurejea.
837
Nayo mvua ikanyesha
Na umeme ukawasha
Dhoruba ikajirusha
Kwa nguvu za kuzidia!
Nayo mvua ikanyesha
Na umeme ukawasha
Dhoruba ikajirusha
Kwa nguvu za kuzidia!
838
Na Nyakiru akasema
“Siwezi kuwa Mukama
Na kuutawala umma
Peke yangu nakwambia.
Na Nyakiru akasema
“Siwezi kuwa Mukama
Na kuutawala umma
Peke yangu nakwambia.
839
“Kanyamaishwa sikiza
Acha sasa kujiliza
Kitini ninakukweza
Sote tutakikalia.”
“Kanyamaishwa sikiza
Acha sasa kujiliza
Kitini ninakukweza
Sote tutakikalia.”
840
Kanyamaishwa kakana
Akasema “Haja sina
Sitayakubali tena
Ambayo wanipangia.”
Kanyamaishwa kakana
Akasema “Haja sina
Sitayakubali tena
Ambayo wanipangia.”
841
Wakabishana kwa nguvu
Saud zikawa kavu
Kila mmoja mvivu
Ufumbuzi kufikia.
Wakabishana kwa nguvu
Saud zikawa kavu
Kila mmoja mvivu
Ufumbuzi kufikia.
842
Nyakiru kasisitiza
Mwenzie kubembeleza
“Mpenzi nakueleza
Vema kiti kukalia.
Nyakiru kasisitiza
Mwenzie kubembeleza
“Mpenzi nakueleza
Vema kiti kukalia.
843
“Tumesafiri pamoja
Tumeteseka pamoja
Na tumeua pamoja
Vipi sasa wanachia?
“Tumesafiri pamoja
Tumeteseka pamoja
Na tumeua pamoja
Vipi sasa wanachia?
844
“Tutakalia kwa zamu
Hiki kid cha adhamu
Sote tuwe mahakimu
Watawala wa raia!”
“Tutakalia kwa zamu
Hiki kid cha adhamu
Sote tuwe mahakimu
Watawala wa raia!”
845
Mwishowe bila kutaka
Mwenzie akaitika
Ukafikiwa mwafaka
Wote Bakama wakawa.
Mwishowe bila kutaka
Mwenzie akaitika
Ukafikiwa mwafaka
Wote Bakama wakawa.
846
Kanyamaishwa lakini
Hakutulia moyoni
Mateseko na huzuni
Rohoni vilibakia.
Kanyamaishwa lakini
Hakutulia moyoni
Mateseko na huzuni
Rohoni vilibakia.
847
Na habari zikafika
Huko nje kwenye nyika
“Mukama kesha ondoka
Mambo yamesha timia!”
Na habari zikafika
Huko nje kwenye nyika
“Mukama kesha ondoka
Mambo yamesha timia!”
848
Watu wote wakatoka
Nyikani wamejitwika
Senene walioshika
Makuu kujionea.
Watu wote wakatoka
Nyikani wamejitwika
Senene walioshika
Makuu kujionea.
849
Walipofika tazama
Nyakiiru ni Mukama
Na Kanyamaishwa mwema
Kandoye kajikalia.
Walipofika tazama
Nyakiiru ni Mukama
Na Kanyamaishwa mwema
Kandoye kajikalia.
850
Nyumao wamejikita
Asikari wa matata
Silaha zametameta
Kivita wamekalia.
Nyumao wamejikita
Asikari wa matata
Silaha zametameta
Kivita wamekalia.
851
Wenyeji wakauliza
“Ewe mgeni eleza
Nani amekutawaza
Ukama kukupatia?”
Wenyeji wakauliza
“Ewe mgeni eleza
Nani amekutawaza
Ukama kukupatia?”
852
Nyakiiru kaeleza
“Watukufu sikiliza
Sisi tumejitokeza
Haki zenu kutetea.
Nyakiiru kaeleza
“Watukufu sikiliza
Sisi tumejitokeza
Haki zenu kutetea.
853
“Tumeiona dhuluma
Aliyotenda Mukama
Tukashikwa na huruma
Ndipo tulipomuua.
“Tumeiona dhuluma
Aliyotenda Mukama
Tukashikwa na huruma
Ndipo tulipomuua.
854
“Mwaweza kutuhukumu
Bali hili lifahamu
Hatuji kuwadhulumu
Tujile kuwakomboa.
“Mwaweza kutuhukumu
Bali hili lifahamu
Hatuji kuwadhulumu
Tujile kuwakomboa.
855
“Kama baya tumetenda
Kwa nyoka kichwa kuponda
Mnaweza kutukinda
Kwani tu wenye hatia.
“Kama baya tumetenda
Kwa nyoka kichwa kuponda
Mnaweza kutukinda
Kwani tu wenye hatia.
856
“Chukueni misu yenu
Noeni mikuki yenu
Sisi tu halali zenu
Mnaweza kutuua.”
“Chukueni misu yenu
Noeni mikuki yenu
Sisi tu halali zenu
Mnaweza kutuua.”
857
Akimaliza Nyakiru
Kuwaeleza udhuru
Raia wakashukuru
Shangwe wakampigia.
Akimaliza Nyakiru
Kuwaeleza udhuru
Raia wakashukuru
Shangwe wakampigia.
