Posts

Showing posts from February, 2018

TABIA KUMI (10) AMBAZO WANAWAKE WENGI HUCHUKIZWA NAZO

Image
TABIA 10 ZA WANAUME AMBAZO WANAWAKE WENGI HUCHUKIZWA NAZO 1. Kijana wa mama Mwanaume wa aina hii wakati wote utamkuta kagandana na mama yake katika kilakitu kuanzia maongezi hadi matendo, hawezi kufanya chochote mpaka apate idhini kutoka kwa mama yake hata kama ana mke na maamuzi yanayofanywa ni ya kuihusu familia yake yeye. Katika familia ya mwanaume huyu mama yake huwa ndiyo mfalme katika kila kitu, yeye ndo ataamua mkae wapi, mjenge wapi, muende wapi, mlenini, na hata maamuzi mengine mkiyaamua ninyi basi yeye ataulizwa na mtoto wake ayakague kama ni maamuzi sahihi au la, na mara zote maamuzi yake ndiyo ya mwisho. Kwa mwanaume kama huyu kama wewe ni mke basi ufahamu mapema kuwa hata ufanyaje kamwe huwezi kuwa mzuri na mwema kama mama yake. 2. Mwanaume mvivu na mchungu: Mwanaume wa jinsi hii ni kati ya wale ambao hawataki kabisa kujishuhulisha, wao hutaka kuwa na wanawake wenye kitu kama vile gari, nyumba, kazi nzuri n.k. utamkuta mwanaume wajinsi hii yeye ni kulala t...

ASILI YA LUGHA YA KISWAHILI, MASSAMBA , FREEMAN GENVILLE KATIKA MEDIAVAL EVIDENCE FOR SWAHILI

Image
ASILI YA KISWAHILI: FREEMAN GENVILLE KATIKA “MEDIEVAL EVIDENCES FOR SWAHILI” Kwanza tutaangalia nini  maana ya  neno asili, pia tutaeleza kwa ufupi mitazamo mbalimbali kuhusu asili ya lugha ya Kiswahili, halafu tutaangalia kwa undani kiini cha mada yetu kwa kuchanganua vyema mawazo ya Freeman Grenville katika makala yake inayoitwa ‘Medieval Evidences for Swahili’ pia tutaonesha ubora pamoja na udhaifu wake na mwisho tutatoa hitimisho. Neno asili kwa mujibu wa Massamba na wenzake (1999:3) ni jinsi kitu au jambo lilivyotokea au lilivyoanza.  Fasili hii ni nzuri na inajitosheleza kwa maana kwamba jambo au kitu kinaweza kutokea kibahati kama ilivyo katika lugha au linaweza kuanzishwa. Hivyo basi asili ya lugha ya kiswahili bado ni mjadala mrefu ambapo wataalamu mbalimbali wanahitilafiana juu ya asili au chimbuko la lugha ya kiswahili. Wapo wanaokinasibisha kiswahili na kiarabu kwa kutumia kigezo cha msamiati na dini ya kiislamu. Wengine wanashikilia kisw...

Waziri Mkuu: Tukikukuta na Binti wa Shule tutakukamata na kukutupa miaka 30 Jela......Ole Wenu Vijana!

Image
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali imedhamiria kuwalinda watoto wa kike na ndiyo maana tunawataka watoe taarifa za watu wanaotaka kuwakwamisha kimasomo kwa watendaji wa vijiji kwenye maeneo yao. Alitoa agizo hilo jana (Jumatatu, Februari 26, 2018) wakati akizungumza kwa nyakati tofauti na wakazi wa wilaya ya Masasi akiwa katika siku ya kwanza ya  ziara yake ya kikazi mkoani Mtwara. Waziri Mkuu alisema watoto wa kike wanatakiwa kuheshimiwa katika jamii kwa kuachwa waendelee na masomo yao bila ya usumbufu wa aina yoyote na atakayebainika kukatisha masomo atachukuliwa hatua kali za kisheria. Alisema Serikali  itatoa adhabu kali ya kifungo cha miaka 30 jela kwa mtu atakayekatisha elimu ya mtoto wa kike iwe kwa kumuoa, kumpa ujauzo na hata ukikutwa naye nyumbani kwako, katika nyumba ya wageni. “Tukikukuta na binti wa shule katika kona isiyoeleweka tunakukamata na kukuchukulia hatua za kisheria. Ole wenu vijana, mkibainika mmewapa mimba mab...

SABABU ZA KUCHELEWA KUPATA HEDHI

Image
    Kwa msichana au mwanamke kuchelewa kupata hedhi huwa hakushitui endapo mwanamke atakua anajua ni nini tatizo au sababu iliyopelekea yeye kukosa hedhi. Na majibu ya kuchelewa kwa hedhi hupatikana pindi hedhi hiyo inapochelewa. Mfano kama ulikua unategemea kupata mimba, ikichelewa inakua ni dalili ya kwanza ya wewe kuanza kufikiria jambo ulilolitaka ninaelekea kutimia na hata ukatabasamu na kuwaza hatua nyingine ya kujipima nyumbani au kuenda hospitali. Na kama hukuwa umetarajia ndio hivyo tena mawazo ya kila aina yatakuja kichwa kutaka kujua kwanini hedhi yako imechelewa na pengine usipate majibu kabisa. Hapa nimekuwekea sababu 6 zinazoweza kusababisha hedhi ya mwanamke kuchelewa, na nimefanya hivi kwa kutambua kwamba wanawake wengi hufikiria sababu moja tu endapo hedhi yao itakua imechelewa. 1 . Mimba Hii ndio sababu ya kwanza kuja kichwani endapo siku za hedhi za mwanamke zitakua zimechelewa. Na inawezekana ukawa sahihi!! Na hii hutokea hata kama mwanamke ...

UKUMUSHAJI, KIKUMUSHI, NA KIVUMISHI

Image
SWALI”  Jadili dhana ya ukumushaji na sifa zake kwa kutumia mifano sahihi. UKUMUSHAJI Ni dhana ambayo hutoa maelezo zaidi au Ya ziada kuhusu nomino, kivumishi, kitenzi, kielezi au kikundi cha maneno KIKUMISHI Ni neno , kirai au kishazi ambacho hutoa maelezo ya ziada kuhusu nomino, kivumishi, kitenzi, kielezi au kikundi cha maneno. Aidha, kikumushi huweza kuwa sentensi itoayo maelezo zaidi kuhusu sentensi nyingine. Mfano. Mtoto  aliyekuja juzi  ameondoka. Katika sentensi hii kishazi tegemezi “ aliye kuja juzi” ni kikumushi ambacho kinatoa maelezo ya ziada kuhusu nomino “ mtoto:. Mwanafunzi mrefu  sana  ameanguka.; Neno “sana” ni kikumushi kinachotoa maelezo ya ziada kuhusu kivumishi “ mrefu” Mifano zaidi Gari lilikimbia kwa kasi  sana Maduhu anaimba vizuri  mno Ninapenda  unavyosema . Mwalimu  aliye kwenda dukani jana  amerudi. Kimsing ukumushaji ni dhana pana zaidi ya uvumishi, kwani ukumusha...