Posts

Madhara ya kunywa pombe kupita kiasi

Image
  UNYWAJI wa pombe kupitia kiasi si mzuri kwa afya yako, kitu kilichothibitishwa kisayansi miaka kadhaa iliopita. Katika kipindi cha miaka ya hivi karibuni, utafiti umeonyesha kuwa imani za zamani kwamba glasi moja ya mvinyo wakati wa chakula ni muhimu ni potofu. Hivi sasa athari za unywaji wa pombe zinazidi kujulikana. Kundi moja la wanasayansi kutoka chuo kikuu cha Rutgers nchini Marekani  na watafiti kutoka chuo cha Yale nchini humo, wamegundua kwamba unywaji wa pombe unaweza kuathiri chembechembe  za vinasaba vya binadamu (DNA) na kumfanya atamani kunywa pombe zaidi. Watu wengi pia wanahoji iwapo kinywaji kimoja kina athari mbaya kwa afya. Ili kupata jibu, kundi hilo la watafiti liliamua kuangazia uchanganuzi wake katika jeni mbili zinazohusiana na kudhibiti tabia wakati tunapokuwa chini ya shinikizo la pombe. Moja ni ile ya PER2 inayoshawishi maisha ya miili yetu na nyingine ya POMC, ambayo inadhibiti utaratibu wetu wa kukabiliana na dhiki.   Wakilinganisha wany...

Ukoo wa Mashelle

Image
Moja ya picha ya maadhimisho ya miaka 100 tangu kufariki kwa Mangi Mashelle wa shimbi Historia ya ukoo wa Mashelle Dhana ya ukoo  Ukoo Ni muunganiko wa kimbari ambao huunganisha familia zilizo na chanzo kimoja (Mababu) ukoo huweza kukua na kupelekea kugawanyika kwa vitongoji kadhaa. Vilevile ukoo huweza kugawanyika kwa sababu za kigeografia. Katika makala hii tutazungumzia ukoo wa Mashelle ambao unaasili ya Mkuu, Shimbi.  HISTORIA YA SHIMBI (chimbuko la ukoo wa Mashelle) Uruka wa Shimbi (nchi ya Shimbi) Ukoo wa Maria kawishe (Kavishe) Shimbi ndio chanzo hasa Cha Mashelle. Ukoo huu wa Maria kawishe ukianza Shimbi Karne nyingi zimepita na mwanzilishi wa ukoo huu aliitwa M'mamba aliyetokea mamba kwa kirie na wakati akitafuta makazi mapya ardhi yenye rutuba ndipo alipoweka maskani yake katika uruka wa Shimbi (nchi ya Shimbi) na hapo ndipo ukoo wa Maria kawishe ulipoanzia.  Kwa mujibu wa sensa ya wanaukoo mwaka 1993 hivi ndivyo vizazi vya wanaukoo M'mamba akamza Kitimbiri, Kit...

SIFA ZA KONSONANTI, UZIADA KANUNI ZA KIUSILIMISHO NA ZISIZO ZA KIUSILIMISHO

SIFA KUU ZA KONSONANTI Sifa hizi zinazingatia mambo makuu matatu 1.      Jinsi konsonanti zinzvyotamkwa 2.      Mahali ambapo konsonanti hutamkiwa 3.      Hali ya nyuzi sauti SIFA ZA JINSI YA MATAMSHI Katika sifa hii konsonanti hugawika katika makundi sita A.    VIPASUO/VIZUIWA Wakati wa utamkaji wa konsonanti hizi huwa kuna mzuio wa mkondohewa na kuachiwa ghafula. Konsonanti hizi zimepewa jina hilo kutokana na kwamba katioka kuachiwa ghafla kwa mkondohewa sauti itokeayo huwa kidogo kama ina mlio wa kupasua. Kwa mfano konsonanti /p/, /b/, /t/, /d/, /k/ na /g/. /p/  kipasuo sighuna cha midomo /b/ kipasuo ghuna cha midomo /t/ kipasuo sighuna cha ufizi /d/ kipasuo ghuna chaa ufizi /k/ kipasuo sighuna cha kaakaa laini /g/ kipasuo ghuna cha kaakaa laini B.     VIZUIO/VIPASUO KWAMIZA Konsonanti hizi zinapotamkwa hewa husukumwa nje kwa nguvu na kuzuiwa halafu nafasi ndogo huachwa ili hewa ipite ikiwa na mkwa...

MOFOLOJIA YA LUGHA KISWAHILI

Image
mofolojia ya lugha ya kiswahili Mofolojia-ni uwanja mdogo ndani ya isimu. Isimu-Ni taaluma inayochunguza lugha ya binadamu kisayansi. Mwanaisimu-ni mwanasayansi achunguzaye lugha ya binadamu katika nafasi zake zote yaani muundo, matumizi yake na nafasi yake katika jamii. Isimu ina nyanja na matawi yake. MATAWI YA ISIMU -Fonolojia -Sintaksia -Mofolojia -Isimu nadharia Nyanja za Isimu hushughulika na jinsi maneno yanavyoundwa. Mfano; mofolojia, fonolojia -Matawi ya Isimu huhusu mikabala ya kuchanganua taarifa mbalimbali za lugha. Mfano; Isimu nadharia huchunguza vipengele mbalimbali vya lugha. MATAWI YA ISIMU ISIMU NADHARIA -Taratibu zinazobuniwa kuwawezesha wachunguzaji fulani wa lugha kufuata taratibu fulani. ISIMU FAFANUZI -Hutoa uchunguzi wa sarufi za lugha na huhusu uchunguzi wa lugha na familia ya lugha fulani na historia ya lugha hiyo katika mazingira yaliyopo ISIMU HISTORIA -Huangalia jinsi lugha ilivyokua hapo awali. Hutumika kulinganisha lugha kulingana na jamii zake ukajua kam...

Love story mama mdogo

Image
SIMULIZI YA MAMA MDOGO SURA YA ........14.......  ILIPOISHIA: Usiku mama mdogo alianzisha tena mazungumzo na baba Jamal kuhusu kumpeleka Jamal shule. Alimsifia Jamal kwamba amebadilika sana na kwamba sasa ni mtoto mzuri, hana kiburi, anajituma katika kazi na ameacha kabisa mambo ya mapenzi. Hivyo alisisitiza kwamba apelekwe shule ili akasome kwa faida yake na mdogo wake. Baada ya kufikiria sana baba Jamal alikubali na kumtaka mama yake mdogo aende shule ya Sekondari ya Jitegemee ili akatafute nafasi na kisha Jamal aanze kusoma mara moja. INAPOENDELEA: Siku iliyofuata baba Jamal alikwenda kazini kama kawaida yake. Jamal aliamka saa tatu siku hiyo, kwani hakupata usingizi vizuri usiku kutokana na kuwa na mawazo mengi. Alikwenda sebuleni na kumwita mama yake mdogo aliyekuwa chumbani. Mama mdogo alipofika tu alimrukia Jamal shingoni na kumbusu shavuni. “Jamal kazi nimemaliza.” Alitamka mama mdogo huku akimwangalia Jamal. “Kweli mama mdogo? Mbona siamini, umetumia m...