Posts

Mifumo ya kidijitali itakayokusaidia kufanya kazi nyumbani

Image
Baadhi ya kampuni zinazotoa huduma ya intaneti zimeimarisha huduma hiyo kuwafikia wafanyakazi wanaofanya kazi zao wakiwa nyumbani.  Zipo baadhi ya programu tumishi kama Google drive, Meet zinazoweza kuongeza ufanisi wa mawasiliano na kazi.  Programu hizo zinasaidia kuwasiliana, kusimamia kazi na kutunza nyaraka mtandaoni.  Dar es Salaam.  Mlipuko wa ugonjwa virusi vya Corona umeathiri shughuli nyingi za kiuchumi na kijamii na baadhi ya kampuni na taasisi kulazimika kufunga ofisi na kuwaruhusu wafanyakazi wao kufanyia kazi nyumbani.  Hata hivyo, teknolojia ya intaneti na programu tumishi (Apps) zinayafanya maisha kuendelea kama kawaida kwa wafanyakazi kutekeleza majukumu yao popote walipo kwa kuunganishwa na mifumo ya kidijitali.  Baadhi ya kampuni za teknolojia ikiwemo ya Liquid Telecom inayotoa huduma ya intaneti nchini Tanzania zimejidhatiti kuhakikisha huduma hiyo inapatikana vizuri ili kazi za uzalishaji ziendelee kama kawaida bila kuathi...

CORONAVIRUS: FAHAMU KINACHOTOKEA NDANI YA MWILI MTU AKIPATA VIRUSI HIVI

Image
Coronavirus ilitokea Desemba mwaka jana lakini tayari dunia nzima inakabiliana na janga hili la - Covid-19. Kwa wengi ugonjwa huu unajitokeza nguvu yake ikiwa ya wastani tu lakini baadhi ya watu hufa. Lakini je virusi hivi vinaathiri vipi wili, kwanini baadhi ya watu wanakufa na je tiba yake ikoje? Muda wa  kuatamia wa kirusi cha Corona Hiki ni kipindi ambacho kirusi kinajiimarisha kwenye mwili. Kirusi huingia kwenye seli zinazotengeneza mwili na kuziteka nyara. Coronavirus, inayojulikana pia kama Sars-CoV-2, inaweza kuvamia kwenye mwili unapopumua yaani baada ya mtu mwenye virusi kukohoa ama kushika sehemu yenye virusi hivyo na kushika uso wako. Kwanza inaambukiza seli za kwenye koo lako, njia za kupumua na kwenye mapafu na kuzibadilisha kuwa sehemu ya utengenezaji wa virusi vya corona, na kuzalisha virusi vingi vipya ambavyo vinaenda kuathiri seli nyingi zaidi. Katika hatua hii, bado utakuwa hujaanza kuumwa na kuna baadhi ya watu ambao hata hawaoneshi ...

Uchapaji na uchapishaji, kurasa za mwisho za kitabu

MADA: *SEHEMU ZA MWISHO ZA KITABU* Wapendwa, karibuni katika somo la leo. Somo la leo litahusu *sehemu za mwisho za kitabu na jalada.* Imani yangu ni kwamba sote tumeshasoma somo la Nne na la Tano na kuelewa sehemu ya kwanza na ya maandishi katika kitabu. Sasa leo, tutamalizia sehemu mbili zilizobaki. *Kurasa za mwisho wa kitabu* Kurasa za mwisho wa kitabu zina vipengele vidogo kadhaa kama *Marejeleo/Bibliografia, Faharasa (Index) na Sherehe/Ufafanuzi wa maneno mapya (Glossary).* Ili kuelewa vizuri, ni vyema tukaangalia vipengele hivyo vidogo vya mwisho wa kitabu kwa umahususi wake. *Marejeleo/Bibliografia* Kuna mambo mawili hapa ambayo tunapaswa kuyafahamu kabla ya kwenda mbali. Jambo la kwanza ni kwamba neno *Marejeleo* limezoeleka kama *Marejeo.* Katika mjadala wetu ninapendekeza tutumie neno Marejeleo kwa maana ya kurejelea vyanzo vya maarifa au taarifa, ukitamka neno marejeo kuna hali ya ukakasi fulani unaoonesha kurudi kwa mtu au kitu. Kwamba mtu fulani hakuwapo kwa mu...

