Yanga wao wameamua kufanya mambo yao kimyakimya wakijiandaa na mechi ya Jumamosi.

Sasa hawana wanachoweza kulaumu maana mechi yao dhidi ya Azam FC itachezwa saa 10 jioni, Jumamosi.

Wanachotaka ni kushinda na Kocha Mkuu, George Lwandamina aliagiza mazoezi makali yafanyike na juzi wachezaji walikuwa hoi.

Sasa wamelegeza ukali wa mazoezi na wanaendelea na mazoezi ya mbinu zaidi kuhakikisha ushindi unapatikana Jumamosi.

Pamoja na kwamba watamkosa Pius Buswita ambaye ana kadi tatu za njano, mshambuliaji Obrey Chirwa kamaliza adhabu yake anarejea.

Lakini Yanga watakuwa na uhakika kwamba ukuta utaimarika tena wakati Kelvin Yondani anarejea pia.

Mechi hiyo inasubiriwa kwa hamu kubwa, Yanga wakitaka kupunguza pengo lao kubwa dhidi ya Simba na Azam pia lakini Azam FC wakitaka kushinda wazidi kuipa presha Simba iliyo kileleni mwa msimamo.