858
Bila kufanya udhia
Wakasujudu raia
Nyakiru wakamwambia
“Nchi umeiokoa.”
Bila kufanya udhia
Wakasujudu raia
Nyakiru wakamwambia
“Nchi umeiokoa.”
Taswira
859
Na wote makabaila
Wakichelea madhila
Wakondoka halahala
Bugandika kwelemea.
Na wote makabaila
Wakichelea madhila
Wakondoka halahala
Bugandika kwelemea.
860
Huko wakajikusanya
Tayari vita kufanya
Wageni kuwanyang'anya
Enzi waliyochukua.
Huko wakajikusanya
Tayari vita kufanya
Wageni kuwanyang'anya
Enzi waliyochukua.
861
Nyakiiru akatoka
Na jeshi lilopanuka
Akaenda Bugandika
Adui kushambulia.
Nyakiiru akatoka
Na jeshi lilopanuka
Akaenda Bugandika
Adui kushambulia.
862
Majeshi yakakutana
Ikawa bimbirishana
Wakatana, wauana
Maid zikazagaa.
Majeshi yakakutana
Ikawa bimbirishana
Wakatana, wauana
Maid zikazagaa.
863
Maid zalaliana
Damu zafurikiana
Waume wanapambana
Wengine waangamia.
Maid zalaliana
Damu zafurikiana
Waume wanapambana
Wengine waangamia.
Taswira
864
Na ikifika jioni
Ikadhihiri yakini
Maadui wako chini
Nguvu zimewaishia.
Na ikifika jioni
Ikadhihiri yakini
Maadui wako chini
Nguvu zimewaishia.
865
Vitani wakajitoa
Na kuanza kukimbia
Hima wakafuatiwa
Wengi wakaangamia.
Vitani wakajitoa
Na kuanza kukimbia
Hima wakafuatiwa
Wengi wakaangamia.
866
Hapo vita vikakoma
Naye Nyakiru Mukama
Akarudi Kigarama
Mukama kampokea.
Hapo vita vikakoma
Naye Nyakiru Mukama
Akarudi Kigarama
Mukama kampokea.
867
Na pamoja kwa sawia
Kiti wakakikalia
Watu wakasujudia
Na kuwatii kwa nia.
Na pamoja kwa sawia
Kiti wakakikalia
Watu wakasujudia
Na kuwatii kwa nia.
868
Na wakaitwa wazee
Waje wawaelezee
Ili siri waijue
Yake Kanyamaishua.
Na wakaitwa wazee
Waje wawaelezee
Ili siri waijue
Yake Kanyamaishua.
869
Na wakiisha tamka
Ikawa hakuna shaka
Mambo yakadhihirika
Jinsi walivyodhania.
Na wakiisha tamka
Ikawa hakuna shaka
Mambo yakadhihirika
Jinsi walivyodhania.
870
Kanyamaishwa kalia
Na matanga kukalia
Babaye kukumbukia
Na tendole kutubia.
Kanyamaishwa kalia
Na matanga kukalia
Babaye kukumbukia
Na tendole kutubia.
871
Na matanga yakapita
Kanyamaishwa kapata
Maradhi yenye matata
Asiweze kujinua.
Na matanga yakapita
Kanyamaishwa kapata
Maradhi yenye matata
Asiweze kujinua.
872
Nyakiru akasumbuka
Daima ashughulika
Waganga akiwasaka
Mwenzie kumtibia.
Nyakiru akasumbuka
Daima ashughulika
Waganga akiwasaka
Mwenzie kumtibia.
873
Mwisho kaona kijana
Dawa hazina maana
Sahibu azidi sana
Mwilini kudidimia.
Mwisho kaona kijana
Dawa hazina maana
Sahibu azidi sana
Mwilini kudidimia.
874
Na muda ulipopita
Mauti yakamuita
Kifo kikamkamata
Mgonjwa akajifia.
Na muda ulipopita
Mauti yakamuita
Kifo kikamkamata
Mgonjwa akajifia.
875
Akafa Kanyamaishwa
Kakoma kutaabishwa
Shimoni kateremshwa
Watu wakamlilia.
Akafa Kanyamaishwa
Kakoma kutaabishwa
Shimoni kateremshwa
Watu wakamlilia.
876
Ndivyo alivyofariki
Huyu kijana wa dhiki
Bila kuacha kisiki
Katika hii dunia.
Ndivyo alivyofariki
Huyu kijana wa dhiki
Bila kuacha kisiki
Katika hii dunia.
877
Nyakiru kamlilia
Akalia, akalia
Akamuombolezea
Mwenzi aliyemfaa.
Nyakiru kamlilia
Akalia, akalia
Akamuombolezea
Mwenzi aliyemfaa.
878
Myezi miwili Nyakiru
Katu hakuona nuru
Kijiji hakukizuru
Nyumbani alitulia.
Myezi miwili Nyakiru
Katu hakuona nuru
Kijiji hakukizuru
Nyumbani alitulia.
879
Nyumbani alitulia
Matanga kumkalia
Rafikiye wa dunia
Ambaye hatarejea.
Nyumbani alitulia
Matanga kumkalia
Rafikiye wa dunia
Ambaye hatarejea.
880
Na matanga yakiisha
Nyakiru akajikosha
Nyumbani kajiondoshi
Nuru kuiangalia.