SEHEMU ZA MWISHO ZA KITABU

MADA: *SEHEMU ZA MWISHO ZA KITABU* Wapendwa, karibuni katika somo la leo. Somo la leo litahusu *sehemu za mwisho za kitabu na jalada.* Imani yangu ni kwamba sote tumeshasoma somo la Nne na la Tano na kuelewa sehemu ya kwanza na ya maandishi katika kitabu. Sasa leo, tutamalizia sehemu mbili zilizobaki. *Kurasa za mwisho wa kitabu* Kurasa za mwisho wa kitabu zina vipengele vidogo kadhaa kama *Marejeleo/Bibliografia, Faharasa (Index) na Sherehe/Ufafanuzi wa maneno mapya (Glossary).* Ili kuelewa vizuri, ni vyema tukaangalia vipengele hivyo vidogo vya mwisho wa kitabu kwa umahususi wake. *Marejeleo/Bibliografia* Kuna mambo mawili hapa ambayo tunapaswa kuyafahamu kabla ya kwenda mbali. Jambo la kwanza ni kwamba neno *Marejeleo* limezoeleka kama *Marejeo.* Katika mjadala wetu ninapendekeza tutumie neno Marejeleo kwa maana ya kurejelea vyanzo vya maarifa au taarifa, ukitamka neno marejeo kuna hali ya ukakasi fulani unaoonesha kurudi kwa mtu au kitu. Kwamba mtu fulani hakuwapo kwa mu...

SEHEMU YA KIINI CHA KITABU

*SOMO LA TANO* MADA: *SEHEMU YA KIINI CHA KITABU* Wapendwa, karibuni katika somo letu la leo. Somo linahusu sehemu za kitabu na mpangilio taarifa. Nianze kwa kukumbusha kwamba, katika somo la Nne, tuliona kuwa kitabu kina sehemu kuu nne. Sehemu hizo ni *kurasa za mwanzo, kurasa za maandishi yenyewe, kurasa za mwisho na hatimaye jalada.* Sasa, tayari tumeshaona sehemu ya kwanza ambayo ni kurasa za utangulizi. *Katika somo la leo tutaendelea na sehemu ya maandishi yenyewe ya kitabu.* *Sehemu ya pili: Maandishi ya kitabu* Sehemu hii ni nyeti sana. Sehemu hii inapaswa kutendewa haki kwa umakini kwa sababu ndiyo uwanja ambao mwandishi anapaswa kuuchezea vyema. Sehemu ya mwanzo ilikuwa ni ya maandalizi tu ili sasa mwandishi aingie uwanjani na kucheza mchezo wake kwa watazamaji ambao ni wasomaji. Hapa kunahitaji umakini katika uteuzi wa lugha ya kutumia, kupangilia hoja vizuri na kimantiki ili wasomaji wafuatilie kile ambacho mwandishi anataka kukisema. Tukumbuke kwamba, wasomaji wali...

AUDIO | Rayvanny – corona | Download

Image
DOWNLOAD

KWA NINI VIRUSI VYA CORONA SIO MWISHO WA DUNIA

Image
Ugonjwa wa kirusi cha corona kitaalam COVID-19 uliripotiwa kwanza tarehe 31 December 2019 jimbo la Wuhan China. Mpaka kufikia juzi March 13 wagonjwa 136,895 wamethibitishwa kati ya hao watu 5,077 wamepoteza maisha katika nchi 123 duniani kote kulingana na takwimu za WHO. Kufikia March 13 nchi 12 za Africa ziliripoti uwepo wa wagonjwa mpaka jana March 14 ziliongezeka Sudan, ambapo mtu mmoja alifariki, Ethiopia, Kenya na Gabon. Wengi wameanza kusema kuwa huu ni mwisho wa dunia wengine wakisema ni ugonjwa wa kutengenezwa. COVID-19 ni nini? Hiki ni kirusi kutoka katika familia kubwa ya virusi vya corona. Virusi vya corona vipo vya aina nyingi na vinaweza kusababisha mafua ya kawaida na pia mafua hatari kama Severe Acute Respiratory Syndrome (SARS) NA Middle East Respiratory Syndrome (MERS). COVID19 ni vinasaba vipya ambavyo havijawahi kutokea hapo awali. Chanzo cha virusi vya corona inaripotiwa kuwa wanyama pori dalili ni pamoja na homa, kikohozi, kukosa pumzi na ...