Posts

UUNDAJI WA KAMUSI , MAANA YA LUGHA KIENZO PDF

Dhana ya Lugha kienzo na umuhimu wake katika utengenezaji wa kamusi Katika kujadili mada hii tutaangalia dhana ya lugha kienzo kama ilivyojadiliwa na wataalamu mbalimbali, mifano ya lugha kienzo kutoka katika kamusi, umuhimu wa lugha kienzo na mwisho tutatoa hitimisho juu mada hii. Dhana ya lugha kienzo imejadiliwa na wataalamu mbalimbali, miongoni mwa wataalamu hao ni pamoja na: Bwenge (1995) kama alivyonukuliwa na Mdee (1997) wanasema kuwa lugha kienzo ni lugha au ni mtindo utumikao kufasili au kueleza leksimu za lugha. Kwa kifupi lugha kienzo ni lugha itumikayo kuifafanua au kuifasili lugha. Anaendelea kusema dhima ya lugha za lugha kienzo ni: kueleza lugha kwa ufasaha, utoshelevu , kwa muhtasari na uwazi ili kumwezesha mtumiaji kupata na kuelewa mara moja kile anachokitafuta bila kumchosha akili. Fasili hii inaelezea dhana ya lugha kienzo kwa ujumla katika lugha, lakini hata hivyo kamusi nayo ina lugha inayotumiwa kuelezea taarifa mbalimbali zinazohus...

SHAABAN ROBERT UHAKIKI WA RIWAYA YA KUFIKIRIKA

Karibu ndugu msomaji tuichambue kwa kina riwaya ya kiswahili iliyo andikwa na Shaaban Robert Riwaya ya kufikirika ni riwaya iliyotungwa na mwandishi mashughuli Shaabani Robert, katika riwaya hii mwandishi anaeleza juu ya mila na desturi zilizopitwa na wakati kuwa hazina nafasi katika kipindi cha sasa. Mwandishi anaeleza kuwa jamii ya watu wakufikirika ilikuwa inaamini juu ya uganga na mambo ya kijadi. Hivyo kupitia mhusika utu busara ambaye alikuwa anaelimu kubwa ya dunia. Utu Busara alijiingiza katika kundi la utabiri ili aweze kuleta mabadiliko katika nchi ya kufikirika. Kutokana na utabiri wake Mfalme na Malkia wanafanikiwa kupata mtoto na baadae Utu Busara tena anakuwa mwalimu wa mtoto wa mfalme na kuanza kumfundisha elimu ya dunia ambayo ni kinyume na matakwa ya mfalme, baada ya kufukuzwa na mfalme, Utu Busara anaamua kujiingiza katika kilimo ambapo ikapelekea kukamatwa kwa kudhaniwa kuwa ni mjinga. Kutokana na elimu na weledi alionao utu busara anafanikiwa kujiokoa kutoka ge...

UHAKIKI DIWANI YA MAPENZI BORA

Katika uhakiki wa diwani ya Mapenzi Bora, utaangazia utangulizi na kiini. Ambapo katika utangulizi utaangazia shabaha ya kitabu hiki na kiini utaangazia vipengele vya fani na maudhui. Utangulizi. Mapenzi Bora ni diwani iliyoandikwa na Shaaban Robert mwaka 1958. Diwani hii yenye beti 700, dhumuni ni kuiadili jamii juu ya maana, faida na hasara za kukosa mapenzi bora. Kusudi la kitabu hiki ni kuandalia mahitaji ya watu waliofikia fahamu ya kuwaza na kuhoji neno au kitu au tendo kwa akili ingawa haitakuwa vibaya kama kitasomwa na watu wowote ambao hawajafikia upeo kama huo wakipenda kujiweka tayari kwa zamu yao. Fani na Maudhui ya kitabu hiki. Kipengele cha Maudhui, kipengele hiki kinahusisha dhamira, ujumbe, falsafa ya mwandishi na msimamo wake. DHAMIRA Samwel na wenzake (2013) wanaeleza kuwa dhamira ni mada, lengo, kusudi, wazo kuu linalozungumzwa na shairi au kazi ya sanaa. Wanaongeza kuwa katika mashairi huweza kuwa na dhamira ya kiuchumi, kijamii, kisiasa na ha...