Na matanga yakiisha
Nyakiru akajikosha
Nyumbani kajiondoshi
Nuru kuiangalia.
881
Akabaki peke yake
Mtawalaji mpweke
Akawa Mukama peke
Kiziba kuangalia.
Akabaki peke yake
Mtawalaji mpweke
Akawa Mukama peke
Kiziba kuangalia.
Taswira
882
Kisha akajenga nyumba
Akaikata na vyumba
Halafu akaipamba
Mapambo ya kuvutia.
Kisha akajenga nyumba
Akaikata na vyumba
Halafu akaipamba
Mapambo ya kuvutia.
883
Akamaliza ujenzi
Akaleta Kachwankizi
Kaiingiza kwa enzi
Iketi na kulowea.
Akamaliza ujenzi
Akaleta Kachwankizi
Kaiingiza kwa enzi
Iketi na kulowea.
884
Ndoto ikakamilika
Kachwankizi ikatika
Di! di! di! di! kutamka
Enzi mpya kwa raia.
Ndoto ikakamilika
Kachwankizi ikatika
Di! di! di! di! kutamka
Enzi mpya kwa raia.
885
Na mjumbe akatoka
Kibumbiro akafika
Moto mpya akateka
Kiziba akarejea.
Na mjumbe akatoka
Kibumbiro akafika
Moto mpya akateka
Kiziba akarejea.
886
Huu moto wa ukama
Uliwashwa kwa heshima
Ngoma ilipochutama
Usiachwe kuzimia.
Huu moto wa ukama
Uliwashwa kwa heshima
Ngoma ilipochutama
Usiachwe kuzimia.
887
Mambo yalipotuliya
Nyakiru wakamtiya
Jina la Kibi - Kibaya
Kwani watu ameua.
Mambo yalipotuliya
Nyakiru wakamtiya
Jina la Kibi - Kibaya
Kwani watu ameua.
888
Akalikubali jina
Kwa moyo wa kiungwana
Na ndivyo ajulikana
Katika historia.
Akalikubali jina
Kwa moyo wa kiungwana
Na ndivyo ajulikana
Katika historia.
Taswira
889
Hapa sasa nakomea
Kituo nimefikia
Nyuma yaliyotokea
Hapa sitasimulia.
Hapa sasa nakomea
Kituo nimefikia
Nyuma yaliyotokea
Hapa sitasimulia.
890
Nimesema ya kutosha
Na wala sikupotosha
Na hadithi imekwisha
Tamati tumefikia.
Nimesema ya kutosha
Na wala sikupotosha
Na hadithi imekwisha
Tamati tumefikia.
891
Mtunzi ni chipukizi
Mugyabuso Mulokozi
Mulokozi ni mzazi
Baba aliyemzaa.
Mtunzi ni chipukizi
Mugyabuso Mulokozi
Mulokozi ni mzazi
Baba aliyemzaa.
892
Ni kijana atokea
Upeo hajafikia
Makosa ukimtoa
Sana atafurahia.
Ni kijana atokea
Upeo hajafikia
Makosa ukimtoa
Sana atafurahia.
Maneno ya Kihaya na lugha nyingine za asili
Ubeti
|
Neno
|
Maelezo
|
13
|
Ruhanga
|
Mungu Mkuu, Muumba.
|
27
|
Kintu
|
Mwanamume wa kwanza kwa mujibu wa imani za baadhi ya watu waishio mkoa wa Kagera na Uganda ya Kusini.
|
28
|
Kikazi
|
Mwanamke wa kwanza, mke wake Kintu.
|
31
|
Mugasha
|
Muungu wa Ziwa Viktoria, na mtawala wa tufani, mvua, kwa mujibu wadini zajadi katika mikoa ya Kagera, Mwanza na Kusini mwa Uganda. Wasukuma humwita Nyangassa, Wakerewe humwita Mugasa na Waganda humwita Mukasa.
|
32
|
Ngassa
|
(Kisukuma) Nyangassa, Mugasha.
|
Mukasa
|
(Kiganda) Mugasha.
| |
33
|
Nyanja
|
Nyanza, Ziwa au mto.
|
Lweru
|
Ziwa Viktoria.
| |
35
|
Nyakalembe
|
Mke wa Mugasha na Muungu wa kilimo kadka dini za jadi.
|
36
|
Kasana
|
Muungu wa uwindaji.
|
37
|
Irungu
|
Muungu wa mapori na uwindaji.
|
38
|
Lyangombe
|
Muungu wa wafugaji.
|
39
|
Kaihura-Nkuba
|
Muungu waradi, mwanawe Mugasha.
|
40
|
Wamala
|
Muungu Kiongozi wa Wachwezi.
|
Wachwezi
|
Kundi la Miungu na Mizimu, hususan lile linalohusishwa na Wamala kiukoo.
| |
Huyamala
|
Huyamaliza.
| |
41
|
Kagoro
|
Mtoto wa Wamala, Muungu wa vita.
|
42
|
Kilo
|
Muungu wa usiku.
|
43
|
Kasi
|
Muungu wa kike anayehusika na kilimo.
|
Rugila
|
Muungu wa kike anayehusika na uzazi.
| |
59
|
Mukama
|
Mfalme, sultani.
|
Bike
|
Mtawala wajadi wa Kiziba aliyeuawa na Ntumwa, labda kwenye karne ya 15.
