Posts

Showing posts from July, 2018

Waitara Asema Kilichomuondoa CHADEMA ni Ugomvi Kati yake Na Mbowe Baada ya Kumtaka Asigombee Tena Uenyekiti wa Chama Hicho

Image
Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara amesema kilichosababisha kujivua uanachama wa Chadema na kujiunga na CCM ni Uenyekiti. Waitara ametangaza uamuzi  wa kujiunga na CCM leo Julai 28 katika mkutano na wanahabari uliofanyika Ofisi za CCM, Lumumba. “Shida ni uenyekiti wa Chadema, ukianzia kwa akina Chacha Wangwe, Zitto Kabwe, hata mimi ni uenyekiti hapo kuna shida,” amesema. Amesema suala la uenyekiti sio lake peke yake bali wapo wabunge wengi wanaoguswa nalo lakini hataki kuwataja kwa majina. “Kuna kikao tulikaa na wabunge wengi wa majimbo na viti maalumu tukawa tunazungumza kwamba Tundu Lissu agombee uenyekiti baadaye hoja hiyo wakaicha mimi nikaendelea nayo. Wakaniambia ninataka Tundu Lissu agombee au ni mimi mwenyewe?” amesema na kuongeza: “Mbowe amewahi kuniambia kamanda unanipinga na mimi ntakushughulikia na kwenye Chadema bado hakuna mtu kama yupo ntamng'oa hikii chama ni mali yangu.” Waitara amesema kwamba ugomvi huo uliibuka kwa sababu mchakato wa Uch...

METHALI MIA SITA NA KUMI ZA KISWAHILI

METHALI MIA SITA NA KUMI (610) 1. Aanguaye huanguliwa. 2. Asiye sikia la mkuu, huvunjika guu. 3. Abebwaye hujikaza. 4. Adhabu ya kaburi aijuae maiti. 5. Adui aangukapo, mnyanyue. 6. Adui mpende. 7. Adui wa mtu ni mtu. 8. Afadhali ya Musa kuliko ya Firauna. 9. Ahadi ni deni. 10. Ajidhaniaye amesimama, aangalie asianguke. 11. Akiba haiozi. 12. Akili ni mali. 13. Akili ni nywele kila mtu ana zake. 14. Akili nyingi huondowa maarifa. 15. Akutukanae hakuchagulii tusi. 16. Akipenda chongo huita kengeza. 17. Akufaae kwa dhiki, ndiye rafiki. 18. Akufanyiaye ubaya, mlipe wema. 19. Akupaye kisogo si mwenzio. 20. Akutendaye mtende, mche asiyekutenda. 21. Alisifuye jua, limeuangaza. 22. Aliye juu msubiri chini. 23. Aliye kando, haangukiwi na mti. 24. Aliye kupa wewe kiti (kibao) ndiye aliye nipa mimi kumbi. 25. Aliye kutwika, ndiye atakaye kutua. 26. Akufukuzae hakwambii toka. 27. Aliyekupa mkeka ndiye aliyenipa kumbesa. 28. Amani haipatikani mpaka kwa ncha ya upanga. ...

AUDIO | Saint Young Master Ft. Chidi Benz - SINA NOMA | Download

Image
DOWNLOAD

VIDEO | Lava Lava - Gundu

Image

KEN WALIBORA, HATUONEI FAHARI LUGHA YETU ASHIRAFU YA KISWAHILI, SI KATIKA UHAI SI KATIKA MAUTI

Image
 Na KEN WALIBORA Kwa Ufupi : Wiki hii nimekwenda kufanya ziara katika maziara ya Wazungu Zanzibar Muhimu ni kwamba niliazimia kujua kumbukumbu za watu hawa makaburini zimeandikwa kwa lugha gani Nimekuta Kijerumani na Kiingereza katika makaburi Zanzibar WIKI hii nimekwenda kufanya ziara katika maziara ya Wazungu Zanzibar. Labda hilo litakushangaza kidogo kama unaelewa maana ya maziara. Maziara ni makaburi. Kwa kifupi nilikwenda kuzuru makaburini eneo la Zanzibar Mjini Magharibi. Huku makaburini sikuwa nimekwenda kutoa heshima zangu kwa jamaa zangu waliokufa, hapana. Sina jamaa zangu hapa Zanzibar, walio hai au wafu. Marafiki ninao na pia “ndugu wa kiroho” kama unanielewa. Rafiki yangu mmoja Mzanzibari alinishangaza majuzi yale kwa kunifikiria miye kuwa nduguye Rais wa Liberia, George Weah. Rafiki yangu kaniambia kwamba yeye hucheza muziki na aliwahi kuzuru Dubai kutumbuiza hotelini alikofikia George Weah. Kwa hiyo kaniambia mimi na George Weah shilingi kwa nyingine...

WAUAJI WA BILIONEA MSUYA WAHUKUMIWA KUNYONGWA HADI KUFA

Image
MAHAKAMA Kuu ya Tanzania Kanda ya Arusha, imewahukumu kunyongwa hadi kufa washitakiwa watano baada ya kukutwa na hatia ya kumuua kwa makusudi aliyekuwa mfanyabiashara wa Arusha na Mirerani mkoani Manyara, Erasto Msuya. Erasto Msuya enzi za uhai wake.. Waliohukumiwa adhabu hiyo ni mshitakiwa wa kwanza, Sharifu Mohamed; mshitakiwa wa tatu, Mussa Mangu; wa tano, Karim Kuhundwa; wa sita Sadick Mohamed na wa saba; Ally Mussa Majeshi. Hukumu hiyo imetolewa leo Julai 23, 2018 na Jaji Salma Maghimbi aliyekuwa akisikiliza kesi hiyo. Aidha, Mahakama imemwachia huru mshitakiwa wa pili, Shwaibu Jumanne baada ya kukosekana ushahidi dhidi yake.

Utoshelevu Wa Fasili Na Visawe Vya Vidahizo Katika Kamusi Ya Kiswahlli Sanifu

H.M. Batibo Utangulizi Katika mkutano wa Chama cha Wanaleksikografia cha Amerika ya Kaskazini uliofanyika Julai 1978, mada moja iliwasisimua sana wajumbe wa mkutano. Mada hiyo ilitolewa na nwanaleksikografia mkongwe Prof. Sherman M. Kuhn, juu ya "Mbinu za Kuandika Fasili" 2  (Kuhn, 1980:115 - 121). Mada hiyo ilieleza matatizo mengi yatokanayo na fasili za vidahizo katika kamusi. Baadhi ya matatizo yaliyojitokeza katika mada ya Kuhn ni kutotosheleza kwa fasili, tofauti za visawe, upana usio na mipaka halisi wa uwanja wa matumizi, na utata wa upambanuzi. Makala haya yatachunguza ubora wa fasili za vidahizo katika  Kamusi ya Kiswahili .Sanif u (kifupi KKS). TUKI (1981), kwa kuangalia jinsi ilivyozingatia kanuni za fasili. Baadaye itachambua namna visawe vilivyotumiwa katika kamusi hiyo. Mwisho, tutatoa mapendekezo ya namna ya kuirekebisha au kuiboresha KKS. hasa pale inapohusu fasili na visawe. Utoshelevu wa Fasihi katika KKS Fasili ni Nini? Swali la fasili ni ...