Walifariki Kwa Ajali Jijini Mbeya Wafika 15


Idadi ya watu waliofariki dunia katika ajali iliyohusisha magari matano eneo la Mlima Igawilo jijini Mbeya imefikia 15.

 Muuguzi Mkuu wa Hospitali  ya Rufaa Kanda ya Mbeya, Dk Petro Seme, alisema jana walipokea majeruhi 15 wa ajali hiyo lakini wawili walifariki wakati wakiendelea kupatiwa matibabu.

Alisema majeruhi wanne walitibiwa na kuruhisiwa na wengine wanaendelea na matibabu.

“Pia tulipokea maiti 13, lakini majeruhi wawili walifariki dunia hapa hospitali. Majeruhi wengine wawili waliopo hapa wapo ICU (chumba cha uangalizi maalum)  na mmoja hali yake si nzuri.” amesema

Ajali hiyo ilitokea jana saa 11 jioni ikihusisha magari mawili yaliyokuwa yamebeba mafuta, mengine mawili yalikuwa yamebeba viazi na ndizi pamoja na daladala iliyokuwa imebeba abiria kutoka Igoma kwenda Mbeya mjini.

Popular posts from this blog

HIZI HAPA SMS TAMU ZA KUMTAKIA USIKU MWEMA MPENZI WAKO

SMS na MESEJI 900+ za mapenzi

MIAKA 22 SASA TANGU KUZAMA KWA MELI KUBWA YA MV BUKOBA, TANZANI TUMEJIFUNZA NINI?