| |
78
|
Nanga
|
Ala ya muziki yenye nyuzi saba na umbo kama la mtumbwi.
|
89
|
Ngisha
|
Hirizi.
|
96
|
Katonda
|
Mungu, Muumba.
|
104
|
Ukama
|
Ufalme.
|
129
|
Mshonge
|
Nyumba ya jadi ya Wahaya, Wachaga, naWaganda, ambayo paa lake huteremka mpaka ardhini; haina kuta za udongo au matofali.
|
133
|
Kanwa
|
Mdomo, kinywa.
|
Matoke
|
Ndizi zilizopikwa.
| |
139
|
Kukaga
|
Kuhisi, kutambua.
|
144
|
Ugino
|
Ufizi.
|
171
|
Wazana
|
Abazana, watumwa wa kike. Mmoja ni muzana.
|
175
|
Bami
|
Machifu au wazee wenye heshima. Mmojani mwami.
|
178
|
Habuka
|
Neno litumikalo kumsalimu mfalme, maana yake kama dhihirika au tokea hadharani.
|
Lugaba
|
Mtoaji wa fadhila, mkarimu.
| |
181
|
Wakazi
|
Bakazi, wanawake. Mmoja ni mukazi.
|
199
|
Ukazi
|
Hali ya kuwa mwanamke.
|
203
|
Mizio
|
Miziro, miiko.
|
230
|
Kanyamaishwa
|
Jina lenye maana yamtoto aliyeokotwa porini kama mnyama.
|
247
|
Kachwankizi
|
Jina la ngoma ya utawala wa Kiziba ambayo Nyakiiru alikuja nayo kutoka Bunyoro.
|
249
|
Kyezailwe
|
Jina la ngoma lenye maana ya Kilichozaliwa.
|
250
|
Kalemaitalula
|
Ngoma ya utawala. Maana yake haibebeki.
|
251
|
Nyabatama
|
Jina la ngoma, maana yake haikupatikana.
|
Matama
|
Mashavu.
| |
252
|
Tabamulibi
|
Jina la ngoma ya utawala lenye maana ya Asiyekosa Soko, Anayehitajika Wakati Wote.
|
261
|
Mihango
|
Amri za mfalme au Mungu.
|
286
|
Balangila
|
Wana wa mfalme. Mmoja ni Mulangila.
|
302
|
Katikiro
|
Waziri Mkuu.
|
357
|
Anakomaga
|
Anatengeneza nguo za milumba.
|
Nyumanju
|
Nyuma ya nyumba.
| |
361
|
Mbugu
|
Milumba, nguo za magamba ya miti.
|
371
|
Kukama
|
Kukamua.
|
520
|
Zinajipogoa
|
Vichane vya ndizi vinakongoloka vyenyewe.
|
526
|
Saza
|
(Kiganda) Jimbo.
|
529
|
Mbito
|
Wa Ukoo wa Babito. Watawala wa ufalme wa Bunyoro na Kiziba.
|
543
|
Mtelele
|
Tambarare.
|
597
|
Nsi
|
Nchi kavu.
|
602
|
Wanyamahanga
|
Wageni kutoka mbali.
|
621
|
Kuyu (nkuyu)
|
Aina ya samaki wa ziwani.
|
658
|
Maka
|
Kaya.
|
664
|
Kikaleni
|
Katika Kikale, yaani Ikulu.
|
683
|
Nyamuhanga
|
Mungu - Jua.
|
712
|
Mihi
|
Vifaa vya ukili vya kubebea senene wakisha kamatwa. Kimoja ni muhi.
|
713
|
Topito
|
Manati.
|
732
|
Watote
|
Walowe.
|
798
|
Kukukuza
|
Kukuua hutumika kwa mfalme tu.
|
855
|
Kutukinda
|
Kutuchinja, kutuua.
|
Maneno magumu au matumizi magumu ya maneno
Ubeti
|
Neno
|
Maelezo
|
0
|
Fasilu
|
Sehemu, sura.
|
1
|
Hisitoria
|
Historia.
|
3
|
Wahenga
|
Wazee wa kale, watangulizi.
|
6
|
Wavyele
|
Wazazi.
|
7
|
Pasina
|
Pasipo.
|
Jadi
|
Asili ya mtu.
| |
8
|
Ufalume
|
Ufalme.
|
9
|
Elufu
|
Elfu.
|
10
|
Walisakini
|
Walikaa, waliishi.
|
12
|
Wali
|
Walikuwa.
|
Miungu
|
Mizimu.
| |
Mizimu
|
Pepo za watu waliokwisha kufa.
| |
Mahoka
|
Pepo za watu waliokwisha kufa.
| |
15
|
Waafirika
|
Waafrika.
|
Kwangamia
|
Kuangamia.
| |
16
|
Kuzimuni
|
Makao ya wafu au mizimu.
|
Auni
|
Misaada.
| |
19
|
Hako
|
Hayuko.
|
22
|
Kwelezawe
|
Kueleza wake.
|
23
|
Umbile
|
Vilivyoumbwa.
|
24
|
Malikia
|
Malkia.
|
25
|
Tufani
|
Upepo unaovuma kwa nguvu sana.
|
26
|
Kuzawana
|
Kuzaliwa pamoja naye.
|
30
|
Ali
|
Alikuwa.
|
31
|
Anafurusha
|
Anarusha.
|
34
|
Mtetemo
|
Tetemeko la ardhi.
|
36
|
Aridhi
|
Ardhi.
|
41
|
Mahiri
|
Bingwa, mjuzi.
|
Chuku
|
Udanganyifu, ulaghai.
| |
42
|
Humpiku
|
Humshindi.
|
44
|
Walihimidiwa
|
Waliabudiwa.
|
45
|
Ezi
|
Enzi.
|
46
|
Kutongoa
|
Kuimba, kusimulia.
|
Kunga
|
Siri za utunzi.
| |
Mahadhi ya halua
|
Sauti tamu ya wimbo.
| |
47
|
Kuhadithi
|
Kuhadithia.
|
Uhabithi
|
Uovu, ubaya.
| |
50
|
Matetano mzomzo
|
Magomvi tele.
|
52
|
Kasheshe
|
Fujo, vurugu.
|
53
|
Waume wa miraba
|
Wanaume wakubwa, wenye nguvu.
|
54
|
Kuwanda
|
Kuwa na neema, kustawi.
|
Kutanda
|
Kuenea, kuzagaa.
| |
Murua
|
Nzuri sana.
| |
55
|
Sulutani
|
Sultani, mfalme.
|
56
|
Kumaizi
|
Kufahamu.
|
57
|
Uzinzani
|
Uzinza, nchi ya Wazinza.
|
58
|
Maliki
|
Mfalme.
|
Miliki
|
Utawala, ufalme.
| |
59
|
Wadhifa
|
Cheo.
|
63
|
Yali
|
Ilikiwa.
|
64
|
Masogora
|
Mafundi wa kuwamba ngoma.
|
66
|
Tambo
|
Wakubwa.
|
Kiambo
|
Kitongoji, makazi.
| |
68
|
Ziwa lahema
|
Ziwa lapandisha nakushusha mawimbi yake.
|
Kaskazi
|
Kaskazini.
| |
70
|
Kufuma
|
Kutoboa kitu.
|
Husuma
|
Chuki.
| |
Hujuma
|
Shambulizi, uharibifu.
| |
72
|
Ngwamba
|
Kazi ngumu.
|
74
|
Mzito mja
|
Mjamzito.
|
76
|
Nadhifu
|
Mzuri, anayevutia.
|
78
|
Yakerereze
|
Yapigekwa msisitizo.
|
80
|
Zikatangaa
|
Zikaenea.
|
81
|
Pukupuku
|
Kwa wingi.
|
82
|
Aso makamu
|
Asiye na umri mkubwa.
|
84
|
Kwa tuwatuwa
|
Kwa kusitasita.
|
85
|
Akikita batobato
|
Akibamiza miguu kama bata.
|
87
|
Linayumkini
|
Linafaa, linastahili.
|
88
|
Janga
|
Maafa.
|
90
|
Afia
|
Afya.
|
Waa
|
Doa, dosari.
| |
Asiyechelea
|
Asiyeogopa.
| |
91
|
Ahodhi
|
Amiliki.
|
92
|
Zisilitindike
|
Zisipungue.
|
95
|
Myezi
|
Miezi.
|
102
|
Labuda
|
Labda.
|
104
|
Hadhari
|
Uangalifu.
|
Liso
|
Lisilo.
| |
Dhila
|
Dhara, ubaya.
| |
105
|
Wakanipalia
|
Wakinipa.
|
109
|
Katu
|
Kamwe, hata kidogo.
|
112
|
Kuzikoroga kwato
|
Kuja haraka haraka.
|
114
|
Mahiri
|
Hodari, mwenye ujuzi.
|
115
|
Hakuita
|
Nimekuita.
|
116
|
Kabula
|
Kabla
|
117
|
Kuikidhi
|
Kuitimiza.
|
120
|
Dhidi
|
Kupinga.
|
122
|
Mtokoto
|
Mkali, unaotokota.
|
125
|
Thawabu
|
Ahsante, shukrani, zawadi.
|
128
|
Tasihili
|
Kwa haraka.
|
Tunguri
|
Vibuyu vidogo vya uganga.
| |
Kili
|
Ukindu.
| |
131
|
Kasabahi
|
Kaamukia, katoa salamu ya asubuhi.
|
Afua
|
Uzima, uponaji.
| |
132
|
Kanagiza
|
Kaniagizia.
|
Kuzinuizia
|
Kuzisalia, kuzisemea maneno ya uganga.
| |
134
|
Yabisi
|
Ngumu.
|
135
|
Panyiza
|
Fanya.
|
137
|
Kishapo
|
Kisha hapo.
|
138
|
Makeke
|
Machachari, hekaheka, fujo.
|
141
|
Kudhalilisha
|
Kupunguza nguvu au hadhi.
|
142
|
Kutobanga
|
Kuvuruga.
|
144
|
Iso kifano
|
Isiyo kifani.
|
146
|
Kafanza
|
Kafanyiza, katengeneza.
|
148
|
Kutangaa
|
Kutajika kila mahali, kuzagaa.
|
149
|
Sudi
|
Bahati njema.
|
150
|
Kamuengeza
|
Kambembeleza.
|
151
|
Kajipangusha
|
Kajipangusa.
|
155
|
Mikiki
|
Tendo la kutumia nguvu.
|
157
|
Hayajangia
|
Hayajaingia, hayajaota.
