Vyuma vimekaza : Sangoma ajiua kwa kukosa wateja



Wakazi wa eneo la Maili Saba katika Jimbo la Trans Nzoia wamepigwa na butwaa baada ya mganga Joshua Shalongo kujiua kwa sababu ya kukosa wateja na hali ngumu ya maisha.

Shalongo ambaye ni mganga maarufu katika eneo la Kitale nchini Kenya inasemekana suala la kukosa wateja lilimtatiza sana kiasi cha kuchukua uamuzi wa kujiua.

Mwili wake umepatikana ukining’inia kwenye paa la nyumba ukiwa umefungwa kamba taarifa hii imeripotiwa katika jarida la Citizen’s Edaily.

Chief wa eneo hilo Esther Waswa amethibitisha tukio la mganga huyo kujiua.

Popular posts from this blog

HIZI HAPA SMS TAMU ZA KUMTAKIA USIKU MWEMA MPENZI WAKO

SMS na MESEJI 900+ za mapenzi

MIAKA 22 SASA TANGU KUZAMA KWA MELI KUBWA YA MV BUKOBA, TANZANI TUMEJIFUNZA NINI?