Skip to main content

Hatimaye Denti UDSM Aliyeuawa na Polisi kwa ‘Ujambazi’ Azikwa Kisutu, Dar



Hatimaye Denti UDSM Aliyeuawa na Polisi kwa ‘Ujambazi’ Azikwa Kisutu, Dar


Mwili wa denti wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Marehemu Salum Almas aliyeuawa kwa kupigwa risasi na polisi kwa madai kuwa alikuwa Jambazi, Mei 14, mwaka huu maeneo ya Uhamiaji Kurasini jijini Dar, ukiwa umebebwa tayari kwa kuzikwa katika makaburi ya Kisutu Jijini Dar.

TAZAMA MAZISHI HAYO

HATIMAYE mwili wa denti wa UDSM (Chuo Kikuu cha Dar es Salaam), Marehemu Salum Almas aliyeuawa kwa kupigwa risasi na polisi kwa madai kuwa alikua jambazi, Mei 14 mwaka huu, maeneo ya Uhamiaji Kurasini jijini Dar es Salaam, leoIjumaa Julai 30, 2017 umezikwa katika makaburi ya Kisutu jijini Dar amba mamia ya watu walijitokeza, ikiwa ni siku 47 tangu auawe kwa tuhuma hizo, ambazo familia ya marehemu imezipinga vikali mahakamani kuwa ndugu yao hakuwa jambazi na kulitaka Jeshi la Polisi kukiri kosa.

Mwili wa Denti huyo wa UDSM uligomewa kuzikwa na ndugu zake kwa madai kuwa aliuawa kimakosa kwa kudhaniwa ni jambazi aliyetaka kupora fedha kwenye ATM iliyopo maeneo ya Uhamiaji, Kurasini jijini Dar.

Mwili wa Marehemu uliswaliwa katika Msikiti wa Kichangani, Magomeni, Dar mara baada ya swala ya Ijumaa. Hapa chini nimekuwekea picha 12 za msafara kuelekea makaburini.
(STORI: BONIPHACE NGUMIJE, GLOBAL TV ONLINE)


Comments

Popular posts from this blog

HIZI HAPA SMS TAMU ZA KUMTAKIA USIKU MWEMA MPENZI WAKO

SMS na MESEJI 900+ za mapenzi

MIAKA 22 SASA TANGU KUZAMA KWA MELI KUBWA YA MV BUKOBA, TANZANI TUMEJIFUNZA NINI?