|
160
|
Laana
|
Balaa inayotokana na kukosa radhiya Mungu.
|
Kitwana
|
Mtumishi wa kiume aliye kama nusu mtumwa.
| |
Kwambua
|
Kuambulia; kukutwa najambo.
| |
162
|
Kwangamia
|
Kuangamia.
|
163
|
Ulozi
|
Uchawi.
|
164
|
Kafi
|
Kasia la kuendeshea mtumbwi; Mugasha ni Muungu wa ziwa, hivyo inasemekana huonekana akitembea huku ameshika kasia.
|
Ghafi kanda
|
Mabaya, maovu, kenea.
| |
Kuwanda
|
Kuwa nene.
| |
166
|
Debe shinda
|
Debe tupu.
|
Panda
|
Parapanda, baragumu.
| |
167
|
Baa
|
Balaa
|
168
|
Kasirini
|
Ikuluni.
|
170
|
Fadhaa
|
Mshtuko.
|
171
|
Kukongolewa
|
Kuopolewa, kukatwakatwa.
|
Kengewa
|
Aina ya mwewe.
| |
172
|
Kulalama
|
Kulaani.
|
175
|
Harara
|
Mbio, haraka.
|
Ghera
|
Hamu, nia.
| |
176
|
Ada
|
Desturi.
|
Jamala
|
Fadhila, wema.
| |
177
|
Malika
|
Maliki, mfalme.
|
180
|
Nafusi
|
Nafsi.
|
183
|
Shari
|
Rabsha, vurugu.
|
Watakasiri
|
Watakasirika.
| |
Wataihasiri
|
Wataiharibu.
| |
184
|
Wajihi
|
Uso, sura.
|
Hutumika wakad wa kuzungumzia mfalme, mathalan kufika wajihi ni kufika mbele ya mfalme.
| ||
185
|
Pulikeni
|
Sikilizeni.
|
187
|
Naugulia
|
Nalilia.
|
Ulezi
|
Kulea.
| |
Vijaluba
|
Vifuko.
| |
188
|
Macho yanasinasina
|
Machozi yataka kutoka.
|
Wakajiondokelea
|
Wakaondoka.
| |
191
|
Kungia
|
Kuingia.
|
194
|
Tunutu
|
Mtoto wa nyuki.
|
196
|
Huba
|
Hamu.
|
199
|
Ajizi
|
Usiri, ugumu wa kufanyajambo.
|
202
|
Midhana
|
Balaa.
|
204
|
Mwanondolea
|
Mwaniondolea.
|
206
|
Utuvu
|
Utulivu.
|
207
|
Kakata
|
Kwa mikiki.
|
Aguta
|
Anahema.
| |
213
|
Wakamgura
|
Wakamuacha.
|
214
|
Msito
|
Kusita, kupumzika.
|
218
|
Magharibi
|
Jioni.
|
Amekwajuka
|
Amechakaa.
| |
219
|
Gharighari la mauti
|
Karibu na kukata roho.
|
Siti
|
Mwanamke.
| |
221
|
Mtima
|
Moyo, nadhiri au fikra ya ndani.
|
222
|
Tumai
|
Tumaini.
|
224
|
Wampapia
|
Unapiga.
|
227
|
Asikari
|
Askari.
|
228
|
Chepechepe
|
Dhaifu.
|
230
|
Azima
|
Kusudio, dhamira, nia.
|
233
|
Msasi
|
Mwindaji.
|
Podo
|
Kifuko cha kubebea mishale.
| |
237
|
Nasabaye
|
Ukoo wake.
|
239
|
Karine
|
Kame.
|
241
|
Heba
|
Haiba, heshima na utukufu.
|
242
|
Wororo
|
Hali ya kuwa laini.
|
Mbaro
|
Kifungo.
| |
244
|
Mziwanda
|
Kitmdamimba, mtoto wa mwisho.
|
246
|
Kakara
|
Kukurukakara, mapambano.
|
247
|
Alihozi
|
Alihodhi, alimiliki.
|
249
|
Iitilwe
|
Inaitwa.
|
Iwambilwe
|
Imewambwa.
| |
251
|
Goma
|
Ngoma kubwa.
|
253
|
Wakifu
|
Takatifu.
|
257
|
Mtunzi
|
Mtunzaji.
|
258
|
Masikiyo
|
Masikio.
|
260
|
Majilisi
|
Baraza.
|
Wasiasi
|
Hawakuasi, walitii.
| |
265
|
Inavyosinyaa
|
Inavyonyong'onyea, inavyopungua.
|
267
|
Mtanza
|
Mtaanza.
|
Kuteta
|
Kuzozana, kugombana.
| |
272
|
Ukakasi
|
Kutumia nguvu, kulazimisha jambo.
|
276
|
Msasa
|
Laini.
|
277
|
Kumusia
|
Kumuusia.
|
279
|
Kamwagizila
|
Kamwagizia.
|
289
|
Lukuki
|
Wengisana.
|
292
|
Akahaha
|
Akahangaika.
|
Asiridhi
|
Asiridhike.
| |
294
|
Wenzo
|
Wenzio.
|
297
|
Budi sina
|
Sina budi.
|
298
|
Tasihili
|
Haraka.
|
300
|
Jamala
|
Fadhila, matendo mazuri.
|
304
|
Tukiamiri
|
Tukiongoza.
|
306
|
Masurufu
|
Chakula cha safari.
|
309
|
Kuwajuza
|
Kuwapa habari, kuwafahamisha.
|
312
|
Dazani
|
Kumi na mbili.
|
Kani
|
Nguvu.
| |
313
|
Pamwe
|
Pamoja.
|
314
|
Kiza kiliposhitadi
|
Kiza kiliposhtadi, giza lilipokoza, liliposhika sana.
|
315
|
Nyatunyatu
|
Kunyaria.
|
316
|
Milumba
|
Mbugu, nguo za magamba ya miti.
|
320
|
Nguu
|
Milima.
|
321
|
Ngisi
|
Aina ya samaki mweupe.
|
323
|
Pamba
|
Chakula cha safari.
|
325
|
Udhia
|
Tabu, usumbufu.
|
326
|
Ikawakeketa
|
Ikawauma.
|
327
|
Wanazivinjari
|
Wanazitembelea, wanazizunguka.
|
331
|
Jikusuru
|
Jihimu, jitahidi.
|
332
|
Kabarizi
|
Kazungumza.
|
Uchizi
|
Utukutu, upuuzi.
| |
333
|
Kujinusuru
|
Kujiponya.
|
334
|
Itajulika
|
Itajulikana.
|
335
|
Litangia
|
Litaingia.
|
338
|
Konde
|
Shamba.
|
339
|
Wakona
|
Wakaona.
|
Azizi
|
Zuri.
| |
345
|
Woto
|
Uoto, mazao.
|
347
|
Limemuumuka
|
Limemvimba.
|
348
|
Kudhukuru
|
Kueleza, kusema.
|
Mashukuru
|
Shukrani.
| |
350
|
Garasha
|
Kitu cha ovyo kisicho na thamani.
|
352
|
Futa
|
Vuta.
|
353
|
Kitala
|
Vita.
|
361
|
Kitanga
|
Chombo cha udongo.
|
365
|
Iliyowasakamia
|
Diyowaandama.
|
369
|
Maridhawa
|
Vingi.
|
372
|
Usasini
|
Katika uwindaji.
|
375
|
Ndumba
|
Hirizi.
|
378
|
Walikozukia
|
Walipotokea.
|
383
|
Nyayu
|
Nyau, paka.
|
Halitaka
|
Hali takataka, hali uchafu.
| |
386
|
Amiri
|
Mkuu, kiongozi
|
388
|
Sichi
|
Sichelei, siogopi.
|
390
|
Ghaidi
|
Jambazi.
|
398
|
Janadume
|
Kijana mkakamavu.
|
Mana
|
Maana.
| |
399
|
Ukibalehe
|
Ukikomaa.
|
404
|
Kuutiringa
|
Kuurusha kasi.
|
Kumtindanga
|
Kumchinja.
| |
405
|
Ugwe
|
Kamba ya upinde.
|
407
|
Tambo litajitambua
|
Fumbo litajifumbua.
|
408
|
Wakakirihi
|
Wakakinai.
|
410
|
Hari
|
Joto.
|
416
|
Walipojia
|
Walipokula chakula cha jioni.
|
419
|
Wakenda
|
Wakaenda.
|
420
|
Kamkabizi
|
Kamkabidhi.
|
421
|
Katukatu
|
Hata kidogo.
|
422
|
Miadini
|
Mahali pa kukutana.
|
425
|
Wahedi
|
Wa kwanza.
|
434
|
Wakamba
|
Wakasema.
|
Wa chaleni
|
Wa chanjo.
| |
437
|
Tangua
|
Vunja.
|
440
|
Wakajizatiti
|
Wakajiandaa.
|
443
|
Suhubia
|
Fanyiana urafiki.
|
450
|
Nadhari
|
Uangalifu.
|
Kuzisasi
|
Kuzipeleleza.
| |
452
|
Tamthili
|
Mfano wa.
|
453
|
Nyatunyatu
|
Tahadhari, nyatia.
|
Matumatu
|
Ghafla.
| |
459
|
Akajitoma
|
Akajirusha.
|
462
|
Nduli
|
Dude, mnyama mkali.
|
Kibahaululi
|
Kijitu, kiumbe duni.
| |
468
|
Bwabwa
|
Sauti za mbwa.
|
469
|
Rabusha
|
Rabsha.
|
470
|
Ananyapa
|
Ananyatia.
|
473
|
Usipombeze
|
Usitingishe.
|
476
|
Wakabwagika
|
Wakaanguka chini kama mzigo.
|
477
|
Yakangia
|
Yakaingia.
|
480
|
Lege
|
Legelege, mlegevu, dhaifu.
|
487
|
Nderemo
|
Vifijo, furaha kubwa.
|
489
|
Ahueni
|
Nafuu.
|
492
|
Ng'ombemwitu
|
Mbogo, nyati.
|
496
|
Tuu
|
Tu.
|
498
|
Halahala
|
Haraka haraka.
|
503
|
Anadhukuru
|
Anakumbuka.
|
508
|
Furifuri
|
Kwa wingi.
|
521
|
Kufura
|
Kufurika.
|
524
|
Nikakamke
|
Niwe mkakamavu.
|
532
|
Kuikita
|
Kuisimamisha.
|
535
|
Sahiba
|
Rafiki mkubwa.
|
537
|
Kaumu
|
Umma wa watu.
|
549
|
Nadhiri
|
Ahadi.
|
560
|
Twishi
|
Tuishi.
|
566
|
Majikalifu
|
Bila kutaka.
|
575
|
Miba
|
Miiba.
|
576
|
Alifajiri
|
Alfajiri.
|
584
|
Kuiegeza
|
Kuigesha.
|
586
|
Kuziratibu
|
Kuzishika (zamu).
|
587
|
Jia kijio
|
Kula chakula cha jioni.
|
Malalio
|
Virago vya kulalia.
| |
589
|
Ja
|
Karpa.
|
Wameipambaja
|
Wameikumbatia.
| |
592
|
Wakaishua
|
Wakaitia, wakaiteremsha.
|
595
|
Kafara
|
Sadakakwa Mizimu.
|
596
|
Kusi
|
Kusini.
|
599
|
Uliokoza
|
Wenye mwanga mkali.
|
622
|
Subalherini
|
Salimio la asubuhi.
|
624
|
Halahala
|
Himahima haraka.
|
627
|
Kwelemea
|
Kwenda, kuelekea.
|
634
|
Jalali
|
Mtukufu.
|
Fadhili
|
Hisani, msaada.
| |
638
|
Kongoni
|
Aina ya mnyama kama nyumbu.
|
Kuro
|
Mnyama wa porini afananaye na ndama.
| |
644
|
Fadhilazo
|
Hisani yako, msaada wako.
|
Mwadhamu
|
Mtukufu.
| |
Masitakimu
|
Maslakimu, makazi.
| |
651
|
Kuiauni
|
Kuilinda, kuitetea.
|
656
|
Wapepezi
|
Watu wanaowapepea watawala kwa vipepeo ili wasisumbuliwe na joto au wadudu warukao.
|
Wakanzi
|
Wakandaji.
| |
660
|
Kukera
|
Kusumbua.
|
669
|
Nyang'au
|
Nduli, madude.
|
670
|
Nemsi
|
Ustawi.
|
682
|
Dia
|
Malipo mema, fidia.
|
690
|
Shahamu
|
Mafuta.
|
Dawamu
|
Bila kukoma, milele.
| |
691
|
Mizungu
|
Maajabu.
|
693
|
Bahau
|
Mpumbavu.
|
694
|
Gomashinda
|
Gomatupu.
|
704
|
Saburi
|
Subira.
|
708
|
Wafane
|
Waliofana, wema, wazuri.
|
714
|
Hirimu
|
Kundi la umri fulani.
|
Rika
|
Watu wa uniri fulani.
| |
716
|
Mifuo
|
Mitaro iliyochimbwa na maji.
|
717
|
Ukufi
|
Kitu kidogo.
|
719
|
Wakajitoma sharini
|
Wakajitosa katika pilikapilika.
|
720
|
Vitimbi
|
Hila, ujanja.
|
728
|
Hio
|
Hiyo.
|
733
|
Janga
|
Balaa, maafa.
|
735
|
Kauri
|
Chombo cha udongo.
|
740
|
Kawashua
|
Kawadharau, kuwashushia hadhi.
|
742
|
Amali
|
Matendo.
|
743
|
Ikacharuka
|
Ikalipuka.
|
746
|
Nti
|
Nchi, ardhi.
|
747
|
Kutowelea
|
Kufanya kitoweo.
|
752
|
Ikaputa
|
Ikavimba kama puto.
|
754
|
Furusa
|
Fursa, nafasi.
|
763
|
Kaumu
|
Umma wa watu.
|
764
|
Walitafakari
|
Waliwaza kwa makini.
|
768
|
Harara
|
Haraka.
|
772
|
Ziwazingile
|
Ziliwazunguka.
|
773
|
Juku
|
Jukumu.
|
776
|
Wasioneke
|
Wasionekane.
|
782
|
Ametarama
|
Amestarehe.
|
783
|
Vikuku
|
Mabangili,
|
785
|
Bwabwaja
|
Porojo.
|
788
|
Adhamu
|
Hadhi, heshima.
|
789
|
Maajuza
|
Wakongwe.
|
791
|
Kujalisi
|
Kuongea, kujadiliana.
|
795
|
Dubwana
|
Dude, nduli.
|
Hiana
|
Uhaini, uadui.
| |
798
|
Kukuambua
|
Kukunyanganya.
|
803
|
Ndwele
|
Maradhs, ugonjwa.
|
804
|
Mtufala
|
Mtu duni, mjinga.
|
805
|
Nadhari
|
Akili, uangalifu.
|
808
|
Maki
|
Kina.
|
825
|
Havaa
|
Nilivaa.
|
828
|
Nimekufuru
|
Nimetenda mambo yenye kuwachukiza Miungu.
|
829
|
Kujisoza
|
Kujiumiza.
|
834
|
Dhalimu
|
Anayedhulumu.
|
835
|
Aliyoiatamia
|
Aliyoimilild.
|
850
|
Nyumao
|
Nyuma yao.
|
853
|
Dhuluma
|
Uonevu.
|
856
|
Misu
|
Majisu makubwa.
|
859
|
Madhila
|
Maafa.
|
862
|
Bimbirishana
|
Angushana.
|
873
|
Sahibu
|
Rafiki.
|
Comments
Post